Bibititi1
JF-Expert Member
- Sep 28, 2014
- 464
- 218
Watanzania si wepesi kuingilia Uhuru wa nchi nyingine Huru zinazoizunguka naweza kusema hivyo haijawahi kutokea Tanzania ikawa kinara wa mambo ya nchi nyingine siku zote wanaishi maisha yao na shida zao.
Ukimya huu wa Tanzania hata kwa Dunia ni nchi ambayo iliamua kutochagua upande wowote hata wakati wavita vya sekeseke la vita baridi haya yamekuwa mazoea ya watanzania kutoingilia migogoro ya nchi nyingine.
Majuzi pameibuka mgogoro wa kuhusu kuhamisha makazi ya jamii ya kimasai kutoka katika pori tengefu la Ngorongoro.
Kuhamishwa huko kunatokana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika Eneo Loliondo idadi ya makazi ni kubwa kuliko Ecolojia ya eneo ambayo inakwenda kuharibika.
Kwanini serikali inapendekeza Kilometa za mraba 1,500 ziendelee kutunzwa?
Ni chanzo cha mito sita inayomwaga maji katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Asilimia 48 ya maji yanayoingia Serengeti yanatoka ndani ya Pori Tengefu la Loliondo. Eneo hili ni muhimu kwa ikolojia ya Serengeti ikiwa na vyanzo sita vya maji, mapito na mazalia ya wanyamapori.
Ripoti za mazingira zinaonyesha kuwepo kwa ukame katika maeneo oevu ya vijiji vya Oloipiri, Soitsambu, Maaloni, Ololosokwan, Piyaya, Malambo, Maaloni.
Wagombea Kenya wanavyonufaika na mgogoro wa Loliondo
Loliondo ni mtaji wa Kura uchaguzi mkuu Kenya;
Kaunti za Maa, Turkana, Meru zimekuwa ni viwanja vya mapambano vya makabiliano ya kisiasa kati ya Naibu Rais Ruto na Raila Odinga.
Mgogoro wa Loliondo katika Bonde La Ufa ndiyo limekuwa eneo muhimu kwasasa katika kutafuta kura haya yalikuwa maeneo yenye muamko hafifu kabisa kwenye uchaguzi huu maeneo ya Nakuru na Laikipia.
Maeneo haya yalikuwa na picha hafifu kwa wagombea wote wa pande zote mbili wameamua kutumia nafasi hii ya Loliondo kujipigia debe kaunti hizi ni za wafugaji ambao wana makundi makubwa ya ng’ombe mpakani na ndani ya pori tengefu la Loliondo.
Kiasili ni maeneo yenye ukame mkubwa yaani Narok na Kajiado nchini Kenya. Hili la ukame wamekuwa wakitumia kama kisingizio lakini ukweli ni kuwa Loliondo ndilo shamba lao. Inapotokea rabsha kama hii ni lazima wapagawe wenyewe kwa wenyewe wanakwenda kukosa malisho kwa jailli ya mafugo Yao.
Haikutushangaza kumuona binti wa marehemu Ole Ntimama akiwa kinara wa kuichafua Tanzania. William ole Ntimama ambaye hadi anakufa nia yake ilikuwa kuwafanya Wamasaai wawe na nchi yao (Maasai Land).
Baadhi ya Wagombea Kenya wa Narok na Kaijado, Laikipia ambayo ni maeneo kame kwa nchi ya Kenya kwa muda mrefu yamekuwa yakinufaika na pori tengefu la Ngorongoro kupitia umoja wajamii ya kimasai.
Jamii hii ya kimasai inayopatikana kwenye bonde la ufa ambayo shughuli yao kubwa ni ufugaji na kilimo kwa kidogo kitakwimu Kenya ndiyo kuna Wamasai wengi zaidi kuliko Tanzania. Ni moja ya kura turufu ya uchaguzi wa Kenya kwa wagombea wa mjimbo haya karibu na Loliondo.
Wamasai wamekuwa na jadi ya kuhama kutafuta malisho. Dai hili ndiyo linawafanya wadai haki ya kulisha mifugo katika hifadhi za Taifa. Jambo ambalo ni kinyume na sharia za hifadhi na mapori tengefu.
