Utofauti wa Mwafrika na watu wengine hauko kwenye rangi tu, hata akili. Mtu mweusi kapunjwa akili

Utofauti wa Mwafrika na watu wengine hauko kwenye rangi tu, hata akili. Mtu mweusi kapunjwa akili

Habari!

Mpaka leo natafakari hivi ni sababu za Kijiografia ndizo zimepelekea utofauti huu mkubwa wa akili baina ya Mwafrika na mtu mweupe?

Sometimes nahisi ni sababu za kibaiolojia (genetic factors) ndizo zimeweka mstari wa akili kati ya Mwafrika na mtu mweupe?

Narudi mezani napata jibu ni Mungu tu kwasababu zake mwenyewe ameamua kumpunja Mwafrika akili maana hata Waaafrika ambao wangezaliwa na kuishi huko Amerika na Asia hawaishiwi ulimbukeni na ushamba.

Nimewahi kufanya kazi na Wazungu Acacia, General manager alikuwa analipwa zaidi ya milioni 60 za Kitanzania kwa mwezi lakini alikuwa hataki kuitwa boss, alikuwa hana dereva wala body guard.

Nimewahi kufanya kazi na Wazungu pia huko Serengeti hotel moja ya gharama na nzuri sana. Ambayo 24 hrs gharama ya chini ilikuwa milioni 1.4 na sasa imepanda nasikia maana mimi niliacha baada ya kupata kibarua Serikalini. Hotel ambayo watu maarufu kama Bush, Beckham n.k hukosi kuwaona kule. Kule hakuna mtalii Mchina, Mhindi wala Mwafrika. Kule madoni walikuwa wanatumia mpaka milioni 20 per day.

General manager alikuwa analipwa pesa nyingi sana ila hakuwa na mlinzi kwake, alikuwa hataki kabisa kumuita boss.

Tukio la juzi la kuapishwa King Charles wa Uingereza mmeoana, hakuwa na mpambe wa kumsogezea daftari la mikataba, kiti alikisogeza mwenyewe.

Turudi Afrika sasa
• Kila mwanamuziki ambaye yuko kwenye chati tu mabody guards kama wote.
• Leo kazini msimamizi wako acha kumwita boss, muite jina lake la kawaida uone kama hutapewa kesi ya wizi wa mali za umma.
• Ufisadi na urasimu.
Afrika huwezi kusajili biashara siku moja, urasimu ni mwingi.
• Kesi inakaa mpaka miaka 7 ndo inatolewa hukumu hasa kesi ya mauaji. Baadaye mtuhumiwa anaachiwa huru kuwa hana hatia huku tayari kakaa mahabusu miaka 7. Mlipeni basi mabilioni ya kumfidia. Maana kumweka mtu ndani miaka saba si uuaji kabisa.
• Huku Afrika karibu kila Kiongozi wa nchi kila anaposimama au kukaa nyuma yake kuna AD kavaa nguo za kijeshi.

Aibu sana.
Sijaona kitu ulicho kiweka katika mada yako kinacho onyesha ya kuwa Wazungu wana akili kuwazidi Waafrika sababu uliyo yaweka hayaonyeshi kuwa na akili. Huo ni utaratibu tu wa mtu binafsi kama walivyo waafrika wengi wanafanya mambo kama uliyo yataja, lakini ajabu umewaongelea Waafrika wote, na ukamili kwa viongozi.

Haya uliyo yataja kwa Waafrika, Wazungu wanafanya maradufu.

Siku ukijua maana ya AKILI utawajua wenye akili ni kina nani. Ukute umeandika huku hujui maana ya AKILI nini ?

Nikirudi nitakuwekea sifa au ishara za kumjua mtu mwenye akili ni nani ?
 
Not irrelevant but practical...anyway tusubiri kujengewa vyoo na kupokea vyandalua! Maybe that is relevant!
Kweli iko kazi! Wanaoijua horsepower huwaoni! Angalau wameleta boda boda kusaidia kundi kubwa lisilo na ajiri! Tumebakia na theory tu ya what is horsepower! Kuweka practical ni kundesha boda boda! Ila wewe unaona sio nongwa!

