Utetetezi wa Sabaya, haupo kisheria, na pia unavunja kanuni za Kijasusi

Utetetezi wa Sabaya, haupo kisheria, na pia unavunja kanuni za Kijasusi

Angekuwa mjanja angerokodi mazungumzo yake na Magufuli kama ni kweli alikuwa anatumwa kufanya uhalifu. Unapotumwa na mtu yoyote yule kufanya uhalifu hakikisha una ushahidi ili baadaye asikuruke. Hii ni bima yako ya maisha ambayo ukipata matatizo itakulipa.


Hata Kama akirekodi bado haitamsaidia Sana ingawaje atajiletea unafuu
 
hawezi kutiwa hatiani kwa majungu na fitina.
Mahakama zinazingatia ushahidi usio na shaka sio hisia zako na mihemuko.
kesi ya sabaya imejaa hisia na mihemuko ya kisiasa!!
chuki za wafanya biashara walio lazimishwa kulipa kodi!
unaazaje kumfunga mtu aliye kuwa amezungukwa na mazingira kama hayo, unawezaje kutofautisha ukweli na chuki za kisiasa?!
Hapo mahakamani anafanya nini kama ni kesi za hisia na mihemko?
 
Sebaya Kama alitumwa na Hayatti Magufuli, hii ilimaanisha taasisi ya Urais ilikuwa inajua misheni hizo, hivyo hakupaswa ajitetee kuwa alitumwa na Rais kufanya Uhalifu kwani Kwa kufanya hivyo anamdhalilisha Hayatti Magufuli na Taasisi ya Urais ya wakati huo.
Sabaya ni roboti yenye damu
 
Mambo ni Moto

Katika sakata linaloendelea linalomkabili Ndugu Lengai Ole Sabaya, utetezi wake unaacha watu midomo wazi.
Mimi sio mwanasheria lakini Kwa akili ndogo tuu niliyonayo namuona Ole Sabaya na mawakili wake wakishindwa kutoa utetezi wenye mantiki.

Utetezi wa Sabaya kuwa alitumwa na Wakuu wake wa kazi waliomteua kufanya Uhalifu ni utetezi wa kijinga Sana ambao mtu mwenye akili asingeweza kuusema Mahakamani.
Kusema alitumwa ni dhahiri anakiri kosa kuwa alifanya, na moja Kwa moja anajitia hatiani.

Ole Sabaya Kiujasusi tayari ameshakosa Weledi katika Kazi yake. Anaposemwa alitumwa na Rais Magufuli ambaye Kwa sasa ni Marehemu, Kwa kazi maalumu, hii inamaanisha kuwa Sabaya yupo katika mfumo wa ujasusi iwe direct au indirectly.
Hivyo Jambo la kwanza kwenye majukumu yake lilipaswa kuwa Siri ndipo mengine yafuate

Moja ya kanuni za kazi maalumu ni siri, hasa kazi maalumu/operations zisizokuwa na majina na zisizoundwa kisheria.
Operations ambazo hazifuati kanuni Rasmi, ni unapigiwa simu na unatekeleza.
Operations za hivi, anayetumwa anapaswa azifanye Kwa weledi pasipo kuleta athari mbaya ambazo zitamtia hatiani, kwani zimtiapo hatiani yeye ndiye atahusika 100% katika adhabu.

Kijasusi, mtu anapopewa kazi maalumu hata akikamatwa hapaswi kusema ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake, hapaswi kuwataja waliomtuma, anapaswa kutumia mbinu zingine za kujihamu au kuficha siri.

Sabaya Kama alitumwa na Hayatti Magufuli, hii ilimaanisha taasisi ya Urais ilikuwa inajua misheni hizo, hivyo hakupaswa ajitetee kuwa alitumwa na Rais kufanya Uhalifu kwani Kwa kufanya hivyo anamdhalilisha Hayatti Magufuli na Taasisi ya Urais ya wakati huo.

Kama ni kweli alitumwa, basi angekaa kimya na kujitetea Kwa namna zingine, alafu Kwa vile alitumwa na taasisi ya Urais, basi mabosi wake Kwa vile wengine wapo na wanatambua misheni hiyo, wangetafuta namna ya kumnasua.
Lakini sio kuwataja, Kwa kuwataja ni tayari ameshavujisha Siri pasipo yeye kujua.

