Uteuzi: Rais Samia, afanya uteuzi wa Makamishna wa Jeshi la Polisi Desemba 9, 2024

Uteuzi: Rais Samia, afanya uteuzi wa Makamishna wa Jeshi la Polisi Desemba 9, 2024

Watu walimtabiria Suzana makubwa sana ile position ya Mkuu wa kazi ila kuna watu walikataa humu humu kuna thread fulani hivi hatimaye yametimia.
Waliomkataa walisemaje changamoto zake.? Mnoko au ni mkimbizi? Au ana misimamo conservative? Au wivu kwa sababu ana akili mingi? Au mbinafsi anachukia wanachofanya wenzake ila yeye akifanya kitu hicho hicho ni sawa?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa Makamishna wa Jeshi la Polisi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo ni kama ifuatavyo:

Soma Pia: Rais Samia afanya uteuzi: Masauni aondolewa Wizara ya Mambo ya ndani, Kabudi apelekwa Wizara ya Habari na Michezo, Janabi kuwa mshauri wa Rais

  1. Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Kombo Khamis Kombo amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar. Atachukua nafasi ya CP. Hamad Khamis Hamad, ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.
  2. Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Tatu Rashid Jumbe amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuwa Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu katika Jeshi la Polisi. Atachukua nafasi ya CP. Suzan Kaganda, ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.
Wananchi wanatekwa na kuuawa.
Mama yupo bize kuteua watu huku akiwaacha wahuni kwenye nafasi zao
 
Hiyo nafasi ya Kamishina wa Utawala na Menejiment ya rasililimali watu ndani ya Jeshi la Polisi uteuzi wake huwa unafanywa na rais? Au mimi ndiye mgeni wa mambo yenu huko mjini?
Rais huwa anateua IGP naibu na wale CP's so inawezekana,na hata hvyo ye ni amiri jeshi mkuu kumbuka.
 
Hakuna mtu aliyewahi kupata urais WA Bure duniani kama Saa100.
Ila anauchezea sana na hajielewi hata kidogo.
Uteuzi Kila siku ,bila kujali gharama za uteuzi huo.
 
Ukiwa Rais kwenye nchi kama Tanzania, unakuwa huna tofauti na mtawala wa kifalme wa Ulaya kipindi cha mfumo wa Unyonyaji. Yaani unakuwa na mamlaka makubwa na pia nguvu za ajabu mpaka inasikitisha.
Ndio maana Mimi siku zote huwa naamini hili taifa hili lisonge mbele kutoka hapa lililopo, labda siku limpate kiongozi mwenye huruma na Nia ya dhati ya kuliongoza taifa hili katika uelekeo chanya, kitu ambacho hakiwezi kutokea afrika hapa.... Hapa viongozi wanapatikana ni WEZI na walafi wanaopenda kuishi kifalme
 
Back
Top Bottom