Utendaji Mbovu wa Tume ya Utumishi wa Umma; Rais Samia tupia jicho lako hapo

Utendaji Mbovu wa Tume ya Utumishi wa Umma; Rais Samia tupia jicho lako hapo

halafu mfumo wao wa kushughulikia rufaa hauna mantiki nzuri; wanawasiliana na mwajiri ila mwajiriwa haitwi ktk kikao chochote.

Ni wazi kuwa kuna changamoto ktk maamuzi
Mwajiri ataombwa kujibu vielelezo na kujibu hoja za mrufani tu.

Kuhusu kuitwa kwenye kikao haitwi yeyote maana kila kitu kipo kwenye rufaa na majibu ya rufaa.

Hope umeelewa
 
Tume itafute mbinu ya kupunguza msongamano wa kesi mfano kesi ambazo zimewasilishwa tmTume nje ya mda, management iwe inaandaa paper na kupeleka kwa makamishna kupitishwa kwa circular resolution. badala ya kuanza kumuandiki mwajiri, kufanya uchambuzi nk huku ni kupoteza mda tuu badala ya kutoa maamuzi mapema within a month say halafu baada ya hapo mlalamikaji achukue hatua zingine stahiki mfano kwenda CMA nk.
Pili tume hebu wafundisheni staff wenu wawe na customer care nzuri wanatoa majibu makavu short na dry hii sio sawa . Simu hawapokei. Kuna siku nilipiga simu nikawapa identity ya uongo wakasena oh shauri lako lipo ktk uchambuzi. Nikagundua kuwa hawa wapokea simu hawana muda wa kufanya kazi kwa wekedi bali wanatia majibu ya uongo. Tabia hii inasababisha malalamiko yasiyo ya lazima.
Tume kwa nini hamtoi taarifa sahihi? mtu akiuliza shauri lake mtalimaliza lini hamsemi ni kumzungusha tuu mtu bila sababu mbona hata Court of appeal hapako hivyo wapo wazi kabisa hamna usiri usiri usio na maana ukienda CA unakuta list ya cases na tarehe gani kuna tukio gari. Tume hebu badilikikeni, mkiona kuna malalamiko msijitetee badala yake rekebisheni kasoro.
 
Tume itafute mbinu ya kupunguza msongamano wa kesi mfano kesi ambazo zimewasilishwa tmTume nje ya mda, management iwe inaandaa paper na kupeleka kwa makamishna kupitishwa kwa circular resolution. badala ya kuanza kumuandiki mwajiri, kufanya uchambuzi nk huku ni kupoteza mda tuu badala ya kutoa maamuzi mapema within a month say halafu baada ya hapo mlalamikaji achukue hatua zingine stahiki mfano kwenda CMA nk.
Pili tume hebu wafundisheni staff wenu wawe na customer care nzuri wanatoa majibu makavu short na dry hii sio sawa . Simu hawapokei. Kuna siku nilipiga simu nikawapa identity ya uongo wakasena oh shauri lako lipo ktk uchambuzi. Nikagundua kuwa hawa wapokea simu hawana muda wa kufanya kazi kwa wekedi bali wanatia majibu ya uongo. Tabia hii inasababisha malalamiko yasiyo ya lazima.
Tume kwa nini hamtoi taarifa sahihi? mtu akiuliza shauri lake mtalimaliza lini hamsemi ni kumzungusha tuu mtu bila sababu mbona hata Court of appeal hapako hivyo wapo wazi kabisa hamna usiri usiri usio na maana ukienda CA unakuta list ya cases na tarehe gani kuna tukio gari. Tume hebu badilikikeni, mkiona kuna malalamiko msijitetee badala yake rekebisheni kasoro.
Hiki ndicho kinachotakiwa kufanywa. Watoe cause list (mkeka) ya kuonesha rufaa zipi zinasikilizwa katika kikao husika na zipi zitasikilizwa kikao kijacho.

Halafu waruhusu warufani na warufaniwa kuhudhuria kesi zao, hata kama hawataongea wakae na kuona huo mchakato wa maamuzi ya Rufaa zao. Mahakamani watu wanaamuliwa kufungwa vifungo vya maisha wakiwepo mahakamani na hawafi, wanaamuliwa kubomoa nyumba wanasikiliza maamuzi na hawazimii, iweje TUME wazuie warufani kufika mbele ya tume kusikiliza maamuzi yao eti kisa TUME inaogopa kuwa watu watazimia wakisikia majibu ya rufaa zao?

