Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Hili ni kosa tuu la photo misplacement ni kosa la kawaida sana kwenye printing ila hilo ni tangazo moja la mtu mmoja yule yule walichanganya picha, wakarekebisha na kurudiwa kutangazwa.

Pasco


si sahihi. Hii ni mtu kacheza na photoshop tu. wala gazeti halina makosa hapo!

angalia namba iliyopo kulia chini ndipo utagundua. Kama gazeti wangerudia basi nafasi hiyo ingekuwa na namba mpya!
 
Chabruma na Kigwa please, jitokezeni hapa kujibu tuhuma zinazowakabili. Pongezi kwake Mh. Lameck Madelu Mkumbo kwa ufafanuzi wake.
 
Mtaumiza vichwa sana. Ukweli ni kwamba Lameck Madelu Mkumbo alifanya mtihana wa darasa la saba akashindwa.

Baada ya kushindwa darasa la saba mara ya kwanza, Lameck Madelu Mkumbo akaamua kurudia shule ya msingi. Kwakuwa miaka hiyo kurudia shule ya msingi ilikuwa hairuhusiwi, ndipo Lameck Madelu Mkumbo, akachukua jina la Mwigulu Nchemba, kijana wa kisukuma aliyekuwa ameacha shule wakati huo akiwa darasa la tano.

Hivyo Lameck Madelu Mkumbo akasoma darasa la tano kwa kutumia jina la Mwigulu Nchemba hadi darasa la saba na akafaulu mtihani kwa jina hilo la Mwigulu Nchemba.

Hivyo Mwigulu Nchemba aka Lameck Madelu Mkumbo hakuiba cheti cha mtu bali alisoma kwa kutumia jina la mtu mwingine aliyekuwa ameacha shule wakati huo kwasababu zake.
ok, kumbe ndio hivyo....na watu mnajua kwanini hamkusema
 
Mfano baba anaitwa john shija masalakolangwa
Mtoto ni lazima aitwe
Emanuel john masalakolangwa,jina la mtoto laweza kubadilika lakini la baba na ukoo ubaki palepale,sasa ikitokea mtoto akaitwa peter samwel nyakukungu hapo kuna walakini
 
Majina yake Ni ya kisukuma Ila yeye si msukuma au nakosea?- tafakari
Mkuu Gigo, unataka watu tutafakari nini wakati mwenyewe kasema hayo majina ni given names tuu na dakitari, angeweza hata kuitwa Joginder Sing na bado hakuna kosa lolote!.

Pasco
 
Dhana ya kwamba atang'oka kwa hii issue haitowezekana. Nadhani tuendelee na maisha yetu tu maana hata yule Diamond siyo jina lake halisi lakini sisikii mtu akiuliza
Kwani ana vyeti vilivyoandikwa jina la Diamond?. Kifupi bwana mheshimiwa alizaliwa akaitwa Lameck na wazazi wake na akasomea jina hilo mpaka alipofeli darasa la saba kilichofuata alirudia au aliiba nafasi ya Mwigulu Nchemba hilo liko wazi sasa mengine yaliyobaki ni story tu. Kama si kosa kisheria aungame yaishe na watu waliopita njia kama zake waachwe maana mtafukua mengi.
 
jina linamiliki vyeti,hivyo basi,mwenye jina ndio mwenye vyeti,mwenye jina akiamua kufuatilia particulars zake shule ya msingi akute taarifa zinaonyesha alifaulu,akaenda chuo lazima alalamike,alalamikie impersonation.

Mbona waliochukua vyeti vya watu leo wanahenyeshwa? kuchukua cheti ni kuchukua jina pia
Kuna muvi moja inaitwa three idiot inaeleza vya kutosha,mwenye jina akijitojeza kuanza kudai jamaaa ana vyake,ndio maana serikali kabla hujafanya mtihani wa kidato cha pili kma ulikuwa unatumia jina la mtu huwa wanapewa fursa ya kubadili majina
 
Mfano baba anaitwa john shija masalakolangwa
Mtoto ni lazima aitwe
Emanuel john masalakolangwa,jina la mtoto laweza kubadilika lakini la baba na ukoo ubaki palepale,sasa ikitokea mtoto akaitwa peter samwel nyakukungu hapo kuna walakini
Mkuu Lazaro, hakuna walakini yoyote as long as huyo baba john shija masalakolangwa, jina hili ndilo lililoko kwenye cheti cha kuzaliwa kama baba wa mtoto, pia ndilo lililopo kwenye vyeti vya kuandikishwa shule, vyeti vya NIDA na Uhamiaji, vikieleza majina ya mtoto ni peter samwel nyakukungu, majina hayo hayana tatizo kabisa popote kwa sababu tangu shule , uhamiaji na NIDA, majina yatakayoonekana ni peter samwel nyakukungu Emanuel john masalakolangwa. Hakuna mwisho wa idadi ya given names, ndio maana namtetea Mhe. Mwigulu kwa haki kwa vile hakuna anayejua birth certicate yake na DN number yake ina majina gani.

