Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Pasco, ni kwa maslahi ya kisiasa ya Mwingulu mwenyewe kusafisha hili wingu la majina fake kwa sababu pia ana ambition kubwa katika safari yake ya kisiasa. Kinachotakiwa hapa siyo uhalali kisheria wa kutumia hayo majina, bali yalipatikanaje. Na muhimu zaidi hiki ni kipimo cha ukweli na uaminifu wa Mwingulu kama kiongozi wa kitaifa. Kadhalika huu ni mtihani wa kupima umahiri wake katika kujibu tuhuma au maswali yanayomhusu. Utetezi wake umezidisha utata kwa sababu hauko straight; na maelezo yake yana makosa mengi ya kisarufi na kiuandishi (poor grammar, phraising, punctuation and capitalization) na hivyo hayaeleweki kirahisi. Hii haiendani na hadhi yake.
 
Kubadilisha jina sio kitu cha ajabu, sijui kama mnajua kuwa Jomo Kenyatta wa Kenya jina lake halisi ni Johnston Kamau na alibatizwa na kusoma elimu ya awali na jina hilo, baadae alipoanza harakati za ukombozi akajiita Jomo Kenyatta, Kenyata maana yake Taa ya Kenya. Na mpaka leo Kenyatta ndo jina rasmi la familia hiyo, japo baadhi ya ndugu wanatumia majina ya Kamau wa Ngengi.
 
Ni ukweli wake na sii lazima uwe ukweli halisi.
Pasco lihurumie taifa acha kumshabikia mwongo.
Mkuu Jogi, nakubaliana na wewe kuwa sometimes ukweli wa mtu sii ukweli halisi!, sisi tunafuata kanuni za Jumuiya ya Madola kuwa manachosema mtu yoyote kuwa ni kweli, kitahesabika kuwa ni kweli hadi mtu mwingine a`pinge tena kwa uthibitisho!, yaani "the one who allege, must prove", Mwigulu kajieleza na huu ndio ukweli wake, anayepinga na aje na uthibitisho!.

Pasco
 
Kumbe wakati fulani majina yana uhusiano mkubwa na mafanikio au mibaraka ya mtu mmoja mmoja, ndiyo maana hata Lameck Mkumbo akajiita Mwigulu Nchemba, hili jina limemng'arisha mno huyu jamaa, na hapa ndipo nawaona Wazazi wake walicheza kama PELLE. Teh teh kumbe ndiyo maana SARAH Akaitwa Sara.
 
Kubadilisha jina sio kitu cha ajabu, sijui kama mnajua kuwa Jomo Kenyatta wa Kenya jina lake halisi ni Johnston Kamau na alibatizwa na kusoma elimu ya awali na jina hilo, baadae alipoanza harakati za ukombozi akajiita Jomo Kenyatta, Kenyata maana yake Taa ya Kenya. Na mpaka leo Kenyatta ndo jina rasmi la familia hiyo, japo baadhi ya ndugu wanatumia majina ya Kamau wa Ngengi.
Mkuu Mpanzi, asante sana kwa hii.
Pasco
 
Wewe wakili msomi jina linawezaje kuwa la bandia? Jina ni nini?

hamna tofauti kati ya mtu aliyetumia jina la mtu kujiendeleza na yule anaye nunua cheti cha mtu mwingne...

na kwa nini mtu aache jina lake na kutumia la mwingine... huo ni udanganyifu.

jina linamiliki vyeti,hivyo basi,mwenye jina ndio mwenye vyeti,mwenye jina akiamua kufuatilia particulars zake shule ya msingi akute taarifa zinaonyesha alifaulu,akaenda chuo lazima alalamike,alalamikie impersonation.

Mbona waliochukua vyeti vya watu leo wanahenyeshwa? kuchukua cheti ni kuchukua jina pia
 
Mkuu nazidi kuwa na mashaka, haiyumkini account yako imedukuliwa.

Maelezo ya mtuhumiwa unaya classify kuwa ya kweli kwa sababu amesema hivyo!!!!?

Hawa watu "hata kama wanaongelea gizani" (anonymity) wanapaaza sauti kusema "MNADANGANYWAAAA" unapendekeza tukubali tu maelezo rahisi ya "verified user"????

MUNGU ALIMTIMUA SHETANI MBINGUNI, MAANA HAKUNA NAMNA UTAFANYA USHETANI KISA UKO MBINGUNI.

Verification of username haitakuwa na maana kama muhusika anashindwa ku clear tuhuma inayomkabili ya kutudanganya kama taifa.

