UTEUZI: Rais Samia ateua Majaji wa Mahakama Kuu

Mbona wengi Sana ,hii imekaaje nyie Wanasheria Wasomi?
kwa maoni yangu hao ni wachache sana ukilinganusha na mahakama zilizopo nchi nzima.
hao Majaji wanapaswa wapangiwe mikoani, haswa Mikoa ya pembezoni ambayo ndio inaupungufu, sio kujazana Dsm, mwanza, arusha, wapelekwe mikoani wakahudumie wananchi.
 
kwa maoni yangu hao ni wachache sana ukilinganusha na mahakama zilizopo nchi nzima.
hao Majaji wanapaswa wapangiwe mikoani, haswa Mikoa ya pembezoni ambayo ndio inaupungufu, sio kujazana Dsm, mwanza, arusha, wapelekwe mikoani wakahudumie wananchi.
Ila kweli aisee maana jamaa wanazidiwa kiasi Kwamba Huwa wanapiga Kazi hadi huruma..

Serikali iongese wengine hususani wa ngazi za chini.
 
Point yako ya nne, kama unazungumzia Waislam wapo 9 kati ya 22. My God nchi inanuka udini hiii
 
Ni mwanenu ndio
 
Wee jamaa nakupinga 100% hivi chukulia mkeo watoto zako wadogo zako wazazi wako wazazi wa mke wadogo wa mk kwa kifupi familia yote wapo nyumban kwako kuna wagonjwa kuna uhahaba wa chakula unaweza kuwaambia ngojeeni nirelax kwanza😂
Hyo sio position ya nirelax mzee,position ya maamuzi magumu muda wote kwa watendaji wako,you anapumzka muda mwingi mbona..ushawahi mkuta anakaa foleni ya barabarani au foleni yoyoyte ya kusubilia kitu
 
Imagine huyo Zuhura anapost vitu saa nane usiku halafu asubuhi saa 7:30 am yupo ofisini!! Pathetic!
Mnastaajabisha sana ninyi!!! Ukisimama nchale ukikimbia nchale ukinyoosha mikono juu rungu! Khaa!
 
Pongeze kwa wote walioteuliwa kuwa majaji.
Ushauri
1).Mchakato wake uwe wazi kwa wadau wote kuepusha manung'uniko Kuna wasajili wa Mahakama au manaibu wasajili wa Mahakama, ambao wamefanya kazi miaka mingi bila kula shavu,
2).Tume ya Mahakama ifanye kazi kwa weledi na bila upendeleo, vigezo na masharti yazingatiwe.
 
Halafu ukiwasikiliza kwa namna fulani wanavyotamka kuwa hawalali huona kama sifa lakini kwa wenye akili hii sio sifa,
Wana tuchosha tu hawa watu, angalia huu mfano, yule sheikh anayeswalisha au kuita adhana kwa mtu asiyefahamu anaweza dhani huwa halali, kisa muda mwingi anashinda msikitini, NO!.

Anapata muda mwingi na mzuri wa kulala (kupumzika) hata kufanya kazi, sema anapanga ratiba yake kwa uzuri, ndivyo hawa wanasiasa wanatuchezea hapa.

Anafanya mambo yake mchana then anampa mtoa habari karatasi anaambiwa itoe usiku wakiwa wamelala ionekane tupo busy masaa yote.

✍🏾 Naendelea kujifunza tabia ya binadamu.
 
Mkuu na wewe utakuwa umechoka unahitaji kupumzika! Hiyo date unahamasishwa kujiandaa kuhesabiwa! Tarehe ya tangazo ni 6 August 2022 iko hapo juu kabisa upande wa kushoto!
Sasa si mpàka uambiwe Kama wewe ulivyoniambia sasa
 
Sisi kama Taifa tuna cha kujifunza kutoka kwa majirani zetu Kenya namna nzuri ya kupata majaji. Hawa wa kwetu ni majaji wa mwendo kasi! Nao wanafika mahali wanakula rushwa!!
Majaji wa UPE voda faster
 
Na pia huwa wanafanya kazi za majaji pale mahakama kuu. Nimeshuhudia kesi yangu moja ilisikilizwa na msajili wa mahakama! Ila hawako competent kama majaji!
Halafu alisaini hukumu Kama Hakimu/ Jaji? Au Msajiri?
 
"Pascal acha kuhoji muda wa uteuzi wa Mwenyekiti wetu,fomu yako ya lile jambo lako tunayo",alisikika kada mmoja wa Chama Twawala,akionya!🤣
 
Kweli hata mimi nimeona majaji wakristo ni wengi kwenye huu mkeka
 
Point yako ya nne, kama unazungumzia Waislam wapo 9 kati ya 22. My God nchi inanuka udini hiii
mara zote nimekuwa nikihubiri "uwiano" ili kujenga umoja thabiti wa Taifa letu, ni jambo la hatari sana kulundika aina mmoja ya watu katika taasisi ya Serikali...jambo hilo halina afya kwa Mustakabali wa Nchi yetu hata kidogo.
tunawarithisha "tatizo" kizazi chetu, "tatizo" ambalo huenda linaweza kuja kulibomoa Taifa letu, hatutaki lije litokee hilo.

kwa sasa kinacho saidia ni uvumilivu lakini hatujui kizazi kijacho kama kitaweza kuvumilia.

hivyo nashauri mamlaka zizingatie UWIANO kwa lengo la kuimarisha umoja wenye nguvu kwa Taifa letu, vinginevyo tunatengeneza tatizo kubwa siku zijazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…