Uwendawazimu wa watu wa dini (Ukristu na Uislamu) upo hapa

Uwendawazimu wa watu wa dini (Ukristu na Uislamu) upo hapa

Ni aidha watu hawana elimu ama ufahamu wa kina kuhusu dini ama ni propaganda zimejaa kichwani ama wanapenda kusikia na kuona wanavyopenda. Binafsi nashangaa sana hasa humu jukwaani watu wakigombana kuhusu dini Fulani, kitu ambacho hakikusaidii chochote na si kwamba utaumiza mtu nk. Kwa Kila mtu akiishi vile dini yake inavyosema ilimradi hadhuru mtu kwani Kuna tabu gani?, wale wa mizimi wafuate mizimu Yao no problems na wengine pia, suala la Imani likimuingia mtu basi muache apambane nalo na si kumlazimisha aamini unavyoamini wewe, lazima tujifunze kuishi maisha yetu na kuacha kufuatiliana Ili basi Kila mtu apambane na Hali yake. Mbona hakuna tabu kuhusu hili, it's very simple.
 
Hapa tunafahamishana tu mkuu,usiwe na hisia kali sana katika mijadala kama hii lakini fikiria kidogo.
Biblia imeruhusu baadhi ya watu wauwawe iyo iko hivyo,"

Luka 22:36 Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko au mkoba auchukue. Asiye na upanga, auze koti lake anunue upanga.
Pia lipo andiko yesu anamzuia mwanafunzi wake asiuwe kwa upanga maana akifanya hivyo na yeye anauwawa kwa upanga.

Pia yesu mwenyewe aliruhusu mtu auwawe mbele yake isipokuwa kwa sharti la mtu aliye safi tu ndio atekeleze hiyo hukumu,haikutekelezeka kwa sababu kila mtu alijihukumu nafsi yake,
hiyo inamaanisha kama wangelikuwepo waliosafi ingelikuwa halali kwao kutekeleza hukumu hiyo.
yohana 8:7 Viongozi wa Kiyahudi waliendelea kumuuliza swali lao hilo. Naye akainuka na kusema, “Yeyote hapa ambaye hajawahi kutenda dhambi awe wa kwanza kumponda jiwe mwanamke huyu.”
Kwahiyo unakuja kuona kwamba kuuwa kwa mujibu wa maandiko kupo,hivyo unakuja kuona kwamba wanaouwa wenzao huwa na sababu zao nyingine nyuma ya pazia ila dini huwa ni kichaka tu cha kuhalalishia uovu wao!
Dini zote zinalinda uhai wa mtu!
Umeandika vizuri ukahitimisha vibaya. Hakuna dini inalinda uhai wa mtu. Soma historia ya ukristo au uislamu uone kama kuna waliolindwa zaidi ya kuuawa pale Imani yao ilipopingana na dini husika. Pia kasome vita ya Majimaji uone jinsi wananchi walivyogoma na kulipiza kisasi baada ya Mungu wao kudharauliwa kule peramiho
 
Ibrahim na mitume wengine walikuwa waislam.
Hapana hawakuwa waislam,ila waislam wameamrishwa kuzifuata mila za hao watu, ndio maana mtu hawezi kuwa muislam kama hamuamini Ibrahim,musa,daudi,yusuph,ayubu,yesu seleman na wengine.muhamad amefundisha kuwa ili uwe muislam wa kweli ni lazima uwaamini hao kwa kufuata mila na mafundisho yao.ndio maana katika uhalisia waislam wanafuata mafundisho ya hao mitume kuliko wakristo kwa sababu imani yao ili ikamilike ni lazima kuwaamini.uislam umekamilishwa na muhamad,kusema kina musa walikua waislam ina leta shida kidogo hasa kama hujaleta ushahidi.
 
Wakristo wanaamini tiketi ya kukupeleka ni kumkiri kristo kuwa bwana na mwokozi hayo mengine ni baadae kwanza.
Mbinguni ndiyo wapi au nini?je bata ,mbwa,miti,nk haitaki kwenda mbingu kwa baba yao?

