Utenguzi: Rais Samia atengua nafasi za Viongozi wafuatao

Utenguzi: Rais Samia atengua nafasi za Viongozi wafuatao

2 Aug 2021 — ... Lino Pius Mwageni wilaya ya Ushetu akichukua nafasi ya Michael Augustino Matomora aliyepelekwa wilaya ya Iramba,

UTOKA MAHAKAMANI WILAYA YA KAHAMA – SHINYANGA​

Januari 13, 2023 imefunguliwa Kesi ya Uhujumu Uchumi ECO. NO. 1/2023 Katika Mahakama ya Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama Mhe. Edmund Kente.

Washitakiwa ni Bw. MICHAEL AUGUSTINO MATOMOLA, aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Iramba na wenzake sita.

Kesi hiyo inaendeshwa na Waendesha Mashtaka wa TAKUKURU, SIMON MASHINGIA na JANE MBUGE, ambao waliwasomea hoja za awali za mashtaka ya kuisababishia hasara Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu ya kiasi cha sh. 138,276,250/- katika ya kipindi cha mwaka 2019.

Makosa haya yanadaiwa kutendeka wakati washtakiwa walipokuwa watumishi wa Halmashauri ya Ushetu.

Washtakiwa wamekana mashitaka na wameshindwa kutimiza masharti ya dhamana hivyo wamepelekwa mahabusu.
Kesi imeahirishwa hadi Januari 17, 2023 itakapokuja kwa ajili ya kusoma hoja za awali
 
Wa Sumbawanga licha ya madudu yote ila Sio PM au Kinana Wala Rais wanaoweza kumtengua..

Aisee atakuwa ana ndagu Kali sana,Kila Kiongozi kuanzia DC na RC Huwa wanatenguliwa wao ila Jamaa yupo tuu mwaka wa 9 huu anadunda na tuhuma za kila aina.
Kwani kafanya nn au anamapungufu gani hadi kutolewa?
 
Nafasi zao zitashikwa na wafuatao

Bwana Idd Mrisho

bwana Juma Khamis

bi husna Rajabu

Na bi Shamsa nasoro

Jamani, nabashiri tuu
Dr kimaro alishamaliza,baadae tukae chini tujitafakari jumba bovu likamwangukia.Sisi sio waaminifu.
 
Wa Sumbawanga licha ya madudu yote ila Sio PM au Kinana Wala Rais wanaoweza kumtengua..

Aisee atakuwa ana ndagu Kali sana,Kila Kiongozi kuanzia DC na RC Huwa wanatenguliwa wao ila Jamaa yupo tuu mwaka wa 9 huu anadunda na tuhuma za kila aina.

Niletee majina yake ili tufanyie kazi haraka sana!
 
Hao wakurugenzi majibu yao yatapatikana siku sio nyingi, kwenye hotuba fulani tutamegewa sababu, hawezi kuamka tu bila sababu akawafyeka hao, she is not mentally sick.
 
Toka maktaba :


Ruangwa, Lindi

MKUU WA WIILAYA YA MBARALI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KESI YA UHUJUMU UCHUMI


Video toka maktaba : Mkuu wa wilaya wa Mbarali Mheshimiwa Reuben Mfune

TAKUKURU imemfikisha Mkuu wa wilaya wa Mbarali Mheshimiwa Reuben Mfune (58) mahakamani kwa kesi ya uhujumu uchumi namba 1 ya mwaka 2023.

Baada ya kusomewa mashtaka, mtuhumiwa alikana tuhuma za makosa na amepewa dhamana. Na kesi hiyo kusikilizwa tena mwezi February 2023 mbele ya Mahakama ya Wilaya.


TOKA MAKTABA :
30 Oktoba 2013
View attachment 2494263
DC Ruangwa kusaka mchawi anayekwamisha maendeleo ya ...

30 Oct 2013 — Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Reuben Mfune aliahidi kufanyia kazi malalamiko hayo ya watumishi .....

TOKA MAKTABA :
18 May 2016
KESI YA DAVID KAFULILA KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI 2015

Aidha katika kipengele cha pili ambacho Kafulila alikuwa anamlalamikia Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Reuben Mfune; aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza kuwa alishinikizwa kumtangaza Mwillima kuwa mshindi wakati msimamizi huyo akijua kwamba yeye Kafulila ndiye.

Kafulila alikuwa anamlalamikia Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Reuben Mfune; aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza kuwa alishinikizwa kumtangaza Mwillima kuwa mshindi wakati msimamizi huyo akijua kwamba yeye Kafulila ndiye ......
Hii hapa sababu ya wa kwanza...
 
Back
Top Bottom