Kama nilivyosema tusubiri kujengewa vyoo, na vyandalua! That is practical manifestation ya akili ya mwafrika.
 
Mkuu ulipoenda kwenye tatizo la Sprituality maybe you are right. Tutafutate pembeni, labda tunaweza kupeana mawazo zaidi
Nahangaishwa mno mimi binafsi kwa nini tuko hapa. Nimesoma nadharia kadhaa za maendeleo ya mwanadamu zimeshindwa kunipa majibu!
Nimefanya kazi kwenye International NGO zinazosema zinaondoa umasikini Africa nikaona ni Scam! Sana umasikini niliondolewa mimi,sio hao tunaowafanyia warsha na kuzunguka na MA Land cruisers! Nikaona nakuwa mnafiki! Mzungu hakufika hapo kwa Warsha na semina! Na kuchimbiwa vyoo na kupewa vyandalua!
Tuwasiliane Mkuu
Kama ukitaka tulizungumze hili, basi tutajadiliana zaidi pembeni....
Nimefurahi tumefanya mjadala mzuri mkuu....
Peace Out ✌️✌️✌️✌️✌️
 
Mwenye akili ni mtumwa wa asiyekua na akili. According to proton pump, (2022) [emoji2398]
 
Akili ni uwezo wa kuleta usawaziko wa fikra Ili uwe perfection ikiwemo utatuzi wa changamoto zinazokukabili
Kipi ni kipimo na vigezo sahihi vya perfection na nani amekiweka kwa malengo?
Na "utatuzi wa changamoto" unahusika vipi na uamuzi wa mtu kutaka au kutokutaka kuitwa boss?
 
Hakuna mwingine wa kulaumiwa bali ni sisi wenyewe. Ukifikiria sana haya mambo utakufuru kama wewe ni mtu wa dini. Kwa nini afrika iko hivi!?

Story za afrika na waafrika ni phenomenal sana. Tupo kwenye dunia ya peke yetu.

Mfano. Mkoloni anaondoka hapa alitupa kbs head start. Alituachia miundombinu karibu nchi nzima i.e. reli, mashamba makubwa kila kona sio kahawa chai katani pamba etc mashule, miji aliyokuwa kaanza kuipanga vzr japo ilikuwa midogo, maviwanda ya kila aina etc etc. Leo viko wapi!? Tungeanzia palepale alipoachia tukaendeleza vzr leo hii si afrika tungekuwa kama south korea tu!?
Nina jamaa yangu tunasukuma nae Guta kwao ni huko kwa Babu.
Anasema:, katika kijiji chao kulikuwa na mashamba makubwa ya miwa yaliachwa na Alliens baada ya Babu kuwafukuza.

Baada ya babu( alale anapostahili) kuwafukuza yale mashamba yakamilikiwa na wapambe wa babu...anasema katika lugha yao ya taifa:, sugarcanes can be havasted 4 times and the fouth time you need to uproot them and put another crops. this is what we were seeing Whitemen doing before being chased away by Babu..bada ya hapo mashamba yakamilikiwa na makada wa babu(tutuchukulie kama makada wa ccm Tanzania) .
Wakavuna mvuno wa kwanza baada ya watu waupe kufukuzwa, Wakavuna wa pili, wa tatu hadi wanne.

Mivuno yote hiyo hakuna aliyekuwa na kumbukumbu kuwa hili ni shamba lina hitaji palizi mbole etc,kila mvuno pesa walikuwa wakiweka mfukoni, mwenye akili kati ya wapumbavu wenzake alibahatika kujenga nyumba, but hadi yale mashamba yanaaisha kwa maana ya kudumaa hakuna muendelezo uliofanywa na wamiliki wapya wapambe wa babu.

Miwa inaweza refuka hadi ft 12 lakini kwasababu kudumaa ikawa inakomea ft 2/3.
Mashamba ya miwa yakafa kwa staili hiyo, baada ya mashamba ya miwa kufa, wale wale walioyaua( wapambe wa merehemu babu) wakaanza kung'oa mabomba yaliyokuwa yaki- supply maji kwa hayo mashamba. Wanang'oa then wanaenda uza vyuma chakavu.
So, hadi sasa pale kijijini kwao yale mashamba yamekufa, yamebaki kuwa mapoli na wenye uwezo, wamechukua hema 2/3 huyu hapa analima mahindi, huyu hapa analima maharagwe, so kilimo cha mpangilio kama walichokuwa wanakifanya Alliens hakipo tena.
 
