Utumwa wa Tume ya Uchaguzi Tanzania: Wasemavyo Maaskofu wa TEC

Utumwa wa Tume ya Uchaguzi Tanzania: Wasemavyo Maaskofu wa TEC

Titicomb,
Umejieleza vizuri. Shida kubwa ambayo hujagusa ni hii: Bosi wa NEC alisema alikuwa anatangaza matokeo anayoletewa na watu wasiojulikana. Tukiziba tobo hilo mengine ni rahisi. Tunataka NEC itoke kwapani mwa bosi wa watu wasiojulikana. Umeelewa?
 
Umejieleza vizuri. Shida kubwa ambayo hujagusa ni hii: Bosi wa NEC alisema alikuwa anatangaza matokeo anayoletewa na watu wasiojulikana
Hii itabidi uniwekee 'reference' ya sauti, maandishi au video ili tuweke sawa kumbukumbu na kuondoa mashaka yoyote ya ukweli wa hoja hii.
Nahofia isijekuwa ni maneno ya kutengenezwa.
 
Umejieleza vizuri. Shida kubwa ambayo hujagusa ni hii: Bosi wa NEC alisema alikuwa anatangaza matokeo anayoletewa na watu wasiojulikana. Tukiziba tobo hilo mengine ni rahisi. Tunataka NEC itoke kwapani mwa bosi wa watu wasiojulikana. Umeelewa?
Jambo lingine la muhimu ni lazima tutambue hatua ya kutangaza matokeo halali ya uchaguzi ni hatua ya mwisho kabisa katika kutupatia viongozi halali na safi kwa njia ya kidemokrasia.

Lazima uwepo msingi mzuri na imara wa kutupatia wagombea safi waliochaguliwa kugombea kupitia vyama vyao kwa njia na fedha safi.
Tusiweke nguvu nyingi kwenye paa la nyumba ambayo imejengwa juu ya msingi mbovu.
Tuweke nguvu sawa kwenye kila hatua ya ujenzi wa nyumba yetu Tanzania.

Namaanisha tusiweke nguvu kwenye hatua ya upigaji kura na utangazji matokeo bila kuwekeza nguvu sawa katika hatua ya kupata wagombea safi kwa njia safi.
 
Hii itabidi uniwekee 'reference' ya sauti, maandishi au video ili tuweke sawa kumbukumbu na kuondoa mashaka yoyote ya ukweli wa hoja hii.
Nahofia isijekuwa ni maneno ya kutengenezwa.

Acha hizo. That is common knowledge. Mwaka 2015 Bosi wa NEC alibanwa na Lowassa aeleze kwa nini taarifa anazotangaza ni tofauti na matokeo halisi yaliyoko vituoni.

Jibu la boss lilikuwa fupi: "Inawezekana ni tofauti kwa kuwa mimi natangaza kile ninacholetewa mezani na wasaidizi wangu".

Hao wasaidizi wake walikuwa ni kina nani? Watu wasiojulikana walioletwa na serikali. Maana boss huyo asingejitofautisha na wasaidizi wake halisi walio chini yake kimamlaka.

Hapo vipi?
 
Mama Amon, Tunayosheria ya gharama ya uchaguzi je, inajitosheleza kwa mantiki ya maelezo yako haijitoshelezi.

Tunasheria ya uchaguzi huoni kama unakubali hoja ya paschal na zangu kuwa system ya nchi ni mbovu ndiyo maana kuanzia vyama na vyombo dola vyote vinajiendesha kivyake.

Sheria ya uchaguz inamilikiwa na TAKUKURu je nani anaiunda takukuru? Inaamrishwa na nani?
Likewise polisi

Kudai tume pekee ni kujichelewesha I hope tumeelewana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi nyingi hazikujengwa na wanasiasa zilijengwa na wanaharakati pamoja na wanataaluma kwa kuwatumia wanasiasa.

Uingereza wenye mamlaka ya kuamua sura ya nchi ni maaskofu na malords achana na wanasiasa WA house of Commons

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ramark,
Jawabu langu tangu jana ni hili:

kuna wakati wa kufanya radical changes na wakati wa kufanya incremental changes; mazingira ya leo hayaruhusu radical changes; hivyo twende na mkakati wa incremental changes kwa kuanza na Tume ya uchaguzi. Simple.
 
Nchi nyingi hazikujengwa na wanasiasa zilijengwa na wanaharakati pamoja na wanataaluma kwa kuwatumia wanasiasa.

Uingereza wenye mamlaka ya kuamua sura ya nchi ni maaskofu na malords achana na wanasiasa WA house of Commons

Sent using Jamii Forums mobile app

Wanasiasa, wanaharakati, wanateolojia, wanafalsafa and so on ni change agents ktk mchakato wa kujenga nchi; kujenga nchi ni mradi wenye majukumu mengi, kila mmoja akianzia upande wake; hivyo, hakuna mwenye monopoly juu ya kila jukumu ktk mradi huu.

