Utendaji kazi uliotukuka wa Rais Samia umedhoofisha upinzani Tanzania

Utendaji kazi uliotukuka wa Rais Samia umedhoofisha upinzani Tanzania

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Kuna kipindi fulani ilikuwa ukisikia kuwa kesho katibu mkuu wa Chadema Mh. Dr Slaa atakuwa na mazungumzo muda fulani, ni kama nchi ilikuwa inasimama. Vyombo vyote vya habari vilikuwa vinafika hata kabla ya muda husika, kila mtanzania alikuwa anatega sikio kusikia nini kitakacho zungumzwa.

Kila Kona ya nchi ilikuwa inakuwa ni gumzo lisilo pimika, ilikuwa ni kana kwamba Rais wa marekani anakuja kutolea tamko Tanzania juu ya kuuwawa kwa Osama bin laden. Watu walikuwa hawatulii walipokaa, wasio na TV walikwenda hata vibanda umiza kuchungulia ilimradi tu asijesubili kusimuliwa.

Hoja nzito nzito zilishushwa huku zikinogeshwa na vijana wa Redbriged waliokuwa wanakaa nyuma ya viongozi wao. Sisi vijana wa CCM wakati mwingine tulikuwa hatuelewi tutajibu nini juu ya nondo zinazokuwa zimeshushwa, hivyo tulibaki tukirusha rusha miguu wakati tukisubili akina Mh. Nape walete silaha za hoja kujibu vijana wenzetu wa upinzani huku site.

Hata mikutano tu ilikuwa ukisikia Dr slaa anakuja Mbeya mjini kwenye uwanja wa Rwanda Nzovwe maarufu kama CCM, jiji lote lilikuwa linasimama, shughuli zote zilikuwa zinasimama. Mimi nilikuwa nikitoka shule Sekondari ya Ivumwe, nilikuwa hata sipiki chakula zaidi ya kwenda mkutanoni ili nijuwe wanasema nini hawa watani zangu.

Alikuwa akija anapokelewa kama Rais wa nchi, shangwe kubwa hata uwe mwanjelwa unasikia. Ilikuwa ni Kama nchi inakwenda kupinduliwa kwa maandano. Ilikuwa ni kama wananchi wote wapo upinzani japo wa CCM tuliogopa hata kuvaa sare kuepuka kupigwa. Ilikuwa ukisikia "PIPOZ" watu walikuwa wanaitikia utazan wanataka kulia jinsi walivyo na hasira!

CCM fundiii bwana, CCM chama kubwa, CCM Ina mbinu hadi za reserve, CCM ndio chama kiongozi, CCM ndio mkombozi wa nchi za kusini mwa Afrika, CCM ndio chama Cha Hayati baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Unajua nini kilifanyika upinzani wakapewa Mh. nguli wa mikakati ya kisiasa Mh. Edward Lowasa waliyemtukana kwa miaka takribani nane kuwa ni fisadi? Ilikuwa ni kwa ajili ya kumsafisha na kumpaka mafuta hadi apendeze.

Hapo ndioo tukaanza kuona mvurugano ndani kwa ndani. Mara Dr slaa akatimka kwa kusema hawezi kazi hiyo, mara Mnyika akazira, mara sijui Mh Sanaa havai makombati yao, Mara huku Askofu Gwajima akasema alikuwa mshenga, mara sijuw nini yaani ikawa furu michanganyo.

Baada ya hapo akaingia Dr John Pombe Magufuli kama Rais wa nchi. Aliwakaba hadi vivuli vyao wakawa wanavikimbia. Hapo ndio ikajulikana pia nani ni mpinzani na nani ni mpinzani njaa. watu waliunga mkono juhudi kama hawana akili nzuri.

Baada ya hapo ndio akaja mama yetu kipenzi cha watanzania, mzalendo wa kweli, mwenye maneno ya upendo na faraja, mwenye tbasamu la upendo na ukarimu, aliyejaa hekima na busara katika kifua chake, mwenye moyo wa huruma na upendo akaanza kusuka serikali yake hatua kwa hatua. Watu wakaanza kushituka maana hawakutegemea jinsi anavyoendesha nchi kwa weledi na utumishi uliotukuka.