Pasco
 
Mwigulu alifeli darasa la 7 akatumia cheti cha mtu aliefaulu darasa la 7 kujiendeleza. Kwahiyo ana cheti bandia na majina bandia.
Pasco anajichanganya tu hivi jamaa kabla ya kuacha shule na kwenda kuchunga alikuwa anaitwa nani?na kwanini alibadili jina ,mimi ninachokiamini huenda jamaa baada ya kurudi shule alichukua jina la mtu kama sio cheti,na hiyo ni kawaida kwa sie tuliosoma kijijini watu hawataki shule wanaenda kuchunga,kwa mfano mimi nimechukua cheti cha mtu cha kidato cha nne nikajiendeleza nikafika mpaka PhD, cheti cha kidato cha sita,digrii,digrii ya uzamili,digrii ya uzamivu vyote vyangu isipokuwa cheti cha kidato cha nne na jina sio vyangu, je hapo nimeghushi au sijaghushi?
 
Pasco umechanganya mambo kuhusu mfumo au utaratibu wa majina. Kwa sehemu kubwa duniani kuna mifumo miwili ya majina, kuna huu wa nchi za magharibi ambao kutokana na ukoloni ndiyo na sisi tumeurithi na upo wa nchi za mashariki. Huu wa magharibi huwa unaanza na "first name" au kama ukipenda "forename" halafu ukimalizia na "surname" yaani jina la ukoo. Unaweza pia kuwa na jina au majina ya kati "middle name/s". Mfano ni Juma Maharage au Juma Pasco Maharage.
Ule wa mashariki huanza na jina la ukoo halafu likaja la kwako au pengine ukawa na jina la kati. Mfano Wachina; ukisikia anaitwa Xi Jinping basi ujue "Xi" siyo first name bali ndiyo jina la ukoo halafu "Jinping" ndiyo la kwake. Kwa maana nyingine kama Juma Maharage angekuwa Mchina basi angeitwa "Maharage Juma".
Sasa basi utaratibu sahihi hata kwa hapa kwetu kwa mfano ni mtu kuitwa jina lolote la kwanza (first name) au hata la kati (middle name) kama wazazi wake watakavyopenda ila jina la ukoo (surname) linabaki lile lile ambalo linatumika kifamilia. Hili linatakiwa liwe la "kilugha" sababu hakuna ukoo wa Kitanzania au Kiafrika wenye jina la kizungu, yote yanapaswa kuwa ya kikwetu.
Kuna utaratibu mbovu hapa kwetu ambapo mtu anayeitwa kwa mfano "Steven Paul Mkama" anazaa mtoto halafu badala ya kumuita mfano "Judith Mkama" au "Judith Roselyn Mkama" utasikia anamuita "Judith Steven" au "Judith Steven Mkama".
Haya ni makosa maarufu sana. Kwa mfano huu, huyu mtoto ni Judith Roselyn, hayo ndiyo majina yake sahihi. Jina pekee analoazima ni "Mkama" ambalo ni la ukoo. "Steven" na "Paul" hapaswi kabisa kuyatumia kwa sababu haya ni "personal names" za baba yake kama vile yeye alivyo na personal names zake mbili yaani Judith Roselyn. Atakapokuwa anatumia personal name yoyote ya baba yake tayari anapoteza huo ukoo. Hili tatizo linajitokeza mara nyingi mno hapa Tanzania.
Kuhusu "nicknames", haya ni majina ya utani ambayo hayachukuliwi kuwa rasmi, mfano yule beki wa Yanga anayeitwa "Canavarro", hakuna mtu yeyote anayeamini kwamba hilo ndiyo jina lake na wala hawezi kulitumia "officially" popote. Yapo pia majina yanayoitwa "stage names" ambayo hutumiwa sana na wanamuziki au wacheza sinema na wengine huamua kuyatumia rasmi kisheria kama majina yao. Mfano mwanamuziki maarufu wa Uingereza anayefahamika kama "Elton John" jina hili ni stage name ambayo amelirasimisha. Majina yake ya kuzaliwa ni Reginald Kenneth Dwight.
Kwa leo niishie hapa.
Mkuu Maseni, asante kwa somo hili
Pasco
 
