Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Ni ajabu Sana kuendelea kuamini vitabu vilipitwa na maarifa.

Sayansi kila siku wanaendelea kufanya tafiti Zaidi, na Ku update taarifa mbalimbali.

Vitabu vya Dini vinamapungufu mengi mpaka unajiuliza huyu mungu, mbona hana Masri sahihi
Vitabu vya dini kama Qur'an ni muongozo kwa watu Sasa vipi kibadilike na kishakuwa muongozo.

Sayansi lazima ibadilike sababu kwa yenyewe siyo "Facts", bali ni mtindo tu maalumu ambao unatumika kuyasoma maumbile na kujua nini chanzo chake, hapa naongelea "Scientific Methods", kama ni msomi kweli na unafatilia kiundani Sayansi utanielewa nasema nini, ila kama ni shabiki na huna misingi ya Sayansi najua hapa huna hoja ya kunipa nguvu Sayansi mbele ya uhalisia.

Hapa unaongelea vitabu gani ? Labda vitabu vingine, ila sio Qur'an ukisema mpaka Qur'an, nitakuomba uweke udhaifu mmoja kisha tuujadili. Tuone nani mkweli.
 
Labda utuambie nani amesha tengeneza mbingu yake na kama hakuna basi ujewe kitu ambacho anakifanya mungu binadamu hakiwezi,
Kuhusu kuendelea na umbaji
Mungu hana mapungufu kila kitu kimekamilika hakuna alicho sahau na ndo maana wana sayansi wanatumia neno "Tumevumbua" ina maana kilikuwepo mungu ametakasika na kila sifa ya mapungufu

Nawa suburi
Hoja yako ya kwamba nani kaweza kutengeneza mbingu yake, na kama hakuna, kitu ambacho anakifanya Mungu mtu hakiwezi, kwa kuanzia, ina makosa ya kimantiki.

Logical fallacy. Logical non sequitur.

Ukweli kwamba mtu hajaweza kutengeneza mbingu yake unathibitisha kuwa mtu hajaweza kutengeneza mbingu yake.

Ukweli kwamba mtu hajaweza kutengeneza mbingu yake, hauthibitishi Mungu yupo kweli. Thibitisha kuwa Mungu yupo kweli.

Yani ni hivi, mimi nikishindwa kutengeneza filamu kama ya James Bond 007, hilo halithibitishi kwamba James Bond 007 yupo kweli.

Ukweli kwamba mimi siwezi kutengeneza filamu ya James Bond unathibitisha tu kuwa mimi siwezi kutengeneza filamu ya James Bond. Inawezekana kabisa nikawa siwezi kutengeneza filamu ya James Bond, na James Bond akawa hayupo, ni muhusika wa kufikirika tu wa riwaya na filamu, nje ya riwaya na filamu hizo hayupo.

Vivyo hivyo, inawezekana kabisa mimi nikashindwa kutengeneza mbingu yangu, na Mungu akawa hayupo. Hakuna contradiction wala logical inconsistency hapo.

Mimi kushindwa kufanya chochote hakuthibitishi Mungu yupo, kunathibitisha nimeshindwa kufanya hicho kitu.

Ukiunganisha mawili haya ambayo hayana uhusiano, unaanxa hoja kwa kufanya logical fallacy ya logical non sequitur.

Actually, mtu anaweza kusema kuwa ukweli kwamba hakuna mtu aliyeweza kutengeneza mbingu yake, unathibitisha Mungu hayupo.

Kwa sababu, Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote na ujuzi wote, angekuwepo, angeruhusu kila mtu awe na uwezo wa kutengeneza mbingu yake. Mungu huyo si mchoyo wa neema. Angetupa tu neema hiyo ambayo yeye haimgharimu kitu.

Kwa hivyo, ukweli kwamba hakuna mtu aliyeweza kutengeneza mbingu yake, unaonesha Mungu huyo hayupo.

Hoja yako ukiitazama kijuujuu, utaona inaonesha Mungu yupo.

Lakini, ukiichambua kwa kina, utaona inaonesha Mungu hayupo.
 
Qur'an pekee ndo haina mapungufu
Nimeshaweka mapungufu ya Quran mengi sana hapa. Mtu aliomba, nilivyomuwekea ayatatue, akakimbia.

Huwa mnaanza hivihivi. Mkiwekewa aya zinazopingana na kuonesha mapungufu ya Quran, mnakimbia.

Bisha nikuwekee aya hapa.
 
Vitabu vya dini kama Qur'an ni muongozo kwa watu Sasa vipi kibadilike na kishakuwa muongozo.

Sayansi lazima ibadilike sababu kwa yenyewe siyo "Facts", bali ni mtindo tu maalumu ambao unatumika kuyasoma maumbile na kujua nini chanzo chake, hapa naongelea "Scientific Methods", kama ni msomi kweli na unafatilia kiundani Sayansi utanielewa nasema nini, ila kama ni shabiki na huna misingi ya Sayansi najua hapa huna hoja ya kunipa nguvu Sayansi mbele ya uhalisia.