Hapa ndio ikawa mwisho na hitimisho la upinzani hapa nchini, kwa sasa hakuna mwananchi atakuelewa juu ya upinzani. Kwa sasa wananchi wapo na mama, kwa sababu mama yetu amewafanya watu wawe na iman naye. Anaendesha nchi kwa uwazi na kwa kuzingatia misingi ya sheria na utawala bora.

Utawaambia nini wakulima juu ya mama Samia wakati wanaona juhudi za mama katika kilimo hasa baada ya kutoa ruzuku kwenye Wizara ya Kilimo takilibani billion mia hamsini na kumkabidhi kijana wake Mh. Hussein Bashe ili asimamie? Utawaambia nini wananchi wakati wanaona mama sasa ameweka elimu bure hadi kidato cha sita? Utawambia nini watu wakati wanaona vyumba vya madarasa, vituo vya afya, zahanati na maji vikisambazwa kila kona ya nchi?

Hakuna anayeweza kukuelewa ukimsema vibaya mama yetu kipenzi mama Samia Suluhu Hassani kwa utendaji wake bora wa kazi. Huku Songwe ni mama anaupiga mwingi na wala huwaambii na wakakuelewa habari za upinzani.

Nakupenda CCM na nitaendelea kuwa mwana CCM. Hapa ni Tanzania na siyo Kenya, hata tuwape upinzani wasimamie uchaguzi bado CCM itashinda tu. CCM ndio tumaini la watanzania katika kuwaletea maendeleo. Upinzaani asante sana kwa kumuunga mkono mama yetu na msisite kushirikiana zaidi na zaidi na mama yetu kuijenga nchi yetu maana upinzani siyo uadui.

Kazi iendelee, sote tumuunge mkono Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassani katika kuijenga Tanzania mpya.​
 
Mijizi ya kura bana, yaani umejiunga hapa jukwaani mwezi uliopita, ili kuleta propaganda ukidhani ndio utaokota watu vibaya sana.
Hapana mkuu kwani Sera za upinzani kwa Sasa Ni zipi zinazogusa maisha yao ya kila siku, unajuwa mwananchi atakuunga mkono na hata kujitolea muda wake atakapoona ajenda ulizobeba zinamgusa,

Lakini mwananchi akikosa sababu ya kuweza kumshawishi hawezi kukuunga mkono zaidi ya Kuendelea na Yule aliyopo, kwa Sasa CCM Ni tumaini la watanzania na bado Wana Imani nayo na ndio maaana wanaendelea kuiunga mkono

Si umeona hata uwanja wa mkapa picha ya mama ilikuwa inapepea bila shida
 
Vp, Ngorongoro, zoezi linaendelea?

Nchi ngumu hii!!!!
 
Hapana mkuu kwani Sera za upinzani kwa Sasa Ni zipi zinazogusa maisha yao ya kila siku, unajuwa mwananchi atakuunga mkono na hata kujitolea muda wake atakapoona ajenda ulizobeba zinamgusa,

Lakini mwananchi akikosa sababu ya kuweza kumshawishi hawezi kukuunga mkono zaidi ya Kuendelea na Yule aliyopo, kwa Sasa CCM Ni tumaini la watanzania na bado Wana Imani nayo na ndio maaana wanaendelea kuiunga mkono

Si umeona hata uwanja wa mkapa picha ya mama ilikuwa inapepea bila shida
Huna unalojua.Rudi Facebook wewe.
 
