Viatu na Kivuli cha Magufuli kwa Tanzania ya Samia - Kuna cha Kuhofia?

Tumekuwa sasa na matumaini ya kuwa watu-huru, matamanio ya waTanzania wengi yalikuwa hivyo bila kujali walikuwa viongozi au tuliopachikwa jina 'wananchi walio wanyonge'.

Sasa hali imebadilika kuna mwangaza unaonekana katika safari yetu ndefu iliyokuwa kizani ndani ya handaki refu kupindukia la miaka mitano iliyopita na mitano-tena tuliyokuwa tumeingizwa kupitia mchakato wa uchaguzi 2020 uliogubikwa na utata mwingi .


Toka Maktaba sauti nyingi zilitaka kuwa watu-huru :

Mwaka 2018 mwezi Machi tarehe 3
Dr. LWAITAMA, AMVAA MAGUFULI ATAKA ADHIBITIWE
Wananchi wanataka Maendeleo ndani ya uhuru, hawataki kupokonywa uhuru wao kwa kisingizio cha Maendeleo ya Vitu
Watu hawataki kuwa mateka wa kikundi cha watu kwa kuwatisha kupitia chama dola. Chama dola siyo chama cha kweli cha kisiasa maana hakina ushawishi bali kinatumia dola kutisha
 
Tutaijua dira yake baada ya siku 100....
 
Reactions: Ame
Tatizo la ninyi "Watumishi wa Serikali" msiojitambua mnahisi na kufikiri kuwa Rais mzuri ni yule anayewalipa ninyi vizuri. Mnasahau ya kwamba nchi hii sio ya kwenu peke yenu. Kama mko "objective", piganieni maslahi yaliyo sawa kwa makundi yote.
Mbona hueleweki? Makundi yote yapi? Kila kundi lina watu wake, na lina wawakilishi wake. Sheria za Utumishi wa Umma ziko wazi na SIYO HISANI!
 
Hapapaswi kuwa na tofauti katika mwelekeo kati ya mama na Magufuli. Hii ni kwa sababu ataongozwa na ilani ya uchaguzi ile ile aliyoinadi pamoja na Magufuli!! Mbinu na kasi zinaweza kutofautiana lakini si majengo!
 

Tatizo watumishi wa umma hapa Tanzania mnajiona nyie ndiyo mnastahili kupewa nyongeza za mishahara kila siku, mnajiona nyie ndio taifa hili leni peke yenu, kila Mtanzania ana haki ktk nchi hii, acheni uninafsi wenu.Kwanza nyie ndiyo wala rushwa namba moja na wavivu mliopitiliza , hata mkiongezewa mishahara bado siyo watu wa kujituma. Mjirekebishe tabia zenu.
 
Mambo ya makundi yafutwe. Hii nchi ilishavurugwa na mambo ya makundi ya chama tawala. TUACHE!

Raisi hana wakati mgumu.
Kaanza vizuri na mengineyo. Na hahitaji kumfuata yoyote zaidi ya uzoefu, busara, hekima na weledi wake.
Hahitaji kuridhisha makundi zaidi ya kuridhisha watanzania, walio wengi, hao wachache na makundi yao potelea pote wakafie mbali.
Hajawekwa pale na mtu au kundi la watu, kawekwa na katiba.

She doesn't owe anybody! Hana deni!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Samia anatosha kupita maelezo aisee;
Kwanza Yuko composed and relaxed....na kwa kuwa team inayomzunguka iko bomba (mpango,majaliwa na katanga)watapata wasaa wa kukunjua uwezo wao na kumsaidia kazi huku yeye akiendelea kuharmonise Mambo...utawala wake utakuwa moja ya tawala Bora kuwahi kutokea Tz.
 
...vipi kuhusu waliohujumiwa na hao jamaa, wao watapataje haki yao?.

..inahitaji mabadiliko makubwa sana ya kiuongozi, na kiutawala, ili kuweza ku-prosecute maovu yaliyofanywa na kundi la WASIOJULIKANA.

..i am trying to be realistic au kuangalia hali halisi ya mazingira yetu ni nini kinawezekana kututoa hapa tulipo.

..Trust me, wasiojulikana, na waliokuwa wakiwatuma wasiojulikana, ni watu wabaya, washenzi, na wasaliti nambari moja ktk nchi yetu.

..Mimi kwa maoni yangu sidhani kama CCM na watawala wetu wanaweza kuwashtaki wahusika wa kundi hilo. Lakini nadhani wanaweza kuacha kulitumia kundi hilo, na likaishia kimyakimya.

