Utendaji Mbovu wa Tume ya Utumishi wa Umma; Rais Samia tupia jicho lako hapo

Utendaji Mbovu wa Tume ya Utumishi wa Umma; Rais Samia tupia jicho lako hapo

Kumekuwa na malalamiko mengi sana kutoka kwa wananchi kuhusu utendaji mbovu wa Tume ya Utumishi wa Umma ikiongozwa na ndugu Muhoji aliyezungukwa na wasaidizi vilaza wavivu kutumia akili katika kushughulikia rufaa za watumishi wa umma walioonewa na waajiri enzi zile!

Kumekuwa na biasness kubwa sana katika kushughulikia rufaa za watumishi wa umma pale Tume.

1. Tume imekuwa ikishirikiana na waajiri katika kuhujumu haki za watumishi.

2. Rufaa zimekuwa zinakaa kwa muda mrefu bila kuzitolea maamuzi. Ningefurahi sana kujua kama kuna kipengele chochote kinachoibana Tume kuhusu muda.

3. Maafisa wa Tume hawako makini katika uchambuzi wa rufaa za watumishi.

4. Maafisa wa Tume wamekosa customer service or care kwenye kazi zao na hivyo kupelekea wwtumishi wanaokwenda kuulizia rufaa kuwafanya kama maadui, they are so defensive and protective.

5. Wamekuwa wakipewa rushwa na waajiri ili watumishi wakandamizwe ktk kudai haki zao kwasababu waajiri wengi wamekuwa wakiwabambikkiza makosa watumishi wao.

Hivyo basi, tunaomba Mh. Rais Samia tupia jicho lako kwenye hiyo Tume, wanafanya kazi kwa mazoea na kuminya haki za watumishi.
hakuna cha tume wala babake nani serikali yote pamoja na vyombo vyake ni uharo mtupu.
 
EINSTEIN112 ngoja nikufundishe kidogo namna ya kusoma sheria (Act), itakusaidia kuelewa mambo na sio kubisha bisha bali kama utabisha basi itakuwa ni kwa hoja. Kama bado unafanya TUME ya Utumishi utaitumia fursa hii kuwaambia makamishna na watumishi wenzako kuwa Tafsiri sahihi ya sheria ni hii na sio hivyo mnavyoelewa. Darasa linaweza kuwa refu lakini SOMA uelewe maana ni muhimu kwako na kwa wenzako mnaoamua hatima za maisha ya watu kwa nguvu za kisheria mlizopewa (ingawa mnazitumia vibaya).

IPO HIVI
CMA ndio chombo pekee chenye mamlaka ya kusuluhisha migogoro itokanayo au ihusianayo na ajira mwajiri na mfanyakazi). Mamlaka hayo CMA imeyapata kupitia kifungu cha 14(1) cha Sheria ya Mahakama/Taasisi za Kazi (The Labour Institutions Act Cap 366 RE 2019)

View attachment 1905293
Hapo unaona kabisa kuwa CMA ina mamlaka ya kusuluhisha mgogoro wowote wa kikazi unaowasilishwa mbele yake kwa Sheria yoyote ya mambo ya ajira (Sheria ya utumishi wa Umma ikiwa ni mojawapo ya sheria za kazi).

Sheria ya Ajira na mahusiano kazini (the Employment and Labour Relations Act CAP 366 R.E 2019) kupitia kifungu cha 2 (1) inaeleza vyema kuwa ITATUMIKA kwa wafanyakazi wote wa sekta binafsi na wa Serikali isipokuwa wachache wa serikali ambao wameainishwa. Wakati kifungu cha 34A cha Sheria ya Utumishi wa Umma kimeeleza kuwa unpotokea mkanganyiko kati ya Sheria ya Utumishi wa Umma na Sheria nyingine inayohusu utumishi wa Umma ( Sio ELRA), basi Sheria ya utumishi wa Umma (CAP 298 R.E 2019) itakuwa na nguvu dhidi ya nyingine (ya serikali). Kwa lugha rahisi ni kwamba, Sheria ya Utumishi wa Umma haina nguvu kuzidi Sheria ya Ajira na Mahusiano kazini (hata kwa watumishi wa Umma).
View attachment 1905296

