Vifo vya marafiki zangu wa karibu vimeniathiri kisaikolojia naogopa sana Ukimwi mpaka napitiliza. Kila nikifanya mapenzi naona zamu yangu imekuja

Vifo vya marafiki zangu wa karibu vimeniathiri kisaikolojia naogopa sana Ukimwi mpaka napitiliza. Kila nikifanya mapenzi naona zamu yangu imekuja

Habari wadau.

Ukweli mchungu najiona nina tatizo la kisaikolojia.

Binafsi chuo nilisoma Mzumbe enzi zile za division one tupu ndio wanapata admission.

Nikiwa chuo nilipata marafiki wengi sana ila hawa watatu wameniathiri kisaikolojia. Mmoja aliitwa Nelson mwingine Frank na mwingine Abdul.

Nelson alikuwa anasomea uhasibu kozi yake ilikuwa maarufu sana kwa vichwa wanaita BAF, Nelson ndie alikuwa best students wa masomo ya biashara kidato cha sita. Alipewa zawadi kwa kuongoza nchi nzima masomo hayo.

Frank alikuwa anasoma Law na yeye alikuwa kichwa sana.

Na Abdul nae alikuwa anasoma BAF na yeye alikuwa vizuri sana darasani.

Baada ya kumaliza chuo nelson alipata kazi kampuni maarufu za uhasibu wanaziita big four.. then akahamia TRA.

Frank alipata kazi baada ya chuo kama mkufunzi ama lecture wa chuo kimoja cha uma maarufu

Abdul na yeye alipata kazi Big four nyingine.. tofauti na ile alienda nelson.

Mimi pia nilipata kazi bank moja maarufu siitaji jina.

Baada ya chuo maisha yalikuwa bata sana maana marafiki wote tulikuwa jijini dar es salaam. Kila siku tunakutana tunakula bata sana siku za weekend.. maana tulipanga nyumba maeneo jirani.

Kwa ufupi marafiki zangu wote walifariki vifo vilivyofuatana.. ndani ya miaka mitano wakaondoka wote na kuniacha mpweke.

Alianza nelson alifariki kwa ini kufeli baada ya kupata hepatitis B

Akaja abdul na yeye alifariki kwa TB ambayo ilisababisha na HIV

Wa mwisho kabisa akawa Frank na yeye alifariki kwa bacteria kwenye ubongo waliosabishwa na HIV complications.

Nje ya hao Pia nilikuwa na rafiki yangu mwingine mwalimu nilijuana nae wakati ananifundisha Physics A level anaitwa Elias Na yeye na yeye akaja kufariki kwa sababu zinazosemekana ni HIV complications.

Ukweli vifo hivyo vya jamaa zangu vimeniathiri sana kisaikolojia.

Nimekuwa na huzuni sana na uoga mkubwa sana. Najiona Naogopa madem sana mpaka napitiliza.
Lesson
Naiusia nafsi yangu na kuwausia ndugu jamaa na marafiki zangu juu ya kumuogopa Allah kwa kufanya aliyotuamrisha na kukatazika kwa aliyotukataza

Hapa issue ni je walishafanya toba ya kweli ili Allah awasamehe huko walikoenda?

Maana kifo si tatizo tatizo ni kuridhiwa na Allah
 
Wasomi wanaondekeza ngono zembe ,ni bure kabisa .
Kila mtu atakufa ila sio kwa ugonjwa wa kishamba ,ugonjwa wa aibu kabisa.

Ushamba mzigo bata na umalaya ni kwa washamba tu ,Nn ambacho hamjui hapo mjini ?...Vijana kaeni kwa kutulia ushapata kazi badala uanze kuporomosha mijengo mnaanza kuwa washamba wa kuzunguka kweny mahoteli .
 
Kuna Kitu Mungu anatupitisha Katika Maisha Yetu kama Fumbo. Ukiwa kijana Mdogo ukamaliza Chuo halafu ukapata Hela Nyingi lakini Bado akili yako ni Ya Ujana Utakufa Kifo Kibaya sana..