MWIGULU katia aibu, kumbe na mbwembwe zote hizo alichukua jina la mtu aliefaulu hili alitumie yeye?, aibuu
 
Sasa mtu anaruhusiwa kutumia majina ya bandia kigombea urais wa nchi? Maana Pasco ameeleza vizuri kabisa kuwa majina ya Mwigulu Nchemba ni ya bandia (fake), lakini huyu mwenye haya majina bandia aligombea urais akitumia majina hayo hayo fake? Jee lilikuwa ni kosa kisheria?
 
Pasco umechanganya mambo kuhusu mfumo au utaratibu wa majina. Kwa sehemu kubwa duniani kuna mifumo miwili ya majina, kuna huu wa nchi za magharibi ambao kutokana na ukoloni ndiyo na sisi tumeurithi na upo wa nchi za mashariki. Huu wa magharibi huwa unaanza na "first name" au kama ukipenda "forename" halafu ukimalizia na "surname" yaani jina la ukoo. Unaweza pia kuwa na jina au majina ya kati "middle name/s". Mfano ni Juma Maharage au Juma Pasco Maharage.
Ule wa mashariki huanza na jina la ukoo halafu likaja la kwako au pengine ukawa na jina la kati. Mfano Wachina; ukisikia anaitwa Xi Jinping basi ujue "Xi" siyo first name bali ndiyo jina la ukoo halafu "Jinping" ndiyo la kwake. Kwa maana nyingine kama Juma Maharage angekuwa Mchina basi angeitwa "Maharage Juma".
Sasa basi utaratibu sahihi hata kwa hapa kwetu kwa mfano ni mtu kuitwa jina lolote la kwanza (first name) au hata la kati (middle name) kama wazazi wake watakavyopenda ila jina la ukoo (surname) linabaki lile lile ambalo linatumika kifamilia. Hili linatakiwa liwe la "kilugha" sababu hakuna ukoo wa Kitanzania au Kiafrika wenye jina la kizungu, yote yanapaswa kuwa ya kikwetu.
Kuna utaratibu mbovu hapa kwetu ambapo mtu anayeitwa kwa mfano "Steven Paul Mkama" anazaa mtoto halafu badala ya kumuita mfano "Judith Mkama" au "Judith Roselyn Mkama" utasikia anamuita "Judith Steven" au "Judith Steven Mkama".
Haya ni makosa maarufu sana. Kwa mfano huu, huyu mtoto ni Judith Roselyn, hayo ndiyo majina yake sahihi. Jina pekee analoazima ni "Mkama" ambalo ni la ukoo. "Steven" na "Paul" hapaswi kabisa kuyatumia kwa sababu haya ni "personal names" za baba yake kama vile yeye alivyo na personal names zake mbili yaani Judith Roselyn. Atakapokuwa anatumia personal name yoyote ya baba yake tayari anapoteza huo ukoo. Hili tatizo linajitokeza mara nyingi mno hapa Tanzania.
Kuhusu "nicknames", haya ni majina ya utani ambayo hayachukuliwi kuwa rasmi, mfano yule beki wa Yanga anayeitwa "Canavarro", hakuna mtu yeyote anayeamini kwamba hilo ndiyo jina lake na wala hawezi kulitumia "officially" popote. Yapo pia majina yanayoitwa "stage names" ambayo hutumiwa sana na wanamuziki au wacheza sinema na wengine huamua kuyatumia rasmi kisheria kama majina yao. Mfano mwanamuziki maarufu wa Uingereza anayefahamika kama "Elton John" jina hili ni stage name ambayo amelirasimisha. Majina yake ya kuzaliwa ni Reginald Kenneth Dwight.
Kwa leo niishie hapa.

