Uchaguzi 2020 Video: OCD wa Hai amwambia Mbowe hata afanyeje hawezi kumshinda mgombea wa CCM Hai

Uchaguzi 2020 Video: OCD wa Hai amwambia Mbowe hata afanyeje hawezi kumshinda mgombea wa CCM Hai

Mmesema sana uwongo, sio polisi tu hata wananchi wengi wa Hai wamewachoka.

Kwa miaka 20 watu wa Hai wanaambiwa Mgombea wa CHADEMA ndio atakuwa Rais, hii ndio matokeo yake wananchi wamechoka kuambiwa kitu ambacho hakitokei.

Kila uchaguzi wananchi wanaambiwa kuwa CHADEMA inashinda Urais.
Tumia akili kidogo bwana Magembe kama utakuwa nayo basi!
Hoja sio ni uongo au ni ukweli bali msemaji anastahili kwa mujibu wa sheria kusema hayo?

Refa wa mchezo kati ya Simba VS Mwadui anaweza kujua moyoni kuwa Simba inaweza kuifunga Mwadui, lakini jee anaweza kubishana na Kapteni wa Mwadui hadharani kuwa "Mwadui kamwe haiwezi kuishinda Simba" wakati mechi haijaanza?
 
Ajiulize yule wa chuga aliekuwa anakata mauno kisisiemu yupo wapi!?
 
Kiranja ameingia choo cha kike, amenasa na kulitia Jeshi la Polisi kwenye mtihani mkubwa, sijui kama hataitwa makao makuu na kubadilishwa kazi, ametumbua usiri wa jeshi la polisi na alilolisema ndilo azimio la jeshi hilo kuhakikisha upinzani haushindi na haupewi ushindi hata kama wakishinda, ni aibu na sasa polisi wana kazi ya ziada kupambana na CCM ili wajipapatue
 
Huyu OCD anatoka ukanda gani wa nchi?

Nakumbuka kazi Kama hizi alizifanya Shana ila Leo yupo wapi? Wananchi wanalojukumu la kupiga Kura, Polisi na yume wanalijukumu lakupingana na wananchi wakidhani wanampendezesha Rais, ila Kama miaka mitano ta Magu ilivyopita ndivyo miaka mingine mitano itakavyopita.

Ila tujiulize haya tunayofanya leo hayawaandai watoto wetu kuwa wakimbizi?

Shana alifariki kama ambavyo wewe utakufa tu mkuu.

Hata huyo Mbowe wako haimaanishi hatakufa.
 
Kitendo cha watu kuona hili alafu wanafurahia ndiyo sababu hata bongo sirudi, makalio wamejaa mavi kichwani. Fanya kitu kama hiki nchi zilizoendelea, tusiende mbali hata Kenya tu huwezi fanya ushenzi huu ukabaki salama, wasomi wamejaa jinga ka hili linaangushwa mapema, ila bongo wamejaa nyani wanashangilia
 
Police si ndio CCM "C" kabisa yule wa Arusha alikua anasema wazi haihitaji mshangao hata
 
Mengi yanasemwa kuhusu kiongozi huyo na clip inatembea mitandaoni.

Nina uhakika aliyoyatamka OCD siyo msimamo wa JESHI LA POLISI na huenda ulimi wake uliteleza kama ilivyo sifa ya sisi wanadamu ie kutokukamilika,mkamilifu ni ALLAH peke yake.

Sijui taratibu za kijeshi kuhusu hilo,lakini tufanye subra huenda tamko rasmi likatolewa...nina amini hivyo ili wananchi wa eneo bunge la HAI wasiache kwenda kupiga kura kwa vile OCD kesha mtaja mshindi.

Nipo tayari kusahihishwa
 
Na asipochukuliwa hatua maana yake hao waliotakiwa kumwajibisha ndo wamemtuma
 
Sasa kama huyo ndiye kiongozi wa polisi anafanya haya hawa wa chini yake watafanya nini

He's a hopeless mofo
 
Yaani askari anaapa kwamba hata afanye nini hawezi kushinda?!

