Video: Vurugu zazuka Kinondoni baada ya raia kugoma mwenzao kuchukuliwa na Polisi wakihofia Polisi huyo kuwa mtekaji

Video: Vurugu zazuka Kinondoni baada ya raia kugoma mwenzao kuchukuliwa na Polisi wakihofia Polisi huyo kuwa mtekaji

Wakuu,

Huko Kinondoni kumetokea zogo na vurugu mtaani baada ya raia kugoma mwenzao kuondoka na mtu aliyejitambulisha kama afisa wa Jeshi La Polisi Ukonga.

Katika video hiyo, mwanaume mmoja alijitambulisha kama Polisi alikuwa akitaka kumchukua kijana mmoja kinyemela.

Wananchi baada ya kuona tukio hilo, walimzingira Polisi huyo na kuanza kumuuliza maswali mbalimbali ikiwemo kwanini hajavaa nguo za kiaskari, kwanini hana gari la Polisi, kama yeye ni Polisi kutoka Ukonga kwanini anakuja Kinondoni kukamata?

Tukio hili linakuja siku chache tangu afisa mmoja wa TRA kupigwa mpaka kufa wakati anajaribu kumkamata raia wa kawaida bila kufuata utaratibu.

Ndio kusema kwamba watanzania wameanza kuamka?

View attachment 3173103


View attachment 3173105
Napata faraja kuona watu wameanza kufunguka akili.

Utaratibu wa Ukamataji uko wazi tangu hapo Mwanzo hakuna Raia anagoma kukanatwa na polisi.

Hawa wasiojulikana siku zote wanajiita asikari polisi.

Utoke Ukonga ukakamate mtu Kinondoni?
 
Wakuu,

Huko Kinondoni kumetokea zogo na vurugu mtaani baada ya raia kugoma mwenzao kuondoka na mtu aliyejitambulisha kama afisa wa Jeshi La Polisi Ukonga.

Katika video hiyo, mwanaume mmoja alijitambulisha kama Polisi alikuwa akitaka kumchukua kijana mmoja kinyemela.

Wananchi baada ya kuona tukio hilo, walimzingira Polisi huyo na kuanza kumuuliza maswali mbalimbali ikiwemo kwanini hajavaa nguo za kiaskari, kwanini hana gari la Polisi, kama yeye ni Polisi kutoka Ukonga kwanini anakuja Kinondoni kukamata?

Tukio hili linakuja siku chache tangu afisa mmoja wa TRA kupigwa mpaka kufa wakati anajaribu kumkamata raia wa kawaida bila kufuata utaratibu.

Ndio kusema kwamba watanzania wameanza kuamka?

View attachment 3173103


View attachment 3173105
Sielewi CCM na Serikali strategy yao ni nini? Walitegemea baada ya watu kutekwa hivyo ingekuaje? Huyu jamaa angelazimisha naye angepigwa mawe hadi afe alafu ungesikia mapovu ya RC na IGP!!

Ni vizuri hatua zichukuliwe, kwani hao TISS kazi yao ni nini? Wanashindwaje kukamata hao watekaji wa Soka, Nondo, Sativa na mamia ya watoto wanaotekwa hovyo nchini!! Mbona hizi kelele zingeisha?

Hii nchi inatia sana hasira
 
KWa utaratibu ninaoujua mimi, mwanajeshi akina mtaani kwetu hata kama ni likizo ni lazima aende kwenye uongozi wa serikali za mtaa akaripoti na nafhani kuna fomu wanaijaza kisha wanatuma kazini kwao.
Polisi anakuja aeneo ambalo kuna uongozi tayari ambao ni Mjumbe wa nyumba kumi, Serikali ya mtaa, Serikali ya kitongoji, Diwani na wajumbe wengine wote, anawaruka bila kutoa taarifa ya uwepo wake kwa hawa wenye mamlaka kwa ngazi hizi za chini na kwenda moja kwa moja kumkamata mtu anayesadikiwa ni mtuhumiwa kweli?
Kwanini hawa watu waliopo serikalini hawapendi kufata sheria kama wanavyotaka sisi tufanye?
Ina maana hizi serikali za mitaa na vijiji viongozi wake ndio hawaheshimiki kiasi hiki?
 
Back
Top Bottom