RUFAA ZA WATUMISHI WA UMMA
Pale ambapo mamlaka ya nidhamu inakuwa imetoa adhabu (maamuzi) dhidi ya mtumishi wa umma kutokana na nguvu iliyopewa na sheria basi mtumishi huyo anaelekezwa kupitia Kifungu cha 25 (1) (b) cha Sheria ya utumishi wa umma kukata Rufaa kwenye TUME ya UTUMISHI WA UMMA.

Msisitizo,
Ni pale tu mamlaka ya nidhamu inapokuwa imetekeleza mamlaka yake kisheria kwa kutoa adhabu kwa mtumishi kama kumshusha cheo, kumshusha mshahara au kumfukuza kazi ndio mtumishi anaweza kukata Rufaa, kama hakuna adhabu iliyotolewa mtumishi hawezi kukata Rufaa.

View attachment 1905301

TUME KUSIKILIZA MALALAMIKO YA WATUMISHI WA UMMA
Tume ya Utumishi wa Umma haina mamlaka ya kisheria ya kusikiliza na kutoa maamuzi ya Malalamiko ya Watumishi wa Umma. TUME haina uhalali wa kusikiliza migogoro mibichi (original jurisdiction) isipokuwa inaweza kusikiliza migogoro katika hatua ya Rufaa tu (Appellate Jurisdiction) kama ilivyoelezwa katika Kifungu cha 10 (1) (d) cha Sheria ya utumishi wa Umma. Kwa hiyo kinachofanyika sasa TUME kusikiliza Malalamiko ya watu pale ambapo mwajiri anakuwa amemkosea au anamuonea mtumishi. Mamlaka haya yapo CMA tu kama nilivyoeleza awali na TUME imeyapora kutoka CMA kwa kisingizo cha mabadiliko ya Sheria ya utumishi wa Umma, kitu ambacho sio kweli, tutakisoma kifungu hicho wanachotumia TUME na ambacho hakiwapi mamlaka hayo. Kazi za TUME ni hizi hapa;

View attachment 1905302

JE NI LAZIMA KISHERIA KWA MTUMISHI WA UMMA KUEXHAUST LOCAL REMEDIES KABLA YA KWENDA CMA?
Jibu ni inategemea na aina ya mgogoro.
Kama kinacholalamikiwa ni maamuzi ya mamlaka ya nidhamu basi mtumishi wa Umma anapaswa kukata Rufaa TUME na baadae kama hajaridhika kukata rufaa kwa Rais na kisha kama hajaridhika na maamuzi ya rais kurudi Mahakama Kuu kwa Judicial Review, hii ndio inaitwa exhaustion of local remedy. Lakini kama mgogoro ni malalamiko juu ya uonevu wa mwajiri basi mtumishi anaruhusiwa kwenda moja kwa moja CMA bila kupita popote sababu CMA ndicho chombo pekee chenye mamala ya kusikiliza migogoro ya kazi/ ajira. Hana local remedy anayotakiwa kuexhaust.