Mkuu cassavaleaves mimi namalizia mjadala kwa kusema kwamba, Afrika yetu ina shida kubwa mno. Naomba nimalize huu mjadala wetu mzuri wa leo, ambao umekuwa na maswali mazito na muhimu kabisa kuulizwa. Binafsi huwa naamini kwamba mbali na matatizo ya kiuchumi na kisiasa ambayo ndiyo tunayazingatia sana, tatizo kubwa la Afrika liko kiroho (Spiritually) kuliko kimwili. Kuna baadhi ya mambo ya hovyo hufanywa na waafrika, They defy common precepts of decency....Ndiyo tunapata viongozi kama Bokassa, Musseveni, Mobuthu n.k
Probably Kuna sehemu tulikosea uko nyuma, spiritually

haiwezekani maisha tunayoishi wa Afrika asilimia kubwa yanafanana, hata akizaliwa nje ya Afrika. Afrika ili ufanikiwe una struggle Ile mbaya, tofauti na jamii nyingine,

Labda Mungu tunaemuabudu sio yeye, tunaomba baraka zinaenda Kwa wengine,

jamii zote nyingine Zina Miungu yao, wachina wana Budha, India Wana Miungu Yao, Wazungu Wana Miungu Yao, wa Arabu hivyo hivyo, ukija kwa Afrika, ni mvurugano, tumechanganywa na Imani za nje hatujui ipi sahihi, Imani zetu za kale zimesahaulika. Labda tuanzie hapo.
 
"Cha kushangaza ni kwamba Babu aliweza kutengneza Mapiramidi Misri ambayo mpaka Sasa imekuwa shida kujua hesabu zake lakini mjuu hata kutengeneza soksi,kijiko, hawezi si mambo ya ajabu aya"

Wahandisi wa Misri walikuwa ngozi nyeusi?

Misri ni nchi ya ulaya iliyopo Afrika.
Nilifanya nukuu mkuu wa mchango wa member sio mawazo yangu haya ,kuhusu misri hilo liko wazi kabisa mbona mkuu

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Tulipomcheka baba yetu akiwa amelewa baba akaacha laana utatawaliwa na ndugu zako shida ilianzia hapo someni biblia
 
Elimu yetu ina madhaifu mengi sana!
Na hii nikuanzia nasari hadi Chuo kikuu; Inapima mtu anayeweza kukariri kuliko wengine
Hivyo anayeweza kukariri eti ndiye mwenye akili; maana yake Elimu yetu imetengenezwa kwa mfumo wa kuandaa wafanyakazi (cheap labour). Anayeweza kukariri ukimtuma kazi hasahau ila hana ubunifu wowote
Namaanisha; Elimu yetu haiandai watu Kufikiria. Vipaji mbalimbali, ubunifu nk havina nafasi kabisa kwenye Elimu yetu

Na ndio sababu unakuta mwanajeshi amekuwa mwalimu (bado hujui kwa nini kuna baadhi ya waalimu ni wakali kupita kiasi), mwalimu amekuwa mkulima, mkuma amekuwa Mwandishi wa habari, Engineer amekuwa bwana shamba, Polisi amekuwa nesi (bado hujui kwa nini kuna manesi wakali ) nk nk nk
Na hii huchangia baadhi ya wafanyakazi kutokufanya vizuri makazini kwani kuna wengi tu wamesomea kazi zisizo kuwa za kwao; yaani kusoma kwetu ni kama bahati nasiku ya BIKO (utakachopata/pangiwa) na maanisha haina mfumo wa kuwapanga watu wasome kulingana na vipaji/ubunifu walio nao
Nakubaliana na ww kwa % zote
 
Hakuna mwingine wa kulaumiwa bali ni sisi wenyewe. Ukifikiria sana haya mambo utakufuru kama wewe ni mtu wa dini. Kwa nini afrika iko hivi!?

Story za afrika na waafrika ni phenomenal sana. Tupo kwenye dunia ya peke yetu.

