Uzi Maalumu wa Vitabu vya maendeleo binafsi (Personal Development)

Uzi Maalumu wa Vitabu vya maendeleo binafsi (Personal Development)

Hili andiko lako nikisema nilisome lote, litaniongezea umasikini Mkuu..

Kwanini usiweke Kwa kifupi tu kuwa unauza Vitabu?
 
1622087027543.png

Hakuna anayeweza kubisha kwamba kumekuwa na ukuaji mkubwa sana wa teknolojia kwenye zama tunazoishi sasa.

Kuna maendeleo makubwa ambayo yametokea tangu kuanza kwa karne ya 21 ambayo hakuna aliyetegemea yangetokea kwa kasi kubwa hivyo.

Nani alidhani angeweza kuwasiliana na mtu aliye bara la mbali kwa kuonana uso kwa uso bila hata ya kutumia gharama kubwa?

Nani alifikiri vitabu vyote duniani vingeweza kuweka mtandaoni na ikawa rahisi mtu kuvipata na kuvisoma?

Nani alifikiri kungekuja simu za mkononi (simu janja) ambazo unaweza kuzitumia kufanya kila kitu kama unavyotumia kompyuta, kuanzia kuwasiliana, kutunza kumbukumbu, kupiga picha, kurekodi sauti na video, kuuza na kununua na hata kujifunza?

Haya ni maendeleo makubwa, ambayo mtu aliyefariki kwenye karne ya 20, akifufuliwa leo atashangaa mno kwa maendeleo haya na angetegemea kuona maisha ya watu yakiwa bora kutokana na maendeleo haya makubwa.

Lakini hapo ndipo atakaposhangazwa zaidi, kwani licha ya maendeleo makubwa ya teknolojia atakayokuwa ameyaona, atagundua maisha ya watu yako hovyo kuliko kipindi ambacho teknolojia hizo hazikuwepo.

Atashangaa kuona watu wakiwa wamechoka, wana msongo na hawana muda kabisa.

Atashangaa kuona watu wakitumia muda wao mwingi kwenye simu zao, kwa mambo ambayo hayana manufaa kwao.

Atashangaa jinsi watu wanaonena wivu kwa mambo ambayo wanayaweka kwenye mitandao ya kijamii.

Ujumbe atakaokuwa ameupata ni mmoja, kwamba teknolojia hizi mpya ambazo zina nguvu ya kufanya maisha ya wengi kuwa bora, zimegeuka kuwa gereza lililowafungia wengi na hawana tena uhuru wa kuyaishi maisha yao.

Ni dhahiri kwamba teknolojia mpya, hasa simu janja na mitandao ya kijamii, vimekuwa tatizo kubwa kwa wengi. Kila mtu analalamika jinsi vitu hivyo vinavyochukua muda mwingi, kuleta uchovu na hata msongo.

Wanaotengeneza na kuendesha teknolojia hizo hawajali kuhusu hilo, kwani kadiri unavyozitumia kwa muda mrefu, ndivyo wao wanavyopata faida. Hivyo wamejipanga kuhakikisha watumiaji wanaendelea kuwa wafungwa kwenye teknolojia hizo.

Na kwa kuwa teknolojia hizi ni mpya, hakuna mwenye uzoefu wa jinsi ya kukabiliana nazo, hivyo watu wanaingia kwenye teknolojia hizo mpya kwa kuhadaiwa watanufaika sana, lakini kinachotokea ni wanageuzwa kuwa wafungwa.

Leo nina habari njema kwako, habari hizo ni kupatikana kwa mwongozo wa kuzitumia teknolojia hizi mpya vizuri na ukombozi wa ufungwa ambao teknolojia hizo zimetengeneza kwako.

Nimekuandalia kitabu kinachoitwa EPUKA UTUMWA WA KIDIJITALI, kitabu kinachokuonesha jinsi teknolojia mpya zinavyokufanya mtumwa na njia za kuondoka kwenye utumwa huo.

Kupitia kitabu hiki utajifunza mambo saba makubwa ambayo yatakufanya uwe huru na utumie teknolojia hizi kwa manufaa makubwa kwako.