This being the case, can you reframe your point?
 
Bosi wa NEC alisema alikuwa anatangaza matokeo anayoletewa na watu wasiojulikana.
Mwaka 2015 Bosi wa NEC alibanwa na Lowassa aeleze kwa nini taarifa anazotangaza ni tofauti na matokeo halisi yaliyoko vituoni.
Jibu la boss lilikuwa fupi: "Inawezekana ni tofauti kwa kuwa mimi natangaza kile ninacholetewa mezani na wasaidizi wangu".
Hapa kipi ni kipi?
Kisheria "wasaidizi wangu" siyo sawa na "watu wasiojulikana".
 
Hapa kipi ni kipi?
Kisheria "wasaidizi wangu" siyo sawa na "watu wasiojulikana".

Kisheria? Sheria ya TISS inaongelea covert operations kwa ajili gani? Na je watu wasiojulikana waliosambaa nchi nzima siku chache kabla ya NEC kutangaza matokeo walikwenda kuchanja kuni au kuteka maji? Tusipoteze muda kuhusu hili. Twende kwenye hoja za msingi hizi:

- hoja ya kupanua uhuru wa Tume inao umantiki, uharaka na umuhimu?

- kama jibu ni ndio, methodolojia ya kuitekeleza iweje?

- na kwa ajili ya matokeo ya haraka nani abebe ajenda hii?
 
Mama Amon,
Kwa hivyo mkuu umehamua kuwa dikteta?
Unapanga peke yako mjadala wa hoja zipi ni za msingi na unataka sisi wachangiaji wengine tuchangie subserviently kile unachotaka kukisikia?

Basi ngoja turudi kwenye hoja kuu kumbe tatizo ni sheria ya TISS?
Au tatizo ni sheria ya uchaguzi au Tume ya Uchaguzi?

Kumbuka sheria inayo zungumzia uundwaji/muundo wa tume ya uchaguzi haijaweka ulazima kwamba wasaidizi wa bosi wa NEC wawe watu wa TISS.
Hatuoni kwamba wanao dai sheria ya uchaguzi na katiba yetu ndiyo tatizo kwenye mchakato wa uchaguzi wanaweza kuwa sahihi?

Angalizo:
Mimi sisemi hakuna udanganyifu kwenye mchakato wa upigaji kura, na utangazaji wa matokeo ya kura.
Nachokoza hoja ili watu wafunguke zaidi maoni yao na mambo yaliyo fichika.
 
Luka 19

47 Naye akawa akifundisha kila siku hekaluni. Lakini wakuu wa makuhani, na waandishi, na wakuu wa watu walikuwa wakitafuta njia ya kumwangamiza;
48 wasione la kutenda, kwa kuwa watu wote walikuwa wakiandamana naye, wakimsikiliza.
 
Basi ngoja turudi kwenye hoja kuu kumbe tatizo ni sheria ya TISS?
Au tatizo ni sheria ya uchaguzi au Tume ya Uchaguzi?


Hili nimelifafanua jana:

RECAP:

Uhusiano uliopo kati ya sheria ya TISS na sheria ya NEC unakuja kwa njia ya BOSS wa TISS kuwa BOSS wa NEC na kuwa BOSS wa CCM.

Ndio maana tunataka katiba izuie Rais kuwa mwenyekiti wa Chama cha siasa na ndio maana tunataka NEC isiwajibike kwa Rais.

Tunataka NEC iwajibike Bungeni na sio kuwajibika kwa BOSS wa TISS ambaye ni BOSS wa CCM pia

Checks and balances are needed now than ever!
 
Kwa hivyo mkuu umehamua kuwa dikteta? Unapanga peke yako mjadala wa hoja zipi ni za msingi na unataka sisi wachangiaji wengine tuchangie subserviently kile unachotaka kukisikia?

Kwa kuwa bandiko hili nimelianzisha mimi, ninalo jukumu la kuhakikisha mjadala unakidhi mahitaji ya hoja niliyoisanifu. Kuna tatizo hapo?
 
Wanasiasa, wanaharakati, wanateolojia, wanafalsafa and so on ni change agents ktk mchakato wa kujenga nchi; kujenga nchi ni mradi wenye majukumu mengi, kila mmoja akianzia upande wake; hivyo, hakuna mwenye monopoly juu ya kila jukumu ktk mradi huu.

This being the case, can you reframe your point?
Sawa wote wanashiriki lakini hoja ipo kwa yupi anayeshika bendera ya badiliko likaleta tija kwa taifa.

