Video: Ni kama masihara hivi lakini polepole Mikocheni na Masaki zinaenda kutawaliwa na Wachina


Its a combination of both wako wengi and pia wana elements za u-apartheid but zimekuwa covered in the name of "kulinda utamaduni wao"


Unatetea Wachina kwa sababu huwajui tabia zao.
 
Sijui lakini hamna kitu kinaniuma kama kuanza kuwarekodi wachina na kusema wamevamia daaah. Hawa wamekuja na passport zao. Hawajazamia, na wote wanashughuli za kulipa kodi, hata sisi tukienda makwao, tunakua na eneo ambalo wengi wetu tunafikia. Why wao watengane. Roho imeniuma sana daaah.
kuna miji kama doha, Qatar, London-Uk, Minneapolis- marekani, kampala nairobi na mombasa, kitwe-zambia. Kuna watanzania wengi unaweza sema kkoo au pale nyegezi mwanza.
What the fck this is trending today.
Hawa wanakaa kwenye appartment uwezo wakununua hizo nyumba hawana.
Mnajua kuna wachina wangapi kiwanda cha dar ceramics, kepa ceramics mkuranga?
Ujinga huu wazee. Kausheni.
 
Mkuu hapo wapo kwenu na umeshika mpini.
Binadamu wote na nchi zote ubaguzi upo ila wakileta za kuleta si mnamtoa?
Kwao ni wabaguzi ukienda India kabisa na hata ukifika Ulaya nao ni hivyo hivyo

Nchi zingine sheria zanawabana na unaweza kushtakiwa kwa ubaguzi
Umeongelea sentence ya kwanza tu mbona mengine umeacha au la husda limekukera zaidi

Fursa hizo acha wawe wabaguzi, hata hapa nilipo wapo hao na maduka yao ila wameajiri mpaka white, blacks na hata wahindi kwa sababu hapa sio China
 
Only in Tanzania wageni wanatoboa na limekuwa shamba la bibi,wanatuona mabwege kweli kweli.
Hilo halikwepeki kwa dunia ya sasa unachotakiwa na wewe upambane ukatumie fursa za kwao. Namshangaa mtoa mada sijui lengo lake ni nini wakati hao wameingia nchini kihalali, anatuletea mentalility za miaka 1960's kama alivyofanya Mugabe kuwafukuza wazungu zimbabwe.
 
Its a combination of both wako wengi and pia wana elements za u-apartheid but zimekuwa covered in the name of "kulinda utamaduni wao"


Unatetea Wachina kwa sababu huwajui tabia zao.
Ukija na uzi wa ubaguzi nitaupinga popote pale na wakati wowote ule sitajali kama ni mchina au ni mswahili mwenzangu hilo jambo sikubaliani nalo kabisa ila na mimi siwezi kubadilika kuwa mbaguzi sababu nipo na mbaguzi (binafsi mbaguzi namuona huruma sababu naona anaishi in the past)...

Nilikutana na waitaliano ni wabaguzi, wanadharau na matusi nje nje lakini hio haijanifanya niwachukie au niwabague bali ninawapokea kama wanavyokuja wakileta ubaguzi ninawadharau lakini hio hainifanyi kuacha kwenda kula spaghetti bolognese au lasagna..

Sijui labda its a globalist in me.., napenda zaidi varieties and different cultures kuliko kubweteka na same old same old...
 

Yaani badala uonee huruma nchi yako ambayo ni 3rd world country unaonea huruma wananchi wa nchi nyingine ambao wana uwezo wa ku-afford apartments Mikocheni na Masaki?

Wachina wameanzisha Supermarkets kila mahali Masaki, Mlimami City, Mikocheni, Africana etc, unawaonea huruma wa nini?

Kama tunamsema hadi Rais wa nchi yetu wachina ni wakina nani wasisemwe?

Sisi tunapoenda makwao tunaruhusiwa kuanzisha supermarkets na car wash na kuanzisha "Swahili Towns?"
 
Linaweza kukwepeka kwa kiwango flani. Haiingii akili kuona wachina wanafanya biashara ndogo ndogo kama machinga huko Kariakoo. Je vigezo na masharti
huzingatiwa kuwapatia vibali vya kuishi hapa ? Nadhani waliopewa dhamana wanatuangusha sana na hii ikiendelea hivyo itakuwa hatari.
 

Unatumiaje "fursa" za kwao wakati wao ukienda kwao ukinunua apartment, then kwenye hiyo apartment ukaaanza kuuza hata karanga unakamatwa?

Meanwhile Wachina wanapanga nyumba Upanga uko then wanazibadilisha zinakuwa viwanda vidogo?

Wafanyabiashara wa Kariakoo wanapolalamikia wingi wa "wageni" unadhani wanaongelea "wageni" gani?

Huwezi kujua how impactful Chinese arw kama upo Kigoma kijijjni ndani ndani unalima mawese!
 

Kwakweli labda it's a globalist in you mkuu.

But in real sense. Wachina ni an existential threat.

Huko Kariakoo wamekuwa Mawinga wanauza hadi soksi na ndo maana hata Rais Samia alimuagiza Jafo aunde tume ya "kuchunguza" influx ya hao wachina pale Kariakoo.

Wachina wangebaki kuwa investors hamna mtu angesumbuana nao. Boomplay, Tekno, Itel, Startiimes zote zao hamna mtu analalamika.

Lakini hao jamaa wako wengi sana na ukiongea na wafanyabiashara watakwambia wanavyo-operate kihuni
 
Kwanini uanze na Warusi [TU] 🤔haijalishi

Hata hivyo unakubali itakuwa ni sera yetu CHADEMA kuwa ni illegal kwa mgeni yeyote yule kukaa na ku-own hoteli n.k hapa Tanzania kwa sababu kwao ni illegal kufanya hivyo.

Tatizo lipo wapi sasa, manake kama ninakuelewa vizuri, unataka kusema hili ni jambo la kisera na linaanguka kwa chama tawala CCM au nitakuwa nimekosea mkuu?



Yaani unasema kama nchi tuanze kutumia kama kioo, sera za Nchi za nje kama zetu??

Mfano rahisi ni kama vile(rationlisation) za Raisi Donald anavyosema, 'tumekuwa tukionewa sana na mataifa mengine', 'wao(nchi za nje) wamekuwa wakituwekea ushuru na vikwazo vingine na hivyo kutusababishia ukwasi katika maendeleo yetu nchini[marekani] -hivyo basi wakiweka ushuru na sie tutaweka n.k n.k

Kwamba ni sera za Democrats.

Awali ya yote, tufanye nini kama Nchi, kisera, kuondokana na kadhia hio? Manake ni dhahiri ni kadhia sasa.
 
Hata Stanley aliwalipa machifu kodi/hongo.
 

Rais analishugulikia alishatengeneza tume ya ku-curb influx ya "wageni" Kariakoo.
 
Mtoa mada naona ni NGUMBARU mwenzetu. Amejaa chuki na ghilba dhidi ya Wachina
 
Inafikirisha sana😳
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…