Utaratibu wa kuishi na ndugu baada ya ndoa unafaa uwe vipi?

Utaratibu wa kuishi na ndugu baada ya ndoa unafaa uwe vipi?

Mkuiu nilifanya hivyo mimi hapa nyumbani kuweka bustani nikaweka na kuku hawa sasso , mbona nilipata hasara sababu wanaona uvivu kulisha chakula badi wanafanya kujaza tu kwenye vyombo bustan haimwagiliwi na mpira nimewanunulia kila wiki wanapanda upya mboga zikiota zinakauka kiufupi ni watu wavivu mimi sio mkabila ila hawa ndugu wanatokea kanda ya kati hapo sisemi wote kanda hiyo wapo hivyo.
🤣🤣🤣Ukoo una laana hao
 
Nakupa mbinu moja ya kibaharia

Hao ndugu zake wa kike tongoza wote atakaekubali pita nae na watakaokataa lazima watamwambia mke wako na mkeo akikuuliza maambie tu wanakaaga sebulen kihasarahasara....lazima awapige marufuku kuja kwake


CASE CLOSED
 
Wewe ni tatizo unajifanya unapesa, unatoa nauli kwa watu wazima !! Watu wavivu hawaingii nyumba yenye njaa!! endelea watakuja na begi next time
 
Ndugu zako wao huwa hawaji kwako?,familia zetu za kimaskini ni jau,wengine walikaa kwa watu na kusaidiwa hadi hapo walipofika!,ndugu kutembeleana ndiyo uungwana ila kuweka kambi ndiyo changamoto.
 
Ambao hawakumuelewa Dinazarde kwenye uzi wake,,,,Basi hiki ndicho Hasa alichokuwa anakizungumza...

Na nawaomba mtumie kisa cha Mleta uzi kama mfano wa kufundishia

Nakuambia tabu sana
 
Kaka yangu alifanya hivi...
Ndugu wakija nyumban kwake kukaa basi ni ndugu wenye faida haijalishi anatoka upande gani hakuwahi kutaka ujinga kabisa na anaishi vizuri mpaka leo kikubwa msimamo tu.

imagine
Ana kila kitu nyumban kaz nzuri, mshahara mnono alichofanya alianza kilimo cha mpunga bondeni kama mnavyojua kaz za mpunga haziishi mwezi wowote ni kazkaz tu kwahyo ndugu wakienda kwake anawasombelea wote kwenda shamban kumsaidia kaz huko maana yye yuko bize ni kutoa maelekezo tu. Walikuwa wakienda kwake ni trip moja tu hawarud tena wanalalamika tu afu maisha frsh tu
Wazo zuri sana
 
Kiongozi nikupe tu ushauri ,ndgu hawabebiki na huwa wanamthamini wakati mtu ana kitu ,
Mtakupa historia fupi ya mzee wangu (binafsi nimepata funzo ) kipindi mzee ana uwezo na mali zake ,nyumbani watu hawakauki ,ndgu walijaa kibao mpaka sisi watoto tukawa tunaminyika au kupunjika maswala ya msosi kwa ajili yao ,maana alikuwepo ma mdogo akijipakulia basi alikuwa anajijazia yeye na sisi kutupunja chakula ,hiki kitu huwa sikisahau mapaka utu uzima huu,Baadae mzee alikuja filisika sana na ndgu hawaji hata kusalimia ,jambo ambalo lilikuwa likimuumiza mama na alikuwa akinilalamikia ,wanavyonyanyapaa ndgu zake kisa hana kitu ,kama mtoto ilikuwa inaniumiza sana ,ni kaapa ntatafuta maisha kwa hali na mali ,
Si haba kwa sasa nnakijiuwezo ,kiasi na nimekuwa na msimamo ,familia yangu kwanza (mke watoto baba na mama ) hao wengine wanasubiri ,Habari mtu kaja kwangu kutembea bila taarifa huwa sitoi nauli hata kama ninayo maana ukiwazoesha huwa wanajenga tabia ,Na ukiwaonyesha kwamba ww unazo watakufanya chuma ulete ,siku huna kitu watakukimbia ,
Nimewekeza nguvu na akili katika kujijenga mm kwanza bila kumtanguliza mtu mwingine na hata nnachopata juwa najitahidi kuwaneemeshe familia yangu na wazazi wangu ,Hao wengine nasaidia panapouhitaji ,
Pia nimeweka msimamu kuwa sibebi mzigo wa mtu (kwa kulea mtoto wa mtu) mimi mwenyewe nimejibana niwe nawatoto wachache ili kuwapa malezi bora ,Kila mtu abebe msalaba wake ,
Usiposimama imara na kuwajengea watoto wako msingi imara kesho na kesho kutwa hao hao ndgu watakuja simanga watoto wako na kuwaambia baba ako alikuwa na pesa ila akachezea ,watasahau kwamba ulikuwa unajitoa kwao na wamesababisha kushinda kuwatimizia watoto wako kwa kuwajengea misingi mizuri
 
Hapo mbinu Ni rahisi tu kila akija ndugu yeyote wa mkeo wewe omba mzigo tu bila kujali jinsia hautaona kiumbe hapo tena kinakuja kuleta mazoea
 
