UWATA wamesambaratisha familia yetu

UWATA wamesambaratisha familia yetu

Angalizo: Ukishakuwa na hela tafuta ama mganga au kinga ya imani, muda wowote unakuwa target ya matapeli wa kiimani.
Utaamua imani yako uikabidhi kwa mababu wa Abrahamu au mababu wa Kiafrika.

It seems hiyo familia haina mtoto wa kiume, ingekuwa mimi ningeshafanya neutralisation fulani kwenye njia za uongo uongo anakopitishwa mzee.
Naomba unipe guidance naweza tumia njia zako
 
Nawafahamu kwa Sehemu, kwa ninavyo wafahamu mengi uliyoongea ni chuki binafsi au chuki na kikundi chao,
Najua wanaumoja sana ila hawavunji ndoa ,kwasababu nawafahamu watu kadhaa wanaosali huko na wana ndoa na watu wa madhehebu mengine,
Kuhusu nguo ni chuki binafsi, wanavaa kiheshima sana kama waisilamu au masista sema hawavai uchungu tu, hawasuki kama wasabato,hawavai heleni na hawana mambo mengi na hata wanaume hawavai vbya,
Ni kikundi cha kilokole ndio na si kanisa

Mwisho
Inawezekana kabla ya huyo kufunga ndoa ndoa ilikuwa na shida, na mahusiano yenu ya familia yapo na shida pia
Endelea kuwatetea maana hayajakufika
 
Hapa kuna uongo mwingi ndugu mtoa post. Kwanza UWATA si dhehebu bali ni kikundi cha watu wa madhehebu mbali mbali wanaojumuika pamoja kusali (fellowship). Kila mtu husali kanisani kwake. Hawafungishi ndoa wala hawabatizi, ndoa utafungisha kanisani kwako (katika madhehebu yako) ni watu wanaoheshimu dini za watu wengine na ni watii. Ni watu wasiopenda kuumiza wengine kabisa. Kujiunga na fellowship yao ni hiyari.


Wanachoamini.
1. Biblia ni NENO la Mungu. Hivyo kila ajiungae huamini hivi si kwa kulazimishwa bali kwa kujua hivyo na kuamini mwenyewe.

2. Mwanauwata anaamini kuwa YESU Kristo ni mwana wa Mungu alizaliwa, akaileta injili kwa ajili ya kumkomboa yeyote amwaminie, akasulubiwa msalabani akafa akazikwa akafufuka na yu hai sasa, naye atawahukumu wote ambao hawakumwamini na kuishi uovu.
3. Wanaamini wokovu ni kwa Yesu tu , na kuufikia ni kutubu, yaani kuungama dhambi na kuzicha. Biblia, Mithali 28:13. Azifichae dhambi zake hatafanikiwa bali yeye aziungamae na kuziacha atapata msamaha.

4. Wanaamini kuwa kuishi wokovu wa Kristo Yesu ni kuwa na amani na watu wote. BIBLIA, Webrania 12:14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;

5. Wanaamini kabisa kuwa familia ilianzishwa na Mungu, hivyo wao hawawezi kamwe kufusa ama kuharibu familia.


Kwa haya tu sidhani kama ndio hao au ni impersonation imefanywa na hao watu wabaya wanaojiita uwata lakini si UWATA niwafahamuo.
We jamaa mtu kama sio mwana-UWATA unaonekana kama shetani mbele yao, sasa upendo gani huo walionao
 
Endelea kuwatetea maana hayajakufika
Dawa,nimeongea kwa nijuavyo ,ninavyo jua wale hawafungishi ndoa,ingawa sina hakika,
Nahisi familia yenu ina shida pahala,na kabda ya ndoa na wasiwasi hamkuwa pamoja,
Kwa sababu hoja kubwa ni ndoa mpya!!?ila je ndoa ilikuwepo kabda?
Ila kuhusu mavazi kwa kweli unawaonea wanavaa vzr mno ,hawana mambo mengi ingawa wanaitana wapendwa na wanaumoja sana
 
Acha blablaa we dogoo
Kwani sisi hatuwaoni huku mtaani nyie wa uwata?

Zamani mlkuwa mnasali kwa makelele mnapiga kama mayoe na miruzi
Mlikuwa mnaboa mno mtaani

Mnamtindo wa kukaa nyumba moja watu zaidi ya 50 na akipatikana tajiri mnahakikisha mmemnyonya abaki hana hata jero
Kusali watu 50 mbona ni jambo la kawaida .. TAFES wanasali hata watu 100 TYCS, ASA.. vivyo hivyo.


Kwa habari ya kusali kwa makelele kila mtu ana mtazamo wake kuhusu kelele. Hivyo kwa kusali kwao kwa namna uiitayo kelele haimaanishi ndio ubaya. Au wataka kila mtu kusali utakavyo wewe? Si ndo kutaka kupotosha watu huko ndugu.