Moja utajifunza jinsi ubongo wako unavyofanya kazi na namna teknolojia mpya zinavyotumia ubongo huo kukufanya kuwa mtumwa. Teknolojia mpya zimetengenezwa kwa namna ambayo zitajenga uteja/uraibu kwenye ubongo wako. Kwa kujua njia hiyo utaweza kuepuka kuingia kwenye utumwa wa teknolojia hizo.

Mbili utajifunza kuhusu zama tunazoishi sasa, zama za maarifa na taarifa lakini ambazo zimegeuka kuwa zama za usumbufu. Utajifunza zama hizi za usumbufu zimetengeneza makundi makubwa mawili, wachache wanaonufaika sana, kama Mark Zuckerberg ambaye ni mmiliki wa Facebook na wengi ambao ni kama watumwa wa wachache hao wanaonufaika.

Tatu utajifunza jinsi ya kujua kama tayari umeshanasa na kuwa mtumwa wa teknolojia hizo mpya. Unaposoma hapa unaweza kusema wewe hujawa mtumwa, unatumia kwa kupanga mwenyewe, lakini nikuambie kitu kimoja, kwa sehemu kubwa sana umeshakuwa na utaziona dalili kwa kusoma kitabu hiki.

Nne utajifunza jinsi ya kuondoka kwenye utumwa wa kidijitali ambao umeshaingia. Baada ya kuona jinsi ambavyo umenasa kwenye utumwa huo, utajifunza njia za kujinasua. Hapa utajifunza jinsi ya kuizidi ujanja simu janja yako.

Tano utajifunza falsafa mpya ya kuendesha maisha yako kwa uhuru katika zama hizi za usumbufu. Pamoja na kujifunza kuhusu zama hizo na jinsi ya kuondokana na utumwa wake, usumbufu wake hautaisha, teknolojia mpya zinaendelea kugunduliwa kila siku na zikiwa na ushawishi mkubwa. Hivyo unahitaji kuwa na falsafa unayoitumia kuchagua huduma za kidijitali utakazochagua kutumia kwa manufaa yako.

Sita utajifunza jinsi ya kutumia akili yako kuvunja uraibu wowote ambao umeshajijengea. Kama tulivyoona, huduma za kidijitali zinatumia jinsi ubongo unavyofanya kazi kukuingiza kwenye utumwa. Hivyo wewe unapaswa kuutumia ubongo wako vizuri kuondoka kwenye utumwa huo.

Saba utajifunza sababu kumi kwa nini unapaswa kuondoka kwenye mitandao yote ya kijamii sasa hivi. Hizi ni sababu ambazo zimechambua jinsi matumizi ya mitandao ya kijamii yalivyo na athari kwenye akili yako, utulivu wako, mahusiano yako, uchumi wako na hata imani yako. Kwa kuzijua sababu hizi kumi, utajionea mwenyewe jinsi ulivyorudi nyuma tangu umeanza kutumia mitandao hiyo na hivyo kuachana nayo ili kuepuka madhara yake.

Mwisho kabisa utajifunza njia za kutumia kufanya maamuzi iwapo utumie huduma ya kidijitali. Utajifunza jinsi ya kutumia vigezo vitatu vya AFYA, UTAJIRI na HEKIMA katika kuchagua na kutumia teknolojia mpya, ambazo zitakuwa na manufaa kwako badala ya kukufanya mtumwa.

Tuko kwenye vita, adui mkuu anajua yuko vitani ila wanaolengwa hawajui. Hivyo unapaswa kuwa na maandalizi mazuri ya kupambana na vita hii ili uweze kutoka salama na siyo kuwa mfungwa.

Pata na usome kitabu cha EPUKA UTUMWA WA KIDIJITALI ili upate mbinu za kupambana kwenye vita hii na kutoka ukiwa mshindi. Kitabu hiki kimechapwa kwa nakala ngumu (hardcopy).

Thamani ya kitabu hiki ni TSH 50,000++,

Ila LEO utakipata kwa bei ya OFA tsh elfu 20 (20,000/=) tu,

OFA hii ni ya watu 20 tu wa kwanza.

Na ili kukipata wasiliana na 0752 977 170 na utaletewa au kutumiwa kitabu popote ulipo Tanzania na Afrika Mashariki.