Nachelea kusema uhafrika labda ni dhambi
 
Ama kweli nyani kaoni kundele
topshot-muslim-worshippers-approach-to-kiss-and-touch-the-hajar-al-aswad-a-rock-set-into-the.jpg

Hata ingekua wewe ungevumilia usicheke huku unaona watu wamenunua mifuko miwili ya cement alafu wametengeneza sanamu kwa mikono yao na wanaliomba toba na baraka ungevumilia kweli?View attachment 3262384
 
Dini unaisingizia tu

Elimu ndiyo inawafanya mtawaliwe kifikra.Elimu inawafanya muwe maroboti ya watu wachache wenye akili ya kugundua vitu.Mfano madaktari ni maroboti ya watu wachache waliobarikiwa uwezo wa kuweza kugundua dawa. Roboti la kisomi kila linapoongea kitu ni lazima liwe na "reference" lilipoyatoa hayo maneno maana roboti la kisomi huwa haliko huru kuongea maneno yake,limefungwa kifikra.

Pale alipo roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.
Roho wa bwana wako ni yupi?kati ya wazazi na yesu au muhamad nani zaidi?
 
Kwenye hili naomba utenganishe Catholicism na Protestantism
Wote hao na wewe ukiwemo ni mbwa wa kizungu ilimradi wewe ni mwafrika.

Yaani ulivyojinga umeshindwa kutambua kuwa "protestantism" inatokana na neno "protest-" ikimaanisha "kupinga" hivyo "waprotestants" ni wakristo wanaopinga "catholism.


Kama huna hata uwezo wa kujua hiliutaweza kujikombia kifikira kweli?
 
Wote hao na wewe ukiwemo ni mbwa wa kizungu ilimradi wewe ni mwafrika.

Yaani ulivyojinga umeshindwa kutambua kuwa "protestantism" inatokana na neno "protest-" ikimaanisha "kupinga" hivyo "waprotestants" ni wakristo wanaopinga "catholism.


Kama huna hata uwezo wa kujua hiliutaweza kujikombia kifikira kweli?
Kwani ni ugomvi mkuu? Tendea haki jina lako ulilolichagua
 
Umeandika vizuri ukahitimisha vibaya. Hakuna dini inalinda uhai wa mtu. Soma historia ya ukristo au uislamu uone kama kuna waliolindwa zaidi ya kuuawa pale Imani yao ilipopingana na dini husika. Pia kasome vita ya Majimaji uone jinsi wananchi walivyogoma na kulipiza kisasi baada ya Mungu wao kudharauliwa kule peramiho
Nakuelewa sana,ila shida ipo hapa,watu wengi hawafuati mafundisho ya dini bali wanafuata na kuamini sana viongozi wao wa dini,sasa hawa viongozi wanapokua wamebeba interest zao binafsi chini ya mwavuli dini,ndipo wanapojaza chuki kwenye vifua vya waumini,vita mwisho mauaji.waumini wanakua wanaamini wanaipambania dini kumbe wanapambania maslahi ya mtu,taasisi,nchi au bara.

Naposema dini zinalinda uhai namaanisha,katika amri kumi za Mungu kwa wakristo.
amri ya 7 kama sio ya sita inasema USIUE.

Na waislam nao kur'an inasema
( Al maida 32);“Aliye muuwa mtu bila ya yeye kuuwa, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote”.
Na wanakatazwa hata kusadiana katika uovu,
(Al maida :2) “Wala msisaidiane katika dhambi na uadui. Na mcheni Mwenyezi Mungu"
Yaani kuua mtu mmoja kwa waislam ni kama umeua watu wote.
Kwahiyo unapoona watu wanashabikia mauaji katika dini au jambo lolote ujue hao watu hawazifuati dini zao ila wanaongozwa na hisia zaidi na chuki(sumu) walizomezeshwa.
 
Unamaanisha ambao hawasali hawana akili?
Umeiona sms kwamba nimeandika hawana akili? Soma text vizuri mkuu au uko bize!!

Hapa duniani, hata kabla ya wazungu na waarabu bado suala la Imani lilikuwepo. Babu zetu waliabudu Hadi pale walipokuja wageni na kubadili mtindo wa kuabudu.