Mfano. Mkoloni anaondoka hapa alitupa kbs head start. Alituachia miundombinu karibu nchi nzima i.e. reli, mashamba makubwa kila kona sio kahawa chai katani pamba etc mashule, miji aliyokuwa kaanza kuipanga vzr japo ilikuwa midogo, maviwanda ya kila aina etc etc. Leo viko wapi!? Tungeanzia palepale alipoachia tukaendeleza vzr leo hii si afrika tungekuwa kama south korea tu!?
Viongozi wengi baada ya mataifa mengi kupata Uhuru waligeuka miungu watu kwa kujifanya Wana akili Sana ndio maana ilifika muda wengine wakajitangaza kuwa marais wa maisha Kama wakina Kamuzu Banda.

Viongozi ambao walikuwa na sifa tele kuja kupinduliwa Kama bwana Nkwame Nkurumah wa Ghana kwa sera mbovu na utawala wa hovyo,Tanzania na sera yetu ya ujamaa iliua Uchumi mpaka kufikia muda sukari ikawa bidhaa ya anasaa na watu kuvaa kaniki mpaka hivi Sasa huwezi ongea suala la umasikini Tanzania pasi kuangalia athari za ujamaa.

Viongozi wengine wasomi wakubwa kufanya Mambo ya hovyo ukilinganisha na elimu zao mfano ni Robert Mugabe na Zimbabwe yake

Ukiangalia kwa umakini mkubwa utakuja kugundua kwamba Afrika ya wakoloni ilikuwa bora kuliko Afrika ya wakoloni weusi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwenye masomo ya kidini, watu weusi wakiongozwa na Mkushi Nimrod ndiyo waliojenga mnara wa Babeli kutaka kufanya vita dhidi ya Mungu. Kamsome mwanahistoria wa kihebrani Flavius Josephus ndiyo utaona vitu vya ajabu kweli. Lakini pia, Afrika ndiyo kilikuwa kitovu cha elimu ya kichawi (Esoteric Knowledge) ambayo ilianza kupitia dini ya kale ya The Mysteries ambayo waganga wa kale wakina Imhotep walikuwa wanaihodhi kwa siri. The Mysteries ndiyo imekuja kuzaa dini za siri kama Free-Masonry na nyingine.

Mwanahistoria wa Kigiriki Herodotus (The Father of History) anasema miungu ya kigiriki kama Poseidon (Neptune) pamoja na masimulizi (Mythologies) mengine kuhusu viumbe wa kale kama Medusa na The Gorgons yalitokea Afrika pale Libya kwa Berbers. Mwanahistoria mwingine Dr. Wallis Budge akathibitisha hili na kusema kwamba hadi miungu ya kimisri kama Osiris asili yake ni Libya kwa waafrika. Kama umesoma Biblia kwenye kitabu cha 2 Timotheo 3:8, Mtume Paulo anawataja Yanesi na Yambre (Jannis and Jambres) ambap walikuwa ni wachawi wa Farao.

Hawa jamaa walikuwa wanatokea kwenye hii dini ya The Mysteries, na ndiyo walikuwa wanashindana na kila jambo la Mungu ambalo Nabii Musa alifanya. Kuanzia kutengeneza nyoka, kugeuza maji kuwa damu, na mengineyo. Sasa kama ukifuatilia hii nadharia ya kidini, utafahamu kwamba kwenye suala zima la mambo ya giza Afrika ni ilikuwa ni sehemu hatari na bado ni sehemu hatari sana.....
Kw nadharia hii mbona secret society zote, illuminati, freemasons, nk zime base ulaya na Amerika? zambi wanazofanya nchi za magharibi mbona ni nyingi kupita sisi, Mbona laana haiwapati.?

Kwa uono wangu mfupi, labda tuseme sisi ni wavamizi sio wakazi wa asili wa Dunia hii, kila tufanyalo nature inatutema,
 
Kwenye masomo ya kidini, watu weusi wakiongozwa na Mkushi Nimrod ndiyo waliojenga mnara wa Babeli kutaka kufanya vita dhidi ya Mungu. Kamsome mwanahistoria wa kihebrani Flavius Josephus ndiyo utaona vitu vya ajabu kweli. Lakini pia, Afrika ndiyo kilikuwa kitovu cha elimu ya kichawi (Esoteric Knowledge) ambayo ilianza kupitia dini ya kale ya The Mysteries ambayo waganga wa kale wakina Imhotep walikuwa wanaihodhi kwa siri. The Mysteries ndiyo imekuja kuzaa dini za siri kama Free-Masonry na nyingine.

