Utambulisho wa "Wakili Msomi" kwa Mawakili au wanaSheria

Utambulisho wa "Wakili Msomi" kwa Mawakili au wanaSheria

Neno Wakili Msomi naona linaenea kwa kasi kubwa huwa sielewi lina maanisha nini linapotumika hasa hasa na Watangazaji wetu wa vyombo vya habari! nikijua kabisa huwezi kuwa wakili kama sio mwanasheria ambaye ni msomi.

Na kila fani kwa waliokwenda shule hasa level za chuo kikuu huwa ni wasomi.

Sasa kwanini wanaitwa Wakili Msomi je Kuna wakili asiye msomi au??

Mimi si mwanasheria!!
Hili neno wakili msomi hata mim nilikua nataka kulijua kinaga ubaga maana hasa mtangazaj maulid kitenge hulitumia
 
Teh naona Jf wameamua kutuumbua tunaotumia tecno halafu kwenye uzi wa tecno tunapondea kinyama..... Hiyo ndio tofauti ya usomi sijui umenielewa

"Sent from Tecno whatever "
Eeeh ndo mambo yanavyokwenda kumbe

Sent from my SM-J100H using JamiiForums mobile app
 
Kwa nini wanaitwa Wakili Msomi........
1:zamani kuna watu walikuwa mawakili bila ya kusomea sheria.
2:walikuwa wanafanya kazi ktk maofisi ya mawakili
3:kutokana na miaka mingi kufanya kazi ktk ofisi hizo walipata ujuzi wa uwakili na kuruhusiwa ku practise bila kusomea uwakili/sheria
4:hivyo basi neno learned friend au wakili msomi likaanza kutumika kwa wale tu waliokwenda kusomea fani hiyo.
5:ambao hawakwenda kusomea fani hiyo wakabakia kuitwa Wakili tu na wala siyo Un learned friend
Niko tayari kusahihishwa.
Kwa mfano jeshini Brigadier General...Major General....Luteni General....na General wote wanaitwa General ingawa wsnapishana ki vyeo.


Sent from my HTC Desire 820G PLUS dual sim using JamiiForums mobile app
Kwa maana hiyo kama kuna watu wa taaluma nyingine kama watangazaji, wahasibu n.k. wanaofanya kazi hizo kutokana tu na uzoefu wao bila kusomea hao waitwe watangazaji na wahasibu. Wale waliosomea waitwe watangazaji wasomi na wahasibu wasomi?
 
Neno Wakili Msomi naona linaenea kwa kasi kubwa huwa sielewi lina maanisha nini linapotumika hasa hasa na Watangazaji wetu wa vyombo vya habari! nikijua kabisa huwezi kuwa wakili kama sio mwanasheria ambaye ni msomi.

Na kila fani kwa waliokwenda shule hasa level za chuo kikuu huwa ni wasomi.

Sasa kwanini wanaitwa Wakili Msomi je Kuna wakili asiye msomi au??

Mimi si mwanasheria!!

Ni sawa na katika Wanaume sisi ambapo kiuhalisia Wanaume wote ni ' Wabanduaji ' ila kuna Wanaume ' Wabanduaji ' wa ' Kutukuka '. Ni matumaini yangu kwa mfano huu ' Kuntu ' kabisa nitakuwa nimeshakidhi haja yako ya Uelewa juu ya ulichokiuliza Mkuu.
 
Kwa maana hiyo kama kuna watu wa taaluma nyingine kama watangazaji, wahasibu n.k. wanaofanya kazi hizo kutokana tu na uzoefu wao bila kusomea hao waitwe watangazaji na wahasibu. Wale waliosomea waitwe watangazaji wasomi na wahasibu wasomi?
HAPANA NA WALA SIDHANI HIZO ZAMA WALIFANYA HIVYO.
kama watu wa fani mbali mbali wangeitwa kama ulivyoandika hapo juu enzi hizo...basi na sisi wa leo tungerithi.

Sent from my HTC Desire 820G PLUS dual sim using JamiiForums mobile app
 
Wakili msomi ni neno/kauli isiyo rasmi inayotumiwa na watu kwa utashi binafsi.

Ndio maana kuna watu uhususani wapinzani wanamuona Tundu Lisu ni wakili msomi lakini ukimwambia Olesendeka Lisu ni wakili msomi hawawezi kukuelewa kabisa.
 
