Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Kenya hakuna kubambikiwa kesi kesi kupigwa risasi wafanyabiashara kubambikiwa kodi na TRA kupewa kesi za uhujumu uchumi kwa njia haramu za kishetani kama Tanzania
 
Kenya hakuna kubambikiwa kesi kesi kupigwa risasi wafanyabiashara kubambikiwa kodi na TRA kupewa kesi za uhujumu uchumi kwa njia haramu za kishetani kama Tanzania


Inahusiana nini na Mada?
 
Mkuu jadili hoja. Simba na Yanga zinakutana uwanjani referi, kibendela na kamisaa na uwanja vyote ni vya Simba, Yanga atakuwa na chake? Hiyo ndo hoja.
mbona simba alifungwa 1-0 na Morrison wakati tff yao, marefa wao, wamesajiri kwa gharama kubwa mwisho wakaona isiwe tabu nahuyo morisson tunamckua
 
Kwa Africa hata kwenye nchi zenye tume huru bado malalamiko huwa ayakosekanagi.
Lakini yanatofautiana kipimo cha uzito.

Kuna unafuu! Kuna wengine wanautafuta unafuu. Kama ni tabia ya nchi wenzetu kwao yanaanza mapambazuko ya asubuhi kwetu ndiyo tunalinyemelea giza la alfajiri.

Sisi hatuyafahamu manufaa ya Jua! Angalau wenzetu wanayafahamu kwa kiasi.
 
Una uhakika Tanzania hakuna ukabila? Angalia jpma alivyojaza wasukuma serikalini CDF, mkurugenzi wa pccb, doto James na mawazili kibao
kwani wao hawaruhusiwi kufanya kazi hizo kama sifa na uwezo wanavyo?
 
Siasa za Kenya ni za ubaguzi wa kikabila.

Kenya wapambane kwanza waondoe hili kabla ya wao kukosoa wengine.
Lakini lakwetu hili ni la kijinga sana, yani kwa hali ya kawaida ni jambo la kitoto sana ...lakn Kuna siku litakuja badilika inshallah
 
CCM ya sasa polepole ndiyo huonwa ana Akili, katumia fursa hiyo kujitajirisha akibuni miradi ya kubomoa vyama vya upinzani kudidimiza demokrasia kudhoofisha chadema kuua upinzani anapewa mabilioni amazifanyia ufisadi mkubwa, aliingia CCM akiwa apeche alolo sasa ni tajiri mkubwa kwa pesa za kusingizia anazitumia kuwahujumu chadema na upinzani kwa ujumla, CCM ya sasa wajanja wachache hutumia udhaifu wa mtukufu magufuli kuichukia chadema kupiga pesa nyingi.
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022

Umemsikiliza alichoongea lakini?msikilize vizuri then toa majibu ya hoja yake. Asante
 
hao wakenya unaowana wanaakili. umesahau kila baada ya uchaguzi mtu analalamika kaibiwa kura mpaka mara ya mwisho kajiapisha mwenyewe.kwa ufupi ni kwamba wao waseme tu maana ni kawaida yao lakini sisi hatuna cha kujifunza kutoka kenya.
 
Sawa bwashee.
wadau wakuu wa mabadiliko ya tume ni vyama vyote vya siasa.lakini cha kushangaza hawaonyeshi kuitaka tume huru kwa mapana mpaka uchaguzi ukaribie ndo unaona madai ya tume huru tena sio kwamsisitizo.
Hii inaonyesha kabisa kwa nchi yetu vyama pinzani havionyeshi nia ya dhati kutaka tumehuru ndo maana wanashiriki uchaguzi bila tume huru.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…