..Mtizamo huo ndio ulionifanya nipendekeze wahusika wa genge la WASIOJULIKANA wapangiwe majukumu mengine.
 
Mwacheni Rais Samia aongoze kwa maono yake na si vivuli au viatu vya wengine
Kumtaka afuate nyayo ni kumkwaza. Samia ana personality yake tofauti na ya mwendazake

Hawezi kutumia personality yake kufanya ya Marehemu, JK, Hayati Mkapa, Mwinyi au Hayati Nyerere!
kila zama na kitabu chake , ni wakati wake kuandika zama hizi kwa kitabu chake

Katika mambo aliyoandika Mzee Mwanakijiji moja ni sisi kuwa Taifa lililogawanyika.
Kazi ngumu mbele ya mama Samia ni kuliunganisha Taifa lilivyovurugwa na Marehemu

Marehemu aliligawa Taifa kwa namna zozote unazofikiri, iwe jinsia, ukabila, udini , hata rangi

Marehemu hakujali Utu alijali Vitu, Mama Samia arudishe hadhi , heshima na utu wa mwananchi
Kiongozi anaongoza watu si madaraja au miti, hivyo kutojali uhai na maisha ya watu si kiatu cha kuvaa

Hivi mnataka Rais Samia avae viatu vya kukataa sayansi na kuhubiri madogori na mapambio kwa gharama kubwa sana za maelefu ya maisha ya wananchi! kiatu hicho mama asikijaribu wala kukifikiri!

Rais Samia halazimiki kufuta kila kilichoachwa na Marehemu lakini analazimika kufuta mabaya aliyoacha na yaliyoliacha Taifa hili na makovu makubwa sana.

Kiongozi hapimwi kwa Vitu bali Utu. Mwendazake anapimwa kwayo ndiyo maana kipimo cha utu wake kipo mgongoni kama si kushoto. Hukumu yake imesimama katika utu licha ya vitu alivyotengeneza

Mwacheni Rais Samia aongoze kwa zama zake na aandike legacy yake kwa maono yake
 
Usiwe na hasira na watumishi wa umma! Unachotakiwa kufanya na wewe ni kupigania haki zako pale ulipo! Sasa kama hutaki mtumishi wa umma aongezewe mshahara au kupandishwa cheo, hizo huduma bora unazotaka kupata utapewa na nani?

Na tukiacha kazi mtahudumiwa na nani nyinyi ndugu zetu wanyonge? Tuishi kwa kupendana basi! Ila haya mambo ya kuoneana wivu na kuombeana mabaya, hayatatufikisha kokote kama Taifa.
 
Siku nyingi Sana sijasoma makala ambayo mleta mada ameandika kwa kutumia akili yake niliyoifahamu miaka mingi.Tangu Rais Magufuli (R.I.P) aingie madarakani(au labda niseme tangu Dr W Slaa alipojiengua chadema),mzee amekuwa anaandika kwa hisia zaidi kuliko hii akili ambayo inaonekana ameitumia kwenye hii makala.

Napongeza marejeo haya ya matumizi ya akili.Japo bado ninahofu kwamba,pengine tunapopata Rais asiye mkatoliki huyu mleta mada huwa ni mtumiaji mzuri wa akili yake.Anapokalia kiti mkatoliki,huyu mleta mada huwa anatumia Sana hisia kuliko akili.Natumai awamu hii atakuwa tena popular humu na atabeba tena wafuasi wake wa JF ambao walikuwa wamemtupa kwa kumuona sio 'mwenzao'!

Nimeisoma hii makala katikati ya mistari.....
 
Hapana ndio amekuwa na maandiko bora kabisa. Mimi naheshimu sana wetu kama MM Mwanakijiji wanaoweza kusimama na wanachoamini bila kujali msimamo wa wengi! Binafsi heshima yangu kwake ilifikia kiwango cha juu nyakati hizo.

Sisi wengine hatupelekwi na upepo, tunaacha akili zitupe majibu sahihi na si matumbo yetu.
 
Tatizo la ninyi "Watumishi wa Serikali" msiojitambua mnahisi na kufikiri kuwa Rais mzuri ni yule anayewalipa ninyi vizuri. Mnasahau ya kwamba nchi hii sio ya kwenu peke yenu. Kama mko "objective", piganieni maslahi yaliyo sawa kwa makundi yote.

Sure wana ubinafsi sana. Everyone deserve same and equal opportunities
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…