Nimeona Vijana Wengi wakipata Kazi Baada tu ya Kuamaliza Chuo na kuanza kulipwa mil 1 kuendelea

1. Wanunuzi wakubwa wa Iphone na Laptop za Apple
2. Atapanga Nyumba ya Laki 2 kwa Mwezi (apartment)
3. Atanunua TV nchi 65
4. Makochi yake ya Ndani mil 1.5
5. Ataanza Kutafita Subaru au IST ya Kutambia Mjini
6. Pub na Viwanja Vingi vitakuwa Vyake
7. Mademu wengi atagonga

Maisha Haya Yote ni kutokana na Kutokuwa na Experience ya Kukosa Kazi au Kukosa Hela... Exposure ya Maisha Hawana Vijana ,hawajawahi Ishi Maisha Ya Shida wakajua Thamani ya Pesa Waipatayo ...Vijana Tubadilike
Mimi kwa utafiti wangu kuna uhusiano mkubwa kati ya wasomi na ushamba ..Hii ni kweli.

Kazi yangu ya kwanza ni baada ya kumaliza chuo ,nilikuwa napata take home ya 2.5 baada ya makato yote nina bima na kila kitu tena kwa taasisi yetu ni VIP.

Wenzangu nilioanza nao ,ni hawa walikuwa toppers sana ila wengine nashangaa walianza kuwa walevi mpaka kushuka kiutendaji...Assume kulipwa hivyo bado watu wanakopa tena kwa utapeli wengine hawakulipi mpaka ugomvi.

Kuna haja gani ya kuanza kulala kweny mahoteli kwa mshahara wa 2.5 mil ?

Ushamba mzigo sana ,baadae ile taasisi tuliondolewa maana licha ya mishahara palikuwa na posa na safari za kudele ,tulipoenda ikawa ni mshahara tu bila ya posho .

Wengi hawana maendeleo kabisa mpake leo ,kwa dili za pale ukijibana kwa kuweka miaka 4 una mjengo na gari bila ya mkopo ...Ila mpaka sasa mtu ana mkopo wa million 60 ndio kajenga .
 
"Akaja abdul na yeye alifariki kwa TB ambayo ilisababisha na HIV"

TB inasabisha HIV ? Hiyo Pathophysiology ya wapi bwana mdogo anyway 1st thing ni kukubaliana hiyo hali iliyotokea kwa hao besties zako ikumbukwe kwamba some days we all gonna die ila kila mmoja kwa mtindo wake sasa wee umeanza kusema unaogopa madem.

Acha woga bwana mdogo.
 
Pole Sana

Ila unaweza kutumia muda huu kujitafakari kwa kuona Pamoja na kufanya Sana ngono je umapata faida gani?

Ukiona faida ni chache kuliko faida unaweza kuamua kumshukuru kwa kukupa nafasi ya kuishi na kitulia na mke mmoja mwaminifu.

Kuathirika kisaikolojia.

Hili jambo linaweza kukupata kutokana kuwapoteza ndugu zako au marafiki wa Kari u

Cha kufanya jifunze kushukuru ,itumie hiyo trauma katika kushukuru itaanza kuondoka yenyewe.


Ila waweza pia kutafakari majira na nyakati za wewe kuwa hai na kuendelea kuishi kuwa ipo sababu ya wewe kufanyika ushuhuda.


Pole Sana Ila zingatia kuishi maisha ya usafi cleanest lifestyle na jitahidi kuwa innocence na kukaa katika presence.


God bless you.
 
Mwalimu wangu sana na rafiki yangu pia alinifanya nipate B ya physics necta A level.

