Vifo vya watoto wa shule Arusha: Mabasi ya shule yapewe vipaumbele barabarani

Vifo vya watoto wa shule Arusha: Mabasi ya shule yapewe vipaumbele barabarani

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kifo ni kifo lakini vifo vya wahanga wa ajali hii, looh! Mtu usemeje?

Watu wazima waliokuwa kwenye gari lile waliotoka salama, wanacho nini cha kumwambia nani leo?

"Kwa hakika mtu mzima aliyekufa na watoto wale akipambana kuwakoa alifanya yote yaliyokuwa sahihi."

Hawa watu ilikuwa muhimu kuwaweka katika kumbukumbu zetu kama taifa na kuhakikisha matukio kama haya yanaepukika.

Ni wazi kuwa wengi wenye akili timamu tungekuwa tayari kufa badala ya malaika hawa. Yawezekana ilikuwa ni alfajiri mno na watu wa kuweza kutoa msaada hawakuwa barabarani bado.

Huu uchukuliwaji watoto mapema alfajiri ulikuwa wa kupigwa marufuku. Kama ilivyo kwa magari ya zimamoto, wagonjwa au ya viongozi; magari ya watoto wa shule yangepewa vipaumbele barabarani. Waanze kuchukua watoto angalau 07:00 kukiwa kumepambazuka kabisa.

Barababara za mwendokasi nazo ziwepo kwa matumizi ya magari haya, njiani kwenda mashuleni. Yapo mangapi magari haya, yatatuathiri nini?

Kama taifa kwa kufanya hivi tutakuwa tumejitahidi tulivyoweza japo kuwatendea haki wahanga hawa wakiwa katika mauti.

Wapumzike kwa amani wahanga wa shule ya msingi Ghati Memorial.
 
Kwani pale lilipitumbukia gorongoni kulikuwa na foleni au kizuizi?

Kipaumbele ni kuboresha miundombinu, na kutoa mafunzo au semina maalum kwa madereva!

Kuna ubaya gani sheria ikawa dereva wa school bus awe na leseni Class C?

Na umri usiwe chini ya miaka 45!

Sahivi schools bus zinaendeshwa kama boda boda, wanachomekea na kutanua hovyohovyo kama bodaboda tu
 
Nadhani hayo yote kufanyika inaweza kuwa ngumu Cha msingi ni ku extend ratiba masomo Yao yaanze saa 3:30 na kumalizika saa 8:30 waanze kurudi nyumbani hivyo wanaweza kufika saa 3:00 au inaweza hata kuwa saa 4:00 kamili asubuhi Wala haitazuia wao kujua kusoma na kuandika
 
Kwani pale lilipitumbukia gorongoni kulikuwa na foleni au kizuizi?

Kipaumbele ni kuboresha miundombinu, na kutoa mafunzo au semina maalum kwa madereva!

Kuna ubaya gani sheria ikawa dereva wa school bus awe na leseni Class C?

Na umri usiwe chini ya miaka 45!

Sahivi schools bus zinaendeshwa kama boda boda, wanachomekea na kutanua hovyohovyo kama bodaboda tu

Kwa sababu ya kuepuka foleni walikwenda kuchukuliwa alfajiri. Hivi ndivyo itokeavyo kote.

Zingatia mantiki hapa uchukuaji watoto mapema alfajiri ni hatarishi.
 
Nadhani hayo yote kufanyika inaweza kuwa ngumu Cha msingi ni ku extend ratiba masomo Yao yaanze saa 3:30 na kumalizika saa 8:30 waanze kurudi nyumbani hivyo wanaweza kufika saa 3:00 au inaweza hata kuwa saa 4:00 kamili asubuhi Wala haitazuia wao kujua kusoma na kuandika
Watoto wanaamshwa alfajiri kwenda shule. Hali hii inapaswa kukoma.
 
Wakati Dereva wa Lile Gari la Shule ameenda kuomba msaada Nani Alifungua Mlango hadi watoto wakazama?
 
Wakati Dereva wa Lile Gari la Shule ameenda kuomba msaada Nani Alifungua Mlango hadi watoto wakazama?

Mtu yeyote mzima aliyeshindwa kufanya lolote kuwanusuru watoto hawa pale anayo kesi ya kujibu japo kwa mola.
 
Kwa kutotaka kuyapisha tu magari yaliyobeba malaika kama hawa? Ila viongozi kwenda kazini?
Kupisha haya magari sio jambo rahisi hapo ni kuibua kosa jipya kwa trafiki kuwasumbua watumiaji wengine wa barabara ambao humo ndani yake Kuna watu wengi wanao wahi makazini wakiwemo walimu Drs n.k ambao nao wakichelewa huduma zitazorota
 
Kupisha haya magari sio jambo rahisi hapo ni kuibua kosa jipya kwa trafiki kuwasumbua watumiaji wengine wa barabara ambao humo ndani yake Kuna watu wengi wanao wahi makazini wakiwemo walimu Drs n.k ambao nao wakichelewa huduma zitazorota

Tuna roho ngumu sana kwa hakika hatuwezi hata kufikiria watoto wetu wote mazingira mazuri zaidi ya kufika hata kutoka shule.

Kwani hata kuyapisha yataka polisi, au common sense tu?
 
Hv kwanza mnamjua tajiri/bosi mmiliki wa shule? Hii kesi ya dereva itapotea tu kimya maisha yanaendelea.
 
Waanze kwa kupitia mikataba ya hawa madereva malipo yao pia na ratiba zao unakuta shule Ina magari machache ila wanafunzi wengi hivyo majukumu ya kuwakusanya na kuwarudisha watoto yanakuwa makubwa kwa dereva lakini pia ukaguzi wa magari yao ni muhimu
 
Waanze kwa kupitia mikataba ya hawa madereva malipo yao pia na ratiba zao unakuta shule Ina magari machache ila wanafunzi wengi hivyo majukumu ya kuwakusanya na kuwarudisha watoto yanakuwa makubwa kwa dereva lakini pia ukaguzi wa magari yao ni muhimu

Ratiba zao ni muhimu zikafahamika na kuidhinishwa. Kabla ya 07:00 ni vyema zikafutwa.
 
Back
Top Bottom