UTAFITI: Juma Nature alikuwa maarufu wakati wake zaidi ya Diamond Alivyo maarufu kwa wakati wake

UTAFITI: Juma Nature alikuwa maarufu wakati wake zaidi ya Diamond Alivyo maarufu kwa wakati wake

Sawa mkuu mda utaongea,kwetu msanii mkubwa ni yule anayetrend kwa kiki na wala si kwa kazi zake,nchi za wenzetu wana taasisi kabisa zinazomonitor performance ya msanii sokoni kwa USA wana RIAA ambayo inamrate msanii,ndio maana utasikia msanii ameuza double platnum hao ndio wanaleta mrejesho lakini kwa huku kwetu Mashabiki ndio wanaoleta data za msanii kama kauza kihasi gani anarun vipi sokoni etc
Mwenzako analeta facts wakati wewe unaleta porojo sema unaonekana age imeenda alafu ufuatilii mziki wa sasa ndo maana vitu vingi ujui.
 
Hebu nitajie mfumo rasmi unao simamia mziki Tanzania? au chombo rasmi kinachosimamia mziki Tanzania ambacho kinaweza kukupa data kuhusiana na maswala ya mziki wa Tanzania?

Kenya wenzetu wana mifumo rasmi ya kusimamia mziki wao ,wana chombo cha kusimamia malipo ya msanii kulipwa endapo nyimbo ikipigwa redioni MSCK.

2015 kupitia report za MSCK Mondi aliingiza Ksh 350,000 za kenya (Tsh 7000000 million) ndani ya miezi mitatu na mwaka uliofuatia Kenya waka implement 60% (Local content) 40%(Foreign content) na pamoja na hiyo ratio bado Mondi anakimbiza.Sasa hiyo 2015 je sasa hivi 2019 itakuwaje?

Karibia digital platforms zote zinazouza mziki Kenya Zipo .Wana mpaka kampuni za kufanya research ktk entertainment industry mwaka jana kuna kampuni ya 8020 ilifanya Research based on 2018 Kenya msanii anayeongoza kwa mauzo kwenye digital platform,streaming,airtime kwenye redio,viewers za Youtube ni Diamond (Najua humpendi).

Na wakatoa picha jinsi jamaa anavyo dominate,sasa hapo ni mwaka jana alikaa mwaka mzima hajatoa nyimbo na akaburuza,je mwaka huu ana utitiri wa nyimbo.

Bongo tulikuwa na chombo kama
MSCK kilikuwa kinasimamiwa na P Funky Majani watu wamekipiga majungu kimekufa.
Ndio maana nikasema kwa TZ mashabiki ndio wanamrate msanii kimauzo na kufanya vizuri sokoni,kitendo cha mashabiki kumrate msanii hapo ndio tunapoangukia kwenye TEAM lakini kungekuwa na chombo maalumu kumonitor perfmance za wasanii wetu ingekuwa easy kujua msanii anafanyaje sokoni.
 
Naona unampa facts sema jamaa anaongozwa na chuki kuliko kuleta facts
Nilishasema tangia awali ukimchallenge mond unaonekana una chuki,cha kushangaza mbona kina AY.FA ni matajiri na wana hela kuliko huyo mondi mbona hakuna sehemu yeyote tunawasema vibaya? Tatizo msaniii wenu yupo Overated sana kisa mnapewa tecno na bando kushinda online kumtetea,nyie mnaendeshwa na hisia tu,domondi kwasasa anaendeshwa kwa fedha za ringtones(hits song za zamani),youtube and the like,matangazo basi ila sijui show hakuna kitu.
 
Mwenzako analeta facts wakati wewe unaleta porojo sema unaonekana age imeenda alafu ufuatilii mziki wa sasa ndo maana vitu vingi ujui.
Hhahahaaaa najua vitu vingi ambavyo naweza kumfundisha hadi dingi wako achilia mbali wewe,kuenda age ni baraka mkuu hauoni vijana wa sasa wanadanja kwenye 20's?? Najua vitu vingi sana kwa undani ambavyo wewe unaona unavijua pia vitu navyojua mimi wewe na ukoo wenu wote mjikusanye hamvijui.

Halafu tofautisha kujua vitu na udaku,wewe unajua sana udaku,kufatilia kina jux na vanesa wanatoka na nani kwa sasa,kufatilia kina uchebe na shishi wametoa kiki gani,kufatilia kina mwijaku na menina etc wewe unafatilia hayo mambo Shallow mind wanafatilia watu lakini great mind wanafatilia issues...kwa mambo ya kujua udaku unanizidi lakini kwa kujua issue mjikusanye ukoo wenu wote hamnipati.

Katika kujua mziki yaani dogo wewe haujui mziki kuliko mimi,naujua mziki nje ndani na nimeufanyia kazi mziki,naujua mziki kabla boss wenu hata kutoa singo bado achana na wimbo wa jisachi wakati domondi anachana produced na lamar ft jeezy mabovu na ngwair,nimeanza kufatilia mziki tangu 1992 unamjua saleh jabir wewe au umemsoma kwenye gugo? Salehe jabir anatoa nyimbo zake sie tunaruka nazo debe.

Naughty By Nature wana hustle na Queen Latifah kutoa OPP? Westlife wametoa Coast to Coast bado mbichi tunasikiliza kwenye walkman,B2K Pandemonium wanatolewa na puffy daddy kabla hata boss wenu hamjui hata omario ndio nani.....STuka wewe haujui kitu wewe hizo nyimbo unaziona ni oldxul lakini sisi tumeshuhudia wanafanya launching MTV/BET/ESPN.