Mkuu maelezo yako mazuri lakini nadhani Tanzania hatuna "Surname System", kwamba ni lazima kuwe na jina la ukoo tena lisiwe la kizungu. Jamii ya Tanzania tuko Waislam, Wakristo na wenye imani zingine. Kwa Waislam mtoto anatakiwa aitwe kwa jina lake na la ubini wake yani baba yake. Kwa hiyo wasemapo jina kamili huwa ni majina matatu yani la mtoto, likifuatiwa na la baba yake nalo likifuatiwa na la baba yake (ambaye ni babu wa mtoto). Majina haya si lazima yawe ya kilugha. Yanaweza kuwa Ali Juma Omari au Fatuma Jumbe Zuberi n.k. Na inaonekana hata jamii ya Wakristo hutumia mfumo huo ingawa kwa ufuatiliaji wangu inaonekana kwa Wakristo ndiko hasa kwenye majina ya Kilugha baada ya yale ya awali na kati ambayo huwa ya kizungu kama Frank John Mnyalukolo, Steven George Mwakatange n.k.
 
jina linamiliki vyeti,hivyo basi,mwenye jina ndio mwenye vyeti,mwenye jina akiamua kufuatilia particulars zake shule ya msingi akute taarifa zinaonyesha alifaulu,akaenda chuo lazima alalamike,alalamikie impersonation.

Mbona waliochukua vyeti vya watu leo wanahenyeshwa? kuchukua cheti ni kuchukua jina pia
Sheria inaruhusu kubadiri jina so hili la majina nadhani aachiwe mwenye maana hata mi Leo nikipenda Nina naadaa deed poll naanza kuyatumia.
jina linamiliki vyeti,hivyo basi,mwenye jina ndio mwenye vyeti,mwenye jina akiamua kufuatilia particulars zake shule ya msingi akute taarifa zinaonyesha alifaulu,akaenda chuo lazima alalamike,alalamikie impersonation.

Mbona waliochukua vyeti vya watu leo wanahenyeshwa? kuchukua cheti ni kuchukua jina pia
 
Pasco tungemuelewa Mh Mwigulu Nchemba kama angefupisha maelezo kwa kusema "..waungwana, vyeti ni vyangu na nimesoma kama vinavyoonyesha, ila nilirudia shule kwa majina ya mtu mwingine ili kuweza kupata nafasi ya kuendelea na masomo shule ya msingi" ingefaa zaidi
Mkuu Samari, alichoeleza humu Mwigulu ndio ukweli wake, usitake kumlisha maneno kwa kulazimishwa ukweli unaotuka wewe!, kuna kweli za aina tatu,
1. Ukweli unaosemwa kuwa ni kweli -spoken truth
2. Ukweli unaotakiwa kuwa ni ukweli-the purported truth
3. Ukweli halisi - the real and plain truth.

Kati ya kweli hizi, ni ukweli halisi tuu ndio utasimama mpaka mwisho, ukweli unaosemwa kuwa ni kweli unaweza kuwa ni uongo unasemwa na kuitwa ni kweli, ukweli unaotakiwa ni ule ukweli unaohitajika, ili uwe ukweli mfano miongini mwa sifa za rais, lazima awe ni Mtanzania, akitokea kijana wa banyamulenge kule mipakani, na anautaka urais, na akaupata, then hata ukweli ukiibua kuwa sio Mtanzania, ukweli unaotakiwa kuwa ni kusemwa ni Mtanzania.

Pasco
 
kama nakuelewa, ishu ni kua mwigulu alifaulu la 7 then hakufaulu kwa jina la mwigulu ila lingine ambalo ndilo analitumuia hadi leo kwenye vyeti, ila hilo mwigulu alipewaga tuu kama nick names
Mkuu Kibao cha Kaburi, alipozaliwa alipewa majina ya kwao unyirambani, alipopelekwa hospitali, dakitari wa Kisukuma akamuuliza mama yake kama ana majina mengine yoyote, mama akasema hana, mama akamruhusu dakitari ampe yeye majina anayotaka, kwani majina ni nini, ndipo dakitari huyo akampa majina hayo na ndio aliandikishwa nayo shule na kuendelea kuyatumia mpaka leo.
Hili la Lameck siyo jina la kinyiramba ni jina la daktari aliyenipokea zahanati ya Iliyopo kijiji cha Mukulu, daktari tunaita hivyo lakini ni Nesi ndiye aliyekuwa anaitwa Mwigulu na jina la kizungu Lameck. Mimi nilipelekwa hosipital nikiitwa Mugulo Mama akaulizwa jina akanitaja Nesi yule akamwambia mama unamwitaje jina hilo hakuna lingine mama akamwambia hakna labda mtaje wewe, basi jamaa akajitaja.
Mwigulu,
Japo ni very interesting!.

Pasco
 
Back
Top Bottom