Uzi wa kushuhudia mazuri ya kwenye ndoa, Tuyaweke pembeni yale mabaya yanayowatia hofu watu wasioe au kuolewa

Kumbe ndoa ni asali na maziwa namna hii? Ila ombeni hela ziwepo tu
Hivi ni kweli masikini hawafurahii ndoa jamani? au mnazungumzia ndoa za kupelekana Paris na ku shop Dubai..maana sielewi. wapo watu tunawaona basic needs zao ni za kuunga unga mno ila wana furaha hadi mtu unawatamani[emoji23][emoji23]
 
[emoji28][emoji23]
 
Halafu wanawake mlio kwenye ndoa kuna wakati ni kama huwa mnawaringishia waume zenu wale wasioolewa. Nimeligundua hili leo Kanisani.

Kuna utaratibu wanawake wanakaa upande wa kushoto na wanaume wanakaa kulia, Sasa wale wanawake walioolewa utakuta wanatoka upande wao na kuja kukaa na waume zao na kusababisha wale wanawake singo muda mwingi wanakuwa wanawapiga kijicho hawa wanandoa. Nayo hii ni faida ya ndoa.

Halafu hata kukiwa na uchaguzi wa viongozi wa Kanisa, shart la kwanza eti ni lazima uwe umeoa au kuolewa. Hawajagundua tu kuwa ndoa ni cheti tu, wakiwa huko majumbani mwao ni full visirani na machukizo.
 

Mkuu umesema vizuri sana. Mimi pia nakazia hiyo sentensi ya mwisho.
 
One thing MUST remain constant...PESA!

Oa halafu upigike, dadeq.

Think positive mkuu.

Kwani ni lazima kila mtu kwamba kuna siku atakuja kupigika? Mbona kuna watu kibao tu wanafanya biashara mpaka wanazeeka na hawajawahi kufilisika au kupigika? Mbona kuna wafanyakazi kibao tu wanafanya kazi mpaka wanazeeka wanastaafu kwa amani na hawajawahi kufukuzwa kazi? Mbona kuna familia kibao tu wanaume wamepigika ila maisha yanaenda na wanaendelea kuishi kwa amani? Na mbona kuna familia kibao ambazo wanaume hawajapigika lakini moto unawaka humo ndani wanaishi kama paka na panya?

Kupigika ni kama ajali tu, mtu huwezi kuacha kuoa eti kisa unaogopa ukija kupigika itakuaje.
 
Hakika mkuu, mimi ni nani nikupinge. Kila ndoa ina uniqueness yake, lakini uchumi ukikaa vibaya ndani ya nyumba ni shida mkuu.
 
Upo sawa kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…