Kwahiyo wasomi wapo kwenye sheria tu? Hakuna wahasibu wasomi? Wanauchumi wasomi? Mainjinia wasomi? kwani msomi si mtu aliyesoma? kwanini wakili ndio wawe wasomi? ina maada kada nyingine sio wasomi(hawajasoma)?
Kwa upande wa mainjinia "wasomi" wao upenda kutambulishwa kwa kuanza na neno "Engineer" na kama ni kuandikwa jina upendelea iandikwe kwa kuanza na Eng. kisha jina lake linafuatia Japo kuna baadhi hawapendi sifa hizo.
 
Wakili msomi ni neno/kauli isiyo rasmi inayotumiwa na watu kwa utashi binafsi.

Ndio maana kuna watu uhususani wapinzani wanamuona Tundu Lisu ni wakili msomi lakini ukimwambia Olesendeka Lisu ni wakili msomi hawawezi kukuelewa kabisa.
Isijekuwa waasisi wa matumizi ya maneno hayo ya "wakili msomi" wakawa ni wafuasi au mashabiki wa wabunge wanasheria au mawakili hasa wale wanaokuwa wanatetea kwenye kesi zinazohusu vyama vya upinzani wa kisiasa kutokana na uzito wa hoja zao bungeni au mahakamani?
 
wanasemaga eti ni mawakili ambao huwa wanakua hawapo upande wa serikali wakati utetezi mahakamani.
 
Kwa nini wanaitwa Wakili Msomi........
1:zamani kuna watu walikuwa mawakili bila ya kusomea sheria.
2:walikuwa wanafanya kazi ktk maofisi ya mawakili
3:kutokana na miaka mingi kufanya kazi ktk ofisi hizo walipata ujuzi wa uwakili na kuruhusiwa ku practise bila kusomea uwakili/sheria
4:hivyo basi neno learned friend au wakili msomi likaanza kutumika kwa wale tu waliokwenda kusomea fani hiyo.
5:ambao hawakwenda kusomea fani hiyo wakabakia kuitwa Wakili tu na wala siyo Un learned friend
Niko tayari kusahihishwa.
Kwa mfano jeshini Brigadier General...Major General....Luteni General....na General wote wanaitwa General ingawa wsnapishana ki vyeo.


Sent from my HTC Desire 820G PLUS dual sim using JamiiForums mobile app
aseeh kumbe
 
Kwa upande wa mainjinia "wasomi" wao upenda kutambulishwa kwa kuanza na neno "Engineer" na kama ni kuandikwa jina upendelea iandikwe kwa kuanza na Eng. kisha jina lake linafuatia Japo kuna baadhi hawapendi sifa hizo.
Kwa upande huo,lazima uende intern kwa miaka mitatu na upeleke ripoti Bodi ndipo usajiliwe kama Mhandisi Mahiri/Mjuzi(Professional Engineer)! Hata kama una PhD,Masters Degree lazima ujisalimishe Bodi kwa andiko fulani la ubobez katika Uhandisi ndipo Bodi ya Wahandisi(ERB) ikupe usajili na kukuandikia barua kuwa kwa usajili huu utaanza jina lako kwa kuanzi kifupisho Eng. CHAZA au CHAZA(PEng-ERB)!
Kipekee ni utaratibu mzuri na makini. Ukiona mtu anaanza na jina au kuandika hivyo nilivyotoa mfano,jua Bodi imebariki atumie jina hivyo. Siyo jambo jepesi hata kidogo. Wapo watu wengi hawajapata hiyo sifa ya kuanza na kifupisho Eng....... badala yake wanajulikana kama Grad Eng,ambapo kisheria haruhusiwi kuanza mwanzon,bali ni mwishoni kwamba bado ni Mhandisi Mwanafunzi,haijalishi una level gani ya Elimu,ikiwa Bodi haijaona ripoti yako kuonyesha umeiva,hutaruhusiwa kuanza na acronomy Eng.

Sent from my G630-U10 using JamiiForums mobile app
 
Ni maneno ya heshima tu(courtesy) kati ya pande mbili za watu ambao kadhia(kesi) inawafanya kuwa kama maadui(adversaries).
Kesi katika mfumo wa 'common law' zinazalisha povu jingi ambalo namna moja ya kulizuia ni matumizi ya lugha ya kiungwana kama mheshimiwa hakimu, wakili msomi(learned brother, learned attorney) n.k
Common law inatumiwa na nchi za Uingereza na yaliyokuwa makoloni yake na kote huko kuna huo msemo. Hivyo maneno hayo hayana uhusiano na attitude za mawakili wa Tanzania pekee au kuwa wao ndio wasomi pekee hapa nchini.
Ila ni kweli pia kuwa mawakili kwenye sheria(attorneys at law)
wana sifa maalum za kisomi zinazowatofafautisha na wadau wengine kwenye daawa.
 
Back
Top Bottom