JE, MABADILIKO YA SHERIA YA UTUMISHI WA UMMA MWAKA 2016 YALIHUSU WATUMISHI WOTE?
Jibu ni HAPANA, mabadiliko hayo ya kuwataka watumishi waexhaust local remedies yaliwahusu watumishi wa umma walio katika ngazi ya OPERATIONAL SERVICE, yaani watumishi wasio na digrii. Ili uelewe vyema jambo hili, unatakiwa kusoma Sub Heading ya Kifungu cha 32 na 32A cha Sheria ya Utumishi wa Umma, kimeandikwa (c) Operational Service. Kwa hiyo Mabadiliko ya Sheria mwaka 2016 yaliongeza Kifungu 32A kuwahusu Watumishi wa Umma ambao wapo katka kundi la Operational Service tu na sio wengineo. BAHATI mbaya, Mawakili wa Serikali wamekuwa wakiipotosha Mahakama kwa kuwaambia kifungu hicho kinahusu waumishi wote wa Umma jambo ambalo sio kweli. Wamekuwa wakiweka Mapingamizi ya Kisheria kila mara mtumishi wa umma anapofungua CMA mgogoro usiohusu adhabu za mamlaka ya nidhamu wakimtaa aexhaust local remedies. Majaji na Waamuzi wa CMA nao wamekuwa wakiingia mtego huu wa mawakili wa serikali, labda kwa kutokusoma kifungu husika au kwa kukisoma vibaya. Maofisa ambao sheria ya utumishi wa Umma imewatambulishakuwa ni wale walioajiriwa kwa digrii (shahada) kama ngazi ya mwanzo kabisa ya ajira zao mfano maafisa kilimo, maafisa watendaji wa Kata, maafisa ugavi nk wanaitwa AFISA. Msingi wa kuongeza Kifungu hiki cha 32A ilikuwa ni kuwazuia watumishi wa Operational Service kwenda CMA moja kwa moja kwa kuwa Sheria ya Utumishi wa Umma hiyohiyo kupitia Kifungu cha 32 iliwaelekeza kuwa watumishi hao wanatawaliwa ama wanaongozwa na Sheria ya Ajira na Mahusiano kazini.
View attachment 1905307

Kwa hiyo, TUME ya Utumishi wa Umma imekwa ikitekeleza jambo amabalo haina mamalaka nalo la kusikiliza malalamiko na kuyatolea uamuzi.
Natumai EINSTEIN112 na wenzako mtakuwa mmenielwa vyema na mmejifunza.

View attachment 1905300
Hii TUME inayofanya mambo ya hovyo ndio iliyoaminiwa na Rais kuwa hategemei kubadilisha uamuzi wao. Kwa maana hiyo Rais amewaamini watu wa TUME wasiowasafi kimaadili na kimaamuzi. Huu ni wakati wa Rais kuifutilia mbali TUME hii ili kuondokana na uozo wake.
 
Lisemwalo lipo,Kama hakipo linanyemelea.Haki inayocheleweshwa ndiyo haki inayonyimwa.Tume ijitafakari na iondoshe malalamiko au upungufu uliopo hivi sasa,waadhirika wanateseka.Kama kazi zimewaelemea ombeni kibali Cha ku review ikams(establishment) ya taasisi yenu na kuomba kuongeza watumishi ili kuleta ufanisi.
 
Lisemwalo lipo,Kama hakipo linanyemelea.Haki inayocheleweshwa ndiyo haki inayonyimwa.Tume ijitafakari na iondoshe malalamiko au upungufu uliopo hivi sasa,waadhirika wanateseka.Kama kazi zimewaelemea ombeni kibali Cha ku review ikams(establishment) ya taasisi yenu na kuomba kuongeza watumishi ili kuleta ufanisi.
Na sio kitu cha kweli (halisia) kuwa wana rufaa nyingi sana, watumishi wanaofukuzwa kazi serikalini ni wachache sana kwa mwaka. Mfano, mahakama, unakuta mwaka mzima hakuna hakimu aliyefukuzwa kazi Tanzania nzima. Halmashauri ya Wilaya yenye watumishi 2500, mwaka mzima wanaweza kufukuzwa kazi watumishi wasozidi 3 kwa mwaka. Halmashauri zipo 152 kama sikosei, kwa hiyo ni rufaa chini ya 600 zinazokwenda TUME kwa mwaka, ukijumlisha na za taasisi nyingine za umma unakuta no rufaa labda 1000 kwa mwaka. Ukigawa kwa wafanyakazi 35 wa Tume unakuta kila mmoja atafanyia kazi rufaa 29 kwa mwaka mzima wenye siku 365 wakati hakimu mmoja wa mahakama ya mwanzo ana jukumu la kusikiliza kesi 70 sijui kwa mwaka na kesi zinaenda. Sasa hao tume huo mzigo wanautoa wapi?

