Pre GE2025 Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa tenguzi hizi mbili, naona mwisho mbaya wa Mh. Samia 2025
Hawa watataftiwa kazi nyengineo, mama kashtuka na wao wanautaka urais angali yeye nae keshanogewa nao, anaona awapumzishe kwanza wasije kumpiku 2025, ila pia asipo wapa kitengo ndo mwanzo wa uhasama na watu hawa wawili, na watamvuruga sana kichwa mpaka kufika ,2025
 
Ni ngumu sana wao kufanya kama walivyofanya kwa Magu. Mbinu zao zinajulikana zote. Hawawezi kumvuruga mtu yoyote akili. Zaidi kama wanabusara, watulizane tu. Wasitumie mitandao kumchafua yoyote, wala wasifanye mbinu chafu kwenye chama. Hapa wanaweza kulainisha watu.

Wananishangaza kweli hawa wakaka.. mitaani kwa vijana waliowengi, hawakubaliki! Kama hapa mama kajizolea point za kutosha kutoka kwa watu waliokuwa hawamkubali, kisa hawa vijana. Kazi wanayo kubwa wao kurudi tena kwenye uWaziri. Na nje ya uWaziri, maisha yao huwa hayana relevance yoyote.
 
Mzee malope alipo fariki JPM ghafla alikua na furaha sasa naona leo atakua hajalala haamini kilicho tokea.Ila Maza ni noma kapiga pale pale kwenye mshono.Bado wawili yule somalia boy na mzee wa tozo hao wakitinduliwa kweli mama atakua kaamua kufanya kazi.
 
Kweli siasa hazina rafiki wa kudumu. Lakini acha watoane manundu, watasaidia kujenga upinzani wa kweli kama baadhi yao wataamua kuondoka CCM.

Wakati wakiandamwa na Magufuli, Samia alikuwa anashinda kutwa nzima na January akilewa na kuvuta sigara zake.

Samia alikuwa na hali ngumu mpaka akafanya aliyoyafanya na Makonda. Magufuli alijua kuwa kuwa January ndiye alikuwa mtunza siri mkubwa wa Samia na ndo sababu ya kumtoa kwenye baraza wakati huo.

Chuki anayoijenga dhidi ya January kwa kuogopa uchaguzi wa 2025 itamtengeneza Magufuli mwingine. Hakuna mtu yoyote ndani ya CCM aliyeamini kuwa Magufuli angekuwa rais 2015 mbali na mtandao wa Kikwete na Lowassa kutumia mabilioni kumuandama toka 2005.

Siasa ni kuvumilia hata wale usiokubaliana nao kama Mkapa alivyofanya kwa Kikwete na Kikwete akafanya kwa Magufuli. Ikitokea January akiupata urais siku moja, sina hakika watoto wa Samia wataendelea kuishi nchi ukizingatia wizi walioufanya.

Tujifunze namna Magufuli alivyomtendea Kikwete na watu wengine kutokana na hasira yake kwa waliomsulubu. Tusubiri, tuone.
 
Serikali kumbe sometmes haina dhamira ya dhati,au tuseme uchawi upo, Jery silaa unamtoaje wizara ya ardhi wakati alikuwa anafanya vizuri zaidi!!? Au ndio matapeli wameenda kuroga ahamishwe wizara au atenguliwe!!! Kweli uchawi upooooo
Slaa ametolewa dhahiri ni wenye pesa wamefanya yao,sio bure.

Kwa mwendo wa slaaa waliona ataenda fukua fukua kila mahali
 
Mzee wa goli la mkono alijisahau sana kamponza Byabato, eti "Nitakufundisha jinsi ya kuiba kura" 🀣 🀣 🀣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…