Tahadhali; uwe atheist, mpagani au vyovyote vile ukumbuke unapokuwa unaponda ibada au dini za watu Ni lazima uhakikishe unaabudu eneo lolote la imani kwa sababu, wanadamu suala la kuabudu Ni maumbile. Tumeumbwa hivyo, Kuna nafasi ya ibada katika maisha ya mwanadamu, hili halikwepeki.

Unapoona watu wanaingia uislamu au ukristo maana yake Ni kuwa tayari dunia imepima na kujiridhisha kuwa mtindo huu ndio mtindo wa kileo wa kuabudu lkn pia unaeleweka na wengi Kama msingi mkuu wa ibada. Ukitaka kujua hili jaribu angalia takwimu za wingi wa waumini ktk dini hizi utajua kitu.
 
Umeiona sms kwamba nimeandika hawana akili? Soma text vizuri mkuu au uko bize!!

Hapa duniani, hata kabla ya wazungu na waarabu bado suala la Imani lilikuwepo. Babu zetu waliabudu Hadi pale walipokuja wageni na kubadili mtindo wa kuabudu.

Tahadhali; uwe atheist, mpagani au vyovyote vile ukumbuke unapokuwa unaponda ibada au dini za watu Ni lazima uhakikishe unaabudu eneo lolote la imani kwa sababu, wanadamu suala la kuabudu Ni maumbile. Tumeumbwa hivyo, Kuna nafasi ya ibada katika maisha ya mwanadamu, hili halikwepeki.

Unapoona watu wanaingia uislamu au ukristo maana yake Ni kuwa tayari dunia imepima na kujiridhisha kuwa mtindo huu ndio mtindo wa kileo wa kuabudu lkn pia unaeleweka na wengi Kama msingi mkuu wa ibada. Ukitaka kujua hili jaribu angalia takwimu za wingi wa waumini ktk dini hizi utajua kitu.
Aisee wingi wa supporters unawezaje kudhihirisha uzuri wa kile kinachofuatwa? Miaka ya zamani kulikuwa na ubaguzi afrika kusini na vitabu vilieleza miongozo ya jinsi ya kubagua wengine. Na weupe wengi waliwabagua weusi, hii haikufanya jambo la ubaguzi liwe jema hata kama Sheria iliruhusu. Mtindo fulani wa maisha siyo mzuri sababu una wafuasi wengi. Mimi naweza kuanzisha jambo jema nikakosa wafuasi ila uzuri wa jambo lenyewe utabaki pale pale
 
Mtu mwenye akili timamu kabisa pia hawezi acha kusali, labda aache ili iwe njia ya kuhalalisha maovu yake.
Kusali?

Kwa maana ipi? Neno kusali lina tafsiri nyingi, hata tahajudi(meditation)wengine wanaita ni kusali.
 
Huko sahihi sana....ila waache waamini hicho wanachokiamini na wewe amini unachokiamini kiongozi
Kuwaacha waamini wanachoamini siyo sahihi sana, hasa ikizingatiwa kuwa wanachoamini kinaweza kikawa kinarudisha nyuma maendeleo, kuchochea chuki na kuleta utengano katika jamii.

Imani zinazotoa mafundisho ya kuua wasiyo wa imani yako kwa mfano, hazitakiwi kufumbiwa macho katika ulimwengu wa watu waungwana, ni barbarism iliyopitwa na wakati.
 
Dini unaisingizia tu

Elimu ndiyo inawafanya mtawaliwe kifikra.Elimu inawafanya muwe maroboti ya watu wachache wenye akili ya kugundua vitu.Mfano madaktari ni maroboti ya watu wachache waliobarikiwa uwezo wa kuweza kugundua dawa. Roboti la kisomi kila linapoongea kitu ni lazima liwe na "reference" lilipoyatoa hayo maneno maana roboti la kisomi huwa haliko huru kuongea maneno yake,limefungwa kifikra.

Pale alipo roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.
Basi Bwana ndiyo Roho😇
 
Back
Top Bottom