Uteuzi Julai 2, 2024: Kidata aondolewa TRA, Jafo na Ashatu wabadilishana Wizara

Uteuzi Julai 2, 2024: Kidata aondolewa TRA, Jafo na Ashatu wabadilishana Wizara

Anatokea Zanzibar. Kwasabb kwa shèria za Zanzibar hairuhusiwi mtanganyika kufanya kazi Zanzibar.

Kama unakumbuka hata Charles Hilary afisa mawasiliano ikulu alikiri kuwa mzazi wake mmoja ni mzanzibari ndiyo maana kateuliwa.
Hapa pana mkanganyiko/mashaka matupu
 
Wamefaulu kushuka zengwe na Kidata kuondolewa.

Mimi nasubiria mwenendo wa makusanyo TRA
Nani alikwambia kuwa hicho ni kigezo cha kukaa hapo?? Kuna mambo mengi sana, kwenye teuzi hizi, unaweza kuwa unakusanya kidogo sana lakini kuna sehemu wakubwa wanafaidika na wewe, utakaa hapo miaka na miaka, hata hatuelewi tunataka nini hasa
 
Ndiyo ujue hata hizo record za makusanyo makubwa ni kanyaboya tu asingeondolewa mtu mwenye ufanisi wote ule
 
Kidata hana shida, shida ipo kwa ma deputy commissioners wanaodili na Divisions, natarajia kuona deputy commissioners na mameneja wa hizi divisions wakijiuzulu hawa ndio wanaom lostisha commissioner
Deputy Commissioners waondolewe faster kurekebisha hali. Na ifuatiwe na mabadiliko ya sheria za kodi na haya matozo
 
Huyu ni balozi pia kwa cheo chake hapo ikulu amekulia sana sema upigaji hata jpm alimtimua na kumvua ubalozi ndio maana anaitwa kidata tu kama amedata vile

USSR
Mbona watu wa mkoa wa Mara ni wapigaji sana japokuwa ni watendaji wazuri pia.
 
Rais wa Zanzibar anaweza kupigwa makofi na kuondolewa ofisini na Rais wa Tanzania. Sasa utajaza kwa upande wa mteuliwa wake.
Kwa maneno mengine Rais wa Zanzibar ni sawa na RC wa Katavi, isipokuwa kwenye neno RC wakaweka Rais.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa illyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-

Mhe. Dkt. Selemani Said Jafo (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Jafo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Kijaji alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.


Mhandisi Yahya Ismail Samamba ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara va Madini. Kabla ya uteuzi huu, Mhandisi Samamba alikuwa Katibu Mendaji wa Tume ya Madini. Mhandisi Samamba anachukua nafasi ya Bw. Kheri Abdul Mahimbali ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Bw. Yusuph Juma Mwenda ameteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mwenda alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).

Bw. Alphayo Japan Kidata ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais, Ofisi ya Rais - Ikulu. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Kidata alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)


Huyu Yusuph Mwenda Hajawahi kuwa Diwani au Meya kwenye Manispaa ya Kinondoni?Au ni majina TU?
 
TRA awabuni mbinu za kodi wala hawana mamlaka hayo.

TRA jukumu lao nii wakusanya kodi tu; kwa mujibu wa sheria zilizopo.

Anae amua kodi ni waziri wa fedha
Hizo sheria unafikiri TRA hawashirikishwi?

Wao ndio wanakuwa field huko kwenye kodi sasa kama hawezi hata kushauri mpaka watu wanagoma kazi yake nini pale?
 
That’s not how a country is run, it’s just stupidity ni kama vlle nchi aina usalama wa ‘civil service’ just pathetic.

Yaani raisi alee wakwepa kodi kulinda maslahi yake na civil services ikae kimya.

Hakuna usalama wa taifa hapo bali jopo la wajinga tu
Huyu comm mpya katumwa kilea wakwepa kodi?
 
Back
Top Bottom