Tume badilikeni
 
Naomba Kanuni inayotoa muda wa rufaa kutolewa uamuzi
Kanuni ya 62 (2) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za 2003, ambayo inaeleza kuwa TUME inatakiwa kuhitimisha Rufaa (kuitolea uamuzi rufaa) ndani ya siku 90 (miezi 3 tu) toka Mwajiri alipowasilisha utetezi wake.

Sasa muda wa mwajiri kuwasilisha majibu ya utetezi wa rufaa ni siku 14 tu toka alipopokea nakala ya rufaa kutoka kwa TUME au kwa mwajiri. Hapa soma Kanuni ya 61 (3) ya Kanuni za Utumishi wa Umma, 2003.

Kwa ufupi, mchakato wote, kuanzia kukata rufaa mpaka kutolwa maamuzi ya Rufaa haipaswi kuzidi miezi 6.
 
Huu ndio tunaita "upotoshaji"

Tume ina maafisa wasiozidi 35

Wanashughulikia rufaa za watumishi wooote wa umma ukiondoa walimu, polisi, magereza, na wanajeshi

Unajua workload ya rufaa au unalalama tu.
===

Ufafanuzi wa taarifa ya upotoshaji kuhusu utendaji kazi wa Tume ya Utumishi wa Umma

NA MWANDISHI MAALUM-PSC

Tume ya Utumishi wa Umma imeanzishwa chini ya Kifungu cha 9 (1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma (Sura ya 298 marejeo ya mwaka 2019), pamoja na majukumu mengine Tume ina jukumu la kupokea na kushughulikia rufaa kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Nidhamu ambao hawakuridhika na uamuzi uliotolewa dhidi yao, kwa mujibu wa Kifungu cha 25 (1) cha Sheria hii na Kanuni ya 60 ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003.


Tume ya Utumishi wa Umma inapenda kutoa ufafanuzi wa taarifa ya upotoshaji kuhusu utendaji kazi wa Tume iliyotolewa kupitia mtandao wa kijamii wa “Jamii Forum” tarehe 12 Agosti 2021 kama ifuatavyo:-

1. Kwa mujibu wa Kifungu cha 9(1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298 (marejeo ya mwaka 2019), Tume inaundwa na Mwenyekiti na Wajumbe 6 ambao huteuliwa na Rais ambao pamoja na majukumu mengine wana jukumu la kisheria la kutolea uamuzi rufaa na malalamiko yanayowasilishwa mbele ya Tume. Aidha, kwa mujibu wa Kifungu cha 14(1) na (2) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298 (marejeo ya mwaka 2019), Tume ina Katibu ambaye ndiye Mtendaji Mkuu. Katibu na Wasaidizi wake (Sekretarieti) ndio watendaji wa kazi za kila siku katika Tume ya Utumishi wa Umma ambao wameteuliwa baada ya kukidhi sifa na vigezo katika nafasi walizo nazo.

2. Pamoja na Sheria zilizopo, Tume inashughulikia rufaa kwa mujibu wa Mwongozo Kuhusu Mashauri ya Nidhamu na Rufaa kwa Watumishi wa Umma wa Mwaka 2009 ambapo rufaa hupokelewa, husajiliwa, huchambuliwa na kupitiwa na Kikao cha Menejimenti na hatimaye kuwasilishwa mbele ya Tume kwa uamuzi. Hatua ya mwisho ni Mrufani na Mrufaniwa kujulishwa kwa barua juu ya uamuzi unaotolewa na Tume. Utaratibu huu umewekwa ili kuimarisha utendaji kazi, kudhibiti upendeleo, rushwa na kuimarisha utoaji wa haki. Aidha, elimu kuhusiana na utaratibu huu imekuwa ikitolewa kwa wadau kupitia majukwaa mbalimbali.

3. Tume katika kushughulikia rufaa na malalamiko haitoi uamuzi kwa shinikizo au ushawishi wa Mwajiri au Mamlaka ya Nidhamu yoyote ili kuwakandamiza watumishi wasipate haki zao. Tafsiri kuwa Tume ni chombo cha kulinda maslahi ya Waajiri na Serikali. Tume inapenda kuufahamisha umma kuwa inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo iliyopo.

4. Rufaa na malalamiko yanayopokelewa Tume yenye vielelezo vilivyokamilika ndio yanayoshughulikiwa na kutolewa uamuzi kwa kadri yalivyopokelewa (First in, First Out).

