Utafiti wa Sauti za Wananchi, Awamu ya 27 wa Aprili 2018 umebaini 55% ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani 2015.
Ado Shaibu kutoka ACT Wazalendo
Napenda kwanza kusema tu Magufuli ndio rais ambaye ni 'Unpopular' kuliko Marais wote, kwa mujibu wa tafiti hizi za Twaweza Mkapa alianza na asilimia 93 na akaondoka na 90, Kikwete asilimia zilipungua kidogo sana ila sasa Magufuli ameanza na 96% kwa sasa yupo 55%
Sasa hili linatokana na Magufuli kutengeneza ugomvi na Wakulima, Wavuvi, Mashangazi, Wafanyakazi na wananchi wote kwa ujumla
Anachokifanya Magufuli ni sawa na kucheza mpira halafu umewafunga kamba wapinzani sasa anacheza mwenyewe maana hakuna uhuru wa vyombo ya habari, vyama vya siasa havipo huru. Je, angeachia huru vitu hivi ingekuwaje?
Mimi nasema Rais Magufuli hizo asilimia zilitakiwa zifike 20