Pre GE2025 Uteuzi na Utenguzi unaofanywa na Samia ni mbwembwe tu za Madaraka

Pre GE2025 Uteuzi na Utenguzi unaofanywa na Samia ni mbwembwe tu za Madaraka

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kuna kila sababu ya kumsaidia Samia kwa kuwa ameonyesha hafahamu nini anataka au anataka kutupeleka wapi!

Samia ni hasara kwa ustawi wa Taifa!
 
Toka maktaba :
leo Januari 10, 2022,



lukuvi-pic-data.jpg

Bungeni Habari Siasa Zetu

Kabudi, Lukuvi wapewa nafasi Nyeti Ikulu​

3 years ago
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema katika Baraza Jipya la Mawaziri ameamua kuwaacha kando Prof, Palamagamba Aidan Kabudi na William Lukuvi kwa ajili ya kumsaidia kazi maalumu Ikulu.
Rais Samia ameyasema hayo leo Januari 10, 2022, katika uapisho wa mawaziri na manaibu waziri wateule aliowateua mwisho wa Juma lilipota akifanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.

Rais samia amesema kuwa wawili hao, kutokana na umri na busara zao ameona wanafaa kuwa washauri kwa viongozi vijana walioteuliwa na kumsaidia kufanya maamuzi ya Ikulu.

“Nimeshasikia jumbe mbalimbali zinawachoma huko hawa kaka zangu kuwa ooh wameachwa, hawafai, Hapana! Hawa wamekaa muda mrefu kwenye Baraza na wanajua kila eneo, hivyo nimeamua kuwapa kazi ya kuja kwangu kuwasimamia nyie vizuri,” alisema.

“Kakaangu Kabudi amefanya kazi nzuri sana ya kusimamia Serikali na Mashirika, na ndio kazi ambayo nataka nimkabidhi sasa kindakindaki aendelee n kazi hiyo. Ila kazi yake kwa sababu haiko kwenye Muundo haitangazwi wala nini lakini atasimamia hiyo kazi. Mashirika yote na kazi zote zitakazoingia ubia na Serikali Kabudi ataongoza hiyo timu. Kwa hiyo yeye ni baba mikataba.” Aliongeza Rais Samia.

Aidha amesema kuwa Lukuvi ana kazi maalumu Ikulu ambayo kwa sasa hakuitaja na akiufahamisha umma kuwa itafahika baadae.

“Wengine wameanza kumletea meseji za ajabu ajabu wakidhani atagombania uspika, hatagombania! Ana kazi na mimi kwa hiyo hatakuwa spika wala hatagombania, msianze kumchafua. Ametumikia nchi hii kwa mda mrefu na kwa uadilifu msianze kumchafua muache aende na mimi tumalize kazi tutakayompangia.” Alisema Rais Samia Suluhu Hassan


View: https://m.youtube.com/watch?v=dcWkS3YpWAs
 
Nia ni kutuzuga tu
Ni kwamba hajui nini la kufanya wala watu sahihi wa kufanya kazi gani! Katika zama hizi unamfanya mwalimu kuwa Waziri wa Afya unategemea nini! Huyu mwalimu atateua watu aina gani kuambatana naye kwenye mikutano ya WHO!
 
Huwa wanasema Mbowe kakaa sana Chadema apishe damu changa. Akina Kabudi na Lukuvi wa nini tangu TANU!
Na utakuta huyo huyo aliyepigwa chini jana, kesho tena utasikia ni waziri, yaani hata huelewi kinachotakiwa nini!! Ila kama hujui uendako huwezi potea
 
Sasa ukiangalia ni lipi la maana anafanya!! Au mama wa ngekewa(mhagama) huwa hata sielewi anafanya nini lakininpanga pangua yumo tu
Ana Mjomba wake ni Chifu kule Songea,alikuwa Bungeni amevaa mangozi ya chui🤣🤣🤣
Mkuu watu wamejipanga!
 
Tumeona kila mara anateua na kutengua! Wale wale aliowatengua anawateua tena na kuwatengua tena. Kwa kiingereza ana recycle watu wake bila kuwapa elimu wala semina elekezi.