MUHIMU; Kama utanunua na kusoma kitabu hiki na ukaona hakina manufaa yoyote kwako, unaruhusiwa kukirudisha na ukarejeshewa fedha zako. Hivyo chukua hatua sasa, huna cha kupoteza lakini una mengi ya kupata, yatakayokuweka huru kwenye zama tunazoishi sasa.
 
Nimekuandalia kitabu kinachoitwa EPUKA UTUMWA WA KIDIJITALI, kitabu kinachokuonesha jinsi teknolojia mpya zinavyokufanya mtumwa na njia za kuondoka kwenye utumwa huo.
Una maana tuepuke usomaji?
Na hata hicho kitabu hakitakuwa na maana
Kumbuka vitabu ni zao jipya la vigae, huko nyuma maandishi yaliwekwa kwenye vigae, vikaja vitabu na sasa digitali
 
1622259869057.png


Mafanikio sio mchezo wa kubahatisha.

Ni mchezo wa kuzifuata kanuni na kuziishi kila siku.

Hakuna kingine kinachowatofautisha wanaotajirika na wanaobaki masikini kama tabia.

Hivyo kwa kuzijua tabia za kitajiri na kuziishi kwenye maisha yako ya kila siku, unakuwa kwenye nafasi nzuri ya kufikia utajiri pia.

Huenda kwa kusoma hapa na kusikia mambo ya utajiri umejisikia vibaya, na kama ndivyo basi hiki kitabu ni chako, kwani kinaenda kuvunja kikwazo kikubwa kinachokuzuia kuwa tajiri.

Mambo mengi sana yamekuwa yanasemwa kuhusu utajiri na matajiri, lakini mengi kati ya mambo hayo siyo sahihi.

Mengi yanayosemwa kuhusu utajiri na matajiri, hasa kwa upande hasi siyo sahihi na yamewafanya wengi kuendelea kubaki kwenye umasikini.

Ukweli ni kwamba utajiri ni mzuri, pale mtu unapoweza kuwa na fedha unazohitaji kwa ajili ya mahitaji ya maisha yako, maisha yanakuwa bora sana kwako.

Na pale unapokosa fedha, maisha yanakuwa siyo bora, kuanzia kwako binafsi na hata kwenye mahusiano yako.

Hivyo yeyote anayesema utajiri siyo muhimu, anajidanganya tu na kujipa moyo.

Fedha na utajiri ni vitu muhimu sana kwenye maisha yetu ya kila siku.

Ukweli wa kuumiza ni kwamba katika kila jamii, yaani ukianza na dunia nzima, ukaja kwenye nchi, ukaenda kwenye mkoa, wilaya na hata mtaa, utajiri umegawanyika kwenye namba ambazo ni sawa kwenye kila eneo.

Namba hizo ni 99/1, 95/5 na 90/10.

Namba ya kwanza ni 99 kwa 1, ikimaanisha asilimia moja ya watu ndiyo wenye utajiri mkubwa mno duniani, kushinda asilimia 99 kwa ujumla.

Hii ina maana katika watu 100, mmoja ana utajiri mkubwa kushinda jumla ya utajiri wa wale wengine tisini na tisa.

Namba ya pili ni 95 kwa 5, ikimaanisha asilimia 5 ya watu kwenye eneo ndiyo wanaokuwa na utajiri na uhuru wa kifedha, huku asilimia 95 wakiwa na maisha ya kawaida au ya chini kabisa.

Wale waliopo kwenye asilimia 5 hata kama siyo matajiri kama asilimia 1, lakini maisha yao yana uhuru mkubwa.

Hawa hutawaona kwenye orodha ya matajiri wakubwa, lakini wameshafikia uhuru wa kifedha na wanaishi maisha bora sana kwao.

Namba ya tatu ni 90 kwa 10, ambapo asilimia 10 ya watu wanakuwa na utajiri au maisha ya juu, huku asilimia 90 ya watu wakiwa na maisha magumu sana.

Hii ina maana katika watu 100, watu 90 wapo kwenye hali ngumu sana kifedha, hawana uhakika kesho au mwezi ujao wanaendeshaje maisha yao.

