Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Kwa taarifa yako mafuta ya upako yanayotumika muda huu, ndiyo yale yale waliyokuwa wanapakwa wfalme wa zamani kama vile akina Daudi na akina Sauli

Kipindi hicho walikuwa ni makuhani pekee waliokuwa wanaweza kuyatamkia baraka, ila baada ya Yesu kufa msalabani hali imebadilika na kuwafanya watu wote waliookoka kuwa Makuhani

Kwa taarifa yako zaidi ni kuwa watu waliokanayagana kwenye tamasha la la kukanyaga mafuta la Mwamposa na kupelekea wengine kufariki dunia, zilikuwa ni hujuma zilizofanyw na wachawi, lengo ilikuwa ni ili azuiwe kuwa anatengeneza mafuta ya upako

Huelwei chochote, mimi ninapoongea usinibishe, nina ushahidi kutoka pande zote, duniani na Mbinguni

Sasa inawezekanaje mtu wa mungu ahujumiwe na wachawi wakati unaupako zote
 
watu weusi wengi hawana uwezo wa kuchambua mambo na kuhoji. Wanapigwa wengi sana.
Ni kweli watu wengi hawana uwezo wa kuchambua mambo na kuhoji. Kwa sababu hiyo sisi tuliojaliwa uwezo wa kuchambua mambo, tusikae kimya, tuwasaidie wenzetu.
 
Dini ni biashara ,ukiona Ukristo umefanywa dini basi Kuna biashara ndani yake

Ukristo ni wokovu wa MUNGU kumtafuta mwanadamu aliyepotea dhambini

Dini ni njia , mishemishe, mbilingembilinge,harakati ,utapeli wa mwanadamu kutafuta pesa na ku manipulate watu kupitia jina la Mungu
Unatoa wapi hizo definition za dini?
 
asante kunitag
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.
Mkuu Achia Huru, Setfree , haya usemayo ni kweli
Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa.
ni kweli
Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.
ni kweli sio mafuta na chumvi tu,
bali maji,mafuta,chumvi na mafusho,moto,moshi,ubani, majivu, udongo, etc ni vifaa vya kiroho,vinapokuwa annointed!
Wakristu Wakatoliki,wanatumia maji na mafuta kubatiza na kwenye kutoa sacramenti zote,Yale maji ya baraka,yamekuwa annointed na chumvi,tunatumia mafuta kwenye sacrament ya upako mtakatifu,tunatimia majivu siku ya Jumatano ya majivu,tunatimia udongo kwenye mazishi na tunatumia mafusho ya ubani kwenye ibada za sikukuu zote。

Matumizi ya vitu hivyo vyote ni natural elements,sio utapeli,they have the induction powers kufungulia imani yako,kufunguka na kufanya miujiza ya uponyaji na mafanikio。Kinachoponya sio maji,mafuta na chumvi, ni imani oliyo ndani yako。Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo? na "Will Powers!", "Faith Healing!"-Nguvu za Kufanya Miujiza ya Uponyaji kwa Imani. Kila Mtu Anazo!
Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.
ni kweli
LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.
true, ni kweli!huo ni utapeli!。
Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.
ni kweli
Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.
ni kweli。
Kwa upande wangu, nilipandisha mabandiko haya kujaribu kusaidia
P
 
Unatoa wapi hizo definition za dini?
Kwani hujionei,?

Dini utaambiwa ni njia ya mwanadamu kumtafuta Mungu ,but in reality Wewe ukipotea huwez kumtafuta Mungu bila yeye kwanza kukutafuta

Dini ndio hizo mambo unazoona za kina mwamposa ,kuuza maji, mafuta, vitisho vingi, au kwenye uislamu, dini imejikita kwenye matendo hasa ya mwili



REJEA Yesu na mafarisayo ,ugomvi mkubwa wale walikuwa na dini sana , ndio maana Yesu aliwaambia Watoza ushauru na makahaba wanawatangulia kuingia mbinguni ,

REJEA yule mwizi pale msalabani alifanya jitihada zipi za dini ?

Aliokolewa kiulaini


Kwahiyo hakikisha unatafuta Wokovu ambao unapatikana kwa njia ya kumuamini Yesu kristo, dini zimejaa utapeli mwingi sana ,humo utatishwa Hadi uliwe nauli utembee km 10,
 
Hana jibu, mtu wa mungu anazidiwaje na shetani au wachawi?
Hujaelewa.

Kilichotumika siyo uchawi, zilitumika hujuma kwa njia ya kawaida ila walioandaa mpango huo walikuwa ni wachawi.