Unamjua DJ JD wewe ndani ya ITV2(Ndio hii inaitwa EATV kabla ya kuitwa Channel 5)? Unamjua DJ HABIB 101.4FM(Ndio hii leo mnaita Capital Radio)? Unawajua MASHARP SHOOTER SAUTI YA MIUJIZA UBANDIDU? Unamjua DOgo Hasheem ushawahi sikiliza interview zake? Nishamsikiliza ndio anarelease singo yake In the Shadow ebu igugo najua hauijui kabisa.

Kujua sijui hamonaizi katoa UNo au Kiba na Mshumaa wake au Abdu Kiba Sherry coco sio kujua mziki ndugu.
 
Usimfananishe Diamond platinumz na juma nature unakosea,diamond ni mbingu na nature ni ardhi.

Hebu angalia mipaka ya umaarufu?
Inatakiwa uwe specific huo umaarufu ni katika eneo gani?

Kibongo bongo?
Afrika mashariki?
Africa?
Au duniani kote?

Diamond platinumz ni maarufu duniani kote
na wakati hao kina juma nature na wenzie ilikuwa ni bongo tu na Africa mashariki Yaani Kenya na Uganda.

Acha kumdhalilisha Diamond na hao wababaishaji wa Kibongo bongo.
Diamond akienda USA na Ulaya anaenda kuwapigia show wabeba mabox wa kiafrica especially EA..ila Jagwa wakienda Ulaya kufanya show 98% ni wazungu kwenye show zao
 
Nilishasema tangia awali ukimchallenge mond unaonekana una chuki,cha kushangaza mbona kina AY.FA ni matajiri na wana hela kuliko huyo mondi mbona hakuna sehemu yeyote tunawasema vibaya? Tatizo msaniii wenu yupo Overated sana kisa mnapewa tecno na bando kushinda online kumtetea,nyie mnaendeshwa na hisia tu,domondi kwasasa anaendeshwa kwa fedha za ringtones(hits song za zamani),youtube and the like,matangazo basi ila sijui show hakuna kitu.
Wewe ndiye unayeongozwa na hisia,sasa kwa kuwa hatuna mfumo rasmi wa kuquantify mziki wetu basi tuseme hatuna wasanii wakubwa ,basi Juma Nature na Prof Jay wapo sawa na Man X na Rado.

Wewe umejuaje hit song za zamani alikua anauza kiasi gani na sasa hauzi?

Eti show hakuna kitu,mtu kwa miaka miwili mfululizo ana show zaidi 70 unasema hana kitu?Juzi kapiga show kapiga Germany ktk ukumbi wa Columbus Germany capacity 3500 one man ,wakati nyuma hakuwahi kupiga show ktk kumbi kama hizo (Najua utahamia Nigeria).

Basi nitajie msanii Africa mashariki na kati mwenye show kama Mondi.

Alafu hata hizo deal za matangazo mpaka unapewa wamejirizisha kwa kufanya research bidhaa yao itawafikia watu wengi so at the end of the day unarudi pale kwenye quantity.

Kitu unachofanya kosa kufananisha mziki wa USA na TZ unafanya dhambi kubwa,sisi hata Kenya hatujawafikia.

So kwa kuwa hatuna mfuma wa kuquantify ,wasanii vipi mpaka hivi tuvionavyo kama viewers youtube,number of show ,ukisoma research ilifanyika mwaka jana Kenya 8020 Mondi anaongoza kwa mauzo mpaka kwenye digital platforms kwa wasanii wa Africa mashariki na kati, tuvikatae manake hatuna mfumo wa kuretrive data kutoka kwenye mifumo rasmi kama USA.

Msanii ambaye wewe unasema hana kitu lkn mwaka huu baada ya kupiga show anglophone countries (Senegal,Cameroon,Burkina Faso,Gunea) atakuwa kakamilisha zaidi 90% ya bara zima la Africa ukizitoa nchi za kiarabu.

Mwaka 2015 label inayosimamia mauzo yake walimpa kama hesma baada ya I nyimbo yake Marry Me kwa Miezi kumi kufikia mauzo ya 6 platnumz (1 platnumz kwa SA =30000,so 6Platnumz=180000)

Na hapo 2015 mziki wake hakuwafikia watu wengi kama sasa,ndani ya miaka hii mitatu amepiga show nchi za kusini mwa Africa na mwaka huu ana show ya baadhi ya Anglophone Countries,hii ina reflect number ya mashabiki inayo hitaji mziki wake inaongezeka kila mwaka,kwa hata mauzo yataongezeka na shows zinaongezeka.

AU WEWE MSANII MKUBWA KWA TZ UNA MQUANTIFY KWA PARAMETERS GANI?
 
huyo nature alikua wakawaida sana. nakumbuka alipambanishwa na profesa j akapigwambali kwa kura. pia hata tuzo hajachukua nyingi kumshinda profesa jay wala lady jaydee. na hata lilipokuja shindano la mkali wa lymz waliochuana vikali walikua ni profesa jay na afande sele na mwisho alichukua afande. na hata alipochomoka wanaume family akaanzisha wanaume halisi hilo kundi lilimshinda. hivyo juma nature alipendwa na wata bangi kwa sababu ndo alikua mkubwa wao. hivyo kumfananisha mondi na huyo mvuta bangi ni kumkosea heshima mondi. hata nyimbo zake nyingi zililenga wavuta bangi. tafuteni mtu mwingine wa kumpambanisha na mondi lkn sio huyo mvuta bangi.
 
Kiroboto aliteka masela nice aliteka rika zote mzee so huyu atakuwa nyuma ya nice
 
Wapiga kura watakua walihongwa na diamond tu..[emoji1787][emoji1787]..alikiba alitakiwa apate hizo kura sema tu hapendi showoff na mambo ya uongaji....[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Diamond ni miaka kumi bado yupo juu.. Toka diamond ameanza kuwa juu, hamna wa juu yake
 
Back
Top Bottom