Wanataka kutuaminisha kuwa taasisi za umma zinafukuza sana watumishi kiasi rufaa ni nyingi sana?
 
Mpigie simu kabisa maana naona unateseka sana.

Unahisi.kwa mfano bado ningekuwa Tume ningekaa natafakari rufaa yako tu kati ya rufaa za watu maelfu ambao tayari wana vielelezo.

Sikia nshakuambia sio.msemaji wa Tume so usinikoti pambana na hali yako
kama mrufani akichelewa kupeleka rufaa yake ndani ya siku 45 inatupiliwa nje kwanini mwajiri nae akichelewa ndani ya siku 14 rufaa isiamuliwe kutumia vielelezo vya upande mmoja? kama huo muda upo kisheria?
 
kama mrufani akichelewa kupeleka rufaa yake ndani ya siku 45 inatupiliwa nje kwanini mwajiri nae akichelewa ndani ya siku 14 rufaa isiamuliwe kutumia vielelezo vya upande mmoja? kama huo muda upo kisheria?
Sio lazima mrufani akichelewa kupeleka rufaa yake inatupiliwa mbali soma Reg.61(4). Mamlaka ya Nidhamu sio kila mara wanachelewa kuleta vielelezo. Ukisoma ufafanuzi wa Kaim Katibu amesema "FIRST IN FIRST OUT"

Pia kumbuka vikao vya TUME vinakaa kila robo mwaka kisheria maana yake baada ya miezi3. kwa mfano rufaa imemalizika kuchambuliwa leo na kikao kimeisha jana, itasubiri next kikao. Kulikuwa na mrundikano mwingi wa kesi lilipoisha zoezi la uhakiki wa vyeti.
 
Sio lazima mrufani akichelewa kupeleka rufaa yake inatupiliwa mbali soma Reg.61(4). Mamlaka ya Nidhamu sio kila mara wanachelewa kuleta vielelezo. Ukisoma ufafanuzi wa Kaim Katibu amesema "FIRST IN FIRST OUT"

Pia kumbuka vikao vya TUME vinakaa kila robo mwaka kisheria maana yake baada ya miezi3. kwa mfano rufaa imemalizika kuchambuliwa leo na kikao kimeisha jana, itasubiri next kikao. Kulikuwa na mrundikano mwingi wa kesi lilipoisha zoezi la uhakiki wa vyeti.
Kwanza kubalini customer care yenu hasa kwenye upande wa simu ni mbaya mnoo halafu pili mnatakiwa mbadilike badala ya kutumia posta muendane na technology inavyoenda mtumie email badala ya kumsumbua mrufani kutembelea posta kuangalia barua au aweze kupata alert kuna barua imepelekwa posta kupitia e-mail halafu kutokana na mabadiliko makubwa kwenye TEHAMA tume wanatakiwa wawe na mfumo ambao kila mrufani atapewa id yake ili aweze kulogin na kuangalia status ya rufaa yake hii itadumu mpaka rufaa yake itakapofikia mwisho. kama idara ya Tehama imeshindwa kulifanyia kazi nendeni e-government kwa msaada zaidi au njoo huku private sector tuwasaidie acheni kuwapeleka watu kizamani kwenye zama hizi ambazo taarifa inapatikana kwenye vidole
 
