Uteuzi wa Biswalo Mganga kuwa Jaji wa Mahakama kuu kupingwa Mahakamani, Yadaiwa hana Maadili, zuio la kuapishwa kwake laandaliwa

Hivi Huwa mkimbizi anajihusishaje na mambo ya nchi yake?mie sijaelewa kabisa.naomba kuelewa
 
Tumeanza maandamo hapa
 
Lema bana,eti kaagiza mawakili wake wazuie uapisho wa jaji
Mtu akisheteuliwa kuwa jaji,ni kamati zao tu za kimaadili zinaweza kupendekeza atenguliwe,sio mahakama
Akiisha apishwa. Kwa sasa hajaapishwa bado. Ndiyo maana Lema anazungumzia kuzuia kuapishwa.
 
Wekeni majina ya hao majaji humu ndani wengine tuko remote bado hatujayaoni
 
Ngoja Mahakama iamue
 
Is there any substantial evidence that backs up that Biswalo Mganga is implicated in office abuse as quoted from the two attached threads and personal opinion by Godbless Lema a none legible fugitive in Canada? Is it justifiable for a none legible fugitive to curse a judiciary appointment into office suggesting Biswalo Mganga was not qualified to be a judge and that he was liable to be imprisoned or lamenting in hell. Does Godbless Lema have the moral authority to subscribe to such a punitive statement against a judiciary appointee?

Were you comfortable quoting such an animosity statement and post on the public shared platform and for what targeted purpose?

Personal hatred is now ground being staged by haters of all colors will surface beyond the expectations as the current regime enjoys seeing these kinds of confrontations prevail in the country.
 
Anakosa vipi credibility wakati bado ni mtanzania? Haki ulizonazo wewe hta lema pia anazo shida ipo wapi?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mkimbizi Godbless Lema unao ushahidi usioacha shaka kwamba Biswalo hana maadili?
Au ni chuki zako binafsi zinakutesa?
 
Chadema wanadeal na mambo ambayo hayagusi kundi kubwa la Watanzania bali ni ya ubinafsi wao tu. Watu wana shida ya maji, barabara mbovu kwa baadhi ya maeneo ya nchi lkn hawayaongelei bali wamebakia umbea tu mara Sabaya, DPP...!!!
Kwamba huoni shida majambazi kuingia kwenye mifumo muhimu ya utoaji haki? Hizo barabara na maji utapatia wapi ukiwa na mijambazi hii? Jipime akili
 
Mi sioni kama kuna shida hapo. Mahakama ipo kwa ajili ya kutafsiri sheria, itaamua Kama ni sahihi ama vp. Tusianze kumpa Mama Samia umungu wa kutokukosea kama tuliompa Magufuli hadi akajiona yeye ni mungu na watu wote ni takataka tusioweza kumfanya kitu
 
Nimevutwa zaidi na sentensi hii, nanukuu;

"...Lema ambaye hana cheo chochote, anaishi kwa kulelewa na wanaume wengine Ulaya, anaweza kuanzisha kampeni ya kipuuzi...."

Nadhani una tatizo ktk fikra zako. Una tatizo kubwa la kufikiri vizuri na kuamua...

Ukipenda na ukiwa na muda tunaweza kujadiliana lakini kwa kwanza wewe kujibu maswali haya muhimu kwa faida yako:

1. Wewe unadhani ukiwa na "cheo fulani" ndiko kunamfanya mtu aishi vizuri? How?

2. Wewe hapo ulipo inaelekea una "cheo fulani kizuri" sana huko CCM na kwa hiyo hulelewi na wanaume/wanawake wenzio, au siyo?

3. Goodbless Lema hajaanzisha kampeni yoyote ili aungwe mkono. Godbless Lema katoa taarifa kuwa atapinga uteuzi wa Biswalo Mganga mahakamani kutokana na sababu za kimaadili. What's wrong with that hata uanze kung'aka kiasi hicho kama vile hiyo no ajabu sana?

Kama sheria zetu zinaruhusu raia kupinga hilo mahakamani, acha iwe hivyo na mahakama itaamua...

4. Mwisho, unaelewa maana ya "analelewa na wanaume wenzake?"

Kwa manufaa yako acha kujivunia dhambi zisizokuwa na sababu kwa kuzushia watu wengine mambo ya hovyo. Mfano una uhakika kuwa Lema "analelewa na wanaume wenzake?"

Au na wewe ni walewale wazushi na wambea wa kuhamisha hamisha maneno bila kuwa na uhakika wanachokisambaza na wakiulizwa unaweza kuthibitisha, wanaishia kusema, "...mimi nimesikia tu wanasema sema huko sokoni...!!"

Acha hizo bwana...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…