Kuna siku nilienda tigo shop kwa ajili ya kujinga na huduma hii lakini walivonambia vimebadilika kwa kupungua kama inavosomeka hapo kweny hii picha nilikimbia wala sikuungwa kuliko hii huduma yao bora hata ya voda ile ya kweny simu kasi internet unanunua mwenyewe kweny cm yako elf50 unapata gb24 mwezi mzima harafu hata zikiisha bado unapata internet mpaka mwezi uishe japo speed inapungua kiasi ili kufikisha mwezi wako ulioijiunga.
Kama mnavoona hapa kweny picha voda unapiga ile menu ya kujiunga vifurushi
149*01 baada ya hapo utachagua namba 6 kasi /siku30 na baadae picha namba 2 itakuja yaani vifurushi vitakuja utachagua namba utakayo iwe namba 1 ya 50k kwa hizo gb24 au 85k gb 34 ni wewe tu vifurushi hivi havikati internet baada ya gb kuisha bali mpka mwezi uishe sema gb zako zikiisha speed ya net inapungua ila mwezi uishe hata ukitumia gb 5 kwa siku ni wewe tu..
NB: KUMBUKA Kupata menu hii ya kasi/siku30 kweny LAINI yako lazima iwezeshwe na hao hao vodacom SIO KILA LAINI INA HII MENU NO utaenda kweny branch za vodashop zao au unapiga simu huduma kwa wateja na utawaambia kusudi lako kuwa unataka kuwezeshwa laini yako kuwa na ile menu ya kasi internet siku30 kweny cm yako ili uwe unajiunga wewe mwenyewe popote mda wowote. Mimi nikienda kabisa vodashop.. Japo kuna baadhi ya maduka yao wahudumu hawana uelewa wa hiki kifurushi.. Kuna vodashop moja ya buguruni lozana niliingia wakanambia hawajui habar hii wanakanielekea niende kariakoo kwa kuwa sio mbali kutoka lozana na kariakoo nilienda. Voda shop nyingine huku mtaani nakoishi wali segerea waliniambia lazima nisajili laini nyingine ili kupata huduma hii kichwa kiliwaka moto maana kuwa na utitiri wa laini nao sio sawa na ni lazima iwe hewani lakini kariakoo wao wakanambia sio lazima usajiri laini nyingine no hata hiyo hiyo laini yako za unayotumia inawezeshwa kwaiyo nikawezesha hii hii na mahali popote nijiunga. ASANTENI UKIKWAMA MAHALI NIAMBIE NIKUSAIDIE.
View attachment 2434454View attachment 2434455