Kwanza kubalini customer care yenu hasa kwenye upande wa simu ni mbaya mnoo halafu pili mnatakiwa mbadilike badala ya kutumia posta muendane na technology inavyoenda mtumie email badala ya kumsumbua mrufani kutembelea posta kuangalia barua au aweze kupata alert kuna barua imepelekwa posta kupitia e-mail halafu kutokana na mabadiliko makubwa kwenye TEHAMA tume wanatakiwa wawe na mfumo ambao kila mrufani atapewa id yake ili aweze kulogin na kuangalia status ya rufaa yake hii itadumu mpaka rufaa yake itakapofikia mwisho. kama idara ya Tehama imeshindwa kulifanyia kazi nendeni e-government kwa msaada zaidi au njoo huku private sector tuwasaidie acheni kuwapeleka watu kizamani kwenye zama hizi ambazo taarifa inapatikana kwenye vidole
Mkuu e-goverment 90% ya Serikali na ASASI zake bado hawajaingia, anyway ni wazo zuri kama ukilifikisha kwa wahusika.

Email kila mtumishi anayo ila tatizo hairuhusiwi kwa namna yoyote MCHAMBUZI KUWASILIANA NA MRUFANI DIRECT.

EMAIL YA KATIBU ANAFUNGUA PS WAKE unadhani atajibu ngapi TZ nzima? tuongee reality.

Barua IM SURE UKIANDIKA LAZIMA UJIBIWE
 
Na sio kitu cha kweli (halisia) kuwa wana rufaa nyingi sana, watumishi wanaofukuzwa kazi serikalini ni wachache sana kwa mwaka. Mfano, mahakama, unakuta mwaka mzima hakuna hakimu aliyefukuzwa kazi Tanzania nzima. Halmashauri ya Wilaya yenye watumishi 2500, mwaka mzima wanaweza kufukuzwa kazi watumishi wasozidi 3 kwa mwaka. Halmashauri zipo 152 kama sikosei, kwa hiyo ni rufaa chini ya 600 zinazokwenda TUME kwa mwaka, ukijumlisha na za taasisi nyingine za umma unakuta no rufaa labda 1000 kwa mwaka. Ukigawa kwa wafanyakazi 35 wa Tume unakuta kila mmoja atafanyia kazi rufaa 29 kwa mwaka mzima wenye siku 365 wakati hakimu mmoja wa mahakama ya mwanzo ana jukumu la kusikiliza kesi 70 sijui kwa mwaka na kesi zinaenda. Sasa hao tume huo mzigo wanautoa wapi?

Wanataka kutuaminisha kuwa taasisi za umma zinafukuza sana watumishi kiasi rufaa ni nyingi sana?
Huyu Msemaji wao humu anasema rufaa nyingi ziliongezeka baada ya wale wenye vyeti feki kutimuliwa kwahiyo nina imani kwa sasa hivi idadi ya wanaokata rufaa itakuwa imepungua sana
 
Mkuu e-goverment 90% ya Serikali na ASASI zake bado hawajaingia, anyway ni wazo zuri kama ukilifikisha kwa wahusika.

Email kila mtumishi anayo ila tatizo hairuhusiwi kwa namna yoyote MCHAMBUZI KUWASILIANA NA MRUFANI DIRECT.

EMAIL YA KATIBU ANAFUNGUA PS WAKE unadhani atajibu ngapi TZ nzima? tuongee reality.

Barua IM SURE UKIANDIKA LAZIMA UJIBIWE
Mimi sizungumzii kutuma rufaa kupitia e-mail hapana !!! ila muwe mnatoa majibu ya rufaa kupitia e-mail badala ya barua au mtumie vyote viwili kumrahishia mrufani badala ya kumaktisha tamaa ya kwenda posta mara kwa mara kwenda kuangalia majibu ya rufaa yake

Halafu wewe ndiye unatakiwa kuyafikisha kwa wahusika
 
Kwanza kubalini customer care yenu hasa kwenye upande wa simu ni mbaya mnoo halafu pili mnatakiwa mbadilike badala ya kutumia posta muendane na technology inavyoenda mtumie email badala ya kumsumbua mrufani kutembelea posta kuangalia barua au aweze kupata alert kuna barua imepelekwa posta kupitia e-mail halafu kutokana na mabadiliko makubwa kwenye TEHAMA tume wanatakiwa wawe na mfumo ambao kila mrufani atapewa id yake ili aweze kulogin na kuangalia status ya rufaa yake hii itadumu mpaka rufaa yake itakapofikia mwisho. kama idara ya Tehama imeshindwa kulifanyia kazi nendeni e-government kwa msaada zaidi au njoo huku private sector tuwasaidie acheni kuwapeleka watu kizamani kwenye zama hizi ambazo taarifa inapatikana kwenye vidole
They operate like an old school!!😆😆😆😆