Hapana mkuu kwani Sera za upinzani kwa Sasa Ni zipi zinazogusa maisha yao ya kila siku, unajuwa mwananchi atakuunga mkono na hata kujitolea muda wake atakapoona ajenda ulizobeba zinamgusa,

Lakini mwananchi akikosa sababu ya kuweza kumshawishi hawezi kukuunga mkono zaidi ya Kuendelea na Yule aliyopo, kwa Sasa CCM Ni tumaini la watanzania na bado Wana Imani nayo na ndio maaana wanaendelea kuiunga mkono

Si umeona hata uwanja wa mkapa picha ya mama ilikuwa inapepea bila shida

Kama wananchi wangekuwa na imani na CCM, kuchezea uchaguzi kunatokana na nini? Picha za mama kuingia uwanja wa Tanzania kuna ugumu gani wakati watu wanapanga waende nazo uwanjani? Bado unaamini watu wamelala kiasi hicho kuwa wakiona picha ya rais mahali, basi ni kiwango cha kukubalika kwake?

Hiyo kusema CCM ni tumaini la watanzania mtu yoyote anayetawala anaweza kusema hivyo ili kuhalalisha uwepo wake madarakani, hata kama hayuko kwa ridhaa ya umma. Wananchi tunaona mara zote wanachagua wapinzani na matakwa yao yanageuzwa kwa nguvu ya dola inayotumika vibaya, sasa sijui ni imani gani unaongelea.
 
Rubbish!

Utendaji kazi mzuri wa mama hauna uhusiano wowote na uwepo wa upinzani.

Upinzani umekandamizwa tangu enzi za shujaa!
Utendaji kazi nzuri wa mh Rais una uhusiano mkubwa Sana tuu, maana mfano labda ingekuwa Rushwa imetawala, wananchi wakienda hospitalini hakuna huduma Bora Wala kusikilizwa, mitaani maji shida halafu hakuna juhudi zinazofanyika, unazani wananchi wangempenda Rais wao, unazani wangeipenda serikali?

Lakini wananchi wanamuunga mkono Rais na serikali yake kwa kuwa wanaona juhudi kubwa anazofanya kuwatumikia wananchi, namna anavyotatua kero na changamoto na namna anavyogusa maisha yao
 
Kama wananchi wangekuwa na imani na CCM, kuchezea uchaguzi kunatokana na nini? Picha za mama kuingia uwanja wa Tanzania kuna ugumu gani wakati watu wanapanga waende nazo uwanjani? Bado unaamini watu wamelala kiasi hicho kuwa wakiona picha ya rais mahali, basi ni kiwango cha kukubalika kwake?

Hiyo kusema CCM ni tumaini la watanzania mtu yoyote anayetawala anaweza kusema hivyo ili kuhalalisha uwepo wake madarakani, hata kama hayuko kwa ridhaa ya umma. Wananchi tunaona mara zote wanachagua wapinzani na matakwa yao yanageuzwa kwa nguvu ya dola inayotumika vibaya, sasa sijui ni imani gani unaongelea.
Ni lini umesikia wananchi nchi hii wameandamana wakidai kupinduliwa sauti zao katika sanduku la kupigia kura,

Changamoto ndogo ndogo mama Anaendelea kuzifanyia kazi ili kuimarisha demokrasia yetu, Ndio maana anataka wadau wote waendelee kutoa mawazo yao ya namna Bora ya kuifanya demokrasia yetu ifanane na wakati tuliopo

Tuendelee kumuamini mh Rais katika dhamira yake hiyo njema ya kukuza demokrasia hapa nchini na Tuendelee kumuunga mkono ili kuijenga nchi yetu
 
Ni lini umesikia wananchi nchi hii wameandamana wakidai kupinduliwa sauti zao katika sanduku la kupigia kura,

Changamoto ndogo ndogo mama Anaendelea kuzifanyia kazi ili kuimarisha demokrasia yetu, Ndio maana anataka wadau wote waendelee kutoa mawazo yao ya namna Bora ya kuifanya demokrasia yetu ifanane na wakati tuliopo

Tuendelee kumuamini mh Rais katika dhamira yake hiyo njema ya kukuza demokrasia hapa nchini na Tuendelee kumuunga mkono ili kuijenga nchi yetu

Pita magereza yote kulikuwa na kuna watu hadi leo wako huko kwa kubambikiwa kesi za uchaguzi kuchezewa. Au kipindi hicho yakitokea ulikuwa hujajiunga hapa jf?
 