Mwanahistoria wa Kigiriki Herodotus (The Father of History) anasema miungu ya kigiriki kama Poseidon (Neptune) pamoja na masimulizi (Mythologies) mengine kuhusu viumbe wa kale kama Medusa na The Gorgons yalitokea Afrika pale Libya kwa Berbers. Mwanahistoria mwingine Dr. Wallis Budge akathibitisha hili na kusema kwamba hadi miungu ya kimisri kama Osiris asili yake ni Libya kwa waafrika. Wagiriki walianza kujifunza haya mambo baada ya kutengeneza koloni lao Afrika, liitwalo Cyrenaica.

Kama umesoma Biblia kwenye kitabu cha 2 Timotheo 3:8, Mtume Paulo anawataja Yanesi na Yambre (Jannis and Jambres) ambap walikuwa ni wachawi wa Farao.Hawa jamaa walikuwa wanatokea kwenye hii dini ya The Mysteries, na ndiyo walikuwa wanashindana na kila jambo la Mungu ambalo Nabii Musa alifanya. Kuanzia kutengeneza nyoka, kugeuza maji kuwa damu, na mengineyo. Sasa kama ukifuatilia hii nadharia ya kidini, utafahamu kwamba kwenye suala zima la mambo ya giza Afrika ni ilikuwa ni sehemu hatari na bado ni sehemu hatari sana.

Mambo ni mengi sanaaa mazee
Japo hii ni nadharia ya kidini (Naomba tuelewane vizuri)........
Sikutaka kuipeleka mada hii uko...Nimrod is mysterious figure kwenye Bible, maybe ndio atakayekuja mwishoni kama Mpinga Kristo...

Anyway kama laana ya Mwafrika inatokea kufanya vita na Mungu through the tower of Babel basi tumekwisha.!

Maybe pia kama sisi ni uzao wa Nimrod, labda ndio maana tumenyimwa technology! Why knowledge ya Pyramid ilipotea! Why civilization ya Ethiopians ilipotea!
Nimekua na conversation recently about Nimrod nilipokuwa nasoma Bible Prophecy! Actually nilikua naanza kusoma deeply kuhusu yeye kabla ya mada hii...
 
Kw nadharia hii mbona secret society zote, illuminati, freemasons, nk zime base ulaya na Amerika? zambi wanazofanya nchi za magharibi mbona ni nyingi kupita sisi, Mbona laana haiwapati.?

Kwa uono wangu mfupi, labda tuseme sisi ni wavamizi sio wakazi wa asili wa Dunia hii, kila tufanyalo nature inatutema,
Mkuu kwa madai ya hoja yako ya mwisho waafrika asili yao itakuwa wapi ? Au walitokea wapi?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Hujafanya tafiti za kutosha ndugu yangu, na pia unanisikitisha sana ambavyo unajiona duni mbele ya jamii nyingine. Huwa nikiwasoma watu wengi kama ninyi, huwa ndiyo napata kufahamu kwamba mzungu alifanikiwa kwa asilimia 100% kumtawala mtu mweusi, kwasababu ameshikilia fikra zetu. Kiufupi mimi nakukubali sana Nankumene japo katika hili naomba niendelee kukukusoa na kama kuna kitu nakosea naomba niambie nifahamu. Niko tayari kujifunza vitu vipya:

Mosi, bila ubishi wowote ule Misri ya kale (Kemet) ilikuwa ni dola la watu weusi. Ushahidi wa kutosha wa hili ninalosema uko kwenye The Egyptian Hieroglyphs. Nafurahi sana kuona umemzungumzia mwana-mahesabu wa Kigiriki Pythagoras. Hivi unafahamu kwamba Pythagoras kama Plato aliwahi kusoma elimu yake ya juu kule Misri ya kale ??? Kiufupi mpaka kufika vita ya Kalkemish (The Battle of Carchemish), vita baina ya Misri na Babeli, Misri ilikuwa inatawaliwa na mafarao waliotoka Sudan (Nubia). Farao Necho II alikuwa ni mnubi wa Sudan. Hili nalo utataka kulipinga ndugu yangu ???

