UWATA wamesambaratisha familia yetu

UWATA wamesambaratisha familia yetu

“Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa”

Matapeli wengi wamejificha kwenye mgongo wa dini, pole sana.

Kuna mdada single maza wa watoto watatu, kila mtoto na baba yake, aliwafukuza watoto wake kisa kaambiwa na mchungaji kazaa na mapepo kwahiyo watoto wake nao ni mapepo. Kukosa msaada wa majirani kuita polisi wamkamate wale watoto wangekufa!!
So sad, ukiongezea na ujinga wa watu wengi kushindwa kuhoji baadhi ya hizo imani kwa mfano ipo dhana moja viongozi wengi wa hizi imani huwaaminisha wafuasi wao eti kwamba kuna laana sijui mizimu ya mababu na mabibi au hata shangazi na watu engineo wa karibu inayoweza kukudhuru. Kutwa kucha wanahubiri uchonganishi kwenye nyumba za ibada.

Hebu imagine Bibi yako au babu aliyemzaa mama/baba yako eti alikuwa na maroho mabaya, hivi inaingia akilini kweli? Jiulize, huyu kiongozi ni mganga au mpiga ramli? Anapata wapi ujuzi wa kutambua kuwa bibi/babu yako alikuwa na hao roho wachafu? Huoni hata na wewe wajukuu zako wakija kuaminishwa imani hizi za kishenzi hata na wewe utakuja kuitwa mchawi au mshirikina wakati huo umeshatangulia mbele za haki? Tuwe na Imani lakini vitu vingine ni lazima tuhoji kama vina ukweli wowote ama ni njia ya wajanja kuchukua sadaka
 
Angalizo: Ukishakuwa na hela tafuta ama mganga au kinga ya imani, muda wowote unakuwa target ya matapeli wa kiimani.
Utaamua imani yako uikabidhi kwa mababu wa Abrahamu au mababu wa Kiafrika.

It seems hiyo familia haina mtoto wa kiume, ingekuwa mimi ningeshafanya neutralisation fulani kwenye njia za uongo uongo anakopitishwa mzee.
Hii ni kweli, hali aliyonayo sasa hivi na maisha aliyokuwa nayo ni huzuni kwakweli
 
Imani ni moyoni,popote pale unaweza abudu iwe ndani ,kanisani,msikitini, njiani popote.....
Kuna tofauti Kati ya imani na dini?
Biblia imekataza kusema vibaya imani ila haijakataza kuikosoa dini,tuzikosoe dini kulingana na Maandiko tuwakosoe hao viongozi kulingana na Maandiko ila tuwe makini sana kuikosoa imani ya Mtu ,kwasababu yeye binafsi anajua maana yake na madhabahu yake
 
Tuwakosoe uwata kulingana na Matendo yao,
Hebu kama kuna mtu atueleze hao uwata wapo wapoje ......najarbu kuwafatilia kwa makini niwaelewe hebu kama mtu alishawahi kuwa ama yupo humo au ana mojambili tatu aseme
 
So sad, ukiongezea na ujinga wa watu wengi kushindwa kuhoji baadhi ya hizo imani kwa mfano ipo dhana moja viongozi wengi wa hizi imani huwaaminisha wafuasi wao eti kwamba kuna laana sijui mizimu ya mababu na mabibi au hata shangazi na watu engineo wa karibu inayoweza kukudhuru. Kutwa kucha wanahubiri uchonganishi kwenye nyumba za ibada.

Hebu imagine Bibi yako au babu aliyemzaa mama/baba yako eti alikuwa na maroho mabaya, hivi inaingia akilini kweli? Jiulize, huyu kiongozi ni mganga au mpiga ramli? Anapata wapi ujuzi wa kutambua kuwa bibi/babu yako alikuwa na hao roho wachafu? Huoni hata na wewe wajukuu zako wakija kuaminishwa imani hizi za kishenzi hata na wewe utakuja kuitwa mchawi au mshirikina wakati huo umeshatangulia mbele za haki? Tuwe na Imani lakini vitu vingine ni lazima tuhoji kama vina ukweli wowote ama ni njia ya wajanja kuchukua sadaka

Ni hatari kwakweli na wajinga ni wengi matapeli wanajipigia tu.
 
Hapana ni Jumuiya ya uamsho wa wakristo Tanzania, ni muungano wa wakristo toka madhehebu mbalimbali walioungana pamoja kwa njia ya kutubu dhambi na kuziacha kwahiyo hapo walutheri hawahusiki
Hata naelewa basi,, bora umenifafanulia nawasikiaga tu hata sijui wanafananaje😌
 
Back
Top Bottom