Sabaya pasipo kujua, kauli yake unazidi kuwapa nguvu Wale wote waliokuwa wakiituhumu serikali na watu wasiojulikana.

Kwa kifupi, Sabaya amekosa Weledi.

Hata Kama akitoka basi tayari ameshavujisha Siri za wakubwa wake, na Hana sifa za kuwa mtu wa vitengo Kwa mambo ya kiusalama.

Ilimpasa afe kiume. Akaze Tai shingoni.Mabosi zake ndio wamnasue.
Lakini utetezi wake bado unamuweka pagumu zaidi.

Robert Heriel
Kwanza ni ajabu hujui sheria halafu unajadili sheria, hii ipo Tanzania tu na wewe siyo wa kwanza. Huko mitandaoni Kuna kijana ana digrii sijui ya matango lakini unakuta anamkosoa Prof. Wa sheria kwenye Mambo ya sheria na wapumbavu wanamshangilia, yes Tanzania inawezekana.
Nikusaidie kitu, Sabaya hakuna sehemu amekiri kutenda kosa, hata aliposomewa charge aliplead not guilty.
Kwenye kesi yake moja ya hoja ambayo imemkalia vibaya ni ilikuwaje yeye Kama mkuu wa Wilaya ya Hai aende kufanya oparation Wilaya ya Arusha kwenye Mamlaka isiyo yake.
So katika kuweka matundu kwenye hoja hiyo, narudia kuweka matundu,( he does not need to prove he is not guilty) ndiyo maana anasema alifanya hiyo oparation kwa maelekezo ya wakubwa na siyo Arusha tu hata DSM na hakuna sehemu amekubali kwamba hiyo oparation ilikuwa kinyume na sheria!
 
Kwanza ni ajabu hujui sheria halafu unajadili sheria, hii ipo Tanzania tu na wewe siyo wa kwanza. Huko mitandaoni Kuna kijana ana digrii sijui ya matango lakini unakuta anamkosoa Prof. Wa sheria kwenye Mambo ya sheria na wapumbavu wanamshangilia, yes Tanzania inawezekana.
Nikusaidie kitu, Sabaya hakuna sehemu amekiri kutenda kosa, hata aliposomewa charge aliplead not guilty.
Kwenye kesi yake moja ya hoja ambayo imemkalia vibaya ni ilikuwaje yeye Kama mkuu wa Wilaya ya Hai aende kufanya oparation Wilaya ya Arusha kwenye Mamlaka isiyo yake.
So katika kuweka matundu kwenye hoja hiyo, narudia kuweka matundu,( he does not need to prove he is not guilty) ndiyo maana anasema alifanya hiyo oparation kwa maelekezo ya wakubwa na siyo Arusha tu hata DSM na hakuna sehemu amekubali kwamba hiyo oparation ilikuwa kinyume na sheria!

Screenshot_2021-08-14-10-31-27-19.jpg
 
Ha ha ha ha , unaona sasa ulivyo tutusa kwenye sheria. Huo ni ushahidi wa mtu ambao siyo conclussive kuwa ni wa kweli, huyo si amesema tu, ameleta hivyo vielelezo kuthibitisha kuwa alilipoti kwenye hiyo Mamlaka. Shahidi hasa wa prosecution anakuwa scrutinized mno ikiwemo his credibility . Kasome kesi ya juzi ya mbowe na wenzake uone High Court ilivyowachana chana askari waliodai kumtambua mbowe wakati wa mkutano. It is not easy eti kwa sababu huyo askari kasema taratibu zimekiukwa Basi zilikiukwa! He is just a witness whose testimonies are subject to scrutinization by the Court!
 
Sebaya Kama alitumwa na Hayatti Magufuli, hii ilimaanisha taasisi ya Urais ilikuwa inajua misheni hizo, hivyo hakupaswa ajitetee kuwa alitumwa na Rais kufanya Uhalifu kwani Kwa kufanya hivyo anamdhalilisha Hayatti Magufuli na Taasisi ya Urais ya wakati huo.
Huyo Rais aliyempeleka mahakamani hakujua kuwa Alitumwa na Rais mwenzake? Kama kweli anajua kuwa alitumwa na labda alifanya ya hovyo kwenye utekelezaji wake, kwanini asimpe tu adhabu kwenye mamlaka yale ya kiutumishi?

