Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Bila kujali uko sahihi au siyo sahihi, ila nimependa umejenga hoja zimenyooka
Hivi kweli,ni haki mpaka wa leo akili zetu zitawaliwe na utapeli wa watu kama sisi,wanaotaka tuiname wapite?
Kila siku wanadai muombeni,unaumwa lakini unaenda hospitali,wengine wanakata pumzi. Matatizo kibao,mara kwa waganga,kesho kanisani. Tena mara mia utapeliwe na mganga unayeona anajifanya anaongea na wakubwa.
Kila unaemuuliza Mungu ni nini? Anakujibu muumba. Kaumba lini? Jibu hamna. Niaminije? Eti we si umezaliwa ukakuta wanaamini?

Kwa hiyo,Mungu ni kufata mkumbo tu basi. Hawa hawa wanaojifanya wanamjua Mungu,wanakuja kwetu huku,ukinunuliwa bodaboda tu za 1500, unatoa ngombe eti fungu la 10 mijama inaenda kuuza na kupiga hela.
 
1.Mungu ni nini?

2.Kwa nini humkubali Mungu wa dini hizi (zipi)?

3. Kama kuna unayemkubali, unayemkubali wewe ni yupi?

4. Unayemkubali wewe ana tabia gani?

5. Kitu gani kinakufanya umkubali?
binafsi naamini MUNGU wangu mimi kaka mimi na hizo dini sjui Islamic au Christian sijui nini nishatoka huko sababu MUNGU wa hizo dini anaubaguzi kabisa.

Lakini MUNGU wangu mimi hana ubaguzi.

staki kukujibu maswali ya kuumiza kichwa saana...sababu bado najifuza hasa pia kupitia nondo zako.

Vipi kwanza ushalipa KODI ya nyumba mkuu?
 
Hivi kweli,ni haki mpaka wa leo akili zetu zitawaliwe na utapeli wa watu kama sisi,wanaotaka tuiname wapite?
Kila siku wanadai muombeni,unaumwa lakini unaenda hospitali,wengine wanakata pumzi. Matatizo kibao,mara kwa waganga,kesho kanisani. Tena mara mia utapeliwe na mganga unayeona anajifanya anaongea na wakubwa.
Kila unaemuuliza Mungu ni nini? Anakujibu muumba. Kaumba lini? Jibu hamna. Niaminije? Eti we si umezaliwa ukakuta wanaamini?

Kwa hiyo,Mungu ni kufata mkumbo tu basi. Hawa hawa wanaojifanya wanamjua Mungu,wanakuja kwetu huku,ukinunuliwa bodaboda tu za 1500, unatoa ngombe eti fungu la 10 mijama inaenda kuuza na kupiga hela.
Hii maada ni ngumu sana, na tatizo linaanzia kwa sababu ni nadharia.
 
Vitabu vya dini kama Qur'an ni muongozo kwa watu Sasa vipi kibadilike na kishakuwa muongozo.

Sayansi lazima ibadilike sababu kwa yenyewe siyo "Facts", bali ni mtindo tu maalumu ambao unatumika kuyasoma maumbile na kujua nini chanzo chake, hapa naongelea "Scientific Methods", kama ni msomi kweli na unafatilia kiundani Sayansi utanielewa nasema nini, ila kama ni shabiki na huna misingi ya Sayansi najua hapa huna hoja ya kunipa nguvu Sayansi mbele ya uhalisia.

Hapa unaongelea vitabu gani ? Labda vitabu vingine, ila sio Qur'an ukisema mpaka Qur'an, nitakuomba uweke udhaifu mmoja kisha tuujadili. Tuone nani mkweli.
Peponi lugha itakayo tumika ni kiarabu bisha na hii
 
Hii maada ni ngumu sana, na tatizo linaanzia kwa sababu ni nadharia.
Vitu vingine havihitaji kufikilia.

Jiulize,miaka kumi iliyopita mtaani kwako kulikuwa na madhehebu mangapi. Leo? Je, kila kukicha kuna Mungu mpya?
Haya,ndo yale yale. Mchungaji akihitaji kodi ya nyumba,ada za shule watoto,godolo kubwa, waumini mchangie. Muumini unaumwa pesa yote ulimalizia kwa matapeli,ohhh njoo uombewe. Gari la mchungaji halina mafuta,toeni elfu 50 apitie shell. Kudadeki zetu. Acha tupigwe tumetaka wenyewe.