Hawa ni watu ambao kila wakati wanaishi kwa wasiwasi kwa sababu hawana msingi wowote kifedha.

Namba sahihi kwa wewe kuwa ni kwenye 95/5, unapaswa kuwa kwenye asilimia 5 ya juu kwenye jamii yako na hata dunia kwa ujumla kwa kuwa na uhuru wa kifedha, kuwa na fedha ambazo unaweza kuendesha maisha yako kwa namna unavyotaka wewe.

Hii ni namba sahihi kwako kuwa kwa sababu huhitaji kushindana na yeyote na wala huhitaji kuwa na bahati kuifikia.

Kwa kujijengea tabia nzuri, kuweka juhudi kubwa na kutokukata tamaa, utaweza kufika kwenye asilimia 5 ya juu na maisha yako yakawa bora sana.

Utajiri ni mchezo, mchezo ambao una kanuni zake na sheria zake, na ili uweze kushinda mchezo huu, lazima uzijue kanuni na uzishike sheria.

Haiwezekani kabisa kwa mtu ambaye hajui kanuni za mpira wa miguu, hana mazoezi akaenda uwanjani na kushinda.

Wengi wamekuwa wanaingia kwenye mchezo wa utajiri kama vile ni kitu cha kubahatisha, hawajui kanuni wala sheria, hawana maandalizi na kinachotokea ni kushindwa vibaya sana.

Kwenye kitabu hiki cha TABIA ZA KITAJIRI, unakwenda kujifunza mambo makubwa matano kuhusu utajiri.

Kwanza utajifunza kuhusu sayansi ya utajiri na kujua kanuni za kufanyia kazi ili uweze kufika kwenye utajiri mkubwa.

Hii ni sayansi inayofanya kazi kwa yeyote anayefuata kanuni sahihi.

Hapa utajifunza kanuni hizo na ukizifuata utajiri ni lazima kwako.

Pili unakwenda kujifunza tabia kumi muhimu za kuishi kwenye kila siku ya maisha yako ili kufika kwenye utajiri.

Hizi ni tabia zilizofanyiwa tafiti na kugundulika matajiri wengi wanaziishi kila siku.

Tabia hizo kumi hazihitaji ufanye mabadiliko makubwa kwenye maisha yako, bali ni kubadili tu mtindo wa kuyaendesha maisha yako kila siku.

Kwa kuwa na mtindo mpya wa kuendesha maisha yako, unajenga utajiri mkubwa kwako bila kujali unaanzia wapi.

Tatu unakwenda kujifunza imani 17 muhimu za kujijengea ili uweze kufikia utajiri mkubwa. Imani na mitazamo tuliyonayo ina athari kubwa kwetu kifedha, ulipo sasa ni matokeo ya imani ulizonazo, ambazo umebeba kutoka kwenye jamii iliyojaa masikini wengi.

Hapa unakwenda kujifunza imani 17 mpya kutoka kwa matajiri na kwa kuziishi, utayabadili maisha yako na kufikia utajiri mkubwa.

Hapa utajifunza jinsi imani zinavyoathiri hisia, ambazo zinaathiri fikra, kisha maamuzi, matendo na matokeo unayopata.

Nne unakwenda kujifunza tabia 50 za kwenda kujijengea kwenye maisha yako ambazo zitakufikisha kwenye utajiri mkubwa na maisha ya mafanikio na furaha. Hapa unapata mkusanyiko na msisitizo wa yote muhimu unayopaswa kufanyia kazi ili kufika kwenye utajiri na furaha.

Na hata baada ya kufika kwenye hatua hizo, tabia hizo 50 zinakuwa kinga kwako usianguke.

Tano ni hatua nane za kufika kwenye utajiri mkubwa. Kitabu hiki siyo tu nadharia ya utajiri, bali pia unaondoka na hatua za kwenda kuchukua ili ufike kwenye utajiri.

Hapa utajifunza hatua nane za kutoka kwenye umasikini mpaka kwenye utajiri mkubwa, hatua ambazo ukizichukua kama unavyojifunza, nakuhakikishia hutaweza kubaki hapo ulipo sasa.

Uzuri hatua hizo hazihitaji usubiri, unaanza nazo mara moja, hapo hapo ulipo na unaanza kujenga utajiri.

