Utumwa wa Tume ya Uchaguzi Tanzania: Wasemavyo Maaskofu wa TEC

Utumwa wa Tume ya Uchaguzi Tanzania: Wasemavyo Maaskofu wa TEC

Nundu_Tanzania,

Ndugu Nundu, umeandika nini hapo? Sikiliza rafiki:

- kazi ya Tume ya uchaguzi ni kusimamia haki ya umma kuamua na kusimika serikali yao kwa sababu wanazozijua wapiga kura hata kama ni wajinga, mbumbu, mabwege au hohehahe.

- Katika suala la haki ya kujitawala (right to self determination) Wapiga kura hawa wanazo haki sawa kabisa na haki walizo nazo wasomi, wajuzi, wajanja, na matajiri.

- ushahidi pekee unaokuwa mikononi mwa Tume sio habari ya elimu, maarifa au ukwasi wa wapiga kura, bali idadi ya kura za ndiyo na hapana mintarafu wagombea.

- kwa hiyo, uhuru wa Tume hautegemei weledi wa wapiga kura.

- badala yake uhuru wa Tume unategeme weledi na uadilifu wa maafisa wa Tume, uimara wa kibajeti wa Tume, kutoingiliwa na serikali, kutoingiliwa na vyama vya siasa, na kutoingiliwa na mahakama pasipo sababu nyeti.

Mjadala uendelee.
 
Aisee uchambuzi ni nadra kufanywa na mwanamke,,,,Nina wasi wasi kama ni mke, kama ndyo basi nampongeza
"Mishenyi" baba wa "Mfumo dume," umeniudhi kupindukia kwa sentensi yako hii.
Yamkini una kutu ubongoni mwako!!!
 
Aisee uchambuzi ni nadra kufanywa na mwanamke,,,,Nina wasi wasi kama ni mke, kama ndyo basi nampongeza

Bw. Mishenyi, tafadhali sana. Nitake radhi. Mimi ni mama Amon. Sasa unashindwa kuelewa hilo. Mwanamume hazai Bwana.

Lakini pia usisahau historia. The first programmer was a woman called ADA LOVELACE.

Tunapoadhimisha siku ya science, technology, engineering and mathematics (STEM Subjects) huwa tunamtumia kama role model.

So, IQ is not always a function of sex. Mjadala uendelee.
 
Mama Amon,
Mmmh Mama Aron uko vizuri sana!Huwa sipendi kusoma mada ndefu lakini bandiko lako hili nimelisoma mara 2 na kupitia page kwa page za wachangiaji!

Hongera sana kwa mada fikirishi na inayovuta hisia za msomaji! Naunga mkono hoja,kuna ulazima wa kufanya mabadiliko makubwa ya kimuundo kwenye Tume yetu ya uchaguzi ili kuifanya iwe huru!

Maeneo yote uliyogusa ni muhimu tujayapigania kama wananchi tunathamini haki yetu ya maamuzi kupitia sanduku la kura!Watakaopuuza hoja zako ni wale ambao hawaoni umuhimu wa kura zao kuwa na maana halisi ya kura!
 
Mama Amon,
Umenikumbusha historia ya teknolojia ya mawasiliano!Kipindi hicho ilikuwa radio communication na ilikuwa wakati wa vita!Sasa ilikuwa ni hatari kuongea kitu kwenye radio call maana mawasiliano yanaweza kuwa intercepted!Tofauti na matarajio ya wengi,mwanadada kutoka Hollywood(jina nimesahau) ndiye aliyekuja na ufumbuzi!Tena alikuja na idea kutoka kwenye piano!

Ambapo kila kibao kilitoa frequency tofauti!Hapo akaona inawezakana kila simu ikapigwa kwa frequency tofauti inayobadilika kila wakati hivyo kuzuia uwezekano wa kujua mawasiliano yanafanyika katika frequency gani!Daaah hii documentary nitaitafuta niione upya maana ni kitambo sana!
 
Sky Éclat . Hawa kina Membe ndiyo wale wale, wakiwa ndani ya system wanashindwa kuidhauri vizuri kiti. Kwa uhusiano aliokuwa nao na JK , alishindwa nini kumshauri waiache nchi ikiwa katika mfumo unaoeleweka na ulio fair kwa kila mwananchi ?!.

Akili zinawakaa sawa wakishakuwa nje ya mfumo, jambo ambalo halisaidii, kwani aliye na kiti anafaidika na ubovu uliopo .