Sidhani! Labda ungesema Wajaluo,Wagogo,Wasambaa ningekuelewa! Lakini changamoto ni kuoa ukoo maskini.
Mbona familia yetu masikin na hatuna tabia yakwenda majumbani Kwa watu tokea wadogo tulilizika na maisha ya home kipatikane chakula kisipatikane hatukuwai kuwaza kwenda kuishi Kwa ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hili wazo nilikuwa nalo na nilimuambia wife nitapanga chumba sababu nyumba imekuwa ghetto kuna madogo ndugu zake walikuwa wanasubiri matokeo ya chuo basi nyumba ni mziki kwa kwenda mbele mara wameunganisha tv na simu. mara wamegawana zase za kuhifadhia miwani wengine wamechukua notebook za kazini ambazo hazijatumika yaani ni vurugu tupu, hili wazo linafanyiwa kazi.
Mkuu vumilia mbona kawaida au wewe hujawai kupitia hayo Maisha? Tatizo umri husiwachukie wapo kwenye mapito

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za siku nyingi watu wa Mungu.

Hivi ni utaratibu gani unafaa kufuatwa katika kuchagua ndugu wa kuishi nao baada ya ndoa. Nakumbuka mwanzo kabisa kipindi namuoa mke wangu nilimjulisha kuwa napenda sana ndugu ila kuishi na ndugu ni mtihani kama mtu ana uhitaji na tuna uwezo wa kumsaidia bora tumsaidie huko huko aliko kukiwa na ulazima sana ndipo ataishi kwetu.

Bahati mbaya huyu mwenzangu na ndugu zake wamefanya nyumba yangu kijiwe ndugu zake wote wapo hapa hapa mjini sasa imekuwa anakuja huyu anakaa wiki anaondoka wanapokezana , likizo watoto zao wanawaleta kwangu na wana vurugu kweli ile likizo ya mwaka mpya walinivunjia side mirror ya gari ikabidi niwafukuze manake walikuwa wakiaanza kukimbizana wanapita mpaka juu ya makochi ilibaki kidogo wakanyage kompyuta niliwafukuza siku hiyo hiyo.

Tatizo la pili kuna ndugu zake hawa watu wazima wakike ambao ni dadazake ni wakubwa kiasi mmoja binti yake ndiyo mwenye watoto niliowafukuza, hawa wanakaa tu nyumbani hawafanyi chochote ni kuangalia tu tamthiliya mpaka kurudi nyumbani sasa naona kero mimi na wife hatujajaliwa watoto sasa hapo nyumbani kuna familia ya watu 4 na wote wanatokea hapo mabibo yaani mimi ndio nimekuwa kama mgeni kwenye familia.

Nikimuambia hawa watu kwanini wasirudi kwenu kwenye nyumba ya familia wakae sisi tutakaa nao mpaka lini anasema soon wataondoka toka mwezi wa pili anasema hivyo soon wataondoka, karibuni mama anataka kuja kwenye matibabu MOI ila kagoma kufikia kwangu hawezi lala kitanda kimoja na mtu mwingine anashida na mifupa.

hapo bado kuna ndugu zake wanakuja tu wikend wakijisikia na wakiondoka hawana nauli wanakuomba tena shemeji nauli hasa namuuliza hawa nao wanakuja kila wikend kufanya nini, anasema kama sitaki ndugu zake waje atawaambia ila tatizo sio kuja tatizo hata nauli hawana ukiwapa ndogo wanakuimbia kuna sehemu ya kupanda bodaboda.

Ajabu wao wenyewe kwa wenyewe hawatembeleani ni kama vile wanaamua kunimalizia pesa hivi. Nipeni busara kudeal na hawa watu nahisi kuanza kukata mahitaji.
Hali ilikuwa hivi kwetu wakati tunakaa Singida mjini. Ukoo mzima wa mama wakitoka Iramba, kwetu ndio palikuwa guest house yao.
Ndio maana nilipoamua kujenga Dar, niliamua kujenga nje ya mji ili ndugu wajifukuze wenyewe kutokana na umbali. 😀😀😀
 
Mkuiu nilifanya hivyo mimi hapa nyumbani kuweka bustani nikaweka na kuku hawa sasso , mbona nilipata hasara sababu wanaona uvivu kulisha chakula badi wanafanya kujaza tu kwenye vyombo bustan haimwagiliwi na mpira nimewanunulia kila wiki wanapanda upya mboga zikiota zinakauka kiufupi ni watu wavivu mimi sio mkabila ila hawa ndugu wanatokea kanda ya kati hapo sisemi wote kanda hiyo wapo hivyo.
Tatizo hukuweka mkazo mkuu brother alikuwa mbogo sio mchezo
 
Mkuu kama huna mtoto hapo Anza kufanya hivi ,acha kununua vyakula hapo nyumbani ,acha kulipia king'amuzi ,wakija usiwe na stori nao kabisa wapite kama huwaoni ,wakija nyumbani unaawapotezea na kuendelea na Mambo mengine ,muoneshe mkeo kwa ukali kuwa hutaki Kijiji cha watu hapo kwako ,,,,,badae wenyewe wataondoka tu ....
Na kwakuongezea kama amepanga atafute nyumba ndogo tuuu yenye chumba seble choo na jiko baaas hao wageni wakose pakulala
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji119][emoji119] family za kiswahili hizo , ndio shida ya kuambatana na watu wasiojua mipaka Yao Ktk Maisha
 
Back
Top Bottom