UTEUZI: Rais Samia Amteua na kumuapisha Mwigulu Nchemba kuwa mjumbe tume ya mipango

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?

Mwigulu Nchemba ateuliwa na Rais Samia kuwa mjumbe tume ya mipango

Taarifa kamili hapo chini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 29 Mei, 2024. Lengo la Tume hii ni kusimamia uchumi, mchakato wa upangaji na utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Taifa.



Soma pia: Dkt Mwigulu Nchemba ameteuliwa kwa mujibu wa Sheria namba 5(1) (b)
 
Waziri wa fedha tena awe kwenye mipango, kunahitaji checks and balance katika utendaji.
 
Kwa nafasi yake mpya, ina maana nafasi yake ya Uwaziri imetamatika?

Au anaendelea nao?
 
Hivi huyu witch wake awe anamlipa sana. Au anawagawia sana wanaomteua?. Kwa utendaji upi ndugu zangu?. Hii nchi kweli ni yale yale aliyoongea mzee Jomo Kenyata. Hii nchi Ukute kweli akaja kuwa presderrr?
Na haishindikani unafikiri? Ni basi tu yani
 
Na haishindikani unafikiri? Ni basi tu yani
Simkubali hata nusu huyu njemba. Huyu ni sehemu ya muendelezo wa waTZ kuishi maisha magumu. Hana aibu huyu njemba. Aliwahi sema waTz wanataka tozo. Huyu ndio chanzo cha TRA kufirisi watu kwa sasa. Huyu kaweka tozo tena kwenye mabank. Ukitoa tu elfu 35000 cash unakatwa 351. Huyu anaamini kuvuna asipopanda. Kukamua ng'ombe asiemlisha. Huyu anaamini chanzo cha mapato ya serikali ni kuwarundikia kodi waTz,kuwafukalisha huku yeye akineemeka. Hii nchi kweli ya kuionea huruma
 
Party after Party...., Bumper to Bumper
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…