5. Tume ya Utumishi wa Umma, inaomba umma kuupuuza upotoshwaji huu uliotolewa kupitia mtandao wa kijamii wa “Jamii Forum” na inatoa wito kwa umma na wadau wote kuwasiliana na Tume kwa ufafanuzi, maoni au suala lolote kuhusu Tume kupitia simu namba 0738166703, 0733 005 974 na barua pepe, secretary@psc.go.tz.

Imetolewa na:

John C. Mbisso

KAIMU KATIBU

TUME YA UTUMISHI WA UMMA

DAR ES SALAAM

13 AGOSTI, 2021


Aya ya 3 na ya 4, tume imepata wapi mamlaka ya kusikiliza malalamiko??

Sheria inaeleza kuwa mamlaka ya kusikiliza malalamiko (migogoro ya kazi) kati ya mwajiri na mwajiriwa yapo tume ya usuluhishi na Uamuzi (CMA). Tume ya utumishi wa umma imejipa kazi ambayo haina mamlaka nayo kisheria. Yenyewe ina mamlaka ya kusikiliza Rufaa tu na si kusikiliza migogoro fresh
We ni boonge la kilaza ukishinda tufaa yako unakula mishahara yako toka umefukuzwa kazi.kwanza ukute hata ajira huna
Unaposema unakula mishahara yote unaonesha kama ni faida hivi wakati mishahara ilitakiwa kulipwa hivyo kama ingelipwa wakati ule mtu aliotakiwa kufanya kazi. Sasa kwa vile inalipwa nje ya utaratibu lazima iwe na fidia maana huyo mfanyakazi kwa ajili ya survival alilazimika kutafuta fedha mahali kwingine (sio mshahara).

Sasa TUME haitoi fidia (compensation) na unasema kuwa unakula mishahara yako yote, unaitamka katika namna ya kuonesha kama ni favour hivi ya TUME
 
Hii Tume ni hovyo kabisa! Wanachezea haki za wafanyakazi kirahisirahisi tu. Sheri zinawekwa halafu wanakuwa wa kwanza kuzikiuka....pumbavu kabisa.

Afisa Mwandamizi mzima eti anajibu very simple kwamba wana workload kubwa, kwani hiyo workload inamsaidia nini mtumishi?, kwani umuhimu umuhimu wa kuweka Sheria na Kanuni ni upi?
Muda wa mwajiri kuwasilisha vielelezo vyake na majibu ya Rufaa ni siku 14, na anatakiwa kumpa nakala ya vielelezo hivyo mrufani (mwajiri).

Sasa TUME inashirikiana na Mwajiri kwa kumbembeleza kutuma vielelezo. Yaani hawaanzi kusikiliza Rufaa isipokuwa mpaka mwajiri awasilishe vielelezo, hata kama atawasilisha baada ya miezi 12 kutoka alipopewa nakala ya Rufaa. Ukifuatilia wanakuambia mwajiri bado hajatuma vielelezo, sasa kama hajatuma si mfuate sheria inavyosema. Msikilize Upande Mmoja

Ukisoma taarifa zao kwa Umma, utaona Rufaa kibao zimekataliwa kwa kuwasilishwa nje ya muda lakini hutaona kama kuna Rufaa imesikilizwa upande mmoja baada ya mwajiri kuwasilisha vielelezo nje ya muda. Hapo ndipo Uharamu na harufu ya Rushwa kati ya mwajiri na TUME vinaposemwa
 
Pia Tume inapata wapi mamlaka ya kukubaliana na summary dismissals? Nina jamaa zangu wawili walifukuzwa kazi na waajiri bila kufuata taratibu yoyote ni asubuhi tuu boss aliamka na kuwaandikia barua ya kuwafukuza bila kuwacharge kuwaita ktkt kikao cha nidhamu na baada ya hapo kuwafukuza. Cha kushangaza Tume imeridhia maamuzi ya boss kuwa utaratibu ulikuwa sawa Hivi hawa Tume wanatumia sheria gani za kazi? hii summary dismissal haipo kwenye Public Service Act wala ELRA na haipo hata kwenye Regulation yoyote. Hii sio sawa ni kuwaonea wafanyakazi na kupendelea waajiri. Msimsumbue Raisi kwa kufanyia kazi rufaa kama hizi.
 
Ni kweli Rushwa imekithiri pale kuna jamaa yangu alitoa milioni tatu ili issue yake iweze kukimbizwa.