Wenzetu hizo sadaka wanaweka akiba,mtoto anakuwa mamilioni yamesogea kwenye akaunti,huku tunawapa wajanja za kujengea kanisa na kununua vyombo vya mziki. Ukihoji viko wapi, mleteni akaombewe huyo ana pepo mchafu
 
Kwa nini unajikita kwenye "anayeweka"?

swali lako lenyewe lina bias.

Hujasoma osmosis?

Soma hapa chini, hawamuhitaji Mungu kuelezea jinsi maji yanavyoingia katika nazi.



View: https://youtu.be/x2vmb_98hYw?feature=shared

Sasa hizi si stori tu za Wana Sayansi, wewe leta ushahidi ya kuwa Maji yanapatikana vipi kwenye nazi, na lazima swali la nani anayaweka liwepo, sababu ya uwezo wa anaye yaweka.

Wewe leta ushahidi utuambie maji yanapatikana vipi kwenye nazi. Usituletee stori za Wanasayansi.
 
Mabikira 72 Mito ya pombe, hizi ni nadharia nzuri sana
Hivi, hujawahi sikia wanaojiita wachungaji wakisema kwamba kila kilichopo duniani huku na huko ni hivyo hivyo? Sasa unajiuliza huko kwa Sir God(bwana Mungu),baamedi wapo,madangulo fulu kujiachia,lodge zenye wale wadudu wanaowatesa wafaransa! Kama huko hakuna tofauti na duniani huku,wanaotaka kwenda watafata nini?
Mara Mungu yupo popote. Waliyopo jera wane huko huko. Kama hama makosa kashikiliwa kwa nini sasa?

Walihopo mochwari,huko huko. Kama kafa,ana msaada gani sasa!

Khe, badala ya mabikra hao 72, bora nipate msukule mi ntamalizana nae kimtindo. Si yale yale
 
binafsi naamini MUNGU wangu mimi kaka mimi na hizo dini sjui Islamic au Christian sijui nini nishatoka huko sababu MUNGU wa hizo dini anaubaguzi kabisa.

Lakini MUNGU wangu mimi hana ubaguzi.

staki kukujibu maswali ya kuumiza kichwa saana...sababu bado najifuza hasa pia kupitia nondo zako.

Vipi kwanza ushalipa KODI ya nyumba mkuu?
Kuamini unaruhusiwa kuamini unavyotaka, hata ukiamini uongo ni haki yako ya kikatiba na kiutu.

Lakini kwenye kutafuta ukweli hayo maswali yanahusika.

Kodi ya nyumba mimi silipi, nalipwa.

"I got cribs in the suburbs, the hood and the city" - AZ
 
Hii maada ni ngumu sana, na tatizo linaanzia kwa sababu ni nadharia.
Ni ngumu kama unataka kulazimisha Mungu ambaye hayupo awepo.

Vinginevyo unaweza kuthibitisha kimantiki kuwa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, hayupo, kama vile unavyoweza kuthibitisha 10 si square root ya 2 katika base 10 math.
 
Hivi, hujawahi sikia wanaojiita wachungaji wakisema kwamba kila kilichopo duniani huku na huko ni hivyo hivyo? Sasa unajiuliza huko kwa Sir God(bwana Mungu),baamedi wapo,madangulo fulu kujiachia,lodge zenye wale wadudu wanaowatesa wafaransa! Kama huko hakuna tofauti na duniani huku,wanaotaka kwenda watafata nini?

Khe, badala ya mabikra hao 72, bora nipate msukule mi ntamalizana nae kimtindo. Si yale yale
Blender mbona unacheka sasa?
 
Suhendra Mungu akiwanunulia feni watu wa Dar bila kuzama mifukoni mwao rudi hapa. Hawezi,nae kama sisi tu.
 
Peponi lugha itakayo tumika ni kiarabu bisha na hii
Sipo hapa kubishana, bali nipo hapa kubainisha haki na ukweli.

Hakuna ushahidi wa kweli kuonyesha hilo. Hadithi inayotumika kuelezea hili. Wanazuoni wetu wa Kiislamu wameidhohofisha. Mfano Imamu al-Albaaniy na wengine walio mtangulia.
 