Kwa habari ya kunyonya matajiri, fafanua wananyonywaje.

Ushauri watafute hao wanauwata ufanye utafiti maana huwajui kabisa.
 
We jamaa mtu kama sio mwana-UWATA unaonekana kama shetani mbele yao, sasa upendo gani huo walionao
Hebu nifafanulie nami nijue jamaa .. maana nataka kujua wakoje. Kwa namna gani wanakuona shetani. Usizungumze hisia lakini nahitaji useme kweli.
 
Ni tatizo la ndugu yako. Mwalimu Andongwisye ni mfuasi mzuri wa UWATA amekuwa mfuasi mzuri wa UWATA kuanzia Diploma na sasa ni DR. Tunae pia mkuu wa shule ya Masukila FUBILE ndiye mwalimu bora zaidi kyela nzima kwa kipindi kirefu sana . Ameingia kichwa kichwa huyo ushauri wangu mumuacheni endeshemni mambo yenu chini ya mama na yeye aendelee na hao watu wake. Amen
Masukila siku hizi inafaulisha?? Chini ya fubile? Japo simjui namsikia tu toka kyela sekondari
 
Kusali watu 50 mbona ni jambo la kawaida .. TAFES wanasali hata watu 100 TYCS, ASA.. vivyo hivyo.


Kwa habari ya kusali kwa makelele kila mtu ana mtazamo wake kuhusu kelele. Hivyo kwa kusali kwao kwa namna uiitayo kelele haimaanishi ndio ubaya. Au wataka kila mtu kusali utakavyo wewe? Si ndo kutaka kupotosha watu huko ndugu.


Kwa habari ya kunyonya matajiri, fafanua wananyonywaje.

Ushauri watafute hao wanauwata ufanye utafiti maana huwajui kabisa.
Sizungumzii kusali
Nazungumzia kuwa huishi nyumba moja watu lukuki!!

Nenda mbeya utawakuta wapo kibao saaaana

Hawa jamaa wanajifanya wanaumoja lakini behind the scenes ni wanyonyaji,
Wakikumata mwenye hela watahakikisha umebaki mtupu, utauza hadi ndoo ili upeleke hilo group liishi

Wanazaliana mno mpaka kero,
Unakuta ndoa ina miaka 10 afu Wana watoto watano na mimba ya sita
 
Dini ni nusu ya uchizi😂😂😂 niliacha kwenda makanisani miaka minne sasa kwa sababu ya kuwa na watu wajinga wajinga tu na imani za uongo uongo
 
Mnamo mwaka 2013 baba yangu alikutana na mchungaji mmoja huko Moshi na baba yangu akamueleza kiu yake ya kuwa karibu na Mungu kwani ujana wake hakuwa mtu wa kwenda kanisani. Mchungaji(jina limenitoka lakini ningemtaja) akamueleza habari za uwata na kwamba angemkutanisha na kiongozi wa dhehebu hilo, basi wakaanza kwenda wote faraghani na hata ilipofika wakati wa kurudi Dar(nyumbani) baba hakufika kabisa nyumbani na baada ya muda tukasikia amepatiwa mke kanisani na hivyo anafunga nae ndoa ( hakuwa anashaurika tena na tuliona walakini kwenye mental health yake, hakuwa tena kama zamani).

Ndugu zake pamoja na mama walijitahidi kuweka mapingamizi kwenye makanisa ya Dar hivyo hawakuweza kufunga ndoa hapa dar ikawalazimu ndoa ifungwe Morogoro tena wazazi fake walisimama kwa upande wa baba yangu umma ukidanganywa baba yangu wazazi wake wamefariki ilhali wako hai. Aliporudi mambo yalikuwa mabaya zaidi kwenye biashara zake mambo yakabadilika alifukuza wafanyakazi wake wote mpaka ndugu zake wa damu na kuajiri watu kutoka Uwata, alikataa malipo kwa njia ya dollar kwa kusema kwamba ni ushetani, wateja walimkimbia na kumwita kichaa! 😭 pesa alizofanikiwa kupata tunasikia amewekeza kwenye vitegauchumi vya UWATA… alipokuwa akija nyumbani kutusalimia ilimbidi aende kanisani akaungame kwa maana amefanya dhambi( huko walimbatiza mama yangu jina dellilah na kwamba yeye ni mchawi!😢) hata ilipobidi ndugu kwenda kumuona ofisini kwake ni lazima hao watu wa uwata nao wawepo hapo ofisini kusikiliza 🤦🏿.

