UTAFITI: Juma Nature alikuwa maarufu wakati wake zaidi ya Diamond Alivyo maarufu kwa wakati wake

UTAFITI: Juma Nature alikuwa maarufu wakati wake zaidi ya Diamond Alivyo maarufu kwa wakati wake

kenge 10, Hapo Nature Alikua anatafuta sifa aonekane naye ni mtu wa watu, read between lines,kwani wasanii wa zamani huwajui tabia zao za kutafuta popularity??, Si ndio Alikiba anasema eti "sitaki bodyguard" nabakigi nawaza, nani atajisumbua kumfanyia fujo kiba hana jipya huyo, watu wanawaza kuwateka kina Diamond sio Kiba.
 
Mondi anahonga redio gani? Wakati redio kubwa tatu TZ hazipigi mziki wake lkn bado yupo juu.
Vizabinazabina hao. Kila siku wanalala wanamuota mond ashuke. Wanafananisha mond marujuana ya arusha.
 
Nedago, Kuna watu kila siku wanamuota mond,wanajaribu kuringanisha huku,wanamtafutia sababu hizi na hizi bado anabaki juu.
 
Mbona Alikiba yuko nyuma kila mahala hii si haki. Anatakiwa kuwa no 1 hapo sema hapendi show off.
Nyie ndiyo mnapotoshs huyu dogo....ndiyi maana ana majivunio wakati hana ishu yeyote zaidi ya sauti nzuri....sasa hivi hana uwezo wa kutoa hit song ...amebakia na yebababaaa tu
 
Kuna watu kila siku wanamuota mond,wanajaribu kuringanisha huku,wanamtafutia sababu hizi na hizi bado anabaki juu.
Imefikia hatua kwamba Mond anapaa kupita kiasi sasa inabidi kumtafutia kasoro zozote
 
Hapa ukimtaja Nature mashabiki maandazi wa Mondi watakwambia ni wivu tu,mashabiki wengi wa Domondi waliozaliwa 1995-2002 ambapo kipindi nature yupo juu anatikisa na kina sinta wao bado walikuwa wanakunjwa uji wa ulezi/lishe na kunywa maziwa kwenye chupa,hawawezi kukuelewa ukisema nature alikuwa maarufu kuliko Dimondi.
Kweli kabisa
 
Umaarufu ndani ya mipaka ya TZ au hadi nje ya mipaka?

Maana ukitazama waliotajwa hapa wote mbinu zao za kuteka soko la muziki zilikuwa/zipo tofauti...

Nature aliimba muziki unaojali watu wa mtaani zaidi na kidogo maisha halisi ya watanzania, muziki wake ulichagizwa na vijimaneno maneno vinavyoweza kujulikana na watu wa mtaani, na ndio ilikuwa wakati sahihi maana bongo flavor ilipendwa zaidi na watu wa rika la katikati.
Ukiacha hilo, Nature alipata kushiriki nyimbo nyingi sana na zote zilikuwa moto kiasi kwamba huwezi choka kumsikiza...

Mr Nice yeye sio tu kuwa aliimba muziki bali alikuja na style yake pekee ya muziki ambayo aliipa jina la Takeu, muziki wake ulitoka nje ya Tanzania lakini ukaishia nchi zinazoizunguka Tanzania...

Alikiba huyu utamu wa sauti yake, simulizi katika nyimbo zake ulifanya apendwe Tanzania na nchi zinazoizunguka Tanzania, wakati akiwa kileleni muziki wa bongo flavor haukuwa ukijulikana sana duniani, na hata wakati ulipoanza kujulikana huyu bwana ni kama alikuwa kwenye likizo ya utunzi na uimbaji...

Diamond huyu bwana mdogo uwezo wake wa kuimba simulizi za mapenzi kwa namna ya kulalamika ulimfanya awe na namna ya pekee kugusa mashabiki zake na ndio umaarufu wake ndani ya mipaka ya mashariki ya Afrika ulipoanza.
Kitu kingine alichoweza kukifanya Diamond ni kuamua mapema sana kuufanya muziki wake uwe biashara na si burudani pekee, aliamua awekeze katika muziki na kuthubutu kujaribu kwenda nje ya mipaka kuzidi walipofika waliomtangulia.
Kwa kifupi Diamond umaarufu wake ni mchanganyiko wa vitu vingi sana na binafsi naona ndiye kijana aliyefanikiwa sana kujulikana nje ya mipaka ya Afrika na hata duniani kwa ujumla
 
Inaelekea hukujua kazi ya bab tale na said fella wewe

Hao ndio mashabiki maandazi wa mondi yaani ni watu wasiojielewa wao wakishanunuliwa bando na mondi kwenye vitekno vyao wao ni kusifu tu,hawajui fitina wanazofanya OSATA(Othmani Suka,SAid Fela na TAle) kwenye media house.
 
Diamond anatumia nguvu nyingi sana kujitangaza, wakati Kina Juma walitangazwa na mziki na kupendwa bila kuhonga maredion
Nyakati zimebadilika sasa ndio maana nature gemu kashindwa sasa toka 2012, iko simpo.
 
Diamind wa kawaida sana. Kinachombeba ni wale managers wake wenye fitna n majungu.
 
Back
Top Bottom