Vetting system ya viongozi ilishindwaje kumchuja Ole Sabaya?

Hayo mambo ya vetting labda nchi za wenzetu lakini sio Bongo hii siamini kabisa kama yapo maana kama yangekuwepo sidhani hata yule aliyemteua yeye ingewezekana kukabidhiwa madaraka.
Bongo Connection ina nguvu kuliko vetting na ndio maana wenye Gpa za 4 wengi wako mtaani ila wenye 2.9 wanapeta maofisini na mishahara mizito
 
TISs walikuwa wamelala na wako mfukoni mwa Jiwe
Hata Magufuli kwa ukweli kabisa, kufika alipofika ni maajabu.
Kuna matatizo makubwa ya kuchuja viongozi.
Tuliyoyaona ndani ya hii miaka mitano ni failure kubwa ya vetting system.

Na hala ndio inabidi katiba isukwe upya ili uwajibikaji wa wateuliwa hadi ngazi ya rais urudishwe kwa wananchi.
Hii ina maana madraka ya Rais yapewe ukomo ili asijefanya kama tulivyoona Hai.
 
Hata enzi za Mwalimu sio kwamba viongozi wote walikuwa wenye maadili. Wapo waliongia hadi watu wakawashangaa kama wewe unavyomshangaa Ole Sabaya. Ushahidi tunao na ukiutaka tutakuwekea.
 
Hata enzi za Mwalimu sio kwamba viongozi wote walikuwa wenye maadili. Wapo waliongia hadi watu wakawashangaa kama wewe unavyomshangaa Ole Sabaya. Ushahidi tunao na ukiutaka tutakuwekea.
Kiongozi kitenda maovu siyo sifa, hata uwe anatumika awamu gani.
Kama unawafahamu waliotenda mabaya waseme tu , umma unataka kufahamu mabaya yao.
 
Huyu alipendekezwa na Mnyeti, Mnyeti na Magufuli ilikuwa ni pete na kidole hapakuwa na namna mkuu
 
Ila Magufuli Bora alipumzika mapema, alipokuwa anatupeleka anajua yeye mwenyewe. Kina Sabaya, Makonda, walikaribia kuwaharibu Ali Hapi na Chalamila. Leo ukienda kwa RC Tabora huwezi kuamini ni yule aliyekuwa Iringa

Sent from my vivo 1915 using JamiiForums mobile app
 
Nchi hii hakuna kuna kuchomekeana majina tu
Watu wapate ulaji

Ova
 
Hapi mpaka alikuwa anamtisha JK eti atamshughulikia, pumbafu kabisa
 
Chujio ilitakiwa lianzie kwa jiwe mwenyewe
maana huyo ndio tatizo lenyewe sema baada ya Mungu kuona midanganyika haijielewi akaamua kutusaidia kupitisha chujio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…