Tazama leo na tangu 1993 imeonekana tume huru ni hoja ya kipinzani na si ya kinchi, sikatai maelezo yako mazuri ya awali lkn bado hayaonekani kuungwa mkono na wananchi wengi, achilia mbali sisi tunaojua
Ebu tueleze mtu mtambaswala, mpeta vvawa anajua tume tuliyonayo si huru kwa muktadha tunaojadili hapa?

Hoja ya kinchi ingeelezwa vizuri na watu wote katika kila pembe ya nchi, utasema sheria mpya ya azaki na kuzuia mikutano sawa, wanaharakati wengi hawajaiona hii kama ajenda ya kuitetea, wasomi hawajaona kama inamsingi kwa maisha yetu hivyo kugubikwa kuwa ya wanasiasa ambao Leo wanataka kuwaambukiza wanaharakati, wanAtaaluma, wanafalsafa na theologist ambapo inachukua muda kuungwa mkono hivyo kuchelewesha mchakato badala ya wanasiasa wangeichukua Leo ili kutekeleza

Na ndiyo maana nabaki na hoja yangu kuwa wanasiasa hutumiwa na wote hao kwa maslahi ya wengi kwani mwanasiasa akiianzisha tunatazama mengi na hasa maslahi yao zaidi badala ya umma, hivyo tunaamini hata Leo Mkipata nafasi ya kuunda tume mtaiunda kwa maslahi ya vyama vya siasa badala ya nchi na umma kwa kuwa wananchi hawajui wanataka chombo cha namna gani kutokana na ufinyu WA maarifa tume bora ya uchaguzi.

Kama jambo hili haliko kisiasa kwa nini marekebisho haya yaje Leo mkiacha marekebisho mengine muhimu kabisa hasa Muundo na uendeshaji WA bunge ambao ndiyo roho ya nchi?

Mkilitengeneza bunge likawa bora tutapata organs nzuri ya nchi na serikali.

Bunge letu ni LA hovyo kuliko hats hiyo tume ya uchaguzi. Tume bora tukiipata itatuletea tena wanasiasa tunaowabeza Leo na CCM dola itakuja kwa jina lingine kupitia chama kingine inaweza kuwa CDM dola hivyo kwangu sioni msingi WA ubatizo WA maji WA MTU mzima bila kitubio ongeza ubatizo WA roho.

Kiufupi, in kuwa, ninyi wanasiasa hamjaamua kuitengeneza Tanzania bora. Hivyo hata huu mkwamo uliopo Leo nahofu unaweza kutokea chini ya chama kingine na ndiyo maana nasema mabadiliko mnayotaka ni ya kisiasa bila wananchi.


We we kumbuka chadema ilipotumiwa na wasomi 2005-2015 ilikuwa matawi yapi? Hoja zilikuwa zinatoka ndani zinapata backup ya wananchi achilia mikutano lkn hoja nzito zenye maslahi ya wengi.

Kama kweli mnataka mngeamua basi kwa kuwatumia hao watu wakati ninyi mnaileta hoja hii basi kila pembe napo ikalipuka kupitia azaki, wanataaluma na theologist achilia muunganiko mficho WA maaskofu WA kilatini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kuwa bandiko hili nimelianzisha mimi, ninalo jukumu la kuhakikisha mjadala unakidhi mahitaji ya hoja niliyoisanifu. Kuna tatizo hapo?
Unaweza kukosa kujuwa suluhisho la kweli la tatizo unalo lalamikia sababu unafunga uwezekano wa kupokea mawazo mbadala.

Bandiko ni lako lakini hoja ni ya wazi kujadiliwa, sioni tatizo kwa hulka ya binadamu kutaka kusikia anachopenda, wewe sio wa kipekee kiasi cha kukosa udhaifu huu wa kibinadamu.
Kwani hata unao walalamikia hawapendi kusikia unayowataka watupatie.
 
Mama Amon, Hivi naomba niulize

Hiyo tume itaundwa wapi?

Mswada utapelekwa na nani?

Mswada utaandaliwa na nani?

Mfumo WA maoni ya wadau utazingatiwa vipi na nani? Je, wanadau na wabunge wanajua tume tunayoitaka?

Ninyi wapinzani mnamajority ya kupitisha jambo linalichefeua serikali na dola yake?

Mnaweza kuwabadilisha wabunge vilaza WA ccm kufikiri kama binadamu WA taifa hili?

Mnaweza kuunda tume huru kwa dikrii ya rais?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama unavyouliza

Ebu tuambie nani abebe hili badiliko?
Jawabu langu tangu jana ni hili:

kuna wakati wa kufanya radical changes na wakati wa kufanya incremental changes; mazingira ya leo hayaruhusu radical changes; hivyo twende na mkakati wa incremental changes kwa kuanza na Tume ya uchaguzi. Simple.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom