Uzi maalum kwa wenye magari mabovu tu: Tupeane uzoefu na motisha na namna ya kuishi nayo

Na mwanangu mmoja huyo anayo Toyota Camry ya 99 inamtesa kinyama, picha inaanza huwa hatoboi nayo safari ya kilometer 9, Utakuta gari iko pembeni ya barabara ukifika mbele unamkuta anatembea kwa mguu huku amevaa kibegi chake cha kuning'iniza

huyu mwamba alikua na akili timam Ila magari mabovu yamemgeuza kashageuka kituko ila ye anaona Yuko sawa.
Ye ukimpelekea gari inayong'aa rangi na Ac iko vizuri tu unamshikisha ananunua.

Hashaurik kabadili magar ma 4 ndan ya miaka 5 na zote hakuna hata moja aliyofanikiwa kuiza baada ya yeye kununua huwa zinamfia mkononi
 
Cami ikianza ujeuri huwa ni jeuri kwelikweli unaweza kanyaga mafuta iko palepale tu inalia ng'eeeh ng'eeeee lakini haiendi!
Ni vigari vizuri sana kubana mafuta lakini vikianza kudeka sasa unaweza omba ukigawe bure
 


Hilo ni pepo, kemea....
 
Oooh ECU ni nini
Electronic Control Unit - hii ni mahali ambapo mfumo wote wa umeme wa gari unaratibiwa ili kuifanya injini kufanya kazi ipasavyo. Mambo ya kubadili gia, uchomaji wa mafuta nk..yaani ndiyo kompyuta ya gari.
 
Mkuu, kununua gari 0km inabidi kwanza uwe na mind za kifisadi, yaani usiwe na mawazo ya kuionea huruma hela. Pale posta DSM kuna agent wa Toyota anauza Toyota Rumion new model TZS 60m. Sasa mzee kutoa milioni 60 kununua Rumion inahitaji kujizima data, maana ukiagiza Japan iliyotumika kidogo unaipata kwa TZS milioni 30 hivi..yaani hapo kwa agent, Harrier used wanauza milioni 80 na wala sio za umeme, ukiwa na akili za kawaida huwezi nunua. Ni mpaka uwe umeizoea sana hela na una mind flani ya kifisadi, kutoionea huruma hela.
 
Lakini watu wananunua tu wala hawajali
 
Cami ikianza ujeuri huwa ni jeuri kwelikweli unaweza kanyaga mafuta iko palepale tu inalia ng'eeeh ng'eeeee lakini haiendi!
Ni vigari vizuri sana kubana mafuta lakini vikianza kudeka sasa unaweza omba ukigawe bure
Jamaa kasema toyota camry na sio cami
 
Doooh ebwana sio mchezo, kwanini sasa hashauriki ilhal anapata Hasara
 
Hahahaaha ni kwel kbasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…