Mkaka fulani maji ya kunde mwembamba mnyarwanda kasingiziwa .
Elimu: Darasa la saba ila mwenye degree mbili anasubiri.
Kazi : kuzurura kwenye nchi kila kona ya nchi ila napata hela ya kula
Kimo: 5.7ft.
Uvaaji: surual za vitambaa kwa sana shati nyeupe au rangi yeyote ila plain, kaunda suit kwa sana tai kama kawa, kadet kwa mbaali na simple shoes.
Chakula: napenda ugali dagaa wa kukaanga , Samaki, matembele, ugali dona, maziwa mgando na matunda na makande ya mahindi na njugu mawe.
Kipato: kwa mwezi Tsh.3.5m
Usafiri:Sina gari
Nyumba nimejenga:
Urafiki wa kijinga sina
Ulevi wangu: kusoma sana habari za siasa, Technolojia, na mengineyo.
Mawasiliano: simu natumia ya mkopo kutoka Tigo
Umri miaka 30
Dini : Mkristo aliemwamini Yesu na Kuzaliwa mara pili.
Sifa za mke nimtakae
Kimo: 5ft
Rangi: yeyote
Umbo: sio mnene na asiwe mwembamba akiwa anapenda kunyoa simple fulani huyo kipaumbele.
Anaefuga kucha mirefu atanisamehe,
Dini: mkristo aliezaliwa mara pili kama wewe ni wa jumapili tu utanisamehe,
Uvaaji: Vitenge fulani vigauni virefu na vifupi ila sio sana, viatu mchuchumio mrefu na mfupi nitakununulia na raba na simple fulani og [emoji1] mda mwingine kisket fulani na t-shirt [emoji1] na raba au blouse fulani na hiv na scafu au kikoti juu hivi daah, suruali nzuri tukiwa out na mazingira mengine utavaa sana tu ila mazingira tunayoishi utanisamehe .
Karibuni jamani khaaa jf hawapo kwel