Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

As I mention Above that spiritual matters is not for low minded but is for those who are already reached at the high peak of being open minded .
Unakimbia kimbia tu As always....kiroho is unfalsifiable n unprovable ninaweza amka nikasema kitu fulani ni kiroho na nyie mna bidi muamini tu coz u got no choice...it's bullshit
 
Unakimbia kimbia tu As always....kiroho is unfalsifiable n unprovable ninaweza amka nikasema kitu fulani ni kiroho na nyie mna bidi muamini tu coz u got no choice...it's bullshit
Hilo chaka la kiroho unaweza ibukia nalo ukajipigia pesa kwa kondoo na apo ndipo matapel wanapojifichia.
 
Unapo anza kubwatuka na kusema hakuna mungu huu tu. niusibitisho tosha wa uwepo wake kama kweli mungu hayupo ume reply ili iweje.???
Unaweza kupoteza muda wako kujadili kitu ambacho hakipo.???
Jibu ni hapana.
Unacho kifanya wewe ni kumpinga.
Fikiria kwanza kabla huja kurupuka chukuwa hiyo itakusaidia.
 
Elimu yako haija kugomboa.
Hivi unaweza kupoteza muda wako kujadili kitu ambacho hakipo serious, usha sema hakuna mungu why bado una reply post za watu. S utulie tuu
Sasa kwa taarifa yako kama unadhani una mpinga mungu unajidanganya.
Unavyozidi kujadili ndo unazidi kumtukuza unless otherwise ukaa kimya.
 
Fikiria mimi nikurupuke huko nianze kuandika humu , aisee Mr melo yupo .
 
Hakikisha unatetea kiumbe unachokijua na sio kutaka kila mtu aamini hadith za kiarabu za juma na uledi.
Nasisitiza hakikisha unakijua unachokijadili, Kuna muda naona uzito kukuuliza. Mfano hiki ulichokiandika nikikuuliza swali kutokana nacho hakika utashindwa kujibu swali hilo.

Nataka uje kuthibitisha ya kuwa hizo ni hadithi za Kiarabu za Juma na Uledi. Hakikisha unachokiandika unakijua, hapo ukute hata Kiarabu hukijui, bali dini yenyewe huijui.

Nyinyi mna matatizo ya akili.
 
Hii maada ni ngumu sana. Any way ngoja kila mtu ashikilie anacho kijua
 
Mm ninachokuliza tu ni kwambs unakubali kwamba kuna realities beyond Logic...
Mfano wewe ndugu usijizime data wewe ni mwafrika je imani za kichawi/ushirikina unakubali zipo au hazipo?
Kama zikiwepo je ni mantiki gani inayoelezea occurences hizo...
Mfano ulioutoa ni kweli kwa mantiki za kibinadamu haiwezekani.... Lakini kuna matukio huripotiwa yanayokosa ufafanuzi kwa mantiki.... Vivyo hivyo swala la uwepo wa Mungu haliwezi kamwe kufit kabisa katika logic.. Lakini kutakuwa na traces chache ambazo zitakuwa na missing links.....
 
Ikiwa kuna ugonjwa mbaya sana, unaua watu vibaya.

Halafu kuna mganga muongo, anasema ana dawa inayotibu ugonjwa huu. Dawa hiyo haipo, lakini mganga huyu muongo anaitangaza kiujanja kuwa ipo, anawauzia watu. Watu wanatumia vidonge vya maboya wakifikiri nindawa inayotibu.

Watu wanakufa sana kwa ugonjwa huu.

Wengine hawajikingi na wanapata maambukizi kwa kutumaini dawa ya kuwaponya ipo.

Akija daktari mwingine anayejua kuwa hii dawa haipo, hiyo inayosemwa ni feki, utamsema vibaya huyu daktari anayeimulika hii dawa feki na kusema kwa nini anatumia muda wake kuisema dawa ambayo haipo?

Hapo unashindwa vipi kuelewa kwamba kumulika uongo na kiweka wazi ukweli ni jambo zuri?

Unamlaumu daktari anayeisema dawa ya uongo kwa kigezo cha kusema kwa nini anajishughulisha na dawa ya uongo?

Unaelewa hoja yako?
 
Mfano wako hauwenda na mada husika.
 
Thor yupo?
 
Nilichokuwa natafuta kwenye mfano huo ni parallel situation kwamba kama maelezo utayakosa huku unaweza tumia phenomenon nyingine ukapata majibu... Hivyo kama unakiri kwamba kuna vitu ambavyo vipo lakini hatuna maelezo ya kuvielezea kwa undani vivyo hivyo kumbe dhana ya kwamba Mungu yupo inaweza kuwa halisi sema tunakosa maelezo ya kimantiki kuelezea hilo... The allegories are just different but parallels..
 
Mimi sikubali uchawi kuwepo kwa sababu zile zile ambazo zinanifanya nisiamini uwepo wa Mungu.

Uchawi ni story ile ile ya miujuza, ni muendelezo wa story ya Mungu.

Hakuna mtu anayeweza kuthibitisha uchawi.

Nikikuuliza wewe kwa mfano, uchawi ni nini na unathibitishaje huu ni uchawi na huu si uchawi ila ni kitu tu ambacho sijakijua bado, utathibitishaje?

Mababu zetu walioishi miaka 300 iliyopita wakija leo na kuona teknolojia ya ndege, internet, TV, watasema uchawi.

Je, hilo linamaanisha teknolojia hizi ni uchawi?

Je, na wewe ukikutana na mtu mjanja mwenye trick ya teknolojia usiyoijua, akakwambia huu ni uchawi, utajuaje huu ni uchawi na si teknolojia tu usiyoijua?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…