Utabiri wa Sheikh Yahya Hussein mwaka 2006 na Tanzania kuwa na Rais Mwanamke

Utabiri wa Sheikh Yahya Hussein mwaka 2006 na Tanzania kuwa na Rais Mwanamke

Wakuu nimepita sehemu nikaikuta hii meme ambayo ilitengenezwa na Wataalam iki mnukuu aliyekuwa mtabiri na msoma nyota mashuhuri Afrika Mashariki na kati marehemu Sheikh Yahya Hussein, vipi huyu marehemu alikuwa anaona mbele zaidi?

Alichokitabiri kwa asilimia kubwa kimetimia, vipi mwaka wa uchaguzi 2025,Vyama vikuu vya upinzani ACT WAZALENDO na CHADEMA, Vitaigeuza CCM kuwa chama cha upinzani?

20240605_201208.jpg
 
 
Wakuu nimepita sehemu nikaikuta hii meme ambayo ilitengenezwa na Wataalam iki mnukuu aliyekuwa mtabiri na msoma nyota mashuhuri Afrika Mashariki na kati marehemu Sheikh Yahya Hussein, vipi huyu marehemu alikuwa anaona mbele zaidi?
Alichokitabiri kwa asilimia kubwa kimetimia, vipi mwaka wa uchaguzi 2025,Vyama vikuu vya upinzani ACT WAZALENDO na CHADEMA, Vitaigeuza CCM kuwa chama cha upinzani?
View attachment 3009639
Rejea tabiri zake 2010,

Aliwahi kutabiri kuwa rais Mstaafu Benjamini Mkapa atapewa kazi kubwa duniani baada ya mwaka mmoj alipewa kazi n UN kusimamia mchakato wa kura ya kujitenga ya Sudan Kusini
 
Huu mwaka 2011 ni mwaka wa ajabu sana

osama alikufa 2011
Gadaffi alikufa 2011
mabomu mbagala 2011
ckujua km nae huyu shekhe alikufa 2011
Km aliyasema haya napata ?
 
Wakuu nimepita sehemu nikaikuta hii meme ambayo ilitengenezwa na Wataalam iki mnukuu aliyekuwa mtabiri na msoma nyota mashuhuri Afrika Mashariki na kati marehemu Sheikh Yahya Hussein, vipi huyu marehemu alikuwa anaona mbele zaidi?
Alichokitabiri kwa asilimia kubwa kimetimia, vipi mwaka wa uchaguzi 2025,Vyama vikuu vya upinzani ACT WAZALENDO na CHADEMA, Vitaigeuza CCM kuwa chama cha upinzani?
View attachment 3009639
Ebu tuwe wakweli, ni upinzani gani wa kuchukua nchi?
 
Ulongo mtupu,leteni video Tuamini.
Kipindi hicho video zilikuwa adimu sana, media zilizokuwa kwenye chati wakati huo ilikuwa magazeti na redio. Huo utabiri ni kweli aliufanya kabla ya kifo chake na sikuuamini sana mpaka nikausahau..... Lakini amepatia kwa kiasi kikubwa, tungoje kuona kama 2025 upinzani utachukua nchi.
 
Nikweli nimeukumbuka utabiri huo aliitisha press conference akasema hayo , nakumbuka kidogo wachungaji walimtangazia Vita ya Imani , ndoto y Raisi mweusi aliisema (magufuli)
 
Wakuu nimepita sehemu nikaikuta hii meme ambayo ilitengenezwa na Wataalam iki mnukuu aliyekuwa mtabiri na msoma nyota mashuhuri Afrika Mashariki na kati marehemu Sheikh Yahya Hussein, vipi huyu marehemu alikuwa anaona mbele zaidi?
Alichokitabiri kwa asilimia kubwa kimetimia, vipi mwaka wa uchaguzi 2025,Vyama vikuu vya upinzani ACT WAZALENDO na CHADEMA, Vitaigeuza CCM kuwa chama cha upinzani?
View attachment 3009639
Mhu! Nilikuwa nafuatilia uchaguzi wa India na Africa Kusini nikajifunza kwamba vyama vikongwe duniani vinaendelea kupoteza 'mass support' nadhani kwa sababu ya kwamba 'mwenye shibe hamjui mwenye njaa'.
 
Natamani mabadiliko yapatikane lakini pia sioni wa kubadili huko upinzani au kama vipi tubeti tu, tuwajaribu na wao.

Kuhusu hiyo meme, hakuna ushahidi kuwa alisema sheikh yahaya, hilo moja pili hata kama kasema siamini mpaka itokee
 
Nyie mwasema. Unajua marekani pamoja na demokrasia yote iliyopo pale, "hakujawahi kuwako raisi mwanamke"
 
Nimesoma hii article pale kwenya magazeti ya Shigongo, ikanishtua kwa vile inaoneka utabiri wake ulikuwa kweli kabisa. je ni coincidence tu au ni kweli alikuwa anajua kupiga mahesabu ya kuona mbele? Najua kuwa aliwahi kutabiri kuwa mtu yeyote atakayechukua formu kumpiga Kikwete mwaka 2010 angekufa ghafla, watu ndani ya CCM ambao walikuwa wameshapanga mkakati wa kumng'oa Kiwkete mwaka 2010 wakaa kimya kabisa.

ALIYEKUWA Mtabiri maarufu Afrika Mashariki, Shehe Yahya Hussein aliitisha mkutano wa wahariri na waandishi wa habari mwaka 2006 na kuzungumzia utawala wa Rais Jakaya Kikwete ukiwa na umri wa mwaka mmoja tu.

Baada ya kuzungumza hayo nilipata nafasi ya kumuuliza. Je Tanzania baada ya Kikwete inaweza kupata rais mwanamke?

Shehe Yahya alinijibu:

“Baada ya vipindi viwili vya Rais Kikwete atakuja rais ambaye ni mweusi mchapa kazi lakini mchekeshaji sana, hata hivyo atatawaka kwa kipindi kifupi tu hapo ndipo Tanzania itapata rais mwanamke.”

Wahariri na waandishi waliguna kuonesha kutokubaliana naye wakiwemo wahariri wakongwe Hemedi Kimwaga, Yasini Sadiki, Magnus Mahenge na wengine ambao siwezi kuwakumbuka.

Shehe Yahya baada ya kuona tunambishia alichukua ubao kama ule wa darasani na mkononi alishika kutabu kilichoandikwa Astrology: Monthly numerology, akaanza kufanya hesabu kwa fomula anazojua yeye na akatuambia kwamba kwa Jakaya inaonesha atamaliza muda wake wa miaka kumi na lakini ajaye ataongoza kwa kipindi kifupi.

Tulimuuliza ataongoza kwa muda mfupi kwa sababu gani, alisema hayo mengine yeye hawezi kujua lakini akasisitiza kwamba hivyo ndivyo itakavyokuwa. Tulitawanyika pale kila mmoja akiwa anaona kama amepigwa ‘changa la macho’.

Lakini sasa nimeng’amua kwamba kumbe alikuwa akimtabiria mama Samia bila yeye mama kujua tulichokuwa tunafanya.

HAKIKA SHEHE YAHYA ALIKUWA MNAJIMU WA KWELI.

Kumbuka haya yanatokea baada ya miaka 15 ya utabiri wake na mtabiri akiwa katangulia mbele za haki. Sheh Yahya alifariki mwaka 2011. Mungu ampe raha ya milele na amnusuru na adhabu ya kaburini.
Weka video ya huo mkutano..
 
Back
Top Bottom