Hapa unaongelea vitabu gani ? Labda vitabu vingine, ila sio Qur'an ukisema mpaka Qur'an, nitakuomba uweke udhaifu mmoja kisha tuujadili. Tuone nani mkweli.
Sayansi Sio fact Tena mkuu.
 
Vitabu vya dini kama Qur'an ni muongozo kwa watu Sasa vipi kibadilike na kishakuwa muongozo.

Sayansi lazima ibadilike sababu kwa yenyewe siyo "Facts", bali ni mtindo tu maalumu ambao unatumika kuyasoma maumbile na kujua nini chanzo chake, hapa naongelea "Scientific Methods", kama ni msomi kweli na unafatilia kiundani Sayansi utanielewa nasema nini, ila kama ni shabiki na huna misingi ya Sayansi najua hapa huna hoja ya kunipa nguvu Sayansi mbele ya uhalisia.

Hapa unaongelea vitabu gani ? Labda vitabu vingine, ila sio Qur'an ukisema mpaka Qur'an, nitakuomba uweke udhaifu mmoja kisha tuujadili. Tuone nani mkweli.
Ndoa za watoto wadogo, hizi sizikubaliani nazo
 
Unasema hayupo anaeweka maji kwenye nazi ni baba yako?
Kwa nini unajikita kwenye "anayeweka"?

swali lako lenyewe lina bias.

Hujasoma osmosis?

Soma hapa chini, hawamuhitaji Mungu kuelezea jinsi maji yanavyoingia katika nazi.



View: https://youtu.be/x2vmb_98hYw?feature=shared
 
Kuna jambo limenisukuma sana kuandika huu Uzi.
Mambo ambayo yanaendelea kuhusu uwepo wa mungu.
Kuna baadhi ya watu wa amini hakuna mungu nk.

Ni ingie kwenye point
Uwepo wa mungu una dhihirika kwa alama zake na viumbe vyake.

Hebu tutafakari kama hakuna mungu nani alieumba bahari, jua, mbingu, binadamu, wanyama hivi vitu vimetokea vipi kama hakuna alieviimba.

Leo hii hata ukimchukuwa mtoto mdogo wa miaka mitatu ukamuuliza nani kaumba mbingu atakujibu mungu.

Vipi mtu mzima mwenye akili timamu unashindwa kutambua hilo.

Yapo mambo mengi sana yana thibitisha uwepo wa mungu naweza kesha kuelezea kiufupi, Tufahamu mungu yupo na yeye ndo ametuumba sisi ili tumuabudu yeye tu.
Huyo mtoto anakujibu hivyo kutoka kwenye utashi wake au kwa kufundishwa na wazee wake
 
Acha mengine yoote, hapo kwenye JUA

Unajua nimekuwa nikitafakari umuhimu wa Jua ni mkubwa sanaaa, bila jua hatupati maji kwsbb ya Evaporation, Transpiration n.k

Bila jua hatupati chakula kwsbb mmea hutengeneza chakula kukiwa na mwanga wa jua

Jua inafanya mifupa ya viumbe vyote vyny skeletons viwe strong

Joto la jua linaneutralize climate yetu

Aliyeumba au kutengeneza jua ni nani? Aliyeweka Ozone Layer ni nani?
Sasa ozone layer chemistry yake mbona inajulikana.. Hata leo binadamu tunaweza tengeneza ozone oxygen na very easy [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]vitu vingine mnajiaminisha kwasababu hamjataka tafuta maarifa
 
Kuna jambo limenisukuma sana kuandika huu Uzi.
Mambo ambayo yanaendelea kuhusu uwepo wa mungu.
Kuna baadhi ya watu wa amini hakuna mungu nk.

Ni ingie kwenye point
Uwepo wa mungu una dhihirika kwa alama zake na viumbe vyake.

Hebu tutafakari kama hakuna mungu nani alieumba bahari, jua, mbingu, binadamu, wanyama hivi vitu vimetokea vipi kama hakuna alieviimba.

Leo hii hata ukimchukuwa mtoto mdogo wa miaka mitatu ukamuuliza nani kaumba mbingu atakujibu mungu.

Vipi mtu mzima mwenye akili timamu unashindwa kutambua hilo.

Yapo mambo mengi sana yana thibitisha uwepo wa mungu naweza kesha kuelezea kiufupi, Tufahamu mungu yupo na yeye ndo ametuumba sisi ili tumuabudu yeye tu.
Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee uliodumu kwa muda mrefu ni huu:

Hebu fikiria; unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwa ajili yetu na ataiangamiza(jiulize akili za huyo Mungu anaewatakia maafa watu wake)

Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza(kama vile hajielewi),

Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na uwezo wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie pepo tu tukale bata


Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyotaka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini,umalaya,ukahaba, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani (magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani( inaelekea huyu hajiwezi mpaka awe na msaidizi mhuni,amuache tu amchanganyie habari)

Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake


Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair


Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima

Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu


Yaani kuna mtoto wa fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwa ajili ya dhambi za watu wote duniani.... Kweli jamani ?

