VIDEO: Mbowe, Lissu wasalimiana kibabe BAWACHA, huku wakicheza kwa bashasha wimbo wa "Tuvushe Mbowe Tuvusheee"

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu wakisalimiana katika mkutano mkuu wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha) unaofanyika leo Alhamisi Januari 16, 2025 katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.

Wote wawili wanamchuano mkali kuelekea Uchaguzi wa nafasi ya Uenyekiti CHADEMA unaotarajiwa kufanyika Januari 21.
Mbowe na Lissu wakicheza kwa furaha katika mkutano mkuu wa wanawake CHADEMA (BAWACHA)
Your browser is not able to display this video.
Pia, Soma:
-
PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kikao cha Kamati Kuu Chadema
- Uzi maalumu wa matokeo Uchaguzi wa Baraza la Vijana (BAVICHA) na Baraza la Wazee (BAZECHA) na wanawake (BAWACHA) CHADEMA Taifa 2025
 
Picha za mwisho mwisho kabla Lissu kushindwa uchaguzi Chadema na kuhama chama na kutimkia ubelgiji
 
kama n'mbwai na iwe mbwai bwana..πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€Safi sana makamanda hiyo ndio demokrasia.. Wale wasingeweza hata kuangaliana machoni achilia mbali kushikana mikono
 
kama n'mbwai na iwe mbwai bwana..πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€Safi sana makamanda hiyo ndio demokrasia.. Wale wasingeweza hata kuangaliana machoni achilia mbali kushikana mikono
Mnyukano nje ya ulingo ndani Demokrasia inatawala πŸ˜€ hapo ndipo kuna watu wanachanganyikiwa hawaelewi lini watasambaratishana ili iwe advantage kwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…