Wanazungumzia FIRST IN FIRST OUT badala ya kuagalia Sheria na Kanuni vinasemaje kuhusu suala la muda, halafu anaeongea hilo eti ni Kaimu Katibu, bure kabisa!!!. Hawa Tume wanacheza na haki za watumishi!!!
 
Mimi sizungumzii kutuma rufaa kupitia e-mail hapana !!! ila muwe mnatoa majibu ya rufaa kupitia e-mail badala ya barua au mtumie vyote viwili kumrahishia mrufani badala ya kumaktisha tamaa ya kwenda posta mara kwa mara kwenda kuangalia majibu ya rufaa yake
Hilo hata kama sifanyi kazi pale tena ila naona HALIWEZEKANI.
GOVERNMENT WORKS ON PAPER.


KUHUSU BARUA KUCHELEWA KUMFIKIA MRUFANI HATA BAADA YA KIKAO IPO HIVI:-
NAKALA ZA RUFAA ZINAENDA OFISI KAMA 6
1.MRUFANI
2 MAMLAKA YA NIDHAMU
3. RAIS/IKULU
4 UTUMISHU
5. TAMISEMI
6. RAS
HIZI ZOTE ZINATAKIWA KUSAINIWA ORIGINAL NA PIA LAZIMA ASAINI MTENDAJI MKUU PEKE YAKE.

IMAGINE KIKAO KIMEAMUA RUFAA 100 NA KILA RUFAA MTU MMOJA ASAINI NAKALA 6 MAANA YAKE ATASAINI BARUA 600 BAADA YA KUHAKIKI MAUDHUI YAKE KAMA YAPO KAMA YALIVYOAMULIWA (KUJIRIDHISHA)

KUMBUKA HAPO BADO ANA DAY TO DAY ACTIVITIES

VUTA SUBIRA HAKI YAKO INAKUJA TU
 
Waache uvivu kuhakiki barua 600 shida ni nini kama wanaona ni kazi waachie ngazi wapo watu wachapa kazi.
Hilo hata kama sifanyi kazi pale tena ila naona HALIWEZEKANI.
GOVERNMENT WORKS ON PAPER.


KUHUSU BARUA KUCHELEWA KUMFIKIA MRUFANI HATA BAADA YA KIKAO IPO HIVI:-
NAKALA ZA RUFAA ZINAENDA OFISI KAMA 6
1.MRUFANI
2 MAMLAKA YA NIDHAMU
3. RAIS/IKULU
4 UTUMISHU
5. TAMISEMI
6. RAS
HIZI ZOTE ZINATAKIWA KUSAINIWA ORIGINAL NA PIA LAZIMA ASAINI MTENDAJI MKUU PEKE YAKE.

IMAGINE KIKAO KIMEAMUA RUFAA 100 NA KILA RUFAA MTU MMOJA ASAINI NAKALA 6 MAANA YAKE ATASAINI BARUA 600 BAADA YA KUHAKIKI MAUDHUI YAKE KAMA YAPO KAMA YALIVYOAMULIWA (KUJIRIDHISHA)

KUMBUKA HAPO BADO ANA DAY TO DAY ACTIVITIES

VUTA SUBIRA HAKI YAKO INAKUJA TU
 
Waache uvivu kuhakiki barua 600 shida ni nini kama wanaona ni kazi waachie ngazi wapo watu wachapa kazi.
Huwezi kuelewa kwa kuwa we ni muhanga. Toka kidogo kwenye lindi la hasira zako halafu weka mbele wako kitabu chenye kurasa 600+ halafu usome kila page na kusaini. Hapo bado una majukumu chungu mzima utaelewa.