Suhendra Mungu akiwanunulia feni watu wa Dar bila kuzama mifukoni mwao rudi hapa. Hawezi,nae kama sisi tu.
Hivi mungu anunue feni wakati kuna watu wana kufa njaa. Halafu hapa duniani sio mahala pa starehe lifahamu hilo kwanza
 
Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee uliodumu kwa muda mrefu ni huu:

Hebu fikiria; unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwa ajili yetu na ataiangamiza(jiulize akili za huyo Mungu anaewatakia maafa watu wake)

Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza(kama vile hajielewi),

Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na uwezo wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie pepo tu tukale bata


Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyotaka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini,umalaya,ukahaba, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani (magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani( inaelekea huyu hajiwezi mpaka awe na msaidizi mhuni,amuache tu amchanganyie habari)

Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake


Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair


Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima

Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu


Yaani kuna mtoto wa fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwa ajili ya dhambi za watu wote duniani.... Kweli jamani ?

Akaitwa neno. Neno huyo alikua Mungu, mtoto wa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani na akapatikana. Shetani aliemuumba mwenyewe.

Mtoto huyu wa fundi kapenta, hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu dogo huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”

Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk


Hebu fikiria huko Arabia kuna maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakaopinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mabikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu.

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa

Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoagiza ili ukale bata sana baada ya kufa


Badhi ya sababu za kutoamini uwepo wake hizo hapo mtoa mada. Zipinge tuone!
Kwanza INA bidi ufahamu kwamba mungu ametakasika na kila sifa ya mapungufu. Haja wahi kukosea kwa lolote lile

Hapa duniani tupo katika mtihani wa majaribio yule ambae atafaulu atapelekwa peponi ambae atafeli atapelekwa Motoni
Allah ametupa akili na maarifa tofauti na wanyama ukifanya dhambi nafsi yako lazima ikusute kwa masaasi uliyo Fanya hiyo ni dalili yakuwa binadamu tuna utashina uelewa

Shetani wala sio msaidizi wa mungu tambua kwanza hilo

Utofauti wa imani unachangiwa na utofauti wa uwelewa kati ya mtu mmoja na mwingine

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hekima ya Allah ili kuepusha mkanganyiko wa dini ya kiislam
Hebu fikiria wee mwenywe ange kuwa anajuwa kusoma na kuandika si mngesema Qur'an ametunga Muhammad hiyo ni hekma ya Allah na ndo mana Qur'an watu wameshindwa kuibadirisha kwa sababu ni maneno ya mungu direct.
 
Kama mungu angekuwepo basi Hata huu Uzi usingekuwepo kabisa
Nonsense
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, si mchoyo wa kuwafunulia watu wajue uwepo wake.

Angekuwepo, angejiweka wazi kwa namna ambayo kila mtu angejua kwa uhakika uwepo wake, kwa namna ambayo, mjadala wowote wa kuwepo Mungu usingewezekana.

Ukiona kuna swali lolote, kuna utata wowote, kuna kitabu, tafsiri, muktadha au sintofahamu yoyote katika kuelewa uwepo wa Mungu huyo, ujue hayupo.

Hapo utapata siasa za watu, saikolojia za watu, hadithi za kutungwa na watu tu.

Watu wananuwezo mkubwa sana wa kutunga hadithi ya uongo na kuifanya ukweli.

Wamelichukua karatasi, wakachora mapichapicha, wanakwambia hii ni noti ya dola 100 za Marekani, ukiwa nazo karatasi hizi 12 thamani yake ninsawa na kazi zote anazofanya Mtanzania wa wastani kwa mwaka mzima.

Tumekubali kwamba karatasi hizo zina thamani kubwa sana.

Hatushindwi kutunga hadithi na kuipa thamani yabukweli ambao haupo.

Tofauti ni kwamba, kwenye kuipa paper money thamani, tunakubali hapa tumeipa thamani tu hii karatasi.

Kwenye Mungu, Mungu naye ni hivyo hivyo tu, watu wamemtunga, wakampa thamani, wakati hayup
Hayo ni mawazo yako lakini haina maana kila mtu aishie hapo kufikiria kama ulivyo ishia wewe
 
Back
Top Bottom