ZAWADI YA EBOOK.

Rafiki yangu mpendwa,

Kwa kuwa umekuwa unafuatilia mafunzo ninayotoa kwa muda mrefu,

Nakwenda kukupa EBOOK hii ya TABIA ZA KITAJIRI KAMA ZAWADI.

Bei halisi ya EBOOK hii ni TSH 10,000/=.

Hivyo kwa siku ya LEO utaipata EBOOK hii kwa TSH elfu moja(1) pekee (1,000/=).

OKOA TSH 9,000 NZIMA LEO.


Lengo langu ni wewe usiwe na sababu yoyote ya kuikosa,

Kwa sababu nataka sana uyabadili na kuyaboresha maisha yako na maarifa yaliyo kwenye kitabu hiki ndiyo unayahitaji sana.

Chukua hatua sasa rafiki yangu,

Zawadi hii ni ya muda mfupi,

Bei ya EBOOK hii itakuwa kubwa zaidi baadaye hivyo usikubali kukosa.


Utajiri ni haki na wajibu wako, kama wapo wengine walioweza kufikia utajiri, na wewe pia unaweza kuufikia.

Unachohitaji ni kuijua kanuni sahihi na kuifuata.

EBOOK hii ya TABIA ZA KITAJIRI ina kanuni hizo, wajibu wako ni kuzijua na kuzifuata na utajiri kwako unakuwa swala la muda tu.
 
1622522548812.png


Siri ya Utajiri ni ubahili,hii ni kauli ambayo wengi wamekuwa wakiitumia, na hufanya zoezi la kutengeneza utajiri kupewa taswira hasi.

Kwa sababu ubahili ni kubana sana fedha na kujinyima, basi wengi huona hayo siyo maisha ya kuishi. Kwa nini ujitese kutengeneza utajiri wa baadaye badala ya kutumia fedha hiyo sasa na ukawa na maisha bora?

Hili ni swali ambalo wengi hujiuliza na lina mantiki kubwa. Kujitesa leo ili kuwa na maisha mazuri kesho siyo mpango mzuri. Lakini msingi wetu wa utajiri bado ni ule ule, matumizi yawe madogo kuliko mapato. Sasa unafikiaje hili huku ukiwa na maisha bora kabisa kwako, yasiyo ya kujitesa?

Hapa ndipo tunapaswa kujifunza kitu muhimu sana kuhusu fedha na matumizi, kipi unachojali wewe, kipi kinachokupa wewe furaha. Kwa kujua hayo, utaweza kudhibiti matumizi yako vizuri, huku ukiwa na maisha bora zaidi kwako.

Nadhani kila mtu amewahi kusikia kauli kwamba fedha haiwezi kununua furaha. Kauli hiyo huwa inatokana na tabia ya watu kuahirisha maisha, wakiamini wakishakuwa na fedha basi watakuwa na furaha, kitu ambacho huwa hakitokei.

Fedha na furaha ni maeneo mawili tofauti kwenye maisha, ambayo yanaweza yasiwe na uhusiano wa utegemezi. Unapaswa kuwa na furaha kabla hata hujawa na fedha.

Katika kujenga maisha bora na yenye furaha, angalia wewe unajali nini. Ni kitu gani ambacho unapenda sana kwenye maisha yako. Na hicho ndicho unachopaswa kutumia kipato chako kuhakikisha unakipata.

Hapo unaweza kufanya matumizi utakavyo, na kuweka juhudi kuhakikisha unapata kipato cha kukuwezesha kupata kile unachotaka. Vitu vingine vyote ambavyo havina maana kwako, unaachana navyo kabisa. Vitu ambavyo huvijali , usiruhusu kabisa vichukue sehemu ya kipato chako.

Kwa njia hii utapata kile ambacho unakifurahia, na kuachana na matumizi ambayo yanakuwa mzigo kwako, wakati hayana maana kwako. Ili kufanya zoezi hili lazima kwanza ujitambue wewe binafsi. Uaache kufanya maamuzi kwa kufuata kundi kubwa la watu wanafanya nini. Badala yake uwe unafanya kile ambacho unakijali wewe, kile ambacho ni muhimu kwako na kina maana kwako.

