Pre GE2025 Video: Makonda ataka mdahalo na Tundu Lissu

Pre GE2025 Video: Makonda ataka mdahalo na Tundu Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,058
Reaction score
14,382
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Paul Makonda amependekeza kufanyike mdahalo wa wazi kati yake na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ili Watanzania wachague ikiwa wataendelea na maandamano au kuchagua maridhiano.

=========================
For English Audience
Secretary of Publicity and Ideology of CCM Paul Makonda, has proposed an open debate between him and the leaders CHADEMA so that Tanzanians can choose whether to continue with protests or opt for reconciliation.

Credit : Swahili Times

Pia soma: CHADEMA yakubali kufanya mdahalo na CCM
 
Ina maana Makonda hajui kwamba maridhiano yalishakufa, ndio maana yeye akawekwa hapo ili kumrahisishia njia yule aliyemweka aliyeshindwa kufanya kulingana na maridhiano?

Samia ndie anayetakiwa kuitisha mdahalo na viongozi wa Chadema, sio Makonda, yeye amepewa cheo juzi tu, hajui A wala B kuhusu maridhiano.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Sioni mtu wa kuandamana,watanzania sio wajinga ambao wanaweza pelekwa na vibaraka wa wazungu ili kuvuruga amani na mstakabali wa taifa letu.Mwenyeki wangu makonda huhitaji kuwa na hofu juu ya hawa watu .
 
Makonda aache kulazimisha sifa! Uwezo wa kufanya mdahalo wa aina yoyote ile na mtu kama Tundu Lissu, John Mnyika, nk. hana!
Asisahau kichwa kimoja cha Tundu Lissu ni sawa na vichwa laki 1 vya makada wa ccm vikiunganishwa kwa pamoja! Na akumbuke huyo Tundu Lissu hajatumia jina la mtu mwingine kama alivyofanya yeye Bashite, kufika hapo alipo.
 
Back
Top Bottom