Utafiti usio rasmi: Kuna vurugu na malumbano kidogo sana ama hakuna kabisa kwenye ndoa zenye wanaume wanaovuta bangi tofauti na wanaokunywa pombe

Utafiti usio rasmi: Kuna vurugu na malumbano kidogo sana ama hakuna kabisa kwenye ndoa zenye wanaume wanaovuta bangi tofauti na wanaokunywa pombe

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Hata kwa nchi zilizoruhusu bangi hesabu zinaonesha ndoa zenye wavuta bangi ni nadra sana kuwa na matatizo tofauti na ndoa za walevi wa pombe ambazo zimejaa kesi kibao za kuvunjika kwa ndoa, kupigana, kutukanana hadharani, watoto kupigwa hovyo, n.k.

Tukija hata hapa bongo tushazoea kuona pombe ikihusika kwenye matatizo mengi sana, mtu akitoka bar huko anaanza kumpiga mke wake, mtu haachi pesa nyumbani anathamini zaidi pombe, mtu analeta magonjwa ya ajabu kwa kulala na ma baamedi, watoto kutukanwa na kupigwa hovyo, n.k.

Mfano wangu ni mke wa mjomba, huwa anatupigia simu mara kwa mara kwamba ndoa imekuwa ngumu maana mume wake hashindi hata nyumbani, huwa anaunganisha baa akitoka kazini na siku nyingine analala huko huko. Marafiki zake wengi ni watu wa baa huko.

Tofauti na pombe hali ni tofauti kabisa kwa wavuta bangi, ndoa zao huwa hazina malumbano sana, vipigo, kutukanana ovyo mbele ya watoto, n.k.


Onyo: kama huna elimu ya kuijua bangi sahihi kaa mbali kunusuru afya yako.

Kwa hapa bongo nimeshuhudia pusha anauza bangi ina sumu ya panya au kaweka unga wa heroid ili apate wateja wa kudumu na cha ajabu hakuna hata mteja moja anayegundua. Hawa ndio watanzania wengi ambao wakivuta bangi watakusimulia kwamba walikuwa wanaoga kwenye matope wakidhani wapo baharini, na wengine kutongoza mama zao, ni kwasababu hawana elimu, wanatumia bila muongozo.

Ni lazima na sio ombi inabidi uwe unaijua bangi iliyochanganywa na sumu ya panya/unga, imevunwa ikiwa bado mbichi, imeshaharibika, haijafanyiwa flushing, n.k, lasivyo kaa mbali na bangi. Inabidi ujue kwamba kunywa maji mengi ni muhimu, uvijue vyakula vya kujizuia kula ukivuta, jinsi ya kuchambua bangi kwa usahihi kujinusuru kuwa hanithi, n.k.

kama huvijui hivi vitu acha, kaa mbali! Bangi haina tatizo bali ni watumiaji washamba wasio na elimu, watu wenye elimu sahihi wanatumia tangu form 2 na mpaka leo ni mabosi na wala huwezi kuja kujua wanatumia kilevi chochote!
 
Bangi nibangue

Jamaa alikuwa akivuta bangi ikikolea anafunga tochi utosini mchana kweupe kisha anaingia zake shamba kupiga jembe...
Bangi ikikukataa unaweza kuonekana chizi kwenye jamii
 
Hata kwa nchi zilizoruhusu bangi hesabu zinaonesha ndoa zenye wavuta bangi ni nadra sana kuwa na matatizo tofauti na ndoa za walevi wa pombe ambaO zimejaa kesi kibao za kuvunjika kwa ndoa, kupigana, kutukanana, n.k.

Tukija hapa bongo tushazoea kuona pombe ikihusika kwenye kuvunja ndoa na wanawake kuomba talaka, pombe hupelekea ugomvi na mpaka vipigo vya waziwazi kwa wake na watoto,

Wake wa wanywa pombe hupiga simu mara kwa mara kwa ndugu za waume zao kwamba ndoa imekuwa ngumu maana waume zao wanalala huko huko kwenye baa na kumalizia haja zao kwa mabaa medi.

Tofauti na pombe hali ni tofauti kabisa kwa wavuta bangi, ndoa zao huwa hazinaga sana malumbano, vipigo, kutukanana ovyo mbele ya watoto, n.k.


Bangi hizi tumesoma na watu kibao tangu sekondari form 2 watu wanavuta mpaka leo wapo makazini, wana biashara zao na wala huji sikia bangi imetia dosari ndoa ....
Kwa hio mkuu unatoa wazo nayo iundiwe tozo au?

Maana walevi wanalipa tozo kupitia pombe

Je! Nasema Uongo Ndugu Zangu nae aundiwe tozo?
 
.bana hawapendi kelel wazee wa msuba pombe ni kelel sana
 
Bangi nibangue

Jamaa alikuwa akivuta bangi ikikolea anafunga tochi utosini mchana kweupe kisha anaingia zake shamba kupiga jembe...
Bangi ikikukataa unaweza kuonekana chizi kwenye jamii
Alikuwa anapewa bangi iliyochanganywa na sumu ya panya huyo, huu mchezo mapusha wengi wanaufanya ili mtu ageuzwe kuwa teja,,,, Mzoefu wa bangi akinunua bangi aina hiyo akiinusa tu anamchana pusha aache uhuni
 
Mwamba anatafuta Justification ya kula mmea, anyways sijawahi kuvuta ila kwa niliyoyaona siwezi kuvuta pia.. Washkaji zangu si chini ya wanne waliharibikiwa kisa Bange, Wawwili wamekuwa confirmed mentals!

Hizi dawa za Kulevya maybe uwe na uchumi mzuri ndo zisiku affect, sio wewe kula yako tu shida ila unakula Bange lazima uwehuke!
 
Mwamba anatafuta Justification ya kula mmea, anyways sijawahi kuvuta ila kwa niliyoyaona siwezi kuvuta pia.. Washkaji zangu si chini ya wanne waliharibikiwa kisa Bange, Wawwili wamekuwa confirmed mentals!

Hizi dawa za Kulevya maybe uwe na uchumi mzuri ndo zisiku affect, sio wewe kula yako tu shida ila unakula Bange lazima uwehuke!
Mtu hawezi kutofautisha bangi iliyochanganywa sumu ya mende na bangi og unategemea nini hapo?

Mtu hata akivutishwa bangi iliyochanganywa heroim hajui chochote zaidi ya kusifia jna stim kali unategemea nini.

Mtu hata hajui bangi iliyokomaa yeye ananunua tu ilimradi unategemea nini?

Elimu, Elimu, Elimu, Kama huna elimu ya kitu ni heri ukae nacho mbali.

Ukienda nchi kama Jamaica, Marekani, udachi, n.k. huji sikia hizo kesi za watu kuwa vichaa kwa bangi, hapa bongo hujawahi kujiuliza kwanini watu wanavuta tangu 13 kama kina p funk ila hawana tatizo ? Jibu ni kwamba inabidi ujue unachokitumia,. Mtu unaenda kununua bangi ya jero kwa pusha ambae nae akili zake walu walu unategemea nn? Pusha akikuwekea sumu ya panya ili uwe teja yeye wala haoni kosa zaidi ya kupata faida kwa uhakika 😂😂. Na kama huna elimu ya hivi vitu unakuwa xhizi kweli kweli,
 
Bangi inafanyiwa figisu na wazee wa nchi hii walio wachawi wote kwa kuwa hua inakwamisha mambo yao.

"Mvuta bangi alogeki"
 
Tatuta mmea og ,nyonga mwenyewe kitu safi, unajimiminia mali yenye uhakika %100 Iko salama
 
Back
Top Bottom