Amefanya mtihani wa darasa la saba mara mbili kwa manufaa yake!!?
Mkuu Jogi, wewe wasema!.
Pasco
 
Kuna watu wameshindwa elewa kuwa hayo majina "feki" ya Nchemba ndo aliyofanyia mitihani yote na kupata vyeti vyake, ni nini kigumu hapa kuelewa? Sioni tatizo lolote maana vyeti vyote ni halali yake kwa jina alilotumia.

itabidi Mwigulu AFUTIWE SHAHADA zake kwa ku CHEAT...

hana tofauti na yule mtu anaye mfanyia mtihani mwenzake...

tunasubiri utekelezaji...
 
Mkuu Jogi, wewe wasema!.
Pasco
JPM amemwondolea mamlaka aliyekuwa DED wa mkinga kule tanga ili cheo chake kisiingilie tuhuma zinazomkabili,

Kwa jinsi iyo hiyo aondolewe mamlaka aliyonayo sasa huyu anayeng'ang'ana kulidanganya Taifa ili asiwe obstacle tutakapokuwa tunaingia kwenye mafaili ya wizara ya elimu kuibua proofs.
Ikibidi hata carbon 14 itatumika kuzihakiki nyaraka. Hasa kwenye "attendance za shule ya msingi (....) na (.....)
 
hamna tofauti kati ya mtu aliyetumia jina la mtu kujiendeleza na yule anaye nunua cheti cha mtu mwingne...
na kwa nini mtu aache jina lake na kutumia la mwingine... huo ni udanganyifu.
Mkuu wa Hapapa, hakuna udanganyifu wowote kwenye hoja iliyo mezani, alichofanya ni kutumia tuu majina megine ila sio ya mtu mwingine, na kuna tofauti kati ya kufanya udanganyifu na kufoji vyeti, Mwigulu hajafoji vyeti amesoma mwenyewe, na hajafanya udanganyifu wa kutumia jina la mtu yoyote bali ametumia given names kama majina yake badala ya majina ya familia, na mfano mzuri ni Jommo Kenyatta, katika majina hayo, hakuna jina lake alipopewa wala majina ya wazazi wake wala ukoo wake, ni majina yake halisi ni Johnston Kamau, akajiita Jommo Kenyata, aliojipa na hajafanya kosa lolote!, ila hilo jina la Jommo Kenyatta ni jina bandia, lakini Uhuru Kenyatta ni jina halisi. Mwigulu Nchemba ni jina bandia lakini vyeti vyake vyote ni vyeti halisi.

Pasco
 
Pasco umetumia criteria gani kusema majina ni universal? Embu Fanya utafiti kuhusu wanaume Wa Java (Indonesia), mbona hawana jina la baba wala ukoo only one given name eg
Suharto
Sukarno
Mkuu nakiri, kukosea ila huku kwetu majina is not a big deal, jee unajua jina Mkapa alilipata wapi, au jina la Magufuli lilitoka wapi?!, cha muhimu aliyesoma na kuhitimu ni Mwigulu Nchemba, jina lilitoka wapi it is immaterial!.
Saubject matter ni vyeti sio fake!.
Pasco
 
Hakuna uthibitisho wa hili hiyo 1984 ni juzi tuu kama ni kweli tungeishawasikia waliosoma nae japo ile kuacha shule kwenda kuchunga mbuzi kisha kurudi kurudi shule ni kali. Lazima taarifa zake zote zipo kwa sababu mtu akiacha shule hufukuzwa, kurudishwa sio issue ndogo hivyo data lazima zipo.
Pasco
kumbuka aliacha shule kwa miaka miwili!
Je aliporudi namba ya usajili ilikua ni ile ile au nyingine?Na hilo jina la nesi alipewa baada ya kuzaliwa au baada ya kuacha shule hiyo darasa la tano?
kama ndio wazazi wake kwanini hawakuona umuhimu wa kuandikishwa jina la nesi toka anaanza shule ila wakaona umuhimu wakati aliporudi?
Kuna walakini....
 
Pasco, ni kwa maslahi ya kisiasa ya Mwingulu mwenyewe kusafisha hili wingu la majina fake kwa sababu pia ana ambition kubwa katika safari yake ya kisiasa. Kinachotakiwa hapa siyo uhalali kisheria wa kutumia hayo majina, bali yalipatikanaje. Na muhimu zaidi hiki ni kipimo cha ukweli na uaminifu wa Mwingulu kama kiongozi wa kitaifa. Kadhalika huu ni mtihani wa kupima umahiri wake katika kujibu tuhuma au maswali yanayomhusu. Utetezi wake umezidisha utata kwa sababu hauko straight; na maelezo yake yana makosa mengi ya kisarufi na kiuandishi (poor grammar, phraising, punctuation and capitalization) na hivyo hayaeleweki kirahisi. Hii haiendani na hadhi yake.
MKUU Nginana, naunga mkono hoja!.
Pasco
 
Back
Top Bottom