Uteuzi Julai 2, 2024: Kidata aondolewa TRA, Jafo na Ashatu wabadilishana Wizara

Uteuzi Julai 2, 2024: Kidata aondolewa TRA, Jafo na Ashatu wabadilishana Wizara

Nchi zote zenye sheria kali za ubadhirifu, rushwa na wizi wa mali za Serikali na umma zina maendeleo yanayoonekana. Mfano mmoja mzuri ni China.

Tanzania tutabadilishana mpaka kufa, bila sheria kali za kuuwa wabadhirifu, wala na watowa rushwa, maendeleo ya haraka tuyaone kwenye TV tu.
 
Kariakoo si issue iliyomuondoa. Mambo ya Kariakoo mbona yashazoeleka?

Issue iliyomuondoa ni barua ya mabalozi wakilalamikia kodi.
Mabalozi hawatakiwi kulipa kodi? Walitozwa kodi zilizo nje ya mfumo wa sheria?
 
AMeisha tengeneza headline ya wiki hii yote ukijumlisha na usajiri wa Chama kazi kwisha, wajinga watajdili wiki nzima wakati huo inatafutwa headline ya next week, Kawatengenewa wajinga wa Taifa hili Mada ya wiki. Wajinga hawatakaa wajadili mambo serious ya hili Taifa.

Maka anajua sana kucheza na akili za wajinga wa hili Taifa.
Hapana, ujinga upo naturally tu hauhitaji kupewa story hata kama haya matukio yasingetokea bado wajinga wasingejadili mambo serious.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa illyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-

Mhe. Dkt. Selemani Said Jafo (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Jafo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Kijaji alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.


Mhandisi Yahya Ismail Samamba ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara va Madini. Kabla ya uteuzi huu, Mhandisi Samamba alikuwa Katibu Mendaji wa Tume ya Madini. Mhandisi Samamba anachukua nafasi ya Bw. Kheri Abdul Mahimbali ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Bw. Yusuph Juma Mwenda ameteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mwenda alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).

Bw. Alphayo Japan Kidata ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais, Ofisi ya Rais - Ikulu. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Kidata alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)


Mwigulu na bashe bado wapo upuuzi mtupu!
 
Mna uhakika mama yupo humu jamiiforum?
Mbona mpaka sasa Lucas wangu hajatajwa🤔
Lucas yupo kamati ya mapambio na usifiaji inayofanya kazi moja kwa moja na kamati ya tiba asili na kafara.

Siku ikihitajika kafara ya mtu kwa mizimu ya kipemba, watampeleka Lucas. Hivyo usihofu yupo kitengo salama.

Tusubiri uzi mrefu tu wa machozi ya furaha ya raia kwa teuzi na tenguzi alizofanya mama.
 
Mwenda ni mtoza ushuru aka Zakayo.
Kazi za akina Zakayo tokea enzi na enzi ni za lawama,licha ya kuwa ni muhimu kukusanya fedha za kuendesha nchi.
Na ni vigumu akina Zakayo kuwa na mikono safi may be one in thousands
Labda washuke chini kutoka juu ya mkuyu kitu ambacho sio rahisi ni kigumu sababu vishawishi,matamanio
ni vingi mno.
 
Hili si tatizo; kila Mzanzibari ni Mtanzania japo siyo kila Mtanzania ni Mzanzibari. Hivyo, Mzanzibari kama Mtanzania mwingine ana haki sawa na Mnyakyusa toka Katumba Songwe.
Halikuwa tatizo lakini siku hizi limekuwa tatizo!

Wazanzibar tena Wabunge walioapa kwa katiba ya Tanzania wanapokana Utanzania ni tatizo.
Watu wanaoweza kuukana Utanzania kwasababu ni Wazanzibar wakatuacha na Utanzania wetu unawezaje kuwaamini katika masilahi ya Tanzania wakiwa wameubeba Uzanzibar Bora kwanza! uchungu wa Tanzania wanaupata wapi!

Kisheria si tatizo, lakini kwavile kuna Uzanzibar hatuwezi kukwepa kama tatizo.
 
Back
Top Bottom