Mimi mtazamo wangu, Rais alipaswa kuchunguza hii issue yeye mwenyewe na kupata ukweli. Kabla ya kuamua kumpelekea mahakamani. Ndio maana sheria ziliweka adhabu kwenye mamlaka ya uteuzi, sababu walijua kuna mazingira heshima ya Taasisi lazima ilindwe. Kesi hii inaivua nguo taasisi ya Urais na Serikali kwa ujumla.
 
Kwa muda wote aliokaa rumande wanampiga miti bila kimbo unatarajia atakuwa kwenye utimamu wa akili?
 
Thus wakitumwa kuuwa watu waliouwa huwa wauaji huwa wanauwawa check Siri zimeshaanza kuwa hadharani.
Ofisi ya raisi imechafuliwa vibaya na Sabaya,hii ni hatari aisee,haya madhara ya kuokota uvccm na kuwapa nafasi nyeti.
Soon tutajua aliyemteka Mo,risasi lisu,nk.
 
Huyo Rais aliyempeleka mahakamani hakujua kuwa Alitumwa na Rais mwenzake? Kama kweli anajua kuwa alitumwa na labda alifanya ya hovyo kwenye utekelezaji wake, kwanini asimpe tu adhabu kwenye mamlaka yale ya kiutumishi?

Mimi mtazamo wangu, Rais alipaswa kuchunguza hii issue yeye mwenyewe na kupata ukweli. Kabla ya kuamua kumpelekea mahakamani. Ndio maana sheria ziliweka adhabu kwenye mamlaka ya uteuzi, sababu walijua kuna mazingira heshima ya Taasisi lazima ilindwe. Kesi hii inaivua nguo taasisi ya Urais na Serikali kwa ujumla.
Sabaya kasema ukweli kumbe kuna serikali zinazotesa raia bila aibu na kukomoa watu, karma is a bitch
 
... Sabaya kuwemo kwenye Mfumo wa ujasusi wa nchi hii haina mashaka! Toka enzi akiwa mtoto UVCCM aliwahi kukutwa na kitambulisho cha TISS kesi ikafunguliwa. Alivyoachiwa ni mamlaka yake ya uteuzi pekee ndio inajua.

In short, ameandaliwa kwa kazi maalum long time so yanayotokea kwenye sakata hili ni long time plan. Alichokisema mahakamani ni sahihi kabisa.
Na unaweza kuta hata hii kesi ya Sabaya,ni special mission ya system inacheza na akili zetu!!
 
Mambo ni Moto

Katika sakata linaloendelea linalomkabili Ndugu Lengai Ole Sabaya, utetezi wake unaacha watu midomo wazi.
Mimi sio mwanasheria lakini Kwa akili ndogo tuu niliyonayo namuona Ole Sabaya na mawakili wake wakishindwa kutoa utetezi wenye mantiki.

Utetezi wa Sabaya kuwa alitumwa na Wakuu wake wa kazi waliomteua kufanya Uhalifu ni utetezi wa kijinga Sana ambao mtu mwenye akili asingeweza kuusema Mahakamani.
Kusema alitumwa ni dhahiri anakiri kosa kuwa alifanya, na moja Kwa moja anajitia hatiani.

Ole Sabaya Kiujasusi tayari ameshakosa Weledi katika Kazi yake. Anaposemwa alitumwa na Rais Magufuli ambaye Kwa sasa ni Marehemu, Kwa kazi maalumu, hii inamaanisha kuwa Sabaya yupo katika mfumo wa ujasusi iwe direct au indirectly.
Hivyo Jambo la kwanza kwenye majukumu yake lilipaswa kuwa Siri ndipo mengine yafuate

Moja ya kanuni za kazi maalumu ni siri, hasa kazi maalumu/operations zisizokuwa na majina na zisizoundwa kisheria.
Operations ambazo hazifuati kanuni Rasmi, ni unapigiwa simu na unatekeleza.
Operations za hivi, anayetumwa anapaswa azifanye Kwa weledi pasipo kuleta athari mbaya ambazo zitamtia hatiani, kwani zimtiapo hatiani yeye ndiye atahusika 100% katika adhabu.

Kijasusi, mtu anapopewa kazi maalumu hata akikamatwa hapaswi kusema ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake, hapaswi kuwataja waliomtuma, anapaswa kutumia mbinu zingine za kujihamu au kuficha siri.

Sabaya Kama alitumwa na Hayatti Magufuli, hii ilimaanisha taasisi ya Urais ilikuwa inajua misheni hizo, hivyo hakupaswa ajitetee kuwa alitumwa na Rais kufanya Uhalifu kwani Kwa kufanya hivyo anamdhalilisha Hayatti Magufuli na Taasisi ya Urais ya wakati huo.

Kama ni kweli alitumwa, basi angekaa kimya na kujitetea Kwa namna zingine, alafu Kwa vile alitumwa na taasisi ya Urais, basi mabosi wake Kwa vile wengine wapo na wanatambua misheni hiyo, wangetafuta namna ya kumnasua.
Lakini sio kuwataja, Kwa kuwataja ni tayari ameshavujisha Siri pasipo yeye kujua.

Sabaya pasipo kujua, kauli yake unazidi kuwapa nguvu Wale wote waliokuwa wakiituhumu serikali na watu wasiojulikana.

Kwa kifupi, Sabaya amekosa Weledi.

Hata Kama akitoka basi tayari ameshavujisha Siri za wakubwa wake, na Hana sifa za kuwa mtu wa vitengo Kwa mambo ya kiusalama.

Ilimpasa afe kiume. Akaze Tai shingoni.Mabosi zake ndio wamnasue.
Lakini utetezi wake bado unamuweka pagumu zaidi.

Robert Heriel

mfumo uliomtuma ndio uliomshitaki wamemwaga mboga yye kaamua kumwaga ugari
 
... Sabaya kuwemo kwenye Mfumo wa ujasusi wa nchi hii haina mashaka! Toka enzi akiwa mtoto UVCCM aliwahi kukutwa na kitambulisho cha TISS kesi ikafunguliwa. Alivyoachiwa ni mamlaka yake ya uteuzi pekee ndio inajua.

In short, ameandaliwa kwa kazi maalum long time so yanayotokea kwenye sakata hili ni long time plan. Alichokisema mahakamani ni sahihi kabisa.
Hilo lisiwe na mashaka sawa,je kwa kulisema mahakaman litamsaidia???
Kaambiwa ana case ya kujibu,hilo linajibu kwa kumuokoa?
 
Yaani ati umetumwa kuua alafu unakamatwa unasema nimetumwa kuua. Hivi hata mtoto mdogo si atakushangaa Kwa ujinga.

Hata Kama umetumwa kazi na mkuu wako, ukaioa jina kazi maalumu na ambayo kimsingi huenda ni Uhalifu lazima utumie akili kuitenda, na ukishikwa utakayewajibika ni wewe 100% .

Sasa hawa ndugu zetu wanakuambia Kwa vile katumwa ataachiwa, inashangaza kweli
Hata kama alitumwa sidhani kama mamlaka ilimtuma kuuwa ama kujeruhi pengine alitumwa kweli ku deal na wahujumu uchumi.......
kupitia mfumo usio rasmi sema yeye alijuongeza negatively.....
 
Mnachukua UVCCM mnawajaza kwenye nafasi nyeti kwa kutumia nguvu za kikatiba kwa Raisi ambaye ni mwenyekiti wa chama automatically inadhoofisha nguvu kwa taasisi nyeti kwa sababu kuna watu wanaoteuliwa sio kwa weledi na uzoefu walionao pata picha huyo ndio jasusi katumwa China halafu kakamatwa nini kitatokea au katumwa Marekani kwenda kubargain Mikataba nyeti nini kitatokea
KATIBA MPYA ni muhimu kuondoa huu upuuzi kwanza sioni logic ya kuwa na mwenyekiti wa ulinzi na usalama anayetokana na mfumo wa kisiasa hao maDC na maRC wangebaki kuwa makada wa chama tu hivyo vyeo havina tija kwa wakati huu wa vyama vingi na Demokrasia
 
Back
Top Bottom