Pili, narudia tena kuhusu Berbers (The Amazigh People). Hii jamii ya kiafrika ndiyo walikuwa wanajeshi wa muhimu wa kalifeti ya Ummay (The Umayyad Caliphate), ambapo walisaidia kwenye uvamizi wa Uhispania. Hata neno GILBRALTAR limetokana na neno la kiarabu Jabal Tarid (The Mountain of Tariq), ambapo walimuenzi kamanda wa kiislamu aliyeongoza uvamizi huo aliyeitwa Tariq Ibn Ziyad. Hawa waafrika (Berbers) ndiyo waliotengeneza falme imara kama Numidia ambazo zilishirikiana na ufalme wa Karthago (Carthage) katika kupambana na Rumi kwa miaka zaidi ya 100 (The Punic Wars).

Baada ya Warumi kumshinda Hannibal mwaka 146 BCE (The Third Punic War), Scipio Africanus aliamuru dola la Karthago lichomwe moto lote na watu wake kuuzwa utumwani. Walifanya sawa na kile ambacho Mongols chini ya Monghke Khan walikifanya kule Baghdad mwaka 1258 (The Siege of Baghdad) ambako kulikuwa na maktaba kubwa na vyuo bora kabisa duniani kwa wakati huo. Leo hii historia ya haya madola hazipo. Lakini, hata kama hazipo, basi tuseme kwamba waafrika wana akili ndogo kuliko jamii nyingine ???

Tatu na mwisho kabisa, waafrika wana historia ambayo haijazungumzwa na kufanyiwa tafiti vilivyo. Wenzetu wazungu wamefanikiwa sana katika kuaminisha weusi kwamba hawana historia. Wengi wetu hili tumelibeba kama lilivyo bila kulipa tafakuri za kina. Naomba nikupe mifano ya mwisho: Kipindi Roma iko chini ya Kaisari Augustus, vilitokea vita vikubwa baina ya Ethiopia (Nubia) na dola la Mrumi mwaka 24 BCE ambapo waliishia kufanya makubaliano ya amani. Hivi mtu mjinga asiye na akili anaweza kuingia kwenye makubaliano ya kidiplomasia na taifa kama Roma kweli ???

Haya, wazungu wamefika zimbabwe (The Great Zimbabwe), wakaandika kwamba ule mji ulijengwa na wazungu kwasababu weusi wasingeweza kufanya hivyo. Kuna watu wanaamini mpaka leo hii kwamba The Great Zimbabwe haukujengwa na watu weusi. Mara ya kwanza Vasco Da Gama anaona rangi iliyopakwa ukutani (Colour Paint) ilikuwa ni kule Kilwa (The Kingdom of Kilwa), hapa nchini kwetu. Ifahamike kwamba Kilwa ilitengeneza hadi sarafu yake ambayo ipo kwenye makumbusho yake, lakini pia ilianzisha mahusiano ya kidiplomasia na Uchina (The Ming Dynasty) mnamo karne ya 14. Hivi watu wasio na akili wanaweza kutengeneza sarafu yao kweli, pamoja na kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia ???

Aidha kuna kitu kimefichika, au waafrika mnajiona ni mapanzi kama ambavyo wapelelezi wa kihebrani walimwambia Nabii Mussa baada ya kutoka kule Kaanani.....Yote, tisa mzungu kafanikiwa sana kushika akili za mwafrika. Katika hili, alifanikiwa mno....
Comments zako zinatakiwa zichapishwe, halafu Kila mwanafunzi WA secondary hadi vyuo vikuu wazisome kwa lazima kwenye mitaala yao.
 
Wanga na mama jusi mmekaa macho mkisubiri mtoto azaliwe mfanye uharibifu na kupokonya alichopewa na God, tutakuwaje na akili kipindi mnatuweka stoo toka utotoni mwetu na kuacha kopi zikipuyanga tu.
Mnatu-remote mno.
 
Back
Top Bottom