Sent using Jamii Forums mobile app
Unafiki ni?1.-----

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha historia ya teknolojia ya mawasiliano!Kipindi hicho ilikuwa radio communication na ilikuwa wakati wa vita!Sasa ilikuwa ni hatari kuongea kitu kwenye radio call maana mawasiliano yanaweza kuwa intercepted!Tofauti na matarajio ya wengi,mwanadada kutoka Hollywood(jina nimesahau) ndiye aliyekuja na ufumbuzi!Tena alikuja na idea kutoka kwenye piano!Ambapo kila kibao kilitoa frequency tofauti!Hapo akaona inawezakana kila simu ikapigwa kwa frequency tofauti inayobadilika kila wakati hivyo kuzuia uwezekano wa kujua mawasiliano yanafanyika katika frequency gani!Daaah hii documentary nitaitafuta niione upya maana ni kitambo sana!

Mdada huyoooo...
Screenshot_20200320-174533.png
 
Mama among
Umeeleza hoja hii vizuri kwa kutumia falsafa iliyotumiwa na maaskofu katika kujenga hoja ya ujumbe wa kwaresma pamoja na mitazamo ya waandishi wa siasa, historia, theolojia na falsafa ya kanisa na jamii ktik kukamilisha ukombozi WA mwanadamu kwa wengi na si kwa wote kwa tafsir ya kigiriki.

Hivyo, tume nayo inatakiwa kutumia neno LA kigiriki kuonesha ukombozi WA wengi na si wote kutokana na uhalisia WA falsafa ya uchaguzi (options) hivyo, nawe na mm pamoja na maaskofu tunataka ukombozi WA wengi kutoka minyororo hiyo tajwa kupitia mamlaka dola iliyotajwa na MC....... Mtendaji huyu Tume abadilike vipi au afutwe vipi bila bidii ya kambi ya Mbowe?

Nimekuwa napinga hoja ya kutaka vitu vya dezo kwani hata yesu hakuleta ukombozi kwa dezo ya Mungu Bali aliipigania hukumu ili aipate na haskwepe kwa faida ya wengi na ndiyo maana hakuomba hukumu kwa pilato wala herode ila aliendelea kuonyesha ridhaa kwa yote yatakayoamriwa vilevile tukiangalia maisha ya Mashahidi na wafia dini hawakuomba kifo kwa dezo ila walionesha determined kutetea walichokiamini na si kufa kibudu Bali kufa baraka, Lengo hapa ni je kweli nia ya marando mtei IPO kwa kambi mbowe au azaki pia siye raia? J

e, kweli tunataka zana hii kwa dhamira thabiti ya kulima na kuvuna mazao? Au tunataka watu WA kulima shamba bila zana ili tuvune mazao machache yatakayotosha mahitaji yetu ya kuendelea kuita tena watu ili tuendelee kulima kwa mikono.

Dhamira ya mtei hatuna tena wala marando. Tunachotafuta sasa ni dezo ya rais ambaye an apply principal- agent theory hivyo uamuzi wake bado utategemea faida za nadharia hiyo. Hivyo tunapiga kwata hapahapa.

Pascal
Tume tunayotaka watu wengi hatutaki shirikishi tunataka kama jibu LA swali la kwanza LA serikali kwa time ya 1999 rejea juu .
Tunataka tume inayojitegemea, najua nchi nyingine kama S.A ambako tume yao ni huru na shirikishi, tunataka tume inayozingatia weledi, uhalisia na siyo hisia za watu ndani ya tume hilo hapana.

Sheria ya uchaguzi inatokana na katiba iliyopo ambayo iliyoiunda Tume, tazama sheria ya uchaguzi ni ya mwaka gani? Achana na mabadiliko ambayo bado hayakuweka uwanja WA vyama vya upinzani.
Hatuweze kubadili sharia nawakati katiba ni ya chama kimoja.

Katiba inasema itikadi yetu ujamaa na wakati chadema katiba yao ni ubepari, mpaka hapo hata timu mbowe akishinda hawezi kuitawala kwa itikadi yake au atafuata katiba ili naye asahau maslahi ya wengi

Katiba yetu ndiyo inatamka rais as head of state na anapoteua tunataka uhalisia WA Mkuu WA nchi hill LA serikali bahati mbaya kupitia katiba.

Tuunde nchi ya wote kupitia wengi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bold statement, though it lacks support. As per standard rules of intellectual engagement, Can you provide grounds, warrants and backings to your claim pls?
State sponsored kidnappings, abductions and killings of his criticisers.
 
We still have plenty of time.

Sent using Jamii Forums mobile app
Muda umekwisha, na hatukujiandaa kuitaka Tume huru tumelazimishwa na timu mbowe kama nchi Sasa ndiyo tutaanza kuitafuta.