Akaitwa neno. Neno huyo alikua Mungu, mtoto wa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani na akapatikana. Shetani aliemuumba mwenyewe.

Mtoto huyu wa fundi kapenta, hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu dogo huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”

Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk


Hebu fikiria huko Arabia kuna maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakaopinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mabikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu.

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa

Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoagiza ili ukale bata sana baada ya kufa


Badhi ya sababu za kutoamini uwepo wake hizo hapo mtoa mada. Zipinge tuone!
 
Kuna jambo limenisukuma sana kuandika huu Uzi.
Mambo ambayo yanaendelea kuhusu uwepo wa mungu.
Kuna baadhi ya watu wa amini hakuna mungu nk.

Ni ingie kwenye point
Uwepo wa mungu una dhihirika kwa alama zake na viumbe vyake.

Hebu tutafakari kama hakuna mungu nani alieumba bahari, jua, mbingu, binadamu, wanyama hivi vitu vimetokea vipi kama hakuna alieviimba.

Leo hii hata ukimchukuwa mtoto mdogo wa miaka mitatu ukamuuliza nani kaumba mbingu atakujibu mungu.

Vipi mtu mzima mwenye akili timamu unashindwa kutambua hilo.

Yapo mambo mengi sana yana thibitisha uwepo wa mungu naweza kesha kuelezea kiufupi, Tufahamu mungu yupo na yeye ndo ametuumba sisi ili tumuabudu yeye tu.
Uko sahihi lakini umeshindwa kutetea dhana yako.

Hoja zako zimekuwa dhaifu mno kwenye kutetea dhana ya uwepo wa Mungu
 
Sasa ozone layer chemistry yake mbona inajulikana.. Hata leo binadamu tunaweza tengeneza ozone oxygen na very easy [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]vitu vingine mnajiaminisha kwasababu hamjataka tafuta maarifa
Mtu anakwambia Mungu yupo, kama hayupo nani kaweka maji kwenye nazi?

Hapo ndipo upeo wake wa kufikiri ulipo.

Yani kaona kauliza swali guuumu hapo.
 
Kuna jambo limenisukuma sana kuandika huu Uzi.
Mambo ambayo yanaendelea kuhusu uwepo wa mungu.
Kuna baadhi ya watu wa amini hakuna mungu nk.

Ni ingie kwenye point
Uwepo wa mungu una dhihirika kwa alama zake na viumbe vyake.

Hebu tutafakari kama hakuna mungu nani alieumba bahari, jua, mbingu, binadamu, wanyama hivi vitu vimetokea vipi kama hakuna alieviimba.

Leo hii hata ukimchukuwa mtoto mdogo wa miaka mitatu ukamuuliza nani kaumba mbingu atakujibu mungu.

Vipi mtu mzima mwenye akili timamu unashindwa kutambua hilo.

Yapo mambo mengi sana yana thibitisha uwepo wa mungu naweza kesha kuelezea kiufupi, Tufahamu mungu yupo na yeye ndo ametuumba sisi ili tumuabudu yeye tu.
Sio MUNGU wa dini hizi lakini.
 
Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee uliodumu kwa muda mrefu ni huu:

Hebu fikiria; unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwa ajili yetu na ataiangamiza(jiulize akili za huyo Mungu anaewatakia maafa watu wake)

Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza(kama vile hajielewi),

Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na uwezo wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie pepo tu tukale bata


Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyotaka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini,umalaya,ukahaba, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani (magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani( inaelekea huyu hajiwezi mpaka awe na msaidizi mhuni,amuache tu amchanganyie habari)

Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake


Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair


Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima

Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu


Yaani kuna mtoto wa fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwa ajili ya dhambi za watu wote duniani.... Kweli jamani ?

Akaitwa neno. Neno huyo alikua Mungu, mtoto wa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani na akapatikana. Shetani aliemuumba mwenyewe.

Mtoto huyu wa fundi kapenta, hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu dogo huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”

Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk


Hebu fikiria huko Arabia kuna maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakaopinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mabikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu.

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa

Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoagiza ili ukale bata sana baada ya kufa


Badhi ya sababu za kutoamini uwepo wake hizo hapo mtoa mada. Zipinge tuone!
Bila kujali uko sahihi au siyo sahihi, ila nimependa umejenga hoja zimenyooka
 
Sio MUNGU wa dini hizi lakini.
1.Mungu ni nini?

2.Kwa nini humkubali Mungu wa dini hizi (zipi)?

3. Kama kuna unayemkubali, unayemkubali wewe ni yupi?

4. Unayemkubali wewe ana tabia gani?

5. Kitu gani kinakufanya umkubali?

6. Unahakikishaje kuwa yupo kweli, na si muhusika wa hadithi za kufikirika tu?
 
Back
Top Bottom