Hali yake kiuchumi imekuwa mbaya mno waliomjua zamani na sasa wanahuzunika. Alikuwa baba, kaka, mume na mtu bora sana nitawalaumu UWATA siku zote za maisha yangu kwa kuwakosesha malezi ya baba wadogo zangu kwa maana si mapenzi tuu hata huduma hapaswi kutoa kwa watoto waliozaliwa na delila!
bado watu wanaamini mambo ya dini hadi leo
 
Sizungumzii kusali
Nazungumzia kuwa huishi nyumba moja watu lukuki!!

Nenda mbeya utawakuta wapo kibao saaaana

Hawa jamaa wanajifanya wanaumoja lakini behind the scenes ni wanyonyaji,
Wakikumata mwenye hela watahakikisha umebaki mtupu, utauza hadi ndoo ili upeleke hilo group liishi

Wanazaliana mno mpaka kero,
Unakuta ndoa ina miaka 10 afu Wana watoto watano na mimba ya sita
Hizi ni chuki kuzaa,ni mihamu yako na Kukosa elimu ya uzazi,
 
Mnamo mwaka 2013 baba yangu alikutana na mchungaji mmoja huko Moshi na baba yangu akamueleza kiu yake ya kuwa karibu na Mungu kwani ujana wake hakuwa mtu wa kwenda kanisani. Mchungaji(jina limenitoka lakini ningemtaja) akamueleza habari za uwata na kwamba angemkutanisha na kiongozi wa dhehebu hilo, basi wakaanza kwenda wote faraghani na hata ilipofika wakati wa kurudi Dar(nyumbani) baba hakufika kabisa nyumbani na baada ya muda tukasikia amepatiwa mke kanisani na hivyo anafunga nae ndoa ( hakuwa anashaurika tena na tuliona walakini kwenye mental health yake, hakuwa tena kama zamani).

Ndugu zake pamoja na mama walijitahidi kuweka mapingamizi kwenye makanisa ya Dar hivyo hawakuweza kufunga ndoa hapa dar ikawalazimu ndoa ifungwe Morogoro tena wazazi fake walisimama kwa upande wa baba yangu umma ukidanganywa baba yangu wazazi wake wamefariki ilhali wako hai. Aliporudi mambo yalikuwa mabaya zaidi kwenye biashara zake mambo yakabadilika alifukuza wafanyakazi wake wote mpaka ndugu zake wa damu na kuajiri watu kutoka Uwata, alikataa malipo kwa njia ya dollar kwa kusema kwamba ni ushetani, wateja walimkimbia na kumwita kichaa! 😭 pesa alizofanikiwa kupata tunasikia amewekeza kwenye vitegauchumi vya UWATA… alipokuwa akija nyumbani kutusalimia ilimbidi aende kanisani akaungame kwa maana amefanya dhambi( huko walimbatiza mama yangu jina dellilah na kwamba yeye ni mchawi!😢) hata ilipobidi ndugu kwenda kumuona ofisini kwake ni lazima hao watu wa uwata nao wawepo hapo ofisini kusikiliza 🤦🏿.

Hali yake kiuchumi imekuwa mbaya mno waliomjua zamani na sasa wanahuzunika. Alikuwa baba, kaka, mume na mtu bora sana nitawalaumu UWATA siku zote za maisha yangu kwa kuwakosesha malezi ya baba wadogo zangu kwa maana si mapenzi tuu hata huduma hapaswi kutoa kwa watoto waliozaliwa na delila!
uwata ndio wale wanaotuhumiwa wamama kutovaa vyupi? wanavaa magauni kama siku ya sikukuu kijijini, wanajitesa sana ila hawafuati njia sahihi ya kumwona Mungu. uwata ni cult.
 
Mimi hapa nilikuwa UWATA japo sasa hivi nakunywa bia. Ulichozungumza mtoa mada napata ukakasi kwa sababu UWATA kama UWATA hawana mamlaka ya kufungisha ndoa bali utafungia kwenye kanisa lako mama.
UWATA wanakutanika faragha kila siku na kufundishana neno la Mungu ili kutimiza andiko lililoandikwa "kutanikeni kila siku maadamu iitwapo leo"
 
U
Mimi hapa nilikuwa UWATA japo sasa hivi nakunywa bia. Ulichozungumza mtoa mada napata ukakasi kwa sababu UWATA kama UWATA hawana mamlaka ya kufungisha ndoa bali utafungia kwenye kanisa lako mama.
UWATA wanakutanika faragha kila siku na kufundishana neno la Mungu ili kutimiza andiko lililoandikwa "kutanikeni kila siku maadamu iitwapo leo"
UKaasi sio?
 
Hebu nifafanulie nami nijue jamaa .. maana nataka kujua wakoje. Kwa namna gani wanakuona shetani. Usizungumze hisia lakini nahitaji useme kweli.
Sio hisia wewe kama sio mpendwa wewe unaambiwa ni wa duniani sasa mi nikajiuliza wenyewe ni wawa wapi uzuri nimekaa nao hata salamu zao za kukumbatiana nazijua
 
Back
Top Bottom