Management imejaa wazee wenye speed ya konokono na mawazo ya kizamani waliorudisha miaka nyuma na wengine wamestaafu lakini bado Katibu Mkuu UTUMISHI anawaongezea ajira za mkataba wakati vijana wapo tu mtaani.

Ushauri wangu kwa UTUMISHI na Katibu Mkuu Kiongozi badilisheni Management nzima ya TUME mlete watu wengine tena wawe vijana wachapa kazi wenye speed ya kukimbiza mashauri ya wakata rufaa. Au kama kuna vijana hapo TUME wachapa kazi wapewe madaraka wapeleke mambo kwa kasi.
 
Sijui ni nani alileta wazo la kuanzishwa kwa hii kitu.

Bora utaratibu wa awali wa taasisi zenyewe kuajiri zirejeshwe.

Mfano wengine walikuwa wanatumia wakufunzi wa vyuo udsm/MU kuwa interview na kupeleka majina ya walioshinda kwenye taasisi husika.
 
Sijui ni nani alileta wazo la kuanzishwa kwa hii kitu.

Bora utaratibu wa awali wa taasisi zenyewe kuajiri zirejeshwe.

Mfano wengine walikuwa wanatumia wakufunzi wa vyuo udsm/MU kuwa interview na kupeleka majina ya walioshinda kwenye taasisi husika.
Unàchanganya, hiyo unayoizungumzia ni Sekretarieti ya Ajira, lakini huu uzi ni kuhusu tume ya utumishi wa umma
 
Ni kweli Rushwa imekithiri pale kuna jamaa yangu alitoa milioni tatu ili issue yake iweze kukimbizwa.

Management imejaa wazee wenye speed ya konokono na mawazo ya kizamani waliorudisha miaka nyuma na wengine wamestaafu lakini bado Katibu Mkuu UTUMISHI anawaongezea ajira za mkataba wakati vijana wapo tu mtaani.

Ushauri wangu kwa UTUMISHI na Katibu Mkuu Kiongozi badilisheni Management nzima ya TUME mlete watu wengine tena wawe vijana wachapa kazi wenye speed ya kukimbiza mashauri ya wakata rufaa. Au kama kuna vijana hapo TUME wachapa kazi wapewe madaraka wapeleke mambo kwa kasi.
Kama lilivyo shirika la Posta Tanzania. Wazee wengi mno na hawaendani na kasi ya teknolojia.

Umetoa ushauri mzuri sana. Mwenyekiti wa Tume ni Jaji wa Mahakama Kuu, anajua vyema kuhusu haki zinazotolewa kwa kuchelewa kuwa ni sawa na haki zilizonyimwa. Sasa sijui anakwama wapi kuimplement hiyo kanuni katika vitendo.
 
Huyo Muhoji ameshastaafu so aliyoyafanya ameshayafanya. Naibu katibu sasa hivi ni John Mbisso, tumamuomba Mh Raisi aangalie utendaji wake je atayapeleka mashauri kawa speed na weledi? akiona yupo vizuri amdhibitishe ktk cheo. La kama viatu vitampwaya Raisi please please mama yetu tafuta mtu mwingine mwenye sifa, mama Tanzania ina watu 60m hivyo hutakosa wa kumuweka hapo ikibidi tafuta mtu nguli wa sheria za kazi mana hao waliopo tume hawajui maana ya 'fair termination of employment' ndio maana wamekuwa wakiridhia maamuzi ya waafiri wanaofukuza wafanyakazi 'unfairly'

Vinginevyo mh Raisi fumua muundo wa Tume mfano weke mediators na arbitrators maana hao makamishna wameshindwa kutoa ufumbuzi wa malalamiko ambayo ni mengi ya warufani.

Inauma sana kupeleka rufaa halafu inapita mwaka au miaka 2 hadi 3 nk hujui hatima ya rufaa yako! Hao Tume hata kuwapata kwa simu au kawaida ni ngumu mno na ukiwapata jibu lao ni moja tuu 'RUFAA YAKO IPO KWENYE UCHAMBUZI' Lol tabia gani hii hata Primary courts hakuko hivyo ni wawazi na wanatoa maamuzi mapema usiporidhika unakata rufaa au unachukua hatua zingine utakazoona zinafaa.
 
Aache kusafiri nje ya Nchi kisa kutupia jicho matatizo yako??
 
Back
Top Bottom