Anachofanya Samia ni kuonyesha nguvu na madaraka aliyonayo kikatiba. Madaraka na nguvu za Rais ndicho anaonyesha. Kama alivyowahi kusema yeye ni Rais mwenye jinsia ya kike! Kwa hiyo anaonyesha namna Rais wa jinsia ya kike anavyoweza kutelekeza madaraka na nguvu yake kama Rais wa kike! Anateua na kutengua kama anabadilisha mavazi.

Kuteua na kutengua anakofanya Samia si kwa lengo la kuongeza ufanisi serikalini au kuleta mabadiliko ya kiutendaji serikalini, bali kuonyesha nguvu na madaraka ya Rais mwanamke!

Badala ya teuzi na tengua zake kuleta maendeleo kwa Taifa zinaleta hasara na kudidimiza maendeleo ya nchi! Tangu aingie madarakani kwa kudra ya Mwenyezi Mungu teuzi na tengua zake zimegharimu Serikali mabilioni ya fedha ambazo zingeweza kujenga shule, zahanati, barabara na miradi kadha wa kadha!

Mungu ibariki Tanzania!

PIA SOMA
- News Alert: - Uteuzi Agosti 14, 2024: Rais Samia kafanya uteuzi, utenguzi na uhamisho wa viongozi mbalimbali
Hii inferiority complex ni ya mwandishi wa huu uzi. Hajiulizi kwa kina ni kwanini anatengua na kuteua wala hatafuti sababu za kitaalam za kwanini teuzi zifanyike mara kwa mara anakimbilia kuja na hoja za kejeli kwa maamuzi ya kikatiba.
 
Alivyomteua yule fala aliyeandaa mkataba wa kuuza nchi kwa DP World kuwa AG,aisee nimecheka.
This man Hamza Johari!!!!
Nchi inaliwa na sasa hivi anakwenda kuhakikisha vikwazo vyote vilivyokuwa kero kwa DP vinaondolewa!
 
Alivyomteua yule fala aliyeandaa mkataba wa kuuza nchi kwa DP World kuwa AG,aisee nimecheka.
This man Hamza Johari!!!!
Hamza Johari kaandaa mikataba mingi sana ya kiserikali kuanzia miaka ile ya 2015 alipoteuliwa na JPM kuwa mkurugenzi wa TCAA, ni mmoja wa wanasheria vichwa sana waliopo hivi sasa hapa Tanzania.

Mkataba wa DP World umeleta ufanisi mkubwa pale TPA hakuna tena magumashi wala upigaji wenye uhusiano na vyeo vya serikalini.
 
Salaam, Shalom!!

HAKIKA ushindi wa Rais mpya wa TLS ndugu na Nabii Mwabukusi umetikisa mamlaka na sasa zinahaha na kupeleka kuwarudisha Ofisini manguli Hawa wawili waliokuwa wamefichwa Ili kujaribu Kupambana vita ya kisheria bungeni na mahakamani Ili kuiokoa Serikali na kushindwa Kwa HOJA.

HAKI za watanganyika, Watanzania zimepata mtetezi sahihi, hivyo, tumuombee mtu huyu Ili alete mabadiliko tunayoyatarajia watanganyika ndani ya Muungano.

Swali: Je ni Kweli, Ushindi wa Nabii Mwabukusi Kwa nafasi ya Rais wa TLS ndio chanzo Cha kurudi Kwa Prof Kabudi kwenye Uwaziri wa KATIBA na Sheria na Ndugu Kabudi Kwa nafasi ya Waziri Sera na Bunge?

Mungu ibariki Tanganyika,

Mungu ibariki TLS, Mbariki pia Nabii Mwabukusi.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿.

Karibuni 🙏
Mwabukusi huyu huyu Kajunjumele ninayemfahamu?
Zero.
 
Tumeona kila mara anateua na kutengua! Wale wale aliowatengua anawateua tena na kuwatengua tena. Kwa kiingereza ana recycle watu wake bila kuwapa elimu wala semina elekezi.