Kwani tuseme wewe hapo ulipo ukichukua kisu halafu ukaenda ukamvizia mtumishi wa Mungu na kumburuza nacho, hakiwezi kumkata kisa ni mtumishi wa Mungu?
 
asante kunitag

ni kweli

ni kweli

ni kweli sio mafuta na chumvi tu,
bali maji,mafuta,chumvi na mafusho,moto,moshi,ubani, majivu, udongo, etc ni vifaa vya kiroho,vinapokuwa annointed!
Wakristu Wakatoliki,wanatumia maji na mafuta kubatiza na kwenye kutoa sacramenti zote,Yale maji ya baraka,yamekuwa annointed na chumvi,tunatumia mafuta kwenye sacrament ya upako mtakatifu,tunatimia majivu siku ya Jumatano ya majivu,tunatimia udongo kwenye mazishi na tunatumia mafusho ya ubani kwenye ibada za sikukuu zote。

Matumizi ya vitu hivyo vyote ni natural elements,sio utapeli,they have the induction powers kufungulia imani yako,kufunguka na kufanya miujiza ya uponyaji na mafanikio。Kinachoponya sio maji,mafuta na chumvi, ni imani oliyo ndani yako。Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo? na "Will Powers!", "Faith Healing!"-Nguvu za Kufanya Miujiza ya Uponyaji kwa Imani. Kila Mtu Anazo!

ni kweli

true, ni kweli!huo ni utapeli!。

ni kweli

ni kweli。
P
We Paschal hujamwelewa vizuri aliyeleta uzi huu. Yeye lengo lake ni ku-dscourage watu wasivitumie vitu hivi kwa sabau anajua nguvu iliyomo ndani yake. Kwa hiyo anajitahidi kuwarubuni watu humu ili watakapokuwa wameacha kuvitumia, aweze kupata ahueni

Yesu alsiema kuwa wanaomwamini watafanya yote aliyowahi kuyafanya, na pia zaidi ya hayo kwa maana kuwa Yesu aliwapatia waumini uwezo wa kufanya hata yale ambayo yeye hakuwahi kuyafanya

Chukulia kwa mfano, muumini anayeweza kuomba halafu mtu aliyekufa akafufuka, anashindwaje kubariki maji au chumvi kwa ajli ya matumizi ya mtu mwingine ambaye imani yake ni ndogo?

Hii nchi sasa hvi tumeshavamiwa na mtandao wa wachawi inabidi tuwe makini sana, ila mbele ya Mungu watanyoosha mikono tu muda siyo mrefu; ni hakika KWA JINA LA YESU!
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
View attachment 3261034View attachment 3261076
Nasemaga imani ikikuzidi ni utumwa wanabisha.
 
Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Sio manabii wa Uongo huo ni mchezo pandikizi la Wanasiasa fulani fulani wa Chama fulani kuwaweka watu km hao ili kuwapumbaza watu wasiamke na kudai haki zao, wote unaowaona wanafanya vile kwa kupitia mkono wa Wanasiasa kuanzia Kimara Temboni mpaka Kawe kote ni pandikizi la Wanasiasa
 
Hahaa, umenivunja mbavu: "kama hajachezea bakora..."

Hata Yesu alipindua meza za waliokuwa wakifanya biashara hekaluni. Ni wakati mwafaka sasa wa kupindua meza za hao wauza viambata vya upako.
Kuna Jamaa Yeye anasema ni Vifaa vya Kiroho pale Morogoro Road.
Mungu atusamehe sana
 
Sio manabii wa Uongo huo ni mchezo pandikizi la Wanasiasa fulani fulani wa Chama fulani kuwaweka watu km hao ili kuwapumbaza watu wasiamke na kudai haki zao, wote unaowaona wanafanya vile kwa kupitia mkono wa Wanasiasa kuanzia Kimara Temboni mpaka Kawe kote ni pandikizi la Wanasiasa
Leta ushahidi, mkuu
 
Wakristu Wakatoliki wanatumia maji na mafuta kubatiza... tunatumia majivu siku ya Jumatano ya majivu... Matumizi ya vitu hivyo vyote ni natural elements,sio utapeli,they have the induction powers kufungulia imani yako
Mkuu, Pascal Mayalla , wewe ni Great Thinker na Biblia unaijua. Kwakuwa Biblia ndio mwongozo wa maisha ya Wakristu(Zaburi 119:105; 2 Timotheo 3:16-17), naomba unitajie mistari ya Biblia inayoagiza hayo uliyoyasema yafanyike. In other words, wanaofanya hayo, wanafanya kwa kuegemea Maandiko yapi ya Biblia.

Nimekuuliza hivyo kwa sababu Yesu alisema tukiwa na chembe ndogo tu ya imani tunaweza kuuambia mkuyu huu ng'oka ukaote baharini(Luka 17:6). So, kwanini tuhangaike tena kutafuta majivu na kuharibu mazingira?

Vile vile Biblia inasema imani huja kwa kusikia ujumbe unaotokana na Neno la Kristo(Rum 10:17), sio kwa kutumia natural elements.
 
Poleni. Ila sasa mmeijua kweli, iwaweke huru.
Ushauri wako ni upi maana utapeli umeenea hata kwa makanisa yasiyouza hivyo vitu sadaka zimekuwa nyingi mno mtu unakamuliwa mpaka Senti ya mwisho uliyo nayo je tukasali wapi sasa maana tunampenda Mungu
 
Mitume na manabii feki wameua soko la wazee wa tiba mbadala waliotuuzia juice za michicha na matembele kwa hela ndefu
 
Back
Top Bottom