NB. sikulazimishi kuelewa na kama nlivokuambia mwanzoni kama una maswali nenda pale Kivukoni, Luthuli st. Kiwanja Na.10 kamuone Katibu uzuri haitaji Apointment kuonana na mteja. atakufafanulia. Uzi uliletwa ili Rais auone nadhani ameshauona, usiniulize mimi maswali zaidi nlijitolea kuelewesha baadhi ya mambokutokana na uelewa wangu wa kufanya kazi pale matokeo mmenigeuza mimi TUME.
 
Kwa nini usaini barua 100 kwa siku? kwa siku zinaweza kuwa drafted barua za watu 30 unaedit zikiwa vizuri una wa- cc wahusika unaprint 30 x 6 = 180 shida nini hapa baada ya wiki imemaliza. kwani anadraft mwenyewe? kuna wakuu wa idara na vitengo. Kwa nini mambo rahisi mnataka kuyafanya magumu. Huo ni UKILAZA!!!
Huwezi kuelewa kwa kuwa we ni muhanga. Toka kidogo kwenye lindi la hasira zako halafu weka mbele wako kitabu chenye kurasa 600+ halafu usome kila page na kusaini. Hapo bado una majukumu chungu mzima utaelewa.

NB. sikulazimishi kuelewa na kama nlivokuambia mwanzoni kama una maswali nenda pale Kivukoni, Luthuli st. Kiwanja Na.10 kamuone Katibu uzuri haitaji Apointment kuonana na mteja. atakufafanulia. Uzi uliletwa ili Rais auone nadhani ameshauona, usiniulize mimi maswali zaidi nlijitolea kuelewesha baadhi ya mambokutokana na uelewa wangu wa kufanya kazi pale matokeo mmenigeuza mimi TUME.
 
Kwa nini usaini barua 100 kwa siku? kwa siku zinaweza kuwa drafted barua za watu 30 unaedit zikiwa vizuri una wa- cc wahusika unaprint 30 x 6 = 180 shida nini hapa baada ya wiki imemaliza. kwani anadraft mwenyewe? kuna wakuu wa idara na vitengo. Kwa nini mambo rahisi mnataka kuyafanya magumu. Huo ni UKILAZA!!!
Lingekuwa rahisi Ungekuwa kazini saivi pimbi wewe.

Ufukuzwe kazi kwa upumbavu wako halafu ufundishe kazi waliopo kazini pathetic!!

Nakuelekeza kwa adabu ila unaonekana kichwa maji.

Print uzi huu ukakabidhi pale geti la ikulu au peleka platforms zingine liende viral [emoji35][emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]
 
Kama wewe sio mhusika wa Tume kwa nini unakuwa kimbelembele hapa kila kinachotumwa unajibu. Nyamaza basi.
Kwa nini usaini barua 100 kwa siku? kwa siku zinaweza kuwa drafted barua za watu 30 unaedit zikiwa vizuri una wa- cc wahusika unaprint 30 x 6 = 180 shida nini hapa baada ya wiki imemaliza. kwani anadraft mwenyewe? kuna wakuu wa idara na vitengo. Kwa nini mambo rahisi mnataka kuyafanya magumu. Huo ni UKILAZA!!!
 
Mbona matusi ndugu kuwa mstaarabu. Tujadili kwa hoja na sio matusi au hasira, wewe kila mtu hapa unamtukana kwa nini uko hivyo?
Lingekuwa rahisi Ungekuwa kazini saivi pimbi wewe.

Ufukuzwe kazi kwa upumbavu wako halafu ufundishe kazi waliopo kazini pathetic!!

Nakuelekeza kwa adabu ila unaonekana kichwa maji.

Print uzi huu ukakabidhi pale geti la ikulu au peleka platforms zingine liende viral [emoji35][emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]
 
Back
Top Bottom