Anachofanya Samia ni kuonyesha nguvu na madaraka aliyonayo kikatiba. Madaraka na nguvu za Rais ndicho anaonyesha. Kama alivyowahi kusema yeye ni Rais mwenye jinsia ya kike! Kwa hiyo anaonyesha namna Rais wa jinsia ya kike anavyoweza kutelekeza madaraka na nguvu yake kama Rais wa kike! Anateua na kutengua kama anabadilisha mavazi.

Kuteua na kutengua anakofanya Samia si kwa lengo la kuongeza ufanisi serikalini au kuleta mabadiliko ya kiutendaji serikalini, bali kuonyesha nguvu na madaraka ya Rais mwanamke!

Badala ya teuzi na tengua zake kuleta maendeleo kwa Taifa zinaleta hasara na kudidimiza maendeleo ya nchi! Tangu aingie madarakani kwa kudra ya Mwenyezi Mungu teuzi na tengua zake zimegharimu Serikali mabilioni ya fedha ambazo zingeweza kujenga shule, zahanati, barabara na miradi kadha wa kadha!

Mungu ibariki Tanzania!

PIA SOMA
- News Alert: - Uteuzi Agosti 14, 2024: Rais Samia kafanya uteuzi, utenguzi na uhamisho wa viongozi mbalimbali
Mchezo wa Draft, kusukuma kete hii hapa na ile kule, kisha unadai umeshinda, loh!
 
Nchi inaliwa na sasa hivi anakwenda kuhakikisha vikwazo vyote vilivyokuwa kero kwa DP vinaondolewa!
Tupunguze hizi negativity za kipuuzi. Hamza ni mwanasheria makini sana kwanza alipigania serikali ikashinda kesi ya Ziwa Malawi.

Pili kapigania shirika la mafuta kiasi kwamba serikali imepewa mkataba mzuri. Akapigania maslahi ya kimkataba kati ya serikali na DPW na tumepata mkataba mzuri ambao unaongeza mapato kule TPA.

Samia kumpa uanasheria mkuu ni baada ya kuifahamu kazi yake vilivyo kuanzia mwaka ule wa 2015 mpaka leo. SSH sio mjinga pengine sisi tunaodhani kuwa yeye ni mjinga ndio wajinga wenyewe.
 
Si mbwembwe ndugu, ni hofu ya 2025 anajaribu kubalance makundi yote ndani ya chama ili ajiweke vizuri na akubalike kwa walau 75% ndani ya chama.
Wewe ulijua kwamba wazee hao 2 watarudi baada ya kutoswa kwa wale vijana 2.
 
Hii inferiority complex ni ya mwandishi wa huu uzi. Hajiulizi kwa kina ni kwanini anatengua na kuteua wala hatafuti sababu za kitaalam za kwanini teuzi zifanyike mara kwa mara anakimbilia kuja na hoja za kejeli kwa maamuzi ya kikatiba.
Hakuna utaalamu wo wote bali ni kuogopa kivuli chake mwenyewe! Hivi kwa D zako mbili ulizopata kuna utaalamu wa kumfukuza kazi mtu na baadaye kumrudisha bila maelezo ya kutosha tena kwenye nafasi ya kisiasa!

Inferiority complex unayo wewe kukubali ujinga wa wazi kwa kivuli cha katiba!
 
Tupunguze hizi negativity za kipuuzi. Hamza ni mwanasheria makini sana kwanza alipigania serikali ikashinda kesi ya Ziwa Malawi.

Pili kapigania shirika la mafuta kiasi kwamba serikali imepewa mkataba mzuri. Akapigania maslahi ya kimkataba kati ya serikali na DPW na tumepata mkataba mzuri ambao unaongeza mapato kule TPA.

Samia kumpa uanasheria mkuu ni baada ya kuifahamu kazi yake vilivyo kuanzia mwaka ule wa 2015 mpaka leo. SSH sio mjinga pengine sisi tunaodhani kuwa yeye ni mjinga ndio wajinga wenyewe.
Acha kujipotosha! Mkataba umepingwa na wanasheria wote nguli wa nchi hii pamoja na TLS iliyokuwa chini ya chawa wake kasoro yeye, huoni walakini hapo?
 
Back
Top Bottom