Japo binafsi nilijua nimeweka kibanda cha physics mapema sana
Kama kihombo kakufundisha basi wewe ni wa juzi tu maana huyu kamaliza Tosamaganga 2006,sasa kwa namna ulivoanza kuelezea stori yake nikahisi ulimaliza mzumbe university miaka hiyo ya 2000's mpaka hapo utakua umegraduate awamu ya mwisho ya kikwete
Kuna walakini kwenye stori yako uliposema enzi za division one tupu,nikadhani awamu ya mwisho ya mkapa na mwanzoni mwa utawala wa kikwete
 
Kama kihombo kakufundisha basi wewe ni wa juzi tu maana huyu kamaliza Tosamaganga 2006,sasa kwa namna ulivoanza kuelezea stori yake nikahisi ulimaliza mzumbe university miaka hiyo ya 2000's mpaka hapo utakua umegraduate awamu ya mwisho ya kikwete
Kuna walakini kwenye stori yako uliposema enzi za division one tupu,nikadhani awamu ya mwisho ya mkapa na mwanzoni mwa utawala wa kikwete

Kwani mzumbe ya leo hii unapata nafasi undergraduate bila division one ?
 
Kwani mzumbe ya leo hii unapata nafasi undergraduate bila division one ?
Pitia bandiko lako ulichoandika then jijibu hilo swali maana ulisema enzi za divison one tupu ndo wanapata nafasi,means kwa sasa ata two na three wanapata,we msomi umeshindwa kung'amua statement yako mwenyewe? Anyway naamini ushajua wapi ulipokosea kwenye statement yako
 
Pitia bandiko lako ulichoandika then jijibu hilo swali maana ulisema enzi za divison one tupu ndo wanapata nafasi,means kwa sasa ata two na three wanapata,we msomi umeshindwa kung'amua statement yako mwenyewe? Anyway naamini ushajua wapi ulipokosea kwenye statement yako

Neno enzi limeibeba mzumbe ya zama zote maana hata ya leo hii bado division one ndio wanapewa admission
 
Wasomi wanaondekeza ngono zembe ,ni bure kabisa .
Kila mtu atakufa ila sio kwa ugonjwa wa kishamba ,ugonjwa wa aibu kabisa.

Ushamba mzigo bata na umalaya ni kwa washamba tu ,Nn ambacho hamjui hapo mjini ?...Vijana kaeni kwa kutulia ushapata kazi badala uanze kuporomosha mijengo mnaanza kuwa washamba wa kuzunguka kweny mahoteli .
Inaonekana bado ni kijana mdogo usiyejua maisha ni nini alafu unaonekana hujawahi shika fedha nyingi kwenye maisha yako
Sikulaumu
Mfano Kuna watu ni wastaarabu ila wenzao wao wamewaletea ukimwi utawalaumu na kuwaita washamba
 
"Akaja abdul na yeye alifariki kwa TB ambayo ilisababisha na HIV"

TB inasabisha HIV ? Hiyo Pathophysiology ya wapi bwana mdogo anyway 1st thing ni kukubaliana hiyo hali iliyotokea kwa hao besties zako ikumbukwe kwamba some days we all gonna die ila kila mmoja kwa mtindo wake sasa wee umeanza kusema unaogopa madem.

Acha woga bwana mdogo.
We ndo mjinga TB ni moja ya dalili ya HiV
HIV maana yake ni ukosefu wa kinga mwilini na unapelekea upate magonjwa mengine kirahisi kama TB

Mimi nilishawah uguza mgonjwa wa TB cha kwanza kabisa hospitalini walimpima ukimwi
 
Wasomi wanaondekeza ngono zembe ,ni bure kabisa .
Kila mtu atakufa ila sio kwa ugonjwa wa kishamba ,ugonjwa wa aibu kabisa.

Ushamba mzigo bata na umalaya ni kwa washamba tu ,Nn ambacho hamjui hapo mjini ?...Vijana kaeni kwa kutulia ushapata kazi badala uanze kuporomosha mijengo mnaanza kuwa washamba wa kuzunguka kweny mahoteli .
Kuna wanawake wamebakwa na wakaambukizwa ukimwi nawao utawaita washamba
 
Back
Top Bottom