Bandiko LA mama amon liwe silaha ya watz pamoja na biografia yake bila kusahau barua ya timu mbowe kwa rais ili tuanze labda na kesi ya mabadiliko ya katiba, sheria pia miswada ya mabadiliko ya katiba na sheria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muda umekwisha, na hatukujiandaa kuitaka Tume huru tumelazimishwa na timu mbowe kama nchi Sasa ndiyo tutaanza kuitafuta.
Bandiko LA mama amon liwe silaha ya watz pamoja na biografia yake bila kusahau barua ya timu mbowe kwa rais ili tuanze labda na kesi ya mabadiliko ya katiba, sheria pia miswada ya mabadiliko ya katiba na sheria

Kwa nini unafikiri muda umekwisha?

Tunahitaji muswada wa mabadiliko ya sheria na katiba kwa ajili ya kusema kuwa:

-tume iwajibike bungeni

- tume isitumie watumishi wa umma kutekeleza kazi zake

- tume ichotewe fedha kutoka consolidated fund kwa mujibu wa sheria na sio kwa mujibu wa huruma ya serikali.

- rais wa nchi asiwe maenyekiti wa chama cha siasa

-kanuni za bunge zinaruhisu muswada huu kwenda kwa hati ya dharula.

-Kwa hiyo muda upo na unatosha.

Unaonaje?
 
Ramark,
Ramark,

Kuhusu Mbowe na Chadema, niseme haya:

- katiba ya chadema inatamka dhamira ya kushika hatamu za uongozi kwa njia ya sanduku la kura

- kama ilivyo kwa kila binadamu team mbowe hufanya maamuzi kwa kutumia motive hii: quest for power--political, economical, social, sexual, religious or otherrwise.

- kwa hiyo sahau propaganda hasi kuwa kina mbowe hawana hamu ya kuingia ikulu. Tujadili bigger issues.

Lkn kuhusu, best alternative to negotiated agreement (batna) iliyo kichwani mwa mbowe endapo nguvu ya hoja kabla ya uchaguzi mkuu itakwama sijui. Tunasubiri kusikia kutoka kwenye kinywa chake.

But, theoretically kuna options mbili:

- ama kususia uchaguzi mkuu na kuendeleza mapambano baada ya uchaguzi

- au kwenda kwenye uchaguzi mkuu hivyo hivyo kwa lengo la kuwaomba wapiga kura ridhaa ya kushika hatamu za uongozi wa nchi na kisha kuibomoa Tume nabkuijenga upya ndani ya SIKU TATU!

Nahisi option ya pili inaweza kumpa mbowe comparative advantage kuliko kambi ya MAGUFULI wanavyofikiri.

Najaribu kufikiri tu.
 
Mama Amon, Unajua namna bunge linavyoendeshwa kufikia mjadala kujadiliwa bungeni? Ukipeleka kwa hati ya dharura inategemea upande wenye majority bungeni hivyo kama hawapendi itarudi haraka.

Mnaotaka hiyo tume tafuteni majority bungeni kupitia tume hii ilirekebishe.

Lasivyo nenden mahakaman

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM inaingia kwenye uchaguzi ikiwa ni chama dola chenye NEC, polisi, vyombo vya dola, huku mgombea mmoja akitumia ving'ora, state cars, state media, state officials, state logistics ambazo pia zinatumika kulipa all the private media kufanyia publicity halafu wanashindana na mgombea mwingine with nothing!.

Kwa mtindo huu, kwa sheria hii iliyopo, CCM itatawala milele!.

P
Pascal, hii hapo juu sio tatizo la sheria ya uchaguzi. Ni sababu tume ya uchaguzi inaogopa kugombeza na uoga huo unatokana na ukweli kuwa tume haiko huru.

Mwenyewe unakiri kuwa CCM inaingia Kwenye uchaguzi ikiwa ni chama dola chenye NEC. Kama unakiri kuwa NEC ni ya CCM unashindwaje kuona kuwa tume haiko huru?
 
Makala nzuri sana, nilishangazwa sana na uamuzi wa mahakama ya rufani wa kuifuta hukumu ya mahakama kuu iliyopiga marufuku wakurugenzi wa halmashauri na miji kuwa wasimamizi wa uchaguzi.

Tume haiko huru kabisa, mbali na mwenyekiti wa tume kuna mtu anaitwa mkurugenzi wa uchaguzi wa tume, huyu pia ni mteule wa rais na ndio bwana mipango wa kuiba kura.
Mahakama iulizwe kukikuwa na uharaka gani wa kuisikiliza hiyo rufaa ya Mwanasheria Mkuu wa serikali? Ndani ya Miezi miwili rufaa imesikilizwa rufaa nyingine zina miaka zaidi ya sita na hazijasikilizwa.
Kulikuwa a nini Kwenye hii rufaa ??????
 
Back
Top Bottom