Utambulisho wa "Wakili Msomi" kwa Mawakili au wanaSheria

Utambulisho wa "Wakili Msomi" kwa Mawakili au wanaSheria

Kwa upande huo,lazima uende intern kwa miaka mitatu na upeleke ripoti Bodi ndipo usajiliwe kama Mhandisi Mahiri/Mjuzi(Professional Engineer)! Hata kama una PhD,Masters Degree lazima ujisalimishe Bodi kwa andiko fulani la ubobez katika Uhandisi ndipo Bodi ya Wahandisi(ERB) ikupe usajili na kukuandikia barua kuwa kwa usajili huu utaanza jina lako kwa kuanzi kifupisho Eng. CHAZA au CHAZA(PEng-ERB)!
Kipekee ni utaratibu mzuri na makini. Ukiona mtu anaanza na jina au kuandika hivyo nilivyotoa mfano,jua Bodi imebariki atumie jina hivyo. Siyo jambo jepesi hata kidogo. Wapo watu wengi hawajapata hiyo sifa ya kuanza na kifupisho Eng....... badala yake wanajulikana kama Grad Eng,ambapo kisheria haruhusiwi kuanza mwanzon,bali ni mwishoni kwamba bado ni Mhandisi Mwanafunzi,haijalishi una level gani ya Elimu,ikiwa Bodi haijaona ripoti yako kuonyesha umeiva,hutaruhusiwa kuanza na acronomy Eng.

Sent from my G630-U10 using JamiiForums mobile app
Shukrani kwa ufafanuzi huo ....na ndiyo maana wanaomaliza uhandisi ni wengi sana lakini wanaanza na jina la Injinia X ni wachache sana
 
!
!
Hivi ikitokea ndani ya week 6 umejichanganya kusema bila baba mkwe na yeye akakosa kuonekana mahabusu kujileta mbele ndio mvua ilipoanza kunyesha
Sio lazima uelewe kila kitu
 
Wakili msomi ni neno/kauli isiyo rasmi inayotumiwa na watu kwa utashi binafsi.

Ndio maana kuna watu uhususani wapinzani wanamuona Tundu Lisu ni wakili msomi lakini ukimwambia Olesendeka Lisu ni wakili msomi hawawezi kukuelewa kabisa.

Hujielewi wewe,Ole sendeka mwanaye ni wakili na kasoma makumira,Kaja hapa tumemwapisha na anafanya kazi ya uwakili.

Hili neno ni rasmi tangu enzi na enzi,Huwezi acha tambua mchango wa wanasheria,Hawa watu wamesoma na kila sikubya mausha yao wanasoma.

Advocates wanajua kila nyanja,Hesabu,Mekanika,siasa,Lugha,Sanaa na etc ndio maana wanaitwa mawakili wasomi.
 
Nijuavyo tangu zama za kale ya ustaarabu huko Ulaya na Marekani Wanasheria huitwa kwa Utani THE LEARNED BROTHERS/SISTERS. Hii imechangiwa pia na nguvu na mbwembwe anazokuwa nazo Hakimu au Wakili pale mahakamani.

Dhana hii ya learned ndiyo miaka ya karibuni imetoholewa na kuwa WAKILI MSOMI.
 
Anataka kuongeza ufahamu, je ni kosa? #mwifwa#

Sent from my TECNO-W3LTE using JamiiForums mobile app
 
Kama kitu huelewi ni bora ukanyamaza....

acheni kuichukulia law simple ndio maana watu wanaenda shule miaka minne... siyo kama ualimu ule... lazima ujue logic na argumentation skills....

NDIO MAANA KWA SEHEMU KUBWA LAW HAINA WATU WABABAISHAJI HAPA TZ KAMA ZILIVYO FANI ZINGINE... WALIO WENGI WANAZITENDEA HAKI TAALUMA ZAO
 
Niliwahi kusoma mahala, hii sio Tanzania tu, ni Dunia nzima kwa wanasheria kuitwa au kujiita wasomi au Learned brothers/sisters.

1. Mawakili wanapokua mahakami na wakawa wanabishana kwa hoja, wakili mmoja haweza kumpinga mwenzake kwa kumuita mjinga au mpumbavu, hapana anatakiwa hata kama hoja ya wakili wa upande wa pili ni ya kijinga, anatakiwa kusema wakili msomi mwenzangu hapo napingana na wewe hivi na hivi na sio kutumia maneno mabaya au majina mabaya katika kupinga hoja. Yani hutakiwi kumuonyesha mtu ni mjinga moja kwa moja, unampaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Kwamba kama mtu ni mjinga usimwambie wewe ni mjinga, mwambie tu brother uwezo wako wa kukubali mambo unashuka ndugu yangu(your level of appriciating things is diminishing)

2. Mawakili au wanasheria wanafundishwa kumshitaki au kumtetea yoyote kutoka katika taaluma yoyote ile, iwe unatoka uhasibu, sheria, uchumi, uinjinia, sayansi, udaktari, wizi, ujambazi, ulawiti, ubakaji, urubani, fani zote.

Hivyo wanajiona kua wanajua mambo karibu yote kama sio yote kwa ujumla yaliyo chini ya jua. Ndio maana huwezi kupeleka kesi mahakamani ya udaktari hakimu akakuambia kua bwana sisi sio madaktari hivyo hiyo kesi haitasikilizwa, hapana , wataipokea na kuisikiliza hadi mwisho na hukumu itatolewa utafikiri wao wanajua udaktari.

Kwa mantiki hiyo wanasheria toka zamani wamekua wakiona fani nyingine kama fani za kiwango cha chini na kijiona wao ni bora na ni wasomi kuliko wengine.
Hata madaktari wanatibu mtu yeyote yule uwe engineer, lawyer, mwizi, Rais, mbakaji nk kwanini hawaitwi Daktari msomi
 
Ni majigambo tu ya kuvutia biashara

Wakili Ni mfanyabiashara, na bidhaa yake Ni utetezi wa kisheria

Maisha yamekua magumu, inabidi nao waweke billboard

"Wakili msomi" is one of their marketing strategy
 
Utaamini hili.......mhadhiri wa sheria wa chuo XYZ ambaye alinifundisha sheria tuliingia naye Shule ya Sheria ili tupate uhalali wa kuwa Wakili.Tulifanya mafunzo mwaka mmoja na tulifanya mitihani mimi mwanafunzi wake nikapita yeye mwalimu wangu akakamatwa...yaani akafeli.Sasa kisheria mimi ni senior kwenye BAR dhidi yake.
 
Hata madaktari wanatibu mtu yeyote yule uwe engineer, lawyer, mwizi, Rais, mbakaji nk kwanini hawaitwi Daktari msomi
Elewa mantiki, daktari anatibu ugonjwa, hatibu taaluma ya mtu. Kwani kuna ugonjwa wa uhasibu au ugonjwa wa uinjinia? Lakini kuna matatizo ya uhasibu, uinjinia, udaktari au wizi nk, haya matatizo yote yanatatuliwa na wanasheria.
 
Elewa mantiki, daktari anatibu ugonjwa, hatibu taaluma ya mtu. Kwani kuna ugonjwa wa uhasibu au ugonjwa wa uinjinia? Lakini kuna matatizo ya uhasibu, uinjinia, udaktari au wizi nk, haya matatizo yote yanatatuliwa na wanasheria.
Taaluma zote zinaingiliana hakuna taaluma muhimu kuliko nyingine. Basi walimu ambao ndio chimbuko la hao wote ilibidi waitwe walimu wasomi
 
Pamoja na Maelezo yako mazuri tu lakini si kweli kuwa fani ya sheria ndiyo kujua Fani zingine si kweli Hata kidogo.

Mwanasheria hawezi kujua medicine, accounts, engineering n.k.

Sana sana yeye ana base kwenye incident in relation to laws basi ili kapata u kweli wa jambo au tukio.
Mkuu hebu rudia kusoma maelezo yangu utanielewa. Mwanasheria hajui uhasibu, madawa, sijui makitu gani, lakini ukipeleka tatizo lolote linalotoka katika taaluma yoyote wanasheria wanashughulika nalo
 
Neno Wakili Msomi naona linaenea kwa kasi kubwa huwa sielewi lina maanisha nini linapotumika hasa hasa na Watangazaji wetu wa vyombo vya habari! nikijua kabisa huwezi kuwa wakili kama sio mwanasheria ambaye ni msomi.

Na kila fani kwa waliokwenda shule hasa level za chuo kikuu huwa ni wasomi.

Sasa kwanini wanaitwa Wakili Msomi je Kuna wakili asiye msomi au??

Mimi si mwanasheria!!

Wakilo msomi wanajiita walioenda school of law,....hawa wenye degree peke yake huwa hawaitwi ivooo,ni maneno mpito kama walimu wa kk
 
Taaluma zote zinaingiliana hakuna taaluma muhimu kuliko nyingine. Basi walimu ambao ndio chimbuko la hao wote ilibidi waitwe walimu wasomi
Mkuu,
Kwanza mimi sio mwanasheria. Nimetoa tu ufahamu wangu kuhusu wanasheria kujiita wasomi.

Haya mambo wote tumeyakuta hapa, walioanzisha haya mambo nadhani ni hao waliotengeneza misingi ya kisheria.

Mkuu wewe kutokuitwa msomi kwenye taaluma yako unaona umedhalilika?
 
Mkuu hebu rudia kusoma maelezo yangu utanielewa. Mwanasheria hajui uhasibu, madawa, sijui makitu gani, lakini ukipeleka tatizo lolote linalotoka katika taaluma yoyote wanasheria wanashughulika nalo
This is a big lie...kwahiyo nikuletee tatizo la bridge failure wewe kama mwanasheria utanipa jibu? Huko ni kujikweza bila sababu za Msingi.

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu,
Kwanza mimi sio mwanasheria. Nimetoa tu ufahamu wangu kuhusu wanasheria kujiita wasomi.

Haya mambo wote tumeyakuta hapa, walioanzisha haya mambo nadhani ni hao waliotengeneza misingi ya kisheria.

Mkuu wewe kutokuitwa msomi kwenye taaluma yako unaona umedhalilika?
Hapana sijadhalilika kwangu ingekua kejeli kuitwa hivyo.
 
Back
Top Bottom