Kwa kufanya hivi, kwa nje bado watu wataona wewe ni bahili, kwa sababu watu wana maana zao wenyewe za namna gani kila mtu anapaswa atumie fedha zake. Bado watu watasema una maisha ya ajabu kwa sababu huishi kama wanavyotaka wao, lakini hilo halitakuwa na shida kwako kwa sababu unafanya kile unachojali, na siyo kuwaridhisha watu. Kwako wewe hautakuwa ubahili bali maisha ambayo yana maana kwako, na hii ndiyo itakayokutofautisha wewe na wengine kifedha.

Changamoto kubwa kwa watu wanaopata fedha ni kuwa watumwa wa watu wengine. Kutaka kuishi kama vile ambavyo watu wengine wenye fedha kamazao wanavyoishi. Na hili ni moja ya vikwazo kwa nini wasomi wengi huwa hawafikii uhuru wa kifedha.

Kwa sababu wengi hufanya mambo ambayo yapo nje ya uwezo wao, kwa sababu ya msukumo ya wale wanaowazunguka. Inahitaji nidhamu ya hali ya juu na kujitoa kweli kama unataka kuishi maisha ambayo yana maana kwako na siyo mzigo kwako.

Moja ya watu matajiri sana ambao wanasemekana ni mabahili ni Bilionea Warren Buffet, ambaye ni tajiri mkubwa wa kipindi kirefu. Mwaka 2017 utajiri wake ulikuwa unakadiriwa kuwa dola bilioni 77. Ukiipeleka hiyo mwaka huo kwenye fedha za kitanzania ni trilioni zaidi ya 150, bajeti ya nchi kwa miaka karibu hata kumi kipindi hicho.

Pamoja na utajiri huo mkubwa, Buffet bado alikuwa anaishi kwenye nyumba yake aliyonunua mwaka 1958 huko OMAHA, Nebraska nchini marekani. Alikaa kwenye nyumba moja kwa miaka 61, na alipoulizwa kwa nini pamoja na utajiri mkubwa bado maisha yake ni ya kawaida , jibu lake lilikuwa ni kwamba mafanikio kwake ni kufanya kile kitu anachopenda , nay eye anapenda kuwekeza. Hivyo anafanya kile anachopenda, na vingine anaachana navyo.

Siyo lazima maisha yako yawe kama Warren Buffet, lakini najua umepata ninachotaka kukuonesha hapa, kwamba ishi maisha kwa kujali vile ambavyo vina maana kwako, vile ambavyo unapenda, siyo kujibebesha mizigo kwa kufanya mambo ili kuwaridhisha watu wengine. Kwa sababu fedha unayotumia kununua vitu usivyojali, ukiiwekeza miaka 20 ijayo itakuwa imeongezeka thamani sana.

Sasa inashangaza unaposoma makala au kitabu kimoja, unapata hamasa na kuona umeshamaliza kila kitu.

Hapo unajidanganya na kujiweka kwenye hatari ya kuishia njiani.

Unapaswa kuendelea kuchochea hamasa yako kila siku kwa kuendelea kujifunza bila kuchoka au kuona umeshajua kila kitu.

Kila siku jifunze vitu vipya na vinavyokusukuma kupiga hatua zaidi.

Baada ya kujua jinsi ya kudhibiti matumizi yako na bado ukawa na maisha bora, kuna rasilimali muhimu unapaswa kuwa nazo ili kufanikiwa.

  • Kitabu cha UNA NGUVU YA KUTENDA MIUJIZA, ambacho kitakusaidia kujitambua.
  • Kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, kitakusaidia kuweka akiba na kuwekeza.
  • Kitabu cha TABIA ZA KITAJIRI, kitakachobadili mtazamo wako kwa ujumla.
  • Kitabu cha MIMI NI MSHINDI, kitakachokufundisha kuishi kwa ushindi kila siku.
  • Jamii ya KISIMA CHA MAARIFA, itakayokusukuma kufika kwenye mafanikio makubwa.
  • Kupata rasilimali hizi wasiliana na 0752977170.
  • Nikutakie kila la kheri kwenye safari hii ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa.
 
Back
Top Bottom