Pita magereza yote kulikuwa na kuna watu hadi leo wako huko kwa kubambikiwa kesi za uchaguzi kuchezewa. Au kipindi hicho yakitokea ulikuwa hujajiunga hapa jf?
Vitu kama hivyo vinaendelea kumalizwa kisheria kwa utaratibu mzuri hatua kwa hatua ili tuijenge Tanzania Yetu kwa Hali ya umoja na mshikamano, hujasikia wale walioachiwa kule katavi, Geita, songwe na hata kule Njombe, wote hao wameachiwa katika utaratibu mmoja

Hata hivyo siyo wote wataachiwa tu kwa namna Kama hiyo, wengine watalazimika kujibu mashitaka yao, maana wapo walioharibu na kujeruhi wengine kwa kimvuli Cha kupambania vyama vyao, hao watawajibishwa kwa mujibu wa Sheria

Tuendelee kushikamana na Tuvumiliane katika siasa zetu, tutangulize mbele utanzania wetu na tubishane kwa hoja na panapobidi tukubaliane na kupongezana, Tukosoane kwa staha na heshima kwa kulinda utu wetu bila kuvunjiana heshima
 
Hapana mkuu kwani Sera za upinzani kwa Sasa Ni zipi zinazogusa maisha yao ya kila siku, unajuwa mwananchi atakuunga mkono na hata kujitolea muda wake atakapoona ajenda ulizobeba zinamgusa,

Lakini mwananchi akikosa sababu ya kuweza kumshawishi hawezi kukuunga mkono zaidi ya Kuendelea na Yule aliyopo, kwa Sasa CCM Ni tumaini la watanzania na bado Wana Imani nayo na ndio maaana wanaendelea kuiunga mkono

Si umeona hata uwanja wa mkapa picha ya mama ilikuwa inapepea bila shida
Uwanja wa Mkapa picha ambayo kabeba Mbunge wa CCM Babu Tale unashangaa?
 
Uwanja wa Mkapa picha ambayo kabeba Mbunge wa CCM Babu Tale unashangaa?
Miaka kadhaa usingeiona hata picha hiyo na asingeweza kusimmama nayo katikati ya umati wa watu, lakini leo imewezekana kutokanaa na watu kuwa na Imani na mh Rais juu ya utendaji kazi wake, wanamwona Rais Ni wao
 
Acha ngonjera tunahitaji katiba mpya itakayotupa tume huru ya uchaguzi
 
Acha ngonjera tunahitaji katiba mpya itakayotupa tume huru ya uchaguzi
Katiba mpya ipo kwenye michakato na ndio maana unaona Kuna kikosi kazi kilichoundwa kinachoongozwa na profesa mkandala kwa ajili ya kukusanya maoni ili Tujuwe tunaanzia wapi kue
lekea kupata katiba mpya

Najuwa Kuna maoni wengine wakitaka tuanzie kwenye rasimi ya mzee warioba na wengine wakitaka tuanzie na kumaliza kwenye katiba pendekezwa ya mh chenge, lakini wengine wakitaka tuanzie kwa warioba lakini mfumo wa wajumbe ubadilike,

Ambapo wengine wanataka wabunge wasishiriki kwenye mchakato Kama awali,huku wengine wakisema na wao ni sehemu ya wananchi na niwawakilishi wao hivyo kuwaengua Ni kuengua sauti za wananchi

Tuwe na Subira tuone watakuja na maoni gani, lakini hata wewe unaweza ukaenda mbele ya kikosi kazi ukatoa mawazo yako na utapokelewa na kusikilizwa,

Tanzanian Ni yetu tuijenge kwa pamoja kwa maendeleo yetu sote
 
Rubbish!

Utendaji kazi mzuri wa mama hauna uhusiano wowote na uwepo wa upinzani.

Upinzani umekandamizwa tangu enzi za shujaa!
Duh! Bado mnamsingizia Marehemu hadi leo!!? Mi nilikua najua baada ya JPM kuondoka,saa hizi CDM mngekua Ikulu ya Chamwino iliyojengwa na JPM!!!??
 
Back
Top Bottom