Uteuzi: Rais Samia, afanya uteuzi wa Makamishna wa Jeshi la Polisi Desemba 9, 2024

Uteuzi: Rais Samia, afanya uteuzi wa Makamishna wa Jeshi la Polisi Desemba 9, 2024

Oooh kumbe ni auto-correction, hapo sawa. Huwa nakereka tu ule ujinga wa kutokujua hata kuandika sawasawa halafu mtu akajifanya ni mwerevu wa mambo mazito zaidi.

Tukirudi katika huo uteuzi wa mara kwa mara unaoungelea ... sasa nikuulize kwanini raisi alipewa fursa hiyo ya kuteua na sio watu kugombania hizo nafasi? Obviously ni nafasi za utekelezaji kulingana na muongozo wa kile kinachosimamiwa na Raisi. Ikiwa hivyo ndivyo basi ana haki ya kuteua na kutengua hata kila wiki ikiwa yule aliyehisi atamfaa kufanya hiyo kazi hajafikia mategemeo yake, ama labda ameona anaweza kumsaidia zaidi kwenye nafasi nyengine.

Loyalty ni muhimu sana kwa nafasi za kuteuliwa otherwise kama mtu haamini katika kile alichotumwa basi ajiuzulu.
Kutengua, kuteua, unasema ana haki. Wateuliwa wana haki kupewa muda sababu, kuangalia track records zao. Niambie kosa la Slaa, Lukuvi, Kabudi, Kalemani kwenye wizara zao.
 
Kutengua, kuteua, unasema ana haki. Wateuliwa wana haki kupewa muda sababu, kuangalia track records zao. Niambie kosa la Slaa, Lukuvi, Kabudi, Kalemani kwenye wizara zao.
Sasa unaniuliza mimi kwani mi ndo nilowatengua? ... mbona kama una makasiriko kamanda?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa Makamishna wa Jeshi la Polisi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo ni kama ifuatavyo:

Soma Pia: Rais Samia afanya uteuzi: Masauni aondolewa Wizara ya Mambo ya ndani, Kabudi apelekwa Wizara ya Habari na Michezo, Janabi kuwa mshauri wa Rais

  1. Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Kombo Khamis Kombo amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar. Atachukua nafasi ya CP. Hamad Khamis Hamad, ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.
  2. Naibu Kamishna wa Polisi DCP. Tatu Rashid Jumbe amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuwa Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu katika Jeshi la Polisi. Atachukua nafasi ya CP. Suzan Kaganda, ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.
Screenshot_20241209-124302~2.jpg
 
Back
Top Bottom