Pale Kenya uliwahi kutokea mgogoro wa kuwaondoa Wamasai katika hifadhi ya Maasai Mara kwa ajili ya kulinda mazingira hakuna Masai wa Tanzania aliyeingilia mgogoro huo iweje wa Kenya waingilie Maslahi ya nchi nyingine? Kuna jambo hapo shtuka.
Ukimya huu wa Tanzania hata kwa Dunia ni nchi ambayo iliamua kutochagua upande wowote hata wakati wavita vya sekeseke la vita baridi haya yamekuwa mazoea ya watanzania kutoingilia migogoro ya nchi nyingine.
Majuzi pameibuka mgogoro wa kuhusu kuhamisha makazi ya jamii ya kimasai kutoka katika pori tengefu la Ngorongoro.
Kuhamishwa huko kunatokana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika Eneo Loliondo idadi ya makazi ni kubwa kuliko Ecolojia ya eneo ambayo inakwenda kuharibika.
Kwanini serikali inapendekeza Kilometa za mraba 1,500 ziendelee kutunzwa?
Ni chanzo cha mito sita inayomwaga maji katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Asilimia 48 ya maji yanayoingia Serengeti yanatoka ndani ya Pori Tengefu la Loliondo. Eneo hili ni muhimu kwa ikolojia ya Serengeti ikiwa na vyanzo sita vya maji, mapito na mazalia ya wanyamapori.
Ripoti za mazingira zinaonyesha kuwepo kwa ukame katika maeneo oevu ya vijiji vya Oloipiri, Soitsambu, Maaloni, Ololosokwan, Piyaya, Malambo, Maaloni.
Wagombea Kenya wanavyonufaika na mgogoro wa Loliondo
Loliondo ni mtaji wa Kura uchaguzi mkuu Kenya;
Kaunti za Maa, Turkana, Meru zimekuwa ni viwanja vya mapambano vya makabiliano ya kisiasa kati ya Naibu Rais Ruto na Raila Odinga.
Mgogoro wa Loliondo katika Bonde La Ufa ndiyo limekuwa eneo muhimu kwasasa katika kutafuta kura haya yalikuwa maeneo yenye muamko hafifu kabisa kwenye uchaguzi huu maeneo ya Nakuru na Laikipia.
Maeneo haya yalikuwa na picha hafifu kwa wagombea wote wa pande zote mbili wameamua kutumia nafasi hii ya Loliondo kujipigia debe kaunti hizi ni za wafugaji ambao wana makundi makubwa ya ng’ombe mpakani na ndani ya pori tengefu la Loliondo.
Kiasili ni maeneo yenye ukame mkubwa yaani Narok na Kajiado nchini Kenya. Hili la ukame wamekuwa wakitumia kama kisingizio lakini ukweli ni kuwa Loliondo ndilo shamba lao. Inapotokea rabsha kama hii ni lazima wapagawe wenyewe kwa wenyewe wanakwenda kukosa malisho kwa jailli ya mafugo Yao.
Haikutushangaza kumuona binti wa marehemu Ole Ntimama akiwa kinara wa kuichafua Tanzania. William ole Ntimama ambaye hadi anakufa nia yake ilikuwa kuwafanya Wamasaai wawe na nchi yao (Maasai Land).
Baadhi ya Wagombea Kenya wa Narok na Kaijado, Laikipia ambayo ni maeneo kame kwa nchi ya Kenya kwa muda mrefu yamekuwa yakinufaika na pori tengefu la Ngorongoro kupitia umoja wajamii ya kimasai.
Jamii hii ya kimasai inayopatikana kwenye bonde la ufa ambayo shughuli yao kubwa ni ufugaji na kilimo kwa kidogo kitakwimu Kenya ndiyo kuna Wamasai wengi zaidi kuliko Tanzania. Ni moja ya kura turufu ya uchaguzi wa Kenya kwa wagombea wa mjimbo haya karibu na Loliondo.
Wamasai wamekuwa na jadi ya kuhama kutafuta malisho. Dai hili ndiyo linawafanya wadai haki ya kulisha mifugo katika hifadhi za Taifa. Jambo ambalo ni kinyume na sharia za hifadhi na mapori tengefu.
Pale Kenya uliwahi kutokea mgogoro wa kuwaondoa Wamasai katika hifadhi ya Maasai Mara kwa ajili ya kulinda mazingira hakuna Masai wa Tanzania aliyeingilia mgogoro huo iweje wa Kenya waingilie Maslahi ya nchi nyingine? Kuna jambo hapo shtuka.