Kwamba hizo kura ataenda kupiga yake na mke wake au labda na mume wake tu, au?!

Au anamaanisha Jeshi la Polisi litafanya lolote kuhakikisha Mbowe hashindi hata kama wananchi wanamchagua?!

Halafu kuna baadhi ya wapumbavu wa CCM (especially Wafuasi wa Jiwe) eti wanafurahia kauli hii wakati walitakiwa kuonea aibu!!
 
Halafu OCD ana lafudhi ya bwana yule kwahiyo anatetea chama cha kabila lake[emoji1787][emoji1787]
 
FREEMAN MBOWE VS OCD MPINA HAI

Imeonekana Video Fupi inayozunguka ikionyesha Mabishano kati ya Freeman Mbowe na OCD wilaya ya Hai.

Ili Kutenda Haki tujiulize na Kujibu maswali machache

1.Je? Freeman Mbowe alipaswa kuwepo pale kwa mujibu wa ratiba ya Tume? Bila shaka hakupaswa ndio maana anaonekana akisema hata Rais akipita anaweza kusimamishwa, kwa maana hyo aliingilia Ratiba na Alivunja kanuni.

2. Mbowe anasikika akimuambia OCD" huyo mnayembeba habebeki' Je? Kwa kiongozi mature na mwenyekiti wa Chama aliyesaini hati ya maadili alipaswa ku-provoke mamlaka inayolinda na Kusimamia mikutano yake?

3.Kitendo cha Mgombea ubunge Mbowe kujilinganisha na Rais badala ya kutii ratiba ambayo polisi wanaisimamia ili kuzuia uvunjifu wa amani ni sahihi?

Kwa vyovyote vile busara ilipaswa na inapaswa kuwa Reciprocal, sio sawa kujadili matamshi ya OCD huku tukijifanya hatuoni muenendo wa matukio yaliyopelekea kauli hiyo na Kupishana huku kutokea.

Kama ambavyo Jeshi la Polisi lina wajibu wake lakini vyama vya siasa vina wajibu mkubwa zaidi wa kutii na kuheshimu Ratiba, kanuni na makubaliano waliyoyaweka hasa katika kipindi hiki cha mpito na Freeman Mbowe hukwepi lawama katika hili.

Nimalizie kwa kusema Hai Vita haitakuwa Lelemama, inaonekana vita Sio nyepesi hata kidogo, Mbowe awekeze kurudisha imani ya Wapiga kura wake na sio confrontation zinazofanya aonekane mwepesi siasani.

Kuwepo au kuwepo sehemu asiyostahili sio tiket ya OCD kumwambia hutoshinda.Hapo haviwiani kabisa,yeye OCD kama nani amwambie kwamba ashindi?Alitakiwa kuhakikisha mbowe anaondoka kama kweli hiyo sehem hakustahili kuwepo.

Kama kweli ungekuwa uko huru basi ungechambua ya Mbowe kisha ukakemea ya OCD sasa kitendo cha kuchagua kuusemea upande mmoja tu na kwingine kukaa kimya manake uko katika kusifu na si kuona haki inatendeka.
 
Alicho kosea Afisa wa polisi ni kusema ukweli, hata wenyewe CHADEMA wanajua kuna majimbo machache sana ambayo wanaweza wakashinda ndio maana hata kwenye kura za urais waneshakata tamaa kabisa.

Usemayo ni kweli lkn ukweli huo unaweza ukawa ushahidi huko mbele
 
Hii nchi imejaa wajinga, wapumbavu na vichaa wengi. Inakuwaje mtu anasema huo ndio ukweli!!!
Shida sio ukweli au si ukweli. Je, ni sahihi kutamkwa neno hili na mdau wa uchaguzi wa kitengo cha usalama?
 
Alicho kosea Afisa wa polisi ni kusema ukweli, hata wenyewe CHADEMA wanajua kuna majimbo machache sana ambayo wanaweza wakashinda ndio maana hata kwenye kura za urais waneshakata tamaa kabisa.
Ukweli anaujuwaje kabla